Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 26.67
Bible en Swahili de l’est


Mort et résurrection de Jésus

Complot contre Jésus

1 Ikawa Yesu alipomaliza maneno hayo yote, aliwaambia wanafunzi wake,
Matthieu 19.1 Matthieu 7.28
2 Mnajua ya kuwa baada ya siku mbili itakuwa Pasaka, na Mwana wa Adamu atasalitiwa asulibiwe.
Luc 22.1-22.2 Marc 14.1-14.2 Jean 11.55 Matthieu 20.18-20.19 Jean 2.13
3 Wakati ule wakuu wa makuhani, na wazee wa watu, wakakusanyika katika behewa ya Kuhani Mkuu, jina lake Kayafa;
Jean 11.47-11.53 Jean 18.24 Matthieu 26.57-26.58 Marc 14.54 Matthieu 21.45-21.46
4 wakafanya shauri pamoja, ili wamkamate Yesu kwa hila na kumwua.
Psaumes 2.2 Actes 13.10 Genèse 3.1 2 Corinthiens 11.3 Actes 7.19
5 Lakini wakasema, Isiwe wakati wa sikukuu, isije ikatokea ghasia katika watu.
Matthieu 27.24 Marc 14.12 Actes 4.28 Matthieu 14.5 Matthieu 21.26

Une femme verse du parfum sur Jésus

6 Naye Yesu alipokuwapo Bethania katika nyumba ya Simoni mkoma,
Matthieu 21.17 Marc 14.3-14.9 Jean 12.1-12.8 Luc 7.37-7.39 Marc 11.12
7 mwanamke mwenye kibweta cha marhamu ya thamani kubwa alimkaribia akaimimina kichwani pake alipoketi chakulani.
Cantique 1.3 Jean 12.2-12.3 Exode 30.23-30.33 Ecclésiaste 9.8 Psaumes 133.2
8 Wanafunzi wake walipoona, wakachukiwa, wakasema, Ni wa nini upotevu huu?
Exode 5.17 1 Samuel 17.28-17.29 Marc 14.4 Ecclésiaste 4.4 Jean 12.4-12.6
9 Maana marhamu hii ingaliweza kuuzwa kwa fedha nyingi wakapewa maskini.
1 Samuel 15.21 2 Pierre 2.15 1 Samuel 15.9 Marc 14.5 Jean 12.5-12.6
10 Yesu akatambua akawaambia, Mbona mnamtaabisha mwanamke? Maana ni kazi njema aliyonitendea mimi.
Tite 3.14 Tite 3.8 Galates 5.12 1 Timothée 3.1 2 Thessaloniciens 2.17
11 Kwa maana siku zote mnao maskini pamoja nanyi; lakini mimi hamnami siku zote.
Deutéronome 15.11 Marc 14.7 Jean 12.8 Matthieu 18.20 Matthieu 28.20
12 Maana kwa kunimwagia mwili wangu marhamu hiyo, ametenda hivyo ili kuniweka tayari kwa maziko yangu.
Marc 16.1 Marc 14.8 Luc 23.56-24.1 2 Chroniques 16.14 Jean 12.7
13 Amin, nawaambieni, Kila patakapohubiriwa Injili hii katika ulimwengu wote, tendo hilo alilolitenda huyu litatajwa pia kwa kumbukumbu lake.
Marc 14.9 Matthieu 24.14 Psaumes 112.6 Hébreux 6.10 1 Samuel 2.30
14 Wakati huo mmoja wa wale Thenashara, jina lake Yuda Iskariote, aliwaendea wakuu wa makuhani,
Matthieu 10.4 Luc 22.3-22.6 Jean 13.30 Jean 13.2 Marc 14.10-14.11
15 akasema, Ni nini mtakachonipa, nami nitamsaliti kwenu? Wakampimia vipande thelathini vya fedha.
Exode 21.32 Zacharie 11.12-11.13 Esaïe 56.11 1 Timothée 6.9-6.10 Genèse 37.26-37.28
16 Tokea wakati huo akawa akitafuta nafasi apate kumsaliti.
Luc 22.6 Marc 14.11

