Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 119.40
Bible en Swahili de l’est


La Parole de Dieu

1 Heri walio kamili njia zao, Waendao katika sheria ya Bwana.
Psaumes 128.1 Ezéchiel 11.20 Luc 1.6 Tite 2.11-2.12 Jacques 1.25
2 Heri wazitiio shuhuda zake, Wamtafutao kwa moyo wote.
Jean 14.23 Ezéchiel 36.27 Psaumes 119.10 Psaumes 119.22 Deutéronome 4.29
3 Naam, hawakutenda ubatili, Wamekwenda katika njia zake.
1 Jean 3.9 1 Jean 5.18
4 Wewe umetuamuru mausia yako, Ili sisi tuyatii sana.
1 Jean 5.3 Deutéronome 12.32 Deutéronome 4.1 Philippiens 4.8-4.9 Deutéronome 4.9
5 Ningependa njia zangu ziwe thabiti, Nizitii amri zako.
Psaumes 51.10 2 Thessaloniciens 3.5 Psaumes 119.36 Jérémie 31.33 Psaumes 119.173
6 Ndipo mimi sitaaibika, Nikiyaangalia maagizo yako yote.
Psaumes 119.80 1 Jean 2.28 Job 22.26 Jean 15.14 1 Jean 3.20-3.21
7 Nitakushukuru kwa unyofu wa moyo, Nikiisha kujifunza hukumu za haki yako
Psaumes 9.1 Psaumes 86.12-86.13 Psaumes 119.12 Psaumes 119.33-119.34 1 Chroniques 29.13-29.17
8 Nitazitii amri zako, Usiniache kabisa
Psaumes 119.176 Psaumes 71.9 Psaumes 119.115-119.117 Psaumes 119.16 Psaumes 51.11
9 Jinsi gani kijana aisafishe njia yake? Kwa kutii, akilifuata neno lako.
Jacques 1.21-1.25 2 Timothée 2.22 Psaumes 25.7 Josué 1.7 Tite 2.4-2.6
10 Kwa moyo wangu wote nimekutafuta, Usiniache nipotee mbali na maagizo yako.
2 Chroniques 15.15 Psaumes 119.118 1 Samuel 7.3 Colossiens 3.22 Esaïe 35.8
11 Moyoni mwangu nimeliweka neno lako, Nisije nikakutenda dhambi.
Psaumes 37.31 Psaumes 40.8 Jérémie 15.16 Psaumes 119.97 Colossiens 3.16
12 Ee Bwana, umehimidiwa, Unifundishe amri zako.
Psaumes 119.108 Psaumes 119.64 Psaumes 119.124 Psaumes 119.66 Psaumes 119.33
13 Kwa midomo yangu nimezisimulia Hukumu zote za kinywa chako.
Psaumes 40.9-40.10 Psaumes 71.15-71.18 Psaumes 34.11 Matthieu 10.27 Psaumes 37.30
14 Nimeifurahia njia ya shuhuda zako Kana kwamba ni mali mengi.
Jérémie 15.16 Psaumes 119.111 Psaumes 119.162 Psaumes 112.1 Psaumes 119.47
15 Nitayatafakari mausia yako, Nami nitaziangalia njia zako.
Psaumes 1.2 Psaumes 119.78 Psaumes 119.23 Psaumes 119.48 Psaumes 119.97
16 Nitajifurahisha sana kwa amri zako, Sitalisahau neno lako.
Psaumes 119.77 Psaumes 119.24 Hébreux 10.16-10.17 Psaumes 119.92-119.93 Psaumes 119.35
