Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Luc 12.43
Bible en Swahili de l’est


1 Wakati huo, makutano walipokutanika elfu elfu, hata wakakanyagana, alianza kuwaambia wanafunzi wake kwanza, Jilindeni na chachu ya Mafarisayo, ambayo ni unafiki.
Jacques 3.17 1 Corinthiens 5.7-5.8 1 Pierre 2.1 Matthieu 16.6-16.12 Actes 21.20
2 Lakini hakuna neno lililositirika ambalo halitafunuliwa, wala lililofichwa ambalo halitajulikana.
Luc 8.17 Marc 4.22 2 Corinthiens 5.10 1 Corinthiens 4.5 Ecclésiaste 12.14
3 Basi, yo yote mliyosema gizani yatasikiwa mwangani; na mliyonena sikioni mwa mtu katika vyumba vya ndani, yatahubiriwa juu ya dari.
Matthieu 10.27 Matthieu 12.36 Jude 1.14-1.15 Job 24.14-24.15 Ecclésiaste 10.12-10.13
4 Nami nawaambia ninyi rafiki zangu, msiwaogope hao wauuao mwili, kisha baada ya hayo hawana wawezalo kutenda zaidi.
1 Pierre 3.14 Jérémie 1.8 Apocalypse 2.10 Esaïe 51.7-51.13 Jean 15.14-15.15
5 Lakini nitawaonya mtakayemwogopa; mwogopeni yule ambaye akiisha kumwua mtu ana uweza wa kumtupa katika Jehanum; naam, nawaambia, Mwogopeni huyo.
2 Pierre 2.4 Matthieu 10.28 Psaumes 9.17 Hébreux 10.31 Jérémie 5.22
6 Je! Mashomoro watano hawauzwi kwa senti mbili? Wala hasahauliwi hata mmojawapo mbele za Mungu.
Matthieu 10.29 Psaumes 147.9 Psaumes 145.15-145.16 Psaumes 113.5-113.6 Psaumes 50.10-50.11
7 Lakini hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Msiogope basi, bora ninyi kuliko mashomoro wengi.
1 Samuel 14.45 Matthieu 6.26 Matthieu 12.12 Job 35.11 Matthieu 10.30-10.31
8 Nami nawaambia, kila atakayenikiri mbele ya watu, Mwana wa Adamu naye atamkiri yeye mbele ya malaika wa Mungu;
Matthieu 10.32-10.33 Luc 15.10 Romains 10.9-10.10 1 Jean 2.23 Matthieu 25.31-25.34
9 na mwenye kunikana mbele ya watu, huyo atakanwa mbele ya malaika wa Mungu.
2 Timothée 2.12 Marc 8.38 Luc 9.26 Matthieu 7.23 1 Jean 2.23
10 Na kila mtu atakayenena neno juu ya Mwana wa Adamu atasamehewa, bali aliyemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
Matthieu 12.31-12.32 1 Jean 5.16 1 Timothée 1.13 Hébreux 10.26-10.31 Luc 23.34
11 Na watakapowapeleka ninyi mbele ya masinagogi na maliwali na wenye mamlaka, msifadhaike kwa kuwaza maneno yenu jinsi mtakavyojibu au kusema;
Matthieu 10.17-10.20 Matthieu 23.34 Actes 4.5-4.7 Luc 21.12-21.14 Luc 12.22
12 kwa kuwa Roho Mtakatifu atawafundisha saa ile ile yawapasayo kuyasema.
