Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 21.37
Bible en Swahili de l’est


Entrée triomphale de Jésus à Jérusalem

1 Hata walipokaribia Yerusalemu, na kufika Bethfage, katika mlima wa Mizeituni, ndipo Yesu alipotuma wanafunzi wawili akiwaambia,
Jean 8.1 Actes 1.12 Matthieu 26.30 Matthieu 24.3 Luc 21.37
2 Enendeni mpaka kijiji kile kinachowakabili, na mara mtaona punda amefungwa, na mwana-punda pamoja naye; wafungueni mniletee.
Jean 2.5-2.8 Marc 14.13-14.16 Marc 11.2-11.3 Matthieu 26.18 Luc 19.30-19.32
3 Na kama mtu akiwaambia neno, semeni, Bwana anawahitaji; na mara huyo atawapeleka.
1 Chroniques 29.14-29.16 2 Corinthiens 8.1-8.2 1 Samuel 10.26 Actes 17.25 Esdras 1.1
4 Haya yote yamekuwa, ili litimie neno lililonenwa na nabii, akisema,
Zacharie 9.9 Jean 19.36-19.37 Matthieu 1.22 Jean 12.15 Matthieu 26.56
5 Mwambieni binti Sayuni Tazama, mfalme wako anakuja kwako, Mpole, naye amepanda punda, Na mwana-punda, mtoto wa punda.
Zacharie 9.9-9.10 Esaïe 62.11 Matthieu 11.29 Genèse 49.10 Esaïe 9.6-9.7
6 Wale wanafunzi wakaenda zao, wakafanya kama Yesu alivyowaamuru,
Genèse 6.22 Exode 40.16 Jean 15.14 Genèse 12.4 Exode 39.43
7 wakamleta yule punda na mwana-punda, wakaweka nguo zao juu yao, naye akaketi juu yake.
Luc 19.32-19.35 2 Rois 9.13 Marc 11.4-11.8
8 Watu wengi katika ule mkutano wakatandaza nguo zao njiani; na wengine wakakata matawi ya miti, wakayatandaza njiani.
Jean 12.13 2 Rois 9.13 Lévitique 23.40
9 Na makutano waliotangulia, na wale waliofuata, wakapaza sauti, wakisema, Hosana, Mwana wa Daudi; ndiye mbarikiwa, yeye ajaye kwa jina la Bwana; Hosana juu mbinguni.
Matthieu 23.39 Psaumes 118.24-118.26 Luc 2.14 Matthieu 21.15 Matthieu 9.27
10 Hata alipoingia Yerusalemu, mji wote ukataharuki, watu wakisema, Ni nani huyu?
Matthieu 2.3 Actes 9.5 1 Samuel 16.4 Cantique 3.6 Ruth 1.19
11 Makutano wakasema, Huyu ni yule nabii, Yesu, wa Nazareti ya Galilaya.
Jean 6.14 Matthieu 2.23 Jean 7.40 Luc 7.16 Jean 9.17

Jésus dans le temple

12 Yesu akaingia ndani ya hekalu, akawafukuza wote waliokuwa wakiuza na kununua hekaluni, akazipindua meza za wabadili fedha, na viti vyao waliokuwa wakiuza njiwa;
Jean 2.14-2.17 Luc 19.45-19.47 Marc 11.15-11.18 Lévitique 1.14 Lévitique 12.8
13 akawaambia, Imeandikwa, Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala; bali ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi.
Jérémie 7.11 Esaïe 56.7 Luc 19.46 Marc 11.17 Psaumes 93.5
14 Na vipofu na viwete wakamwendea mle hekaluni, akawaponya.
Matthieu 4.23 Esaïe 35.5 Actes 10.38 Matthieu 9.35 Matthieu 11.4-11.5
15 Lakini wakuu wa makuhani na waandishi walipoyaona maajabu aliyoyafanya, na watoto waliopaza sauti zao hekaluni, wakisema, Hosana, Mwana wa Daudi! Walikasirika,
Matthieu 21.9 Luc 19.39-19.40 Luc 20.1 Matthieu 27.20 Matthieu 22.42
16 wakamwambia, Wasikia hawa wasemavyo? Yesu akawaambia, Naam; hamkupata kusoma, Kwa vinywa vya watoto wachanga na wanyonyao umekamilisha sifa?
Psaumes 8.2 Matthieu 11.25 Matthieu 12.3 Matthieu 22.31 Matthieu 19.4
17 Akawaacha, akatoka nje ya mji mpaka Bethania, akalala huko.
Jean 11.18 Marc 11.11 Jean 11.1 Matthieu 16.4 Marc 11.1
18 Hata asubuhi alipokuwa akienda mjini, aliona njaa.
Matthieu 4.2 Marc 11.12-11.14 Marc 11.20-11.24 Matthieu 12.1 Hébreux 4.15
19 Akaona mtini mmoja kando ya njia, akauendea, asione kitu juu yake ila majani tu; akauambia, Yasipatikane matunda kwako tangu leo hata milele. Mtini ukanyauka mara.
Marc 11.14 Luc 13.6-13.9 Tite 1.16 Luc 3.9 Jude 1.12
20 Wanafunzi walipoona, walistaajabu, wakisema, Jinsi gani mtini umenyauka mara?
Jacques 1.10-1.11 Marc 11.20-11.21 Esaïe 40.6-40.8
21 Yesu akajibu, akawaambia, Amin, nawaambia Mkiwa na imani, msipokuwa na shaka, mtafanya si hilo la mtini tu, lakini hata mkiuambia mlima huu, Ng’oka, ukatupwe baharini, litatendeka.
Matthieu 17.20 Jacques 1.6 Romains 4.19-4.20 1 Corinthiens 13.2 Matthieu 8.12
22 Na yo yote mtakayoyaomba katika sala mkiamini, mtapokea.
Matthieu 7.7 Jean 15.7 Jean 16.24 1 Jean 3.22 1 Jean 5.14-5.15
23 Hata alipokwisha kuingia hekaluni, wakuu wa makuhani na wazee wa watu wakamwendea alipokuwa akifundisha, wakasema, Ni kwa amri gani unatenda mambo haya? Naye ni nani aliyekupa amri hii?
Actes 4.7 Actes 7.27 Exode 2.14 1 Chroniques 24.1-24.19 Luc 19.47-20.8
24 Yesu akajibu akawaambia, Na mimi nitawauliza neno moja; ambalo mkinijibu, nami nitawaambia ni kwa amri gani ninatenda haya.
Colossiens 4.6 Luc 6.9 Matthieu 10.16 Proverbes 26.4-26.5
25 Ubatizo wa Yohana ulitoka wapi? Ulitoka mbinguni, au kwa wanadamu? Wakahojiana wao kwa wao, wakisema, Tukisema, Ulitoka mbinguni, atatuambia, Mbