Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 26.7
Bible en Swahili de l’est


Mort et résurrection de Jésus

Complot contre Jésus

1 Ikawa Yesu alipomaliza maneno hayo yote, aliwaambia wanafunzi wake,
Matthieu 19.1 Matthieu 7.28
2 Mnajua ya kuwa baada ya siku mbili itakuwa Pasaka, na Mwana wa Adamu atasalitiwa asulibiwe.
Luc 22.1-22.2 Marc 14.1-14.2 Jean 11.55 Matthieu 20.18-20.19 Luc 24.6-24.7
3 Wakati ule wakuu wa makuhani, na wazee wa watu, wakakusanyika katika behewa ya Kuhani Mkuu, jina lake Kayafa;
Jean 11.47-11.53 Jean 18.24 Marc 14.54 Matthieu 26.57-26.58 Jérémie 18.18-18.20
4 wakafanya shauri pamoja, ili wamkamate Yesu kwa hila na kumwua.
2 Corinthiens 11.3 Actes 7.19 Matthieu 23.33 Matthieu 12.14 Psaumes 2.2
5 Lakini wakasema, Isiwe wakati wa sikukuu, isije ikatokea ghasia katika watu.
Matthieu 27.24 Marc 14.27 Lamentations 3.37 Esaïe 46.10 Marc 14.2

Une femme verse du parfum sur Jésus

6 Naye Yesu alipokuwapo Bethania katika nyumba ya Simoni mkoma,
Matthieu 21.17 Jean 12.1-12.8 Luc 7.37-7.39 Marc 14.3-14.9 Jean 11.1-11.2
7 mwanamke mwenye kibweta cha marhamu ya thamani kubwa alimkaribia akaimimina kichwani pake alipoketi chakulani.
Ecclésiaste 9.8 Psaumes 133.2 Esaïe 57.9 Ecclésiaste 10.1 Luc 7.37-7.38
8 Wanafunzi wake walipoona, wakachukiwa, wakasema, Ni wa nini upotevu huu?
Exode 5.17 1 Samuel 17.28-17.29 Marc 14.4 Aggée 1.2-1.4 Amos 8.5
9 Maana marhamu hii ingaliweza kuuzwa kwa fedha nyingi wakapewa maskini.
Marc 14.5 Jean 12.5-12.6 2 Rois 5.20 Josué 7.20-7.21 1 Samuel 15.21
10 Yesu akatambua akawaambia, Mbona mnamtaabisha mwanamke? Maana ni kazi njema aliyonitendea mimi.
Tite 3.14 Tite 3.8 Hébreux 13.21 Colossiens 1.10 Tite 1.16
11 Kwa maana siku zote mnao maskini pamoja nanyi; lakini mimi hamnami siku zote.
Deutéronome 15.11 Marc 14.7 Matthieu 28.20 Jean 16.28 Jean 12.8
12 Maana kwa kunimwagia mwili wangu marhamu hiyo, ametenda hivyo ili kuniweka tayari kwa maziko yangu.
2 Chroniques 16.14 Jean 12.7 Marc 16.1 Marc 14.8 Luc 23.56-24.1
13 Amin, nawaambieni, Kila patakapohubiriwa Injili hii katika ulimwengu wote, tendo hilo alilolitenda huyu litatajwa pia kwa kumbukumbu lake.
Marc 14.9 Matthieu 24.14 1 Samuel 2.30 Esaïe 52.9 Psaumes 98.2-98.3
14 Wakati huo mmoja wa wale Thenashara, jina lake Yuda Iskariote, aliwaendea wakuu wa makuhani,
Matthieu 10.4 Luc 22.3-22.6 Jean 13.2 Jean 13.30 Jean 6.70-6.71
15 akasema, Ni nini mtakachonipa, nami nitamsaliti kwenu? Wakampimia vipande thelathini vya fedha.
Zacharie 11.12-11.13 Exode 21.32 2 Pierre 2.14-2.15 Juges 17.10 Matthieu 27.3-27.5
16 Tokea wakati huo akawa akitafuta nafasi apate kumsaliti.
Luc 22.6 Marc 14.11