Matthieu 10.20 Luc 21.15 Actes 4.8 Exode 4.11 Actes 7.55

Les biens matériels

13 Mtu mmoja katika mkutano akamwambia, Mwalimu, mwambie ndugu yangu anigawie urithi wetu.
1 Timothée 6.5 Actes 8.18-8.19 Luc 6.45 Ezéchiel 33.31 Psaumes 17.14
14 Akamwambia, Mtu wewe, ni nani aliyeniweka mimi kuwa mwamuzi au mgawanyi juu yenu?
Romains 2.1 Romains 2.3 Romains 9.20 Exode 2.14 Jean 18.35-18.36
15 Akawaambia, Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo.
Hébreux 13.5 1 Timothée 6.6-6.10 Proverbes 16.16 Psaumes 62.10 Jérémie 22.17-22.18
16 Akawaambia mithali, akisema, Shamba la mtu mmoja tajiri lilikuwa limezaa sana;
Psaumes 73.3 Psaumes 73.12 Genèse 26.12-26.14 Actes 14.17 Job 12.6
17 akaanza kuwaza moyoni mwake, akisema, Nifanyeje? Maana sina pa kuyaweka akiba mavuno yangu.
1 Timothée 6.17 Luc 18.22 Luc 12.22 Luc 16.3 Esaïe 58.7
18 Akasema, Nitafanya hivi; nitazivunja ghala zangu, nijenge nyingine kubwa zaidi, na humo nitaweka nafaka yangu yote na vitu vyangu.
Luc 18.4 Jacques 3.15 Psaumes 17.14 Jacques 4.15 Luc 18.6
19 Kisha, nitajiambia, Ee nafsi yangu, una vitu vyema vingi ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi; pumzika basi, ule, unywe, ufurahi.
Ecclésiaste 11.9 1 Corinthiens 15.32 Jacques 4.13-4.15 Proverbes 27.1 1 Timothée 5.6
20 Lakini Mungu akamwambia, Mpumbavu wewe, usiku huu wa leo wanataka roho yako! Na vitu ulivyojiwekea tayari vitakuwa vya nani?
Jérémie 17.11 Psaumes 39.6 Job 27.8 Luc 11.40 Ecclésiaste 5.14-5.16
21 Ndivyo alivyo mtu ajiwekeaye nafsi yake akiba, asijitajirishe kwa Mungu.
Luc 12.33 Matthieu 6.19-6.20 Osée 10.1 Luc 6.24 Romains 2.5
22 Akawaambia wanafunzi wake, Kwa sababu hiyo nawaambia, Msisumbukie maisha yenu, mtakula nini; wala miili yenu, mtavaa nini.
Philippiens 4.6 Hébreux 13.5 Matthieu 6.25-6.34 Luc 12.29 1 Corinthiens 7.32
23 Kwa kuwa maisha ni zaidi ya chakula, na mwili ni zaidi ya mavazi.
Job 1.12 Job 2.6 Proverbes 13.8 Job 2.4 Genèse 19.17
24 Watafakarini kunguru, ya kwamba hawapandi wala hawavuni; hawana ghala wala uchaga, na Mungu huwalisha. Bora ninyi mara nyingi kuliko ndege!
Job 38.41 Psaumes 147.9 Luc 12.7 Matthieu 10.31 Psaumes 145.15-145.16
25 Na yupi kwenu ambaye akijisumbua aweza kujiongeza kimo chake hata mkono mmoja?
Matthieu 5.36 Luc 19.3 Matthieu 6.27
26 Basi, ikiwa hamwezi hata neno lililo dogo, kwa nini kujisumbua kwa ajili ya yale mengine?
Psaumes 39.6 Ecclésiaste 7.13 1 Pierre 5.7 Luc 12.29
27 Yatafakarini maua jinsi yameavyo; hayatendi kazi wala hayasokoti; nami nawaambia ya kwamba hata Sulemani katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo la hayo.
1 Rois 10.1-10.13 2 Chroniques 9.1-9.12 Jacques 1.10-1.11 Luc 12.24 Matthieu 6.28-6.30
28 Basi, ikiwa Mungu huvika hivi majani ya kondeni, yaliyopo leo na kesho hutupwa kalibuni, je! Hatawatendea ninyi zaidi, enyi wa imani haba?