Institution de la cène

17 Hata siku ya kwanza ya mikate isiyotiwa chachu, wanafunzi wake wakamwendea Yesu, wakamwambia, Ni wapi utakapo tukuandalie uile Pasaka?
Exode 12.18-12.20 Exode 12.6 Marc 14.12-14.16 Matthieu 26.19 Lévitique 23.5-23.6
18 Akasema, Enendeni mjini kwa mtu fulani, mkamwambie, Mwalimu asema, Majira yangu ni karibu; kwako nitafanya Pasaka pamoja na wanafunzi wangu.
Jean 7.6 Jean 13.1 Jean 7.30 Jean 17.1 Jean 7.8
19 Wanafunzi wakafanya kama Yesu alivyowaagiza, wakaiandaa Pasaka.
Matthieu 21.6 Jean 2.5 Exode 12.4-12.8 Jean 15.14 2 Chroniques 35.10-35.11
20 Basi kulipokuwa jioni aliketi chakulani pamoja na wale Thenashara.
Marc 14.17-14.21 Jean 13.21 Luc 22.14-22.16 Exode 12.11 Cantique 1.12
21 Nao walipokuwa wakila, alisema, Amin, nawaambia, Mmoja wenu atanisaliti.
Jean 13.21 Jean 6.70-6.71 Apocalypse 2.23 Matthieu 26.2 Luc 22.21-22.23
22 Wakahuzunika sana, wakaanza kumwuliza mmoja mmoja, Ni mimi, Bwana?
Luc 22.23 Jean 13.22-13.25 Jean 21.17 Marc 14.19-14.20
23 Akajibu akasema, Yeye aliyetia mkono wake pamoja nami katika kombe, ndiye atakayenisaliti.
Jean 13.18 Psaumes 41.9 Jean 13.26-13.28 Luc 22.21
24 Mwana wa Adamu aenda zake, kama alivyoandikiwa; lakini ole wake mtu yule ambaye amsaliti Mwana wa Adamu! Ingekuwa heri kwake mtu yule kama asingalizaliwa.
Luc 24.46 Actes 26.22-26.23 Matthieu 18.7 Marc 9.12 1 Corinthiens 15.3
25 Yuda, yule mwenye kumsaliti, akajibu, akasema, Ni mimi, Rabi? Akamwambia, Wewe umesema.
Matthieu 26.64 Matthieu 27.11 Matthieu 26.49 Matthieu 23.7 2 Rois 5.25
26 Nao walipokuwa wakila Yesu alitwaa mkate, akabariki, akaumega, akawapa wanafunzi wake, akasema, Twaeni, mle; huu ndio mwili wangu
1 Corinthiens 11.23-11.29 Matthieu 14.19 Marc 14.22-14.25 Actes 20.7 Luc 22.18-22.20
27 Akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, akisema, Nyweni nyote katika hiki;
Psaumes 116.13 Marc 14.23-14.24 Esaïe 55.1 1 Corinthiens 10.16 Esaïe 25.6
28 kwa maana hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la dhambi.
Matthieu 20.28 Exode 24.7-24.8 Apocalypse 7.14 1 Corinthiens 11.25 Hébreux 10.4-10.14
29 Lakini nawaambieni, Sitakunywa kabisa tangu sasa uzao huu wa mzabibu, hata siku ile nitakapokunywa mpya pamoja nanyi katika ufalme wa Baba yangu.
Matthieu 13.43 Marc 14.25 Actes 10.41 Apocalypse 7.17 Hébreux 12.2
30 Nao walipokwisha kuimba, wakatoka nje kwenda mlima wa Mizeituni.
Luc 22.39 Matthieu 21.1 Colossiens 3.16-3.17 Ephésiens 5.19-5.20 Marc 14.26-14.31
31 Ndipo Yesu akawaambia, Ninyi nyote mtachukizwa kwa ajili yangu usiku huu kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika.
Zacharie 13.7 Jean 16.32 Marc 14.27-14.28 Matthieu 11.6 Ezéchiel 34.5-34.6
32 Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.
Matthieu 28.16 Luc 18.33-18.34 Matthieu 28.10 Marc 16.7 Matthieu 20.19
33 Petro akajibu, akamwambia, Wajapochukizwa wote kwa ajili yako, mimi sitachukizwa kamwe.
Luc 22.33 Jean 21.15 Jean 13.36-13.38 1 Pierre 5.5-5.6 Psaumes 119.116-119.117
34 Yesu akamwambia, Amin, nakuambia wewe, usiku huu kabla ya kuwika jogoo, utanikana mara tatu.
Jean 13.38 Luc 22.34 Matthieu 26.75 Marc 14.30-14.31
35 Petro akamwambia, Ijaponipasa kufa nawe, sitakukana kamwe. Na wanafunzi wote wakasema vivyo hivyo.
Jean 13.37 Proverbes 29.23 1 Corinthiens 10.12 Romains 11.20 Philippiens 2.12

