Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Luc 9.32
Bible en Swahili de l’est


Mission des douze apôtres

1 Akawaita wale Thenashara, akawapa uwezo na mamlaka juu ya pepo wote na kuponya maradhi.
Actes 4.30 Marc 6.7-6.13 Actes 3.16 Luc 10.19 Marc 3.13-3.19
2 Akawatuma wautangaze ufalme wa Mungu, na kupoza wagonjwa.
Matthieu 10.7-10.8 Luc 10.9 Luc 10.1 Luc 9.11 Matthieu 3.2
3 Akawaambia, Msichukue kitu kwa safari yenu, fimbo, wala mkoba, wala mkate, wala fedha, wala mmoja wenu asiwe na kanzu mbili.
Luc 22.35 Luc 10.4-10.12 2 Timothée 2.4 Psaumes 37.3 Matthieu 10.9-10.14
4 Na nyumba yo yote mtakayoingia kaeni humo, mpaka mtoke mjini.
Luc 10.5-10.8 Matthieu 10.11 Marc 6.10 Actes 16.15
5 Na wale wasiowakaribisha, mtokapo katika mji huo, yakung’uteni hata mavumbi ya miguuni mwenu, kuwa ushuhuda juu yao.
Actes 13.51 Actes 18.6 Néhémie 5.13 Matthieu 10.14-10.15 Luc 10.10-10.12
6 Wakaenda, wakazunguka katika vijiji, wakihubiri injili, na kupoza watu kila mahali.
Marc 6.12-6.13 Actes 5.15 Marc 16.20 Luc 9.1-9.2 Actes 4.30
7 Na Herode mfalme akasikia habari za yote yaliyotendeka, akafadhaika kwa sababu watu wengine walisema ya kwamba Yohana amefufuka katika wafu,
Marc 6.14-6.28 Matthieu 14.1-14.12 Luc 3.1 Esaïe 22.5 Job 18.11-18.12
8 na wengine ya kwamba Eliya ametokea, na wengine ya kwamba mmojawapo wa manabii wa kale amefufuka.
Luc 9.19 Jean 1.21 Matthieu 17.10 Marc 6.15 Marc 8.28
9 Lakini Herode akasema, Yohana nilimkata kichwa; basi ni nani huyu ambaye ninasikia mambo haya juu yake? Akataka kumwona.
Luc 23.8 Luc 13.31-13.32

Multiplication des pains pour cinq mille hommes

10 Basi wale mitume waliporudi walimweleza mambo yote waliyoyatenda; akawachukua, akaenda nao faraghani mpaka mji mmoja uitwao Bethsaida.
Matthieu 11.21 Luc 10.17 Jean 6.5-6.13 Jean 1.44 Zacharie 1.10
11 Na makutano walipojua walimfuata; akawakaribisha, akawa akisema nao habari za ufalme wa Mungu, akawaponya wale wenye haja ya kuponywa.
Actes 28.31 Jean 6.37 Luc 1.53 Matthieu 14.14 Luc 8.10
12 Na jua likaanza kushuka; wakamwendea wale Thenashara, wakamwambia, Uage mkutano, ili waende katika vijiji na mashamba ya kandokando wapate mahali pa kulala na vyakula, maana hapa tulipo ni nyika tupu.
Matthieu 15.23 Jean 6.1 Osée 13.5 Ezéchiel 34.25 Matthieu 14.15-14.21
13 Akawaambia, Wapeni ninyi chakula. Wakasema, Hatuna kitu zaidi ya mikate mitano na samaki wawili, tusipokwenda tukawanunulie watu hawa wote vyakula.
2 Rois 4.42-4.43 Nombres 11.21-11.23 Jean 6.5-6.9 Proverbes 11.24-11.25 Marc 6.37-6.38
14 Kwa kuwa wanaume waliokuwako walipata kama elfu tano. Akawaambia wanafunzi wake, Waketisheni watu kwa safu, kila safu watu hamsini.
1 Corinthiens 14.40 Marc 8.6 Marc 6.39-6.40
15 Wakafanya hivyo, wakawaketisha wote.
16 Akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni akavibariki, akavimega, akawapa wanafunzi wake ili wawaandikie mkutano.
Marc 7.34 Matthieu 14.19 Luc 24.30 Jean 6.11 Psaumes 121.1-121.2
17 Wakala, wakashiba wote; na katika vile vipande vilivyowabakia walikusanya vikapu kumi na viwili.
2 Rois 4.44 Proverbes 13.25 Matthieu 16.9-16.10 Marc 8.8-8.9 Jean 6.11-6.13