17 Umtendee mtumishi wako ukarimu, Nipate kuishi, nami nitalitii neno lako.
Psaumes 13.6 Psaumes 116.7 Ephésiens 2.10 Philippiens 4.19 1 Jean 5.3-5.4
18 Unifumbue macho yangu niyatazame Maajabu yatokayo katika sheria yako.
Ephésiens 1.17-1.18 Esaïe 29.18 Actes 26.18 Esaïe 32.3 Hébreux 8.5
19 Mimi ni mgeni katika nchi, Usinifiche maagizo yako.
1 Chroniques 29.15 Genèse 47.9 Esaïe 63.17 Psaumes 39.12 2 Corinthiens 5.6
20 Roho yangu imepondeka kwa kutamani Hukumu zako kila wakati.
Psaumes 63.1 Psaumes 84.2 Psaumes 119.40 Psaumes 119.131 Psaumes 42.1-42.2
21 Umewakemea wenye kiburi, Wamelaaniwa waendao mbali na maagizo yako.
Psaumes 119.10 Psaumes 119.118 Esaïe 10.12 Jérémie 44.16 Psaumes 138.6
22 Uniondolee laumu na dharau, Kwa maana nimezishika shuhuda zako.
Psaumes 39.8 Psaumes 119.39 1 Pierre 2.20 Job 19.2-19.3 Psaumes 42.10
23 Wakuu nao waliketi wakaninena, Lakini mtumishi wako atazitafakari amri zako.
1 Samuel 20.31 Psaumes 2.1-2.2 1 Samuel 22.7-22.13 Luc 22.66 Luc 23.1-23.2
24 Shuhuda zako nazo ndizo furaha yangu, Na washauri wangu.
Psaumes 119.16 Job 27.10 Colossiens 3.16 Psaumes 119.104-119.105 Psaumes 119.77
25 Nafsi yangu imeambatana na mavumbi, Unihuishe sawasawa na neno lako.
Psaumes 143.11 Psaumes 119.40 Psaumes 44.25 Psaumes 119.159 Psaumes 119.93
26 Nalizisimulia njia zangu ukanijibu, Unifundishe amri zako.
Psaumes 86.11 Psaumes 25.4 Psaumes 27.11 Proverbes 28.13 Psaumes 143.8-143.10
27 Unifahamishe njia ya mausia yako, Nami nitayatafakari maajabu yako.
Psaumes 105.2 Actes 2.11 Exode 13.14-13.15 Psaumes 71.17 Apocalypse 15.3
28 Nafsi yangu imeyeyuka kwa uzito, Unitie nguvu sawasawa na neno lako.
Psaumes 107.26 Psaumes 22.14 Philippiens 4.13 Esaïe 40.31 Josué 2.24
29 Uniondolee njia ya uongo, Unineemeshe kwa sheria yako.
Psaumes 119.104 1 Jean 1.8 Jérémie 16.19 1 Jean 2.4 Jérémie 31.33-31.34
30 Nimeichagua njia ya uaminifu, Na kuziweka hukumu zako mbele yangu.
Jean 3.19-3.21 Jean 8.45 Proverbes 1.29 Psaumes 119.24 2 Jean 1.4
31 Nimeambatana na shuhuda zako, Ee Bwana, usiniaibishe.
Esaïe 45.17 Deutéronome 4.4 Psaumes 25.20 Jérémie 17.18 Psaumes 119.6
32 Nitakwenda mbio katika njia ya maagizo yako, Utakaponikunjua moyo wangu.
1 Rois 4.29 2 Corinthiens 3.17 Jean 8.32 1 Corinthiens 9.24-9.26 Esaïe 60.5
33 Ee Bwana, unifundishe njia ya amri zako, Nami nitaishika hata mwisho.
Psaumes 119.12 Philippiens 1.6 1 Jean 2.27 Psaumes 119.8 Matthieu 24.13
34 Unifahamishe nami nitaishika sheria yako, Naam, nitaitii kwa moyo wangu wote.
Matthieu 7.24 Psaumes 119.69 Psaumes 119.73 Proverbes 2.5-2.6 Jacques 1.5
35 Uniendeshe katika mapito ya maagizo yako, Kwa maana nimependezwa nayo.
Psaumes 23.3 Esaïe 48.17 1 Jean 5.3 Hébreux 13.21 Proverbes 4.11
36 Unielekeze moyo wangu na shuhuda zako, Wala usiielekee tamaa.
Marc 7.21-7.22 Hébreux 13.5 Luc 12.15 1 Rois 8.58 Ezéchiel 33.31
37 Unigeuze macho yangu nisitazame visivyofaa, Unihuishe katika njia yako.
Esaïe 33.15 Nombres 15.39 Psaumes 119.25 Proverbes 4.25 Matthieu 5.28
38 Umthibitishie mtumishi wako ahadi yako, Inayohusu kicho chako.
Jérémie 32.39-32.41 Psaumes 147.11 2 Samuel 7.25-7.29 Psaumes 145.19 2 Corinthiens 1.20
39 Uniondolee laumu niiogopayo, Maana hukumu zako ni njema.
1 Timothée 3.7 Psaumes 119.22 Tite 2.8 Psaumes 19.9 Deutéronome 4.8
40 Tazama, nimeyatamani mausia yako, Unihuishe kwa haki yako.
Psaumes 119.20 Jean 10.10 Philippiens 3.13-3.14 Marc 9.24 Romains 7.24
41 Ee Bwana, fadhili zako zinifikie na mimi, Naam, wokovu wako sawasawa na ahadi yako.
Psaumes 119.76-119.77 Psaumes 119.58 Psaumes 106.4-106.5 Psaumes 119.132 Psaumes 69.16
