Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Luc 4.43
Bible en Swahili de l’est


Tentation de Jésus

1 Na Yesu, hali amejaa Roho Mtakatifu, alirudi kutoka Yordani, akaongozwa na Roho muda wa siku arobaini nyikani,
Marc 1.12-1.13 Matthieu 4.1-4.11 Luc 3.3 Luc 4.18 Actes 10.38
2 akijaribiwa na Ibilisi. Na siku hizo alikuwa hali kitu; hata zilipotimia, aliona njaa.
1 Rois 19.8 Exode 34.28 Hébreux 2.18 Hébreux 4.15 Deutéronome 9.9
3 Ibilisi akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, liambie jiwe hili liwe mkate.
Matthieu 4.3 Luc 3.22
4 Yesu akamjibu, Imeandikwa ya kwamba mtu hataishi kwa mkate tu.
Deutéronome 8.3 Ephésiens 6.17 Luc 4.10 Luc 4.8 Jérémie 49.11
5 Akampandisha juu, akamwonyesha milki zote za ulimwengu kwa dakika moja.
Marc 4.8-4.9 Psaumes 73.19 Ephésiens 2.2 1 Jean 2.15-2.16 1 Corinthiens 7.31
6 Ibilisi akamwambia, Nitakupa wewe enzi hii yote, na fahari yake, kwa kuwa imo mikononi mwangu, nami humpa ye yote kama nipendavyo.
Jean 12.31 Jean 14.30 Ephésiens 2.2 1 Jean 5.19 Apocalypse 13.2
7 Basi, wewe ukisujudu mbele yangu yote yatakuwa yako.
Esaïe 46.6 Esaïe 45.14 Apocalypse 5.8 Apocalypse 4.10 Luc 8.28
8 Yesu akajibu akamwambia, Imeandikwa, Msujudie Bwana Mungu wako, umwabudu yeye peke yake.
Deutéronome 6.13 Matthieu 4.10 Deutéronome 10.20 Luc 4.4 1 Samuel 7.3
9 Akamwongoza mpaka Yerusalemu, akamweka juu ya kinara cha hekalu, akamwambia, Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini;
Matthieu 4.5-4.6 Luc 4.3 Romains 1.4 2 Chroniques 3.4 Matthieu 8.29
10 kwa maana imeandikwa, Atakuagizia malaika zake wakulinde;
Psaumes 91.11-91.12 Hébreux 1.14 2 Corinthiens 11.14 Luc 4.3 Luc 4.8
11 na ya kwamba,mikononi mwao watakuchukua, Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.
Psaumes 91.12
12 Yesu akajibu akamwambia, Imenenwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.
Deutéronome 6.16 1 Corinthiens 10.9 Hébreux 3.8-3.9 Malachie 3.15 Psaumes 95.9
13 Basi alipomaliza kila jaribu, Ibilisi akamwacha akaenda zake kwa muda.
Jean 14.30 Hébreux 4.15 Matthieu 4.11 Jacques 4.7

Ministère de Jésus en Galilée

Jésus à Nazareth

14 Yesu akarudi kwa nguvu za Roho, akenda Galilaya; habari zake zikaenea katika nchi zote za kandokando.
Matthieu 4.12 Matthieu 4.23-4.25 Actes 10.37 Luc 4.37 Marc 1.14
15 Naye alikuwa akifundisha katika masinagogi yao, akitukuzwa na watu wote.
Matthieu 4.23 Matthieu 9.8 Marc 1.27 Esaïe 55.5 Luc 13.10
16 Akaenda Nazareti, hapo alipolelewa; na siku ya sabato akaingia katika sinagogi kama ilivyokuwa desturi yake, akasimama ili asome.
Matthieu 2.23 Actes 13.14-13.16 Actes 17.2 Luc 2.39 Luc 2.51
17 Akapewa chuo cha nabii Isaya, akakifungua chuo, akatafuta mahali palipoandikwa,
Esaïe 61.1-61.3 Actes 13.15 Luc 20.42 Actes 7.42
18 Roho wa Bwana yu juu yangu, Kwa maana amenitia mafuta kuwahubiri maskini habari njema. Amenituma kuwatangazia wafungwa kufunguliwa kwao, Na vipofu kupata kuona tena, Kuwaacha huru waliosetwa,
Esaïe 61.1 Matthieu 11.5 Psaumes 146.7-146.8 Actes 10.38 Luc 7.22
19 Na kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa.
Esaïe 61.2 Esaïe 63.4 Lévitique 25.50-25.54 Lévitique 25.8-25.13 2 Corinthiens 6.1
20 Akakifunga chuo, akamrudishia mtumishi, akaketi; na watu wote waliokuwamo katika sinagogi wakamkazia macho.
Luc 4.17 Luc 19.48 Jean 8.2 Matthieu 26.55 Luc 5.3
21 Akaanza kuwaambia, Leo maandiko haya yametimia masikioni mwenu.
Jean 5.39 Matthieu 13.14 Actes 2.29-2.33 Jean 4.25-4.26 Actes 2.16-2.18
22 Wakamshuhudia wote, wakiyastaajabia maneno ya neema yaliyotoka kinywani mwake, wakasema, Huyu siye mwana wa Yusufu?
Jean 6.42 Psaumes 45.2 Jean 7.46 Ecclésiaste 12.10-12.11 Tite 2.8
23 Akawaambia, Hapana shaka mtaniambia mithali hii, Tabibu, jiponye nafsi yako; mambo yote tuliyosikia kwamba yametendeka Kapernaumu, yatende na hapa pia katika nchi yako mwenyewe.
Marc 6.1 Matthieu 4.13 Luc 4.16 Jean 4.46-4.53 Marc 2.1-2.12
24 Akasema, Amin, nawaambia ya kwamba, Hakuna nabii mwenye kukubaliwa katika nchi yake mwenyewe.
Matthieu 13.57 Jean 4.44 Marc 6.4-6.5 Actes 22.3
25 Lakini, kwa hakika nawaambia, Palikuwa na wajane wengi katika nchi ya Israeli zamani za Eliya, wakati mbingu zilipofungwa miaka mitatu na miezi sita, njaa kuu ikaingia nchi nzima;
Jacques 5.17 1 Rois 17.1 Romains 9.15 Esaïe 55.8 1 Rois 18.1-18.2
26 wala Eliya hakutumwa kwa mmojawapo, ila kwa mjane mmoja wa Sarepta katika nchi ya Sidoni.
1 Rois 17.9-17.24 Matthieu 11.21
27 Tena, palikuwa na wenye ukoma wengi katika Israeli zamani za nabii Elisha, wala hapana aliyetakaswa ila Naamani, mtu wa Shamu.
2 Rois 5.1-5.27 Jean 17.12 1 Rois 19.19-19.21 Job 36.23 Matthieu 12.4
28 Wakajaa ghadhabu wote waliokuwa katika sinagogi walipoyasikia hayo.
Actes 22.21-22.23 1 Thessaloniciens 2.15-2.16 Actes 5.33 2 Chroniques 24.20-24.21 Jérémie 38.6
29 Wakaondoka wakamtoa nje ya mji, wakampeleka mpaka ukingo wa kilima ambacho mji wao umejengwa juu yake, wapate kumtupa chini;
Nombres 15.35 Jean 8.37 Jean 8.40 Psaumes 37.14 Jean 15.24-15.25
30 lakini yeye alipita katikati yao, akaenda zake.
Jean 10.39 Jean 8.59 Jean 18.6-18.7 Actes 12.18