Institution de la cène

17 Hata siku ya kwanza ya mikate isiyotiwa chachu, wanafunzi wake wakamwendea Yesu, wakamwambia, Ni wapi utakapo tukuandalie uile Pasaka?
Exode 12.18-12.20 Exode 12.6 Lévitique 23.5-23.6 Luc 22.7-22.13 Exode 13.6-13.8
18 Akasema, Enendeni mjini kwa mtu fulani, mkamwambie, Mwalimu asema, Majira yangu ni karibu; kwako nitafanya Pasaka pamoja na wanafunzi wangu.
Jean 7.6 Jean 13.1 Jean 7.30 Jean 17.1 Jean 7.8
19 Wanafunzi wakafanya kama Yesu alivyowaagiza, wakaiandaa Pasaka.
Matthieu 21.6 Jean 15.14 2 Chroniques 35.10-35.11 Jean 2.5 Exode 12.4-12.8
20 Basi kulipokuwa jioni aliketi chakulani pamoja na wale Thenashara.
Marc 14.17-14.21 Jean 13.21 Luc 22.14-22.16 Exode 12.11 Cantique 1.12
21 Nao walipokuwa wakila, alisema, Amin, nawaambia, Mmoja wenu atanisaliti.
Jean 13.21 Jean 6.70-6.71 Matthieu 26.2 Luc 22.21-22.23 Hébreux 4.13
22 Wakahuzunika sana, wakaanza kumwuliza mmoja mmoja, Ni mimi, Bwana?
Marc 14.19-14.20 Luc 22.23 Jean 13.22-13.25 Jean 21.17
23 Akajibu akasema, Yeye aliyetia mkono wake pamoja nami katika kombe, ndiye atakayenisaliti.
Jean 13.18 Psaumes 41.9 Luc 22.21 Jean 13.26-13.28
24 Mwana wa Adamu aenda zake, kama alivyoandikiwa; lakini ole wake mtu yule ambaye amsaliti Mwana wa Adamu! Ingekuwa heri kwake mtu yule kama asingalizaliwa.
Luc 24.46 Actes 26.22-26.23 Actes 17.2-17.3 Matthieu 26.56 Matthieu 26.54
25 Yuda, yule mwenye kumsaliti, akajibu, akasema, Ni mimi, Rabi? Akamwambia, Wewe umesema.
Matthieu 26.64 Matthieu 27.11 2 Rois 5.25 Proverbes 30.20 Jean 18.37
26 Nao walipokuwa wakila Yesu alitwaa mkate, akabariki, akaumega, akawapa wanafunzi wake, akasema, Twaeni, mle; huu ndio mwili wangu
1 Corinthiens 11.23-11.29 Matthieu 14.19 Actes 20.7 Luc 22.18-22.20 Luc 24.30
27 Akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, akisema, Nyweni nyote katika hiki;
1 Corinthiens 10.16 Esaïe 25.6 1 Corinthiens 11.28 Cantique 5.1 Luc 22.20
28 kwa maana hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.
Matthieu 20.28 Apocalypse 7.14 Exode 24.7-24.8 Hébreux 13.20 Hébreux 9.14-9.22
29 Lakini nawaambieni, Sitakunywa kabisa tangu sasa uzao huu wa mzabibu, hata siku ile nitakapokunywa mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu.
Actes 10.41 Matthieu 13.43 Marc 14.25 Apocalypse 7.17 Hébreux 12.2
30 Nao walipokwisha kuimba, wakatoka nje kwenda mlima wa Mizeituni.
Matthieu 21.1 Luc 22.39 Marc 14.26-14.31 Jean 14.31 Jean 18.1-18.4
31 Ndipo Yesu akawaambia, Ninyi nyote mtachukizwa kwa ajili yangu usiku huu kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika.
Zacharie 13.7 Jean 16.32 Marc 14.27-14.28 Matthieu 11.6 Ezéchiel 34.5-34.6
32 Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.
Matthieu 28.16 Luc 18.33-18.34 Matthieu 28.10 Marc 16.7 1 Corinthiens 15.6
33 Petro akajibu, akamwambia, Wajapochukizwa wote kwa ajili yako, mimi sitachukizwa kamwe.
Luc 22.33 1 Pierre 5.5-5.6 Psaumes 119.116-119.117 Proverbes 20.6 Psaumes 17.5
34 Yesu akamwambia, Amin, nakuambia wewe, usiku huu kabla ya kuwika jogoo, utanikana mara tatu.
Jean 13.38 Luc 22.34 Matthieu 26.75 Marc 14.30-14.31
35 Petro akamwambia, Ijaponipasa kufa nawe, sitakukana kamwe. Na wanafunzi wote wakasema vivyo hivyo.
Jean 13.37 Romains 11.20 Philippiens 2.12 1 Pierre 1.17 Matthieu 20.22-20.24