42 Nami nitamjibu neno anilaumuye, Kwa maana nalitumainia neno lako.
Actes 27.25 2 Samuel 7.12-7.16 Psaumes 42.10 Psaumes 119.74 Matthieu 27.63
43 Usiliondoe neno la kweli kinywani mwangu kamwe, Maana nimezingojea hukumu zako.
Psaumes 119.175 Psaumes 51.14-51.15 Psaumes 43.1 Esaïe 59.21 Psaumes 7.6-7.9
44 Nami nitaitii sheria yako daima, Naam, milele na milele.
Apocalypse 7.15 Psaumes 119.33-119.34 Apocalypse 22.11
45 Nami nitakwenda panapo nafasi, Kwa kuwa nimejifunza mausia yako.
Psaumes 119.94 Proverbes 4.12 2 Pierre 2.19 Jean 5.39 Jean 8.30-8.36
46 Nitazinena shuhuda zako mbele ya wafalme, Wala sitaona aibu.
Actes 26.1-26.2 Romains 1.16 Daniel 4.25-4.27 Philippiens 1.20 Matthieu 10.18-10.19
47 Nami nitajifurahisha sana kwa maagizo yako, Ambayo nimeyapenda.
Psaumes 119.48 Psaumes 119.127 Psaumes 119.97 Psaumes 119.16 Psaumes 119.140
48 Na mikono yangu nitayainulia maagizo yako niliyoyapenda, Nami nitazitafakari amri zako.
Psaumes 119.15 Jean 15.14 Matthieu 7.21 Michée 5.9 Psaumes 1.2
49 Likumbuke neno ulilomwambia mtumishi wako, Kwa sababu umenitumainisha.
Psaumes 71.14 2 Samuel 7.25 Psaumes 119.81 Psaumes 106.45 Psaumes 119.74
50 Hii ndiyo faraja yangu katika taabu yangu, Ya kwamba ahadi yako imenihuisha.
Romains 15.4 Psaumes 28.7 Psaumes 42.8 Psaumes 42.11 Psaumes 94.19
51 Wenye kiburi wamenidharau mno, Sikujiepusha na sheria zako.
Job 23.11 Psaumes 44.18 Jérémie 20.7 Psaumes 119.157 Psaumes 119.21
52 Nimezikumbuka hukumu zako za kale, Ee Bwana, nikajifariji.
Nombres 16.3-16.35 2 Pierre 2.4-2.9 Psaumes 77.11-77.12 Exode 14.29-14.30 Deutéronome 1.35-1.36
53 Ghadhabu imenishika kwa sababu ya wasio haki, Waiachao sheria yako.
Esdras 9.3 Psaumes 119.158 Jérémie 13.17 Daniel 4.19 Luc 19.41-19.42
54 Amri zako zimekuwa nyimbo zangu, Katika nyumba ya ugeni wangu.
Genèse 47.9 Psaumes 10.1 Psaumes 89.1 Hébreux 11.13-11.16
55 Wakati wa usiku nimelikumbuka jina lako, Ee Bwana, nikaitii sheria yako.
Psaumes 42.8 Psaumes 63.6 Actes 16.25 Esaïe 26.9 Psaumes 139.18
56 Hayo ndiyo niliyokuwa nayo, Kwa sababu nimeyashika mausia yako.
Psaumes 18.18-18.22 Psaumes 119.165 1 Jean 3.19-3.24
57 Bwana ndiye aliye fungu langu, Nimesema kwamba nitayatii maneno yake.
Psaumes 16.5 Lamentations 3.24 Psaumes 119.115 Psaumes 119.106 Josué 24.15
58 Nimekuomba radhi kwa moyo wangu wote, Unifadhili sawasawa na ahadi yako.
Psaumes 119.41 Psaumes 119.10 Psaumes 119.170 Psaumes 4.6 Psaumes 51.1-51.3
59 Nalizitafakari njia zangu, Na miguu yangu nalizielekezea shuhuda zako.
Luc 15.17-15.20 Lamentations 3.40 Ezéchiel 33.14-33.16 2 Corinthiens 13.5 Ezéchiel 18.30
60 Nalifanya haraka wala sikukawia, Kuyatii maagizo yako.
Galates 1.16 Ezéchiel 10.6-10.8 Ecclésiaste 9.10 Proverbes 27.1 Psaumes 95.7-95.8
61 Kamba za wasio haki zimenifunga, Sikuisahau sheria yako.
Psaumes 119.176 1 Samuel 24.9-24.11 Psaumes 3.1 Psaumes 119.95 1 Samuel 26.9-26.11
62 Katikati ya usiku nitaamka nikushukuru, Kwa sababu ya hukumu zako za haki.
Actes 16.25 Psaumes 119.137 Marc 1.35 Deutéronome 4.8 Psaumes 119.7
63 Mimi ni mwenzao watu wote wakuchao, Na wale wayatiio mausia yako.
Psaumes 101.6 Proverbes 13.20 Psaumes 119.115 2 Corinthiens 6.14-6.17 Psaumes 119.79
64 Bwana, dunia imejaa fadhili zako, Unifundishe amri zako.
Psaumes 33.5 Psaumes 119.12 Psaumes 27.11 Psaumes 145.9 Psaumes 104.13
65 Umemtendea mema mtumishi wako, Ee Bwana, sawasawa na neno lako.
1 Chroniques 29.14 Psaumes 116.7 Psaumes 30.11 Psaumes 119.17 Psaumes 13.6
66 Unifundishe akili na maarifa, Maana nimeyaamini maagizo yako.
Philippiens 1.9 Jacques 3.13-3.18 Proverbes 2.1-2.9 1 Rois 3.9 Proverbes 8.20
67 Kabla sijateswa mimi nalipotea, Lakini sasa nimelitii neno lako.
Jérémie 31.18-31.19 Psaumes 119.71 Psaumes 119.75 Osée 5.15-6.1 2 Chroniques 33.9-33.13