Miracles à Capernaüm

31 Akashuka mpaka Kapernaumu, mji wa Galilaya, akawa akiwafundisha siku ya sabato;
Matthieu 4.13 Actes 17.16-17.17 Actes 17.10-17.11 Marc 1.21-1.28 Actes 20.1-20.2
32 wakashangaa mno kwa mafundisho yake, kwa kuwa neno lake lilikuwa na uwezo.
Luc 4.36 Matthieu 7.28-7.29 Jean 6.63 1 Thessaloniciens 1.5 2 Corinthiens 4.2
33 Na ndani ya sinagogi mlikuwa na mtu mwenye roho ya pepo mchafu, akalia kwa sauti kuu,
Marc 1.23
34 akisema, Acha! Tuna nini nawe, Yesu wa Nazareti? Umekuja kutuangamiza? Nakujua u nani, Mtakatifu wa Mungu.
Marc 1.24 Matthieu 8.29 Jacques 2.19 Apocalypse 3.7 Actes 3.14
35 Yesu akamkemea, akisema, Fumba kinywa, mtoke. Ndipo yule pepo akamwangusha katikati, akamtoka asimdhuru neno.
Luc 4.41 Luc 4.39 Matthieu 8.26 Apocalypse 12.12 Matthieu 17.18
36 Mshangao ukawashika wote, wakasemezana wakisema, Ni neno gani hili, maana awaamuru pepo wachafu kwa uwezo na nguvu, nao hutoka.
Luc 4.32 Actes 19.12-19.16 Marc 16.17-16.20 Marc 7.37 Marc 1.27
37 Habari zake zikaenea kila mahali katika nchi ile.
Luc 4.14 Matthieu 9.26 Esaïe 52.13 Marc 6.14 Matthieu 4.23-4.25
38 Akatoka katika sinagogi, akaingia katika nyumba ya Simoni. Naye mkwewe Simoni, mamaye mkewe, alikuwa ameshikwa na homa kali, wakamwomba kwa ajili yake.
Marc 1.29-1.31 Matthieu 8.14-8.15 1 Corinthiens 9.5 Jean 11.3 Jean 11.22
39 Akasimama karibu naye, akaikemea ile homa, ikamwacha; mara hiyo akaondoka, akawatumikia.
Luc 4.35 Luc 8.24 Psaumes 116.12 Luc 8.2-8.3 Luc 4.41
40 Na jua lilipokuwa likichwa, wote waliokuwa na wagonjwa wenye maradhi mbali mbali waliwaleta kwake, akaweka mikono yake juu ya kila mmoja akawaponya.
Marc 5.23 Matthieu 8.16-8.17 Marc 1.32-1.34 Luc 7.21-7.23 Actes 5.15
41 Pepo nao waliwatoka watu wengi, wakipiga kelele na kusema, Wewe u Mwana wa Mungu. Akawakemea, asiwaache kunena, kwa sababu walimjua kuwa ndiye Kristo.
Marc 1.34 Actes 16.17-16.18 Matthieu 4.3 Marc 3.11 Matthieu 26.63
42 Hata kulipokucha alitoka akaenda mahali pasipokuwa na watu; makutano wakawa wakimtafuta-tafuta, wakafika kwake, wakataka kumzuia asiondoke kwao.
Jean 4.34 Jean 4.40 Marc 1.45 Marc 1.35-1.38 Luc 24.29
43 Akawaambia, Imenipasa kuihubiri habari njema ya ufalme wa Mungu katika miji mingine pia; maana kwa sababu hiyo nalitumwa.
Marc 1.38-1.39 Esaïe 48.16 Esaïe 42.1-42.4 Actes 10.38 Esaïe 61.1-61.3
44 Basi, alikuwa akihubiri katika masinagogi ya Galilaya.
Matthieu 4.23 Marc 1.39 Luc 4.15

Cette Bible est dans le domaine public.