Arrestation de Jésus

36 Kisha Yesu akaenda pamoja nao mpaka bustani iitwayo Gethsemane, akawaambia wanafunzi wake, Ketini hapa, hata niende kule nikaombe.
Matthieu 26.39 Luc 22.39-22.46 Matthieu 26.42 Psaumes 22.1-22.2 Marc 14.32-14.42
37 Akamchukua Petro na wale wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuhuzunika na kusononeka.
Matthieu 4.21 Matthieu 17.1 Marc 5.37 Luc 22.44 Marc 14.33-14.34
38 Ndipo akawaambia, Roho yangu ina huzuni nyingi kiasi cha kufa; kaeni hapa, mkeshe pamoja nami.
Jean 12.27 Matthieu 25.13 Matthieu 26.40-26.41 1 Pierre 3.18 Esaïe 53.3
39 Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifulifuli, akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwezekana, kikombe hiki kiniepuke; walakini si kama nitakavyo mimi, bali kama utakavyo wewe.
Jean 6.38 Matthieu 26.42 Jean 5.30 Philippiens 2.8 Hébreux 5.7
40 Akawajia wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, Je! Hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja?
Matthieu 25.5 Matthieu 26.35 Matthieu 26.43 Luc 9.32 Marc 14.37
41 Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.
Matthieu 6.13 1 Corinthiens 16.13 Luc 22.46 1 Corinthiens 9.27 Matthieu 25.13
42 Akaenda tena mara ya pili, akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwa haiwezekani kikombe hiki kiniepuke nisipokunywa, mapenzi yako yatimizwe.
Matthieu 26.39 Hébreux 4.15 Marc 14.39-14.40 Psaumes 69.1-69.3 Psaumes 22.1-22.2
43 Akaja tena, akawakuta wamelala; maana macho yao yamekuwa mazito.
Luc 9.32 Romains 13.1 Jonas 1.6 Proverbes 23.34 Actes 20.9
44 Akawaacha tena, akaenda, akaomba mara ya tatu, akisema maneno yale yale.
2 Corinthiens 12.8 Daniel 9.17-9.19 Matthieu 6.7 Luc 18.1
45 Kisha akawajia wanafunzi wake, akawaambia, Laleni sasa, mpumzike tazama, saa imekaribia, na Mwana wa Adamu anatiwa katika mikono ya wenye dhambi.
Jean 13.1 Jean 17.1 Luc 22.53 1 Rois 18.27 Matthieu 26.18
46 Ondokeni, twende zetuni! Tazama, yule anayenisaliti amekaribia.