68 Wewe U mwema na mtenda mema, Unifundishe amri zako.
Psaumes 106.1 Psaumes 119.12 Matthieu 19.17 Psaumes 107.1 Psaumes 86.5
69 Wenye kiburi wamenizulia uongo, Kwa moyo wangu wote nitayashika mausia yako.
Job 13.4 Actes 24.5 Psaumes 109.2-109.3 Psaumes 35.11 Jérémie 43.2-43.3
70 Mioyo yao imenenepa kama shahamu, Mimi nimeifurahia sheria yako.
Actes 28.27 Psaumes 17.10 Esaïe 6.10 Psaumes 119.16 Psaumes 119.35
71 Ilikuwa vema kwangu kuwa naliteswa, Nipate kujifunza amri zako.
Psaumes 119.67 Psaumes 94.12-94.13 1 Corinthiens 11.32 Hébreux 12.10-12.11 Esaïe 27.9
72 Sheria ya kinywa chako ni njema kwangu, Kuliko maelfu ya dhahabu na fedha.
Psaumes 19.10 Proverbes 8.10-8.11 Psaumes 119.162 Psaumes 119.127 Proverbes 8.19
73 Mikono yako ilinifanya ikanitengeneza, Unifahamishe nikajifunze maagizo yako.
Psaumes 139.14-139.16 Psaumes 138.8 Psaumes 111.10 Psaumes 119.144 Psaumes 119.169
74 Wakuchao na wanione na kufurahi, Kwa sababu nimelingojea neno lako.
Psaumes 66.16 Psaumes 119.42 Genèse 32.11-32.12 Psaumes 34.2-34.6 Psaumes 119.147
75 Najua ya kuwa hukumu zako ni za haki, Ee Bwana, na kwa uaminifu umenitesa.
Apocalypse 3.19 Hébreux 12.10-12.11 Deutéronome 32.4 Romains 3.4-3.5 Genèse 18.25
76 Nakuomba, fadhili zako ziwe faraja kwangu, Sawasawa na ahadi yako kwa mtumishi wako.
2 Corinthiens 1.3-1.5 Psaumes 106.4-106.5 Psaumes 86.5
77 Rehema zako zinijie nipate kuishi, Maana sheria yako ni furaha yangu.
Psaumes 119.41 Psaumes 1.2 Psaumes 119.47 Daniel 9.18 Lamentations 3.22-3.23
78 Wenye kiburi waaibike, maana wamenidhulumu kwa uongo, Mimi nitayatafakari mausia yako.
1 Samuel 24.17 Psaumes 119.51 Jérémie 50.32 Psaumes 109.3 Psaumes 25.3
79 Wakuchao na wanirudie, Nao watazijua shuhuda zako.
Psaumes 119.63 Psaumes 119.74 Psaumes 7.7 Psaumes 142.7
80 Moyo wangu na uwe mkamilifu katika amri zako, Nisije mimi nikaaibika.
Deutéronome 26.16 2 Corinthiens 1.12 1 Jean 2.28 Psaumes 25.2-25.3 2 Chroniques 25.2