Arrestation de Jésus

36 Kisha Yesu akaenda pamoja nao mpaka bustani iitwayo Gethsemane, akawaambia wanafunzi wake, Ketini hapa, hata niende kule nikaombe.
Psaumes 22.1-22.2 Matthieu 26.39 Luc 22.39-22.46 Matthieu 26.42 Jean 18.1-18.11
37 Akamchukua Petro na wale wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuhuzunika na kusononeka.
Matthieu 4.21 Matthieu 17.1 Marc 5.37 Matthieu 4.18 Jean 12.27
38 Ndipo akawaambia, Roho yangu ina huzuni nyingi kiasi cha kufa; kaeni hapa, mkeshe pamoja nami.
Jean 12.27 Psaumes 116.3 1 Pierre 4.7 Esaïe 53.10 Romains 8.32
39 Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifulifuli, akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwezekana, kikombe hiki kiniepuke; walakini si kama nitakavyo mimi, bali kama utakavyo wewe.
Matthieu 26.42 Jean 6.38 Jean 5.30 Philippiens 2.8 Jean 12.27-12.28
40 Akawajia wale wanafunzi, akawakuta wamelala, akamwambia Petro, Je! Hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja?
Matthieu 25.5 Matthieu 26.35 Matthieu 26.43 Matthieu 26.38 Luc 22.45
41 Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.
Matthieu 6.13 1 Corinthiens 9.27 Matthieu 25.13 Marc 14.38 1 Corinthiens 16.13
42 Akaenda tena mara ya pili, akaomba, akisema, Baba yangu, ikiwa haiwezekani kikombe hiki kiniepuke nisipokunywa, mapenzi yako yatimizwe.
Matthieu 26.39 Marc 14.39-14.40 Hébreux 4.15 Psaumes 69.17-69.18 Psaumes 69.1-69.3
43 Akaja tena, akawakuta wamelala; maana macho yao yamekuwa mazito.
Luc 9.32 Actes 20.9 1 Thessaloniciens 5.6-5.8 Romains 13.1 Jonas 1.6
44 Akawaacha tena, akaenda, akaomba mara ya tatu, akisema maneno yale yale.
2 Corinthiens 12.8 Matthieu 6.7 Luc 18.1 Daniel 9.17-9.19
45 Kisha akawajia wanafunzi wake, akawaambia, Laleni sasa, mpumzike tazama, saa imekaribia, na Mwana wa Adamu anatiwa katika mikono ya wenye dhambi.
Jean 13.1 Jean 17.1 Luc 22.53 Jean 12.27 Matthieu 26.14-26.15
46 Ondokeni, twende zetuni! Tazama, yule anayenisaliti amekaribia.