Jean 14.31 Luc 12.50 Actes 21.13 1 Samuel 17.48 Luc 22.15
47 Basi alipokuwa katika kusema, tazama, Yuda, mmoja wa wale Thenashara akaja, na pamoja naye kundi kubwa wenye panga na marungu, wametoka kwa wakuu wa makuhani na wazee wa watu.
Matthieu 26.55 Actes 1.16 Matthieu 26.14 Marc 14.43-14.50 Luc 22.47-22.53
48 Na yule mwenye kumsaliti alikuwa amewapa ishara, akisema, Nitakayembusu, huyo ndiye; mkamateni.
Marc 14.44 Psaumes 55.20-55.21 2 Samuel 3.27 Psaumes 28.3 2 Samuel 20.9-20.10
49 Mara akamwendea Yesu, akasema, Salamu, Rabi, akambusu.
Matthieu 26.25 Jean 19.3 Matthieu 27.29-27.30 Luc 7.45 Marc 14.45-14.46
50 Yesu akamwambia, Rafiki, fanya ulilolijia. Wakaenda, wakanyosha mikono yao wakamkamata Yesu.
Matthieu 20.13 Matthieu 22.12 Psaumes 41.9 Luc 22.48 Psaumes 55.13-55.14
51 Na tazama, mmoja wao waliokuwa pamoja na Yesu akanyosha mkono wake, akaufuta upanga wake, akampiga mtumwa wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.
Marc 14.47 2 Corinthiens 10.4 Jean 18.36 Luc 22.49-22.51 Luc 9.55
52 Ndipo Yesu akamwambia, Rudisha upanga wako mahali pake, maana wote waushikao upanga, wataangamia kwa upanga.
Genèse 9.6 Apocalypse 13.10 Romains 12.19 1 Pierre 3.9 1 Pierre 2.21-2.23
53 Ama wadhani ya kuwa mimi siwezi kumsihi Baba yangu, naye ataniletea sasa hivi zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika?
Matthieu 4.11 2 Rois 6.17 Luc 8.30 Daniel 7.10 Matthieu 25.31
54 Yatatimizwaje basi maandiko, ya kwamba hivyo ndivyo vilivyopasa kujiri?
Matthieu 26.24 Zacharie 13.7 Luc 24.25-24.26 Actes 1.16 Jean 10.35
55 Saa ile Yesu akawaambia makutano, Je, mmetoka kama kumkamata mnyang’anyi, wenye panga na marungu, ili kunishika? Kila siku naliketi hekaluni nikifundisha, msinikamate.
Jean 8.2 Marc 12.35 Luc 22.52-22.53 Jean 18.20-18.21 Jean 7.28
56 Lakini haya yote yamekuwa, ili maandiko ya manabii yatimizwe. Ndipo wanafunzi wote wakamwacha, wakakimbia.
Matthieu 26.31 Jean 16.32 Jean 18.15-18.16 Matthieu 26.54 Zacharie 13.7