81 Nafsi yangu imefifia kwa kuutamani wokovu wako, Nimelingojea neno lako.
Psaumes 84.2 Cantique 5.8 Apocalypse 3.15-3.16 Psaumes 119.20 Psaumes 119.114
82 Macho yangu yamefifia kwa kuitazamia ahadi yako, Nisemapo, Lini utakaponifariji?
Psaumes 69.3 Psaumes 119.123 Esaïe 38.11 Psaumes 86.17 Proverbes 13.12
83 Maana nimekuwa kama kiriba katika moshi, Sikuzisahau amri zako.
Job 30.30 Psaumes 119.61 Psaumes 102.3-102.4 Psaumes 22.15 Psaumes 119.16
84 Siku za mtumishi wako ni ngapi, Lini utakapowahukumu wale wanaonifuatia?
Job 7.6-7.8 Psaumes 39.4-39.5 Psaumes 89.47-89.48 Psaumes 90.12 Psaumes 7.6
85 Wenye kiburi wamenichimbia mashimo, Ambao hawaifuati sheria yako.
Psaumes 35.7 Psaumes 7.15 Jérémie 18.20 Psaumes 119.78 Jérémie 18.22
86 Maagizo yako yote ni amini, Wananifuatia bure, unisaidie.
Psaumes 119.78 Psaumes 35.19 Psaumes 109.26 Psaumes 119.138 Romains 7.12
87 Walikuwa karibu na kunikomesha katika nchi, Lakini sikuyaacha mausia yako.
1 Samuel 23.26-23.27 Psaumes 119.61 1 Samuel 24.6-24.7 Psaumes 119.51 Matthieu 10.28
88 Unihuishe kwa fadhili zako, Nami nitazishika shuhuda za kinywa chako.
Psaumes 119.159 Psaumes 119.40 Psaumes 119.2 Psaumes 119.146 Psaumes 119.25
89 Ee Bwana, neno lako lasimama Imara mbinguni hata milele.
1 Pierre 1.25 Psaumes 89.2 Matthieu 24.34-24.35 Matthieu 5.18 Psaumes 119.160
90 Uaminifu wako upo kizazi baada ya kizazi, Umeiweka nchi, nayo inakaa.
Psaumes 89.1-89.2 Psaumes 148.6 Ecclésiaste 1.4 Psaumes 36.5 Deutéronome 7.9
91 Kwa hukumu zako vimesimama imara hata leo, Maana vitu vyote ni watumishi wako.
Jérémie 33.25 Esaïe 48.13 Genèse 8.22 Matthieu 8.9 Deutéronome 4.19
92 Kama sheria yako isingalikuwa furaha yangu, Hapo ningalipotea katika taabu zangu.
Psaumes 119.143 Psaumes 119.24 Psaumes 119.77 Psaumes 94.18-94.19 Psaumes 27.13
93 Hata milele sitayasahau maagizo yako, Maana kwa hayo umenihuisha.
Psaumes 119.16 Jean 6.63 1 Pierre 1.23 Psaumes 119.50
94 Mimi ni wako, uniokoe, Kwa maana nimejifunza mausia yako.
Psaumes 86.2 Psaumes 119.27 Sophonie 3.17 Psaumes 119.40 Josué 10.4-10.6
95 Wasio haki wameniotea ili kunipoteza, Nitazitafakari shuhuda zako.
Actes 23.21 Actes 12.11 Psaumes 119.129 Psaumes 119.24 Matthieu 26.3-26.5
96 Nimeona ukamilifu wote kuwa na mwisho, Bali agizo lako ni pana mno.
Hébreux 4.12-4.13 Ecclésiaste 1.2-1.3 Romains 7.7-7.12 1 Samuel 9.2 Matthieu 5.18
97 Sheria yako naipenda mno ajabu, Ndiyo kutafakari kwangu mchana kutwa.
Psaumes 1.2 Psaumes 119.48 Psaumes 119.127 Proverbes 2.10 Psaumes 119.113
98 Maagizo yako hunitia hekima kuliko adui zangu, Kwa maana ninayo sikuzote.
Deutéronome 4.6 Deutéronome 4.8 Psaumes 119.30 Jacques 1.25 1 Samuel 18.30
99 Ninazo akili kuliko wakufunzi wangu wote, Maana shuhuda zako ndizo nizifikirizo.
Deutéronome 4.6-4.8 Matthieu 15.6-15.9 Jérémie 2.8 2 Timothée 3.15-3.17 Jérémie 8.8-8.9
100 Ninao ufahamu kuliko wazee, Kwa kuwa nimeyashika mausia yako.
Job 12.12 Psaumes 111.10 Matthieu 7.24 1 Rois 12.6-12.15 Job 32.7-32.10
101 Nimeiepusha miguu yangu na kila njia mbaya, Ili nilitii neno lako.
Proverbes 1.15 1 Pierre 3.10-3.11 Jérémie 2.36 Tite 2.11-2.12 1 Pierre 2.1-2.2
102 Sikujiepusha na hukumu zako, Maana Wewe mwenyewe umenifundisha.
Psaumes 18.21 Jérémie 32.40 1 Thessaloniciens 2.13 1 Jean 2.27 Proverbes 5.7
103 Mausia yako ni matamu sana kwangu, Kupita asali kinywani mwangu.
Proverbes 8.11 Psaumes 19.10 Proverbes 24.13-24.14 Psaumes 63.5 Cantique 5.1
104 Kwa mausia yako najipatia ufahamu, Ndiyo maana naichukia kila njia ya uongo.
Psaumes 119.128 Matthieu 7.13 Psaumes 119.29-119.30 Proverbes 14.12 Proverbes 8.13
105 Neno lako ni taa ya miguu yangu, Na mwanga wa njia yangu.
Proverbes 6.23 Psaumes 43.3 2 Pierre 1.19 Psaumes 18.28 Psaumes 19.8
106 Nimeapa nami nitaifikiliza, Kuzishika hukumu za haki yako.
Néhémie 10.29 2 Corinthiens 8.5 Ecclésiaste 5.4-5.5 Psaumes 56.12 Psaumes 66.13-66.14
107 Nimeteswa mno; Ee Bwana, unihuishe sawasawa na neno lako.
Psaumes 119.25 Psaumes 143.11 Psaumes 6.1 Psaumes 34.19 Psaumes 119.88
108 Ee Bwana, uziridhie sadaka za kinywa changu, Na kunifundisha hukumu zako.
Osée 14.2 Hébreux 13.15 Psaumes 119.12 Psaumes 119.169 Nombres 29.39
109 Nafsi yangu imo mkononi mwangu daima, Lakini sheria yako sikuisahau.
Job 13.14 Juges 12.3 Romains 8.36 1 Samuel 19.5 2 Corinthiens 11.23
110 Watendao uovu wamenitegea mtego, Lakini sikuikosa njia ya mausia yako.
Psaumes 141.9 Psaumes 140.5 Psaumes 119.85 Psaumes 10.8-10.18 Proverbes 1.11-1.12