Jean 14.31 1 Samuel 17.48 Luc 22.15 Luc 9.51 Luc 12.50
47 Basi alipokuwa katika kusema, tazama, Yuda, mmoja wa wale Thenashara akaja, na pamoja naye kundi kubwa wenye panga na marungu, wametoka kwa wakuu wa makuhani na wazee wa watu.
Matthieu 26.55 Actes 1.16 Luc 22.47-22.53 Jean 18.1-18.11 Matthieu 26.14
48 Na yule mwenye kumsaliti alikuwa amewapa ishara, akisema, Nitakayembusu, huyo ndiye; mkamateni.
2 Samuel 3.27 Psaumes 28.3 2 Samuel 20.9-20.10 Marc 14.44 Psaumes 55.20-55.21
49 Mara akamwendea Yesu, akasema, Salamu, Rabi, akambusu.
Matthieu 26.25 1 Samuel 10.1 1 Thessaloniciens 5.26 Genèse 27.26 Jean 19.3
50 Yesu akamwambia, Rafiki, fanya ulilolijia. Wakaenda, wakanyosha mikono yao wakamkamata Yesu.
Matthieu 20.13 Matthieu 22.12 Psaumes 55.13-55.14 2 Samuel 16.17 Psaumes 41.9
51 Na tazama, mmoja wao waliokuwa pamoja na Yesu akanyosha mkono wake, akaufuta upanga wake, akampiga mtumwa wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.
Marc 14.47 Jean 18.36 2 Corinthiens 10.4 Luc 22.36-22.38 Jean 18.10-18.11
52 Ndipo Yesu akamwambia, Rudisha upanga wako mahali pake, maana wote waushikao upanga, wataangamia kwa upanga.
Genèse 9.6 Apocalypse 13.10 Romains 12.19 1 Pierre 3.9 1 Pierre 2.21-2.23
53 Ama wadhani ya kuwa mimi siwezi kumsihi Baba yangu, naye ataniletea sasa hivi zaidi ya majeshi kumi na mawili ya malaika?
Matthieu 4.11 2 Rois 6.17 Daniel 7.10 Luc 8.30 Matthieu 25.31
54 Yatatimizwaje basi maandiko, ya kwamba hivyo ndivyo vilivyopasa kujiri?
Matthieu 26.24 Zacharie 13.7 Luc 24.25-24.26 Actes 1.16 Luc 24.44-24.46
55 Saa ile Yesu akawaambia makutano, Je, mmetoka kama kumkamata mnyang’anyi, wenye panga na marungu, ili kunishika? Kila siku naliketi hekaluni nikifundisha, msinikamate.
Marc 12.35 Jean 8.2 Marc 14.48-14.50 Jean 7.14 Luc 22.52-22.53
56 Lakini haya yote yamekuwa, ili maandiko ya manabii yatimizwe. Ndipo wanafunzi wote wakamwacha, wakakimbia.
Matthieu 26.31 Jean 16.32 Jean 18.15-18.16 Matthieu 26.54 Marc 14.50-14.52