Matthieu 14.31 Matthieu 17.20 Matthieu 17.17 Matthieu 8.26 Luc 8.25
29 Ninyi msitafute mtakavyokula wala mtakavyokunywa; wala msifanye wasiwasi,
Luc 22.35 Matthieu 6.31 Luc 12.22 Luc 10.7-10.8
30 kwa maana, hayo yote ndiyo watafutayo mataifa ya duniani, lakini Baba yenu anajua ya kuwa mna haja na hayo.
Matthieu 6.32 Matthieu 6.8 Matthieu 10.20 Matthieu 18.14 1 Pierre 4.2-4.4
31 Bali utafuteni ufalme wa Mungu, na hayo mtaongezewa.
1 Timothée 4.8 1 Rois 3.11-3.13 Matthieu 6.33 Psaumes 84.11 Jean 6.27
32 Msiogope, enyi kundi dogo; kwa kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ule ufalme.
Esaïe 40.11 Hébreux 12.28 Matthieu 14.27 Philippiens 2.13 Ephésiens 1.5-1.9
33 Viuzeni mlivyo navyo, mtoe sadaka. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, akiba isiyopungua katika mbingu, mahali pasipokaribia mwivi, wala nondo haharibu.
Matthieu 19.21 Actes 2.45 Actes 4.34-4.35 Luc 18.22 Matthieu 6.19-6.21
34 Kwa kuwa hazina yenu ilipo, ndipo itakapokuwapo na mioyo yenu.
Matthieu 6.21 Colossiens 3.1-3.3 Philippiens 3.20

Appel à être prêts

35 Viuno vyenu na viwe vimefungwa, na taa zenu ziwe zinawaka;
1 Pierre 1.13 Matthieu 25.4-25.10 Ephésiens 6.14 Matthieu 25.1 Esaïe 5.27
36 nanyi iweni kama watu wanaomngojea bwana wao, atakaporudi kutoka arusini, ili atakapokuja na kubisha, wamfungulie mara.
Apocalypse 3.20 Cantique 5.5-5.6 Matthieu 24.42-24.44 Genèse 49.18 Matthieu 25.1-25.13
37 Heri watumwa wale, ambao bwana wao ajapo atawakuta wanakesha. Amin, nawaambieni, atajifunga na kuwakaribisha chakulani, atakuja na kuwahudumia.
Matthieu 24.42 Apocalypse 14.13 Jean 13.4-13.5 Philippiens 1.23 1 Pierre 5.1-5.4
38 Na akija zamu ya pili, au akija zamu ya tatu, na kuwakuta hivi, heri watumwa hao.
Matthieu 25.6 1 Thessaloniciens 5.4-5.5
39 Lakini fahamuni neno hili, Kwamba mwenye nyumba angalijua saa atakayokuja mwivi, angalikesha, wala asingaliacha nyumba yake kuvunjwa.
2 Pierre 3.10 Matthieu 24.43-24.44 Apocalypse 3.3 Apocalypse 16.15 1 Thessaloniciens 5.2-5.3
40 Nanyi jiwekeni tayari, kwa kuwa saa msiyodhani ndipo ajapo Mwana wa Adamu.
Apocalypse 19.7 2 Pierre 3.12-3.14 Matthieu 24.44 1 Thessaloniciens 5.6 Romains 13.14
41 Petro akamwambia, Bwana, mithali hiyo umetuambia sisi tu, au watu wote pia?
Marc 13.37 1 Pierre 5.8 Marc 14.37 1 Pierre 4.7
42 Bwana akasema, Ni nani, basi, aliye wakili mwaminifu, mwenye busara, ambaye bwana wake atamweka juu ya utumishi wake wote, awape watu posho kwa wakati wake?
Matthieu 24.45-24.46 Luc 19.15-19.19 Matthieu 25.20-25.23 1 Timothée 3.15 Hébreux 13.7
43 Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta anafanya hivyo.
44 Kweli nawaambia, atamweka juu ya vitu vyake vyote.
Luc 22.29-22.30 Apocalypse 3.18 Daniel 12.2-12.3 Luc 19.17-19.19 Matthieu 24.47
45 Lakini, mtumwa yule akisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia kuja, akaanza kuwapiga wajoli wake, wanaume kwa wanawake, akila na kunywa na kulewa;
Matthieu 24.48-24.50 3 Jean 1.9-1.10 Matthieu 22.6 Esaïe 65.6 Esaïe 56.10-56.12
46 bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani na saa asiyojua, atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wasioamini.