111 Shuhuda zako nimezifanya urithi wa milele, Maana ndizo changamko la moyo wangu.
Deutéronome 33.4 Psaumes 16.5 Psaumes 119.74 Psaumes 19.8 Psaumes 119.92
112 Nimeuelekeza moyo wangu nizitende amri zako, Daima, naam, hata milele.
Psaumes 119.33 Psaumes 119.36 Apocalypse 2.10 1 Rois 8.58 Josué 24.23
113 Watu wa kusita-sita nawachukia, Lakini sheria yako naipenda.
Psaumes 94.11 Psaumes 119.103 Psaumes 119.97 Esaïe 55.7 2 Corinthiens 10.5
114 Ndiwe sitara yangu na ngao yangu, Neno lako nimelingojea.
Psaumes 91.1-91.2 Psaumes 32.7 Psaumes 3.3 Esaïe 32.2 Psaumes 119.81
115 Enyi watenda mabaya, ondokeni kwangu, Niyashike maagizo ya Mungu wangu.
Psaumes 6.8 Psaumes 139.19 Matthieu 7.23 1 Corinthiens 15.33 Psaumes 26.5
116 Unitegemeze sawasawa na ahadi yako, nikaishi, Wala usiniache niyaaibikie matumaini yangu.
Romains 5.5 Psaumes 25.2 Psaumes 37.17 Psaumes 37.24 Psaumes 63.8
117 Unisaidie nami nitakuwa salama, Nami nitaziangalia amri zako daima.
Psaumes 119.6 Romains 14.4 Psaumes 17.5 Psaumes 119.48 Esaïe 41.13
118 Umewakataa wote wazikosao amri zako, Kwa maana hila zao ni uongo.
Psaumes 119.10 Psaumes 119.21 Esaïe 25.10 Esaïe 63.3 Esaïe 44.20
119 Wabaya wa nchi pia umewaondoa kama takataka, Ndiyo maana nimezipenda shuhuda zako.
Malachie 3.2-3.3 1 Samuel 15.23 Psaumes 119.126-119.128 Matthieu 13.49-13.50 Ezéchiel 22.18-22.22
120 Mwili wangu unatetemeka kwa kukucha Wewe, Nami ninaziogopa hukumu zako.
Habakuk 3.16 2 Chroniques 34.21 1 Samuel 6.20 Lévitique 10.1-10.3 Hébreux 12.21
121 Nimefanya hukumu na haki, Usiniache mikononi mwao wanaonionea.
2 Samuel 8.15 Actes 25.10-25.11 2 Corinthiens 1.12 1 Samuel 24.11-24.15 1 Samuel 25.28
122 Uwe mdhamini wa mtumishi wako, apate mema, Wenye kiburi wasinionee.
Hébreux 7.22 Job 17.3 Psaumes 36.11 Genèse 43.9 Psaumes 119.21
123 Macho yangu yamefifia kwa kuutamani wokovu wako, Na ahadi ya haki yako.
Psaumes 143.7 Lamentations 4.17 Psaumes 119.81-119.82 Psaumes 130.6 Psaumes 69.3
124 Kama zilivyo rehema zako umtendee mtumishi wako, Na amri zako unifundishe.
Psaumes 119.12 Psaumes 143.10-143.12 Psaumes 130.7 Psaumes 119.76-119.77 Psaumes 119.26
125 Mimi ni mtumishi wako, unifahamishe, Nipate kuzijua shuhuda zako.
Psaumes 116.16 2 Chroniques 1.7-1.10 Psaumes 119.18-119.19 Psaumes 86.16 2 Corinthiens 3.5-3.6
126 Wakati umewadia Bwana atende kazi; Kwa kuwa wameitangua sheria yako.
Habakuk 1.4 Malachie 2.8 Jérémie 8.8 Romains 4.14 Matthieu 15.6
127 Ndiyo maana nimeyapenda maagizo yako, Kuliko dhahabu, naam, dhahabu iliyo safi.
Psaumes 19.10 Proverbes 3.13-3.18 Proverbes 8.11 Ephésiens 3.8 Psaumes 119.72
128 Maana nayaona mausia yako yote kuwa ya adili, Kila njia ya uongo naichukia.
Psaumes 119.104 Romains 7.22 Psaumes 19.7-19.8 Deutéronome 4.8 Job 33.27
129 Shuhuda zako ni za ajabu, Ndiyo maana roho yangu imezishika.
Psaumes 139.6 Psaumes 119.18 Psaumes 25.10 Psaumes 119.146 Psaumes 119.31
130 Kufafanusha maneno yako kwatia nuru, Na kumfahamisha mjinga.
Proverbes 6.23 Psaumes 19.7 Psaumes 119.105 Actes 26.18 2 Corinthiens 4.6
131 Nalifunua kinywa changu nikatweta, Maana naliyatamani maagizo yako.
Psaumes 42.1 Psaumes 119.20 Psaumes 119.40 Psaumes 81.10 Esaïe 26.8-26.9
132 Unigeukie, unirehemu mimi, Kama iwahusuvyo walipendao jina lako.
Psaumes 106.4 Psaumes 25.16 1 Samuel 1.11 2 Thessaloniciens 1.6-1.7 2 Samuel 16.12