Pierre reconnaît Jésus comme le Messie

18 Ikawa alipokuwa akisali kwa faragha, wanafunzi wake walikuwapo pamoja naye, akawauliza, Je! Makutano hao wanasema ya kuwa mimi ni nani?
Luc 11.1 Matthieu 16.13-16.16 Luc 22.39-22.41 Matthieu 26.36 Marc 8.27-8.30
19 Wakamjibu wakisema, Yohana Mbatizaji; lakini wengine, Eliya; na wengine kwamba mmojawapo wa manabii wa kale amefufuka.
Luc 9.7-9.8 Marc 6.15 Jean 1.21 Matthieu 14.2 Jean 9.17
20 Akawaambia, Nanyi mwasema ya kwamba mimi ni nani? Petro akamjibu akasema, Ndiwe Kristo wa Mungu.
Jean 1.49 Jean 11.27 Matthieu 16.15-16.17 Jean 6.68-6.69 Matthieu 26.63
21 Akawaonya, akawakataza wasimwambie mtu neno hilo;
Matthieu 16.20 Matthieu 17.9 Marc 8.30-8.31
22 akisema, Imempasa Mwana wa Adamu kupata mateso mengi, na kukataliwa na wazee na wakuu wa makuhani na waandishi, na kuuawa na siku ya tatu kufufuka.
Luc 24.7 Luc 18.31-18.34 Marc 9.31 Matthieu 16.21-16.28 Genèse 3.15
23 Akawaambia wote, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate.
Matthieu 10.38-10.39 Marc 8.34-8.38 Luc 14.26-14.27 Tite 2.12 Colossiens 3.5
24 Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu ndiye atakayeisalimisha.
Luc 17.33 Hébreux 11.35 Apocalypse 2.10 Jean 12.25 Actes 20.23-20.24
25 Kwa kuwa yamfaa nini mtu kuupata ulimwengu wote, kama akijiangamiza, au kujipoteza mwenyewe?
Luc 12.19-12.21 Marc 8.36 Matthieu 13.50 Matthieu 16.26 Psaumes 49.6-49.8
26 Kwa sababu kila atakayenionea haya mimi na maneno yangu, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wake na wa Baba na wa malaika watakatifu.
Matthieu 10.32-10.33 2 Timothée 2.12 Matthieu 16.27 Romains 1.16 Matthieu 25.31
27 Nami nawaambia kweli, Wapo katika hawa wanaosimama hapa, ambao hawataonja mauti kabisa, hata wauone kwanza ufalme wa Mungu.
Matthieu 16.28 Hébreux 2.9 Jean 21.22-21.23 Jean 8.51-8.52 Marc 14.25

La transfiguration

28 Baada ya maneno hayo yapata siku nane, aliwatwaa Petro na Yohana na Yakobo, akapanda mlimani ili kuomba.
Psaumes 109.4 Luc 6.12 Marc 9.2-9.13 Marc 1.35 Matthieu 26.37-26.39
29 Ikawa katika kusali kwake sura ya uso wake ikageuka, mavazi yake yakawa meupe, yakimeta-meta.
Marc 9.2-9.3 Marc 16.12 2 Pierre 1.16-1.18 Exode 34.29-34.35 Matthieu 17.2
30 Na tazama, watu wawili walikuwa wakizungumza naye, nao ni Musa na Eliya;
Hébreux 3.3-3.6 Marc 9.4-9.6 Luc 24.44 Luc 1.17 Luc 24.27
31 walioonekana katika utukufu, wakanena habari za kufariki kwake atakakotimiza Yerusalemu.
2 Pierre 1.15 1 Corinthiens 1.23-1.24 Jean 1.29 Luc 9.22 1 Pierre 1.11-1.12
32 Petro na wale waliokuwa pamoja naye walikuwa wamelemewa na usingizi; lakini walipokwisha amka waliuona utukufu wake, na wale wawili waliosimama pamoja naye.
Jean 1.14 Daniel 8.18 Exode 33.18-33.23 Matthieu 26.40-26.43 Luc 22.45-22.46
33 Ikawa hao walipokuwa wakijitenga naye, Petro alimwambia Yesu, Bwana mkubwa, ni vizuri sisi kuwapo hapa; na tufanye vibanda vitatu; kimoja chako wewe, na kimoja cha Musa, na kimoja cha Eliya; hali hajui asemalo.
Marc 9.5-9.6 Psaumes 73.28 Marc 10.38 Jean 14.8 Psaumes 27.4
34 Alipokuwa akisema hayo, lilitokea wingu likawatia uvuli, wakaogopa walipoingia katika wingu hilo.
Marc 9.7-9.8 Apocalypse 1.17 Esaïe 19.1 Daniel 10.8 Juges 6.22
35 Sauti ikatoka katika wingu, ikisema, Huyu ni Mwanangu, mteule wangu, msikieni yeye.
Matthieu 3.17 Esaïe 42.1 Luc 3.22 Actes 3.22-3.23 Hébreux 12.25-12.26
36 Na sauti hiyo ilipokwisha, Yesu alionekana yu peke yake. Nao wakanyamaza, wasitangaze kwa mtu siku zile lo lote katika hayo waliyoyaona.
Matthieu 17.9 Marc 9.9-9.10 Marc 9.6 Ecclésiaste 3.7