Luc 12.40 Job 20.29 Psaumes 94.14 Psaumes 11.5 Matthieu 13.49-13.50
47 Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana.
Jacques 4.17 Deutéronome 25.2-25.3 Jean 9.41 Jean 15.22-15.24 Actes 17.30
48 Na yule asiyejua, naye amefanya yastahiliyo mapigo, atapigwa kidogo. Na kila aliyepewa vingi, kwake huyo vitatakwa vingi; naye waliyemwekea amana vitu vingi, kwake huyo watataka na zaidi.
Lévitique 5.17 Jacques 3.1 1 Timothée 1.13 Luc 16.10-16.12 Matthieu 25.14-25.29
49 Nimekuja kutupa moto duniani; na ukiwa umekwisha washwa, ni nini nitakalo zaidi?
Malachie 4.1 Joël 2.30-2.31 Matthieu 3.10-3.12 Malachie 3.2-3.3 Esaïe 11.4
50 Lakini nina ubatizo unipasao kubatiziwa, nami nina dhiki kama nini hata utimizwe!
Jean 19.30 Jean 12.27-12.28 Actes 20.22 Jean 7.6-7.8 Jean 10.39-10.41
51 Je! Mwadhani ya kwamba nimekuja kuleta amani duniani? Nawaambia, La, sivyo, bali mafarakano.
Matthieu 10.34-10.36 Luc 12.49 Zacharie 11.14 Zacharie 11.7-11.8 Zacharie 11.10-11.11
52 Kwa kuwa tokea sasa katika nyumba moja watakuwamo watu watano wamefarakana, watatu kwa wawili, wawili kwa watatu.
Actes 14.1-14.4 Actes 28.24 Actes 13.43-13.46 Jean 10.19-10.21 Michée 7.5-7.6
53 Watafarakana baba na mwanawe, na mwana na babaye; mama na binti yake, na binti na mamaye; mkwe mtu na mkwewe, mkwe na mkwe mtu.
Michée 7.6 Zacharie 13.2-13.6 Matthieu 24.10 Matthieu 10.21-10.22
54 Akawaambia makutano pia, Kila mwonapo wingu likizuka pande za magharibi mara husema, Mvua inakuja; ikawa hivyo.
1 Rois 18.44-18.45 Matthieu 16.2-16.4
55 Na kila ivumapo kaskazi, husema, Kutakuwa na joto; na ndivyo ilivyo.
Matthieu 20.12 Job 37.17
56 Enyi wanafiki, mwajua kuutambua uso wa nchi na mbingu; imekuwaje, basi, kuwa hamjui kutambua majira haya?
Matthieu 16.3 Matthieu 24.32-24.33 Daniel 9.24-9.26 Malachie 4.2 Actes 3.24-3.26
57 Na mbona ninyi wenyewe kwa nafsi zenu hamwamui yaliyo haki?
Matthieu 15.10-15.14 Deutéronome 32.29 Luc 21.30 Actes 13.26-13.38 Jean 7.24
58 Maana, unapofuatana na mshitaki wako kwenda kwa mwamuzi, hapo njiani fanya bidii kupatanishwa naye, asije akakuburuta mpaka mbele ya kadhi; yule kadhi akakutia mikononi mwake mwenye kulipiza, na yule mwenye kulipiza akakutupa gerezani.
Matthieu 18.30 Matthieu 5.23-5.26 Job 23.7 Esaïe 55.6 Luc 13.24-13.28
59 Nakuambia, Hutoki humo kamwe hata uishe kulipa senti ya mwisho.
Marc 12.42 Matthieu 18.34 Matthieu 25.46 2 Thessaloniciens 1.3 Luc 16.26

Cette Bible est dans le domaine public.