133 Uzielekeze hatua zangu kwa neno lako, Uovu usije ukanimiliki.
Psaumes 19.13 Psaumes 17.5 Psaumes 32.8 Romains 6.12-6.14 Psaumes 119.116
134 Unikomboe na dhuluma ya mwanadamu, Nipate kuyashika mausia yako.
Psaumes 56.1-56.2 Psaumes 119.122 Luc 1.74-1.75 Ezéchiel 11.17-11.20 Psaumes 142.6
135 Umwangazie mtumishi wako uso wako, Na kunifundisha amri zako.
Psaumes 4.6 Psaumes 119.12 Psaumes 80.7 Psaumes 80.3 Psaumes 80.19
136 Macho yangu yachuruzika mito ya maji, Kwa sababu hawaitii sheria yako.
Jérémie 9.18 Ezéchiel 9.4 Jérémie 9.1 1 Samuel 15.11 Jérémie 14.17
137 Ee Bwana, Wewe ndiwe mwenye haki, Na hukumu zako ni za adili.
Esdras 9.15 Jérémie 12.1 Psaumes 145.17 Daniel 9.7 Daniel 9.14
138 Umeziagiza shuhuda zako kwa haki, Na kwa uaminifu mwingi.
Psaumes 19.7-19.9 Psaumes 119.144 Psaumes 119.86 Deutéronome 4.8 Deutéronome 4.45
139 Juhudi yangu imeniangamiza, Maana watesi wangu wameyasahau maneno yako.
Psaumes 69.9 Jean 2.17 1 Rois 19.10 Matthieu 21.16 Matthieu 22.29
140 Neno lako limesafika sana, Kwa hiyo mtumishi wako amelipenda.
Psaumes 12.6 Psaumes 19.8 Proverbes 30.5 Romains 7.12 1 Pierre 2.2
141 Mimi ni mdogo, nadharauliwa, Lakini siyasahau mausia yako.
Psaumes 22.6 Proverbes 19.1 Psaumes 119.176 Psaumes 40.17 Proverbes 15.16
142 Haki yako ni haki ya milele, Na sheria yako ni kweli.
Psaumes 19.9 Psaumes 119.151 2 Thessaloniciens 1.6-1.10 Esaïe 51.8 Psaumes 36.6
143 Taabu na dhiki zimenipata, Maagizo yako ni furaha yangu.
Psaumes 119.107 Psaumes 119.16 Psaumes 116.3 Jean 4.34 Psaumes 18.4-18.5
144 Haki ya shuhuda zako ni ya milele, Unifahamishe, nami nitaishi.
Daniel 12.10 Jérémie 4.22 Esaïe 27.11 Proverbes 10.21 Psaumes 119.169
145 Nimeita kwa moyo wangu wote; Ee Bwana, uitike; Nitazishika amri zako.
Psaumes 119.10 Psaumes 142.1-142.2 Psaumes 62.8 Jérémie 29.13 1 Samuel 1.10
146 Nimekuita Wewe, uniokoe, Nami nitazishika shuhuda zako.
Tite 3.4-3.8 Tite 2.14 Matthieu 1.21 Juges 10.15-10.16 Psaumes 119.134
147 Kutangulia mapambazuko naliomba msaada, Naliyangojea maneno yako kwa tumaini.
Psaumes 5.3 Marc 1.35 Psaumes 130.5-130.6 Psaumes 119.74 Hébreux 6.17-6.19
148 Macho yangu yalitangulia makesha ya usiku, Ili kuitafakari ahadi yako.
Psaumes 63.6 Lamentations 2.19 Psaumes 139.17-139.18 Luc 6.12 Psaumes 63.1
149 Uisikie sauti yangu sawasawa na fadhili zako, Ee Bwana, unihuishe sawasawa na hukumu yako.
Psaumes 119.25 Psaumes 55.2 Esaïe 63.7 Psaumes 109.21 Psaumes 119.40
150 Wanakaribia wanaonifuatia kwa chuki, Wamekwenda mbali na sheria yako.
1 Samuel 23.16 Job 21.14 2 Samuel 17.16 Proverbes 1.7 Psaumes 27.2
151 Ee Bwana, Wewe U karibu, Na maagizo yako yote ni kweli.
Psaumes 145.18 Psaumes 119.142 Psaumes 34.18 Deutéronome 4.7 Psaumes 119.138
152 Tokea zamani nimejua kwa shuhuda zako, Ya kuwa umeziweka zikae milele.
Luc 21.33 Psaumes 89.34-89.37 Ecclésiaste 3.14 Psaumes 111.7-111.8 Psaumes 119.144