Guérison d’un démoniaque

37 Ikawa siku ya pili yake, waliposhuka mlimani, mkutano mkubwa ulikutana naye.
Matthieu 17.14-17.20 Marc 9.14-9.29
38 Na tazama, mtu mmoja katika mkutano alipaza sauti, akisema, Mwalimu, nakuomba umwangalie mwanangu; kwa kuwa yeye ni mwanangu pekee.
Luc 7.12 Zacharie 12.10 Luc 8.41-8.42 Genèse 44.20 Jean 4.47
39 Na tazama, pepo humpagaa, naye mara hupiga kelele; tena humtia kifafa, huku anatokwa na povu, wala hamwachi ila kwa shida, akimchubua-chubua.
Luc 4.35 1 Pierre 5.8 Marc 5.4-5.5 Jean 8.44 Luc 8.29
40 Nikawasihi wanafunzi wako wamtoe, wasiweze.
Luc 9.1 Matthieu 17.20 Actes 19.13-19.16 2 Rois 4.31 Luc 10.17-10.19
41 Yesu akajibu akasema, Enyi kizazi kisicho na imani, kilichopotoka, nitakaa nanyi na kuwachukulia hata lini? Mlete mwanao hapa.
Jean 14.9 Jean 20.27 Deutéronome 32.5 Psaumes 78.8 Hébreux 3.9-3.11
42 Alipokuwa katika kumwendea, pepo akambwaga chini, akamtia kifafa. Yesu akamkemea pepo mchafu, akamponya mtoto, akamrudishia babaye.
Luc 7.15 Marc 9.20 2 Rois 4.36 Actes 9.41 1 Rois 17.23
43 Wote wakashangaa, wakiuona ukuu wa Mungu. Nao walipokuwa wakiyastaajabia mambo yote aliyoyafanya, aliwaambia wanafunzi wake,
Luc 8.25 Luc 5.26 2 Pierre 1.16 Actes 3.10-3.13 Matthieu 17.22
44 Yashikeni maneno haya masikioni mwenu, kwa kuwa Mwana wa Adamu anakwenda kutiwa katika mikono ya watu.
Luc 9.22 Actes 2.23 Matthieu 21.38-21.39 1 Thessaloniciens 3.3-3.4 Esaïe 32.9-32.10
45 Lakini hawakulifahamu neno lile, likafichwa kwao wasilitambue; wakaogopa kumwuliza maana yake neno lile.
Luc 18.34 Marc 9.32 Jean 16.17-16.18 Jean 12.16 Luc 2.50