Jésus devant le conseil juif

57 Nao waliomkamata Yesu wakampeleka kwa Kayafa, Kuhani Mkuu, walikokuwa wamekutanika waandishi na wazee.
Matthieu 26.3 Jean 11.49 Luc 22.54-22.55 Marc 14.53-14.65 Jean 18.12-18.14
58 Na Petro akamfuata kwa mbali mpaka behewa ya Kuhani Mkuu, akaingia ndani, akaketi pamoja na watumishi, auone mwisho.
Jean 7.32 Jean 7.45 Jean 18.15-18.16 Jean 18.25
59 Basi wakuu wa makuhani na baraza yote wakatafuta ushuhuda wa uongo juu ya Yesu, wapate kumwua;
Deutéronome 19.16-19.21 Actes 6.11-6.13 Matthieu 5.22 Psaumes 27.12 Actes 24.1-24.13
60 wasiuone wangawa walitokea mashahidi wa uongo wengi.
Deutéronome 19.15 Psaumes 35.11 Psaumes 27.12 Marc 14.57-14.59 Daniel 6.4-6.5
61 Hata baadaye wawili wakatokea, wakasema, Huyu alisema, Naweza kulivunja hekalu la Mungu, na kulijenga kwa siku tatu.
Matthieu 27.40 Marc 15.29 Esaïe 53.3 Esaïe 49.7 Actes 22.22
62 Kisha Kuhani Mkuu akasimama akamwambia, Hujibu neno? Hawa wanakushuhudia nini?
Matthieu 27.12-27.14 Marc 14.60 Luc 23.9 Jean 18.19-18.24 Jean 19.9-19.11
63 Lakini, Yesu akanyamaza. Kuhani Mkuu akamwambia, Nakuapisha kwa Mungu aliye hai, utuambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu.
Lévitique 5.1 Matthieu 16.16 Matthieu 27.12 Jean 10.24 Esaïe 53.7
64 Yesu akamwambia, Wewe umesema; lakini nawaambieni, Tangu sasa mtamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kuume wa nguvu, akija juu ya mawingu ya mbinguni.
Daniel 7.13 Hébreux 1.3 Matthieu 26.25 Marc 14.62 Psaumes 110.1
65 Ndipo Kuhani Mkuu akararua mavazi yake, akisema, Amekufuru; mna haja gani tena ya mashahidi? Tazameni, sasa mmesikia hiyo kufuru yake;
Jean 10.36 Matthieu 9.3 Lévitique 21.20 1 Rois 21.10-21.13 Jérémie 36.24
66 mwaonaje ninyi? Wakajibu, wakasema, Imempasa kuuawa.
Jean 19.7 Lévitique 24.11-24.16 Actes 13.27-13.28 Actes 7.52 Jacques 5.6
67 Ndipo wakamtemea mate ya uso, wakampiga makonde; wengine wakampiga makofi,
Matthieu 27.30 Esaïe 50.6 Jean 18.22 Esaïe 53.3 Esaïe 52.14
68 wakisema, Ewe Kristo, tufumbulie; ni nani aliyekupiga?
Marc 14.65 Luc 22.63-22.65 Jean 19.2-19.3 Marc 15.18-15.19 Matthieu 27.28-27.29
69 Na Petro alikuwa ameketi nje behewani; kijakazi mmoja akamwendea, akasema, Wewe nawe ulikuwapo pamoja na Yesu wa Galilaya.
Matthieu 26.71 2 Pierre 2.7-2.9 Psaumes 1.1 Jean 7.52 Matthieu 26.3
70 Akakana mbele ya wote, akisema, Sijui usemalo.
Apocalypse 21.8 1 Corinthiens 10.12 Matthieu 26.34-26.35 Psaumes 119.115-119.117 Jérémie 17.9
71 Naye alipotoka nje hata ukumbini, mwanamke mwingine alimwona, akawaambia watu waliokuwako huko, Huyu alikuwapo pamoja na Yesu Mnazareti.
Marc 14.68-14.69 Luc 22.58 Jean 18.25-18.27
72 Akakana tena kwa kiapo, Simjui mtu huyu.
Zacharie 5.3-5.4 Zacharie 8.17 Matthieu 5.34-5.36 Malachie 3.5 Matthieu 26.74
73 Punde kidogo, wale waliohudhuria wakamwendea, wakamwambia Petro, Hakika wewe nawe u mmoja wao; kwa sababu hata usemi wako wakutambulisha.
Juges 12.6 Néhémie 13.24 Luc 22.59-22.60 Jean 18.26-18.27
74 Ndipo akaanza kulaani na kuapa akisema, Simjui mtu huyu. Na mara akawika jogoo.
Apocalypse 3.19 Matthieu 10.28 Actes 23.12-23.14 1 Corinthiens 16.22 Jean 18.27
75 Petro akalikumbuka lile neno la Yesu alilolisema, Kabla ya kuwika jogoo, utanikana mara tatu. Akatoka nje, akalia kwa majonzi.
Matthieu 26.34 Jean 13.38 Romains 7.18-7.20 Luc 22.61-22.62 Luc 22.31-22.34

Cette Bible est dans le domaine public.