153 Uyaangalie mateso yangu, uniokoe, Maana sikuisahau sheria yako.
Lamentations 5.1 Psaumes 119.16 Proverbes 3.1 Psaumes 119.176 Psaumes 25.19
154 Unitetee na kunikomboa, Unihuishe sawasawa na ahadi yako.
Michée 7.9 1 Samuel 24.15 Psaumes 35.1 Psaumes 119.25 Jérémie 50.34
155 Wokovu u mbali na wasio haki, Kwa maana hawajifunzi amri zako.
Job 5.4 Psaumes 18.27 Luc 16.24 Romains 3.11 Esaïe 57.19
156 Ee Bwana, rehema zako ni nyingi, Unihuishe sawasawa na hukumu zako.
Psaumes 86.13 Esaïe 55.7 Psaumes 86.5 Psaumes 86.15 2 Samuel 24.14
157 Wanaonifuatia na watesi wangu ni wengi, Lakini sikujiepusha na shuhuda zako.
Psaumes 119.51 Psaumes 44.17 Psaumes 7.1 Matthieu 24.9 Psaumes 119.110
158 Nimewaona watendao uhaini nikachukizwa, Kwa sababu hawakulitii neno lako.
Psaumes 139.21 Psaumes 119.53 Ezéchiel 9.4 Marc 3.5 Psaumes 119.136
159 Uangalie niyapendavyo mausia yako, Ee Bwana, unihuishe sawasawa na fadhili zako.
Néhémie 13.22 2 Rois 20.3 Psaumes 119.153 Psaumes 119.97 Néhémie 5.19
160 Jumla ya neno lako ni kweli, Na kila hukumu ya haki yako ni ya milele.
Psaumes 119.142 Psaumes 119.144 Psaumes 119.152 Matthieu 5.18 Proverbes 30.5
161 Wakuu wameniudhi bure, Ila moyo wangu unayahofia maneno yako.
1 Samuel 26.18 1 Samuel 24.9-24.15 Psaumes 119.23 Job 31.23 Néhémie 5.15
162 Naifurahia ahadi yako, Kama apataye mateka mengi.
Jérémie 15.16 Psaumes 119.111 1 Samuel 30.16 Psaumes 119.72 Esaïe 9.3
163 Nimeuchukia uongo, umenikirihi, Sheria yako nimeipenda.
Psaumes 119.128 Proverbes 30.8 Psaumes 101.7 Ephésiens 4.25 Proverbes 6.16-6.19
164 Mara saba kila siku nakusifu, Kwa sababu ya hukumu za haki yako.
Psaumes 119.62 Psaumes 55.17 Psaumes 48.11 Psaumes 97.8 Apocalypse 19.2
165 Wana amani nyingi waipendao sheria yako, Wala hawana la kuwakwaza.
Esaïe 32.17 1 Jean 2.10 Proverbes 3.1-3.2 Proverbes 3.17 Matthieu 24.24
166 Ee Bwana, nimeungojea wokovu wako, Na maagizo yako nimeyatenda.
Genèse 49.18 Psaumes 4.5 Psaumes 119.174 Psaumes 119.81 1 Jean 2.3-2.4
167 Nafsi yangu imezishika shuhuda zako, Nami nazipenda mno.
Romains 7.22 Hébreux 10.16 Psaumes 119.159 Jean 15.9-15.10 Jean 14.21-14.24
168 Nimeyashika mausia yako na shuhuda zako, Maana njia zangu zote zi mbele zako.
Proverbes 5.21 Psaumes 139.3 Hébreux 4.13 Psaumes 98.8 Job 34.21
169 Ee Bwana, kilio changu na kikukaribie, Unifahamishe sawasawa na neno lako.
Psaumes 18.6 Proverbes 2.3-2.5 Psaumes 119.144-119.145 2 Chroniques 30.27 2 Chroniques 1.10
170 Dua yangu na ifike mbele zako, Uniponye sawasawa na ahadi yako.
Psaumes 119.41 2 Samuel 7.25 Psaumes 28.2 Genèse 32.9-32.12 Psaumes 89.20-89.25
171 Midomo yangu na itoe sifa, Kwa kuwa unanifundisha mausia yako.
Psaumes 71.23-71.24 Psaumes 51.15 Psaumes 71.17 Psaumes 94.12 Psaumes 119.7
172 Ulimi wangu na uiimbe ahadi yako, Maana maagizo yako yote ni ya haki.
Psaumes 119.138 Romains 7.14 Colossiens 4.6 Matthieu 12.34-12.35 Psaumes 119.46
173 Mkono wako na uwe tayari kunisaidia, Maana nimeyachagua mausia yako.
Josué 24.22 Luc 10.42 Philippiens 4.13 Psaumes 119.117 Psaumes 119.30
174 Ee Bwana, nimeutamani wokovu wako, Na sheria yako ndiyo furaha yangu.
Psaumes 119.24 Psaumes 119.16 Romains 8.23-8.25 Psaumes 119.47 2 Samuel 23.5
175 Nafsi yangu na iishi, ipate kukusifu, Na hukumu zako zinisaidie.
Psaumes 9.13-9.14 Romains 8.28 Esaïe 26.8-26.9 Psaumes 30.9 Esaïe 55.3
176 Nimetanga-tanga kama kondoo aliyepotea; Umtafute mtumishi wako; Kwa maana sikuyasahau maagizo yako.
Philippiens 2.13 Jean 10.16 1 Pierre 2.25 Ezéchiel 34.6 Esaïe 53.6

Cette Bible est dans le domaine public.