Jésus devant le conseil juif

57 Nao waliomkamata Yesu wakampeleka kwa Kayafa, Kuhani Mkuu, walikokuwa wamekutanika waandishi na wazee.
Matthieu 26.3 Psaumes 56.5-56.6 Jean 18.19-18.24 Jean 11.49 Luc 22.54-22.55
58 Na Petro akamfuata kwa mbali mpaka behewa ya Kuhani Mkuu, akaingia ndani, akaketi pamoja na watumishi, auone mwisho.
Jean 7.32 Jean 18.15-18.16 Jean 18.25 Jean 7.45
59 Basi wakuu wa makuhani na baraza yote wakatafuta ushuhuda wa uongo juu ya Yesu, wapate kumwua;
Deutéronome 19.16-19.21 Marc 14.55-14.56 Psaumes 94.20-94.21 1 Rois 21.8-21.13 Actes 6.11-6.13
60 wasiuone wangawa walitokea mashahidi wa uongo wengi.
Deutéronome 19.15 Psaumes 35.11 Psaumes 27.12 Tite 2.8 1 Pierre 3.16
61 Hata baadaye wawili wakatokea, wakasema, Huyu alisema, Naweza kulivunja hekalu la Mungu, na kulijenga kwa siku tatu.
Matthieu 27.40 Esaïe 49.7 Marc 15.29 Esaïe 53.3 2 Rois 9.11
62 Kisha Kuhani Mkuu akasimama akamwambia, Hujibu neno? Hawa wanakushuhudia nini?
Luc 23.9 Jean 18.19-18.24 Jean 19.9-19.11 Matthieu 27.12-27.14 Marc 14.60
63 Lakini, Yesu akanyamaza. Kuhani Mkuu akamwambia, Nakuapisha kwa Mungu aliye hai, utuambie kama wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu.
Lévitique 5.1 Matthieu 16.16 Matthieu 27.12 1 Samuel 14.26 Jean 10.24
64 Yesu akamwambia, Wewe umesema; lakini nawaambieni, Tangu sasa mtamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kuume wa nguvu, akija juu ya mawingu ya mbinguni.
Daniel 7.13 Matthieu 26.25 Marc 14.62 Psaumes 110.1 Hébreux 1.3
65 Ndipo Kuhani Mkuu akararua mavazi yake, akisema, Amekufuru; mna haja gani tena ya mashahidi? Tazameni, sasa mmesikia hiyo kufuru yake;
Jean 10.36 Matthieu 9.3 Jean 10.33 Luc 5.21 Actes 14.14
66 mwaonaje ninyi? Wakajibu, wakasema, Imempasa kuuawa.
Jean 19.7 Actes 13.27-13.28 Actes 7.52 Jacques 5.6 Lévitique 24.11-24.16
67 Ndipo wakamtemea mate ya uso, wakampiga makonde; wengine wakampiga makofi,
Esaïe 50.6 Matthieu 27.30 Jean 18.22 Esaïe 53.3 Esaïe 52.14
68 wakisema, Ewe Kristo, tufumbulie; ni nani aliyekupiga?
Marc 14.65 Luc 22.63-22.65 1 Pierre 2.4-2.8 Juges 16.25 Matthieu 27.39-27.44
69 Na Petro alikuwa ameketi nje behewani; kijakazi mmoja akamwendea, akasema, Wewe nawe ulikuwapo pamoja na Yesu wa Galilaya.
Matthieu 26.71 Matthieu 2.22-2.23 1 Rois 19.9 Jean 18.25-18.27 Jean 18.16-18.18
70 Akakana mbele ya wote, akisema, Sijui usemalo.
Apocalypse 21.8 1 Corinthiens 10.12 Proverbes 28.26 Matthieu 26.56 Proverbes 29.25
71 Naye alipotoka nje hata ukumbini, mwanamke mwingine alimwona, akawaambia watu waliokuwako huko, Huyu alikuwapo pamoja na Yesu Mnazareti.
Marc 14.68-14.69 Luc 22.58 Jean 18.25-18.27
72 Akakana tena kwa kiapo, Simjui mtu huyu.
Exode 20.7 Esaïe 48.1 Luc 22.34 Zacharie 5.3-5.4 Zacharie 8.17
73 Punde kidogo, wale waliohudhuria wakamwendea, wakamwambia Petro, Hakika wewe nawe u mmoja wao; kwa sababu hata usemi wako wakutambulisha.
Juges 12.6 Luc 22.59-22.60 Jean 18.26-18.27 Néhémie 13.24
74 Ndipo akaanza kulaani na kuapa akisema, Simjui mtu huyu. Na mara akawika jogoo.
Actes 23.12-23.14 1 Corinthiens 16.22 Apocalypse 3.19 Matthieu 10.28 Marc 14.71-14.72
75 Petro akalikumbuka lile neno la Yesu alilolisema, Kabla ya kuwika jogoo, utanikana mara tatu. Akatoka nje, akalia kwa majonzi.
Matthieu 26.34 Jean 13.38 Luc 22.61-22.62 Luc 22.31-22.34 Romains 7.18-7.20

Cette Bible est dans le domaine public.