Petits et grands dans le royaume de Dieu

46 Wakaanza kuhojiana, ni nani atakayekuwa mkubwa miongoni mwao.
Matthieu 18.1-18.5 Marc 9.33-9.37 Matthieu 20.20-20.22 Philippiens 2.3 3 Jean 1.9
47 Naye Yesu alipotambua mawazo ya mioyo yao, alitwaa mtoto mdogo akamweka karibu naye,
Psaumes 139.23 Apocalypse 2.23 1 Pierre 2.1-2.2 Jean 21.17 Jean 16.30
48 akawaambia, Ye yote atakayempokea mtoto huyu kwa jina langu anipokea mimi; na ye yote atakayenipokea mimi ampokea yeye aliyenituma. Kwa kuwa aliye mdogo miongoni mwenu nyote huyo ndiye mkubwa.
Matthieu 23.11-23.12 Jean 13.20 Luc 10.16 Luc 22.26 Luc 14.11
49 Yohana akajibu akamwambia; Bwana mkubwa, tuliona mtu anatoa pepo kwa jina lako; tukamkataza, kwa sababu hafuatani na sisi.
Marc 9.38-9.40 Nombres 11.27-11.29 3 Jean 1.9-1.10 Actes 4.18-4.19 Marc 10.13-10.14
50 Yesu akamwambia, Msimkataze, kwa kuwa yeye ambaye si kinyume chenu yu upande wenu.
Luc 11.23 Matthieu 12.30 Philippiens 1.15-1.18 Proverbes 3.5-3.6 Josué 9.14

De la Galilée à Jérusalem

Jésus en Samarie

51 Ikawa, siku za kupaa kwake zilipokuwa karibu kutimia, yeye aliukaza uso wake kwenda Yerusalemu;
Marc 16.19 Luc 13.22 Luc 18.31 Luc 17.11 Luc 19.28
52 akatuma wajumbe kutangulia mbele ya uso wake; wakaenda wakaingia katika kijiji cha Wasamaria, ili kumtengenezea mahali.
Matthieu 10.5 Luc 10.33 Luc 17.16 Luc 10.1 Luc 7.27
53 Lakini wenyeji hawakumkaribisha kwa vile alivyouelekeza uso wake kwenda Yerusalemu.
Jean 4.9 Luc 9.48 Jean 4.40-4.42
54 Wanafunzi wake Yakobo na Yohana walipoona hayo, walisema, Bwana, wataka tuagize moto ushuke kutoka mbinguni, uwaangamize; [kama Eliya naye alivyofanya]?
Jacques 1.19-1.20 Jacques 3.14-3.18 2 Rois 1.10-1.14 Actes 4.29-4.30 2 Rois 10.16
55 Akawageukia, akawakanya. [Akasema, Hamjui ni roho ya namna gani mliyo nayo.]
Jacques 3.10 1 Pierre 3.9 Matthieu 26.33 Job 26.4 Job 35.2-35.4
56 Kwa maana Mwana wa Adamu hakuja kuziangamiza roho za watu, bali kuziokoa. Wakaondoka wakaenda mpaka kijiji kingine.
Matthieu 20.28 Romains 12.21 Jean 3.17 1 Timothée 1.15 Jean 10.10
57 Nao walipokuwa wakienda njiani, mtu mmoja alimwambia, Nitakufuata ko kote utakakokwenda.
Matthieu 8.19-8.22 Exode 19.8 Luc 9.51 Luc 9.57-9.60 Jean 13.37
58 Yesu akamwambia, Mbweha wana pango, na ndege wa angani wana viota, lakini Mwana wa Adamu hana pa kujilaza kichwa chake.
Jacques 2.5 Luc 14.26-14.33 Matthieu 8.20 2 Corinthiens 8.9 Luc 18.22-18.23
59 Akamwambia mwingine, Nifuate. Akasema, Bwana, nipe ruhusa kwanza niende nikamzike baba yangu.
Matthieu 6.33 Aggée 1.2 Matthieu 8.21-8.22 1 Rois 19.20 Matthieu 4.19-4.22
60 Akamwambia Waache wafu wawazike wafu wao; bali wewe enenda ukautangaze ufalme wa Mungu.
2 Timothée 2.3-2.4 Jean 21.15-21.17 1 Timothée 5.6 Ephésiens 2.1 Ephésiens 2.5
61 Mtu mwingine pia akamwambia, Bwana, nitakufuata; lakini, nipe ruhusa kwanza nikawaage watu wa nyumbani mwangu.
1 Rois 19.20 Luc 14.18-14.20 Luc 14.26 Deutéronome 33.9 Ecclésiaste 9.10
62 Yesu akamwambia, Mtu aliyetia mkono wake kulima, kisha akaangalia nyuma, hafai kwa ufalme wa Mungu.
Hébreux 10.38 Philippiens 3.13 2 Pierre 2.20-2.22 Luc 17.31-17.32 Psaumes 78.8-78.9

Cette Bible est dans le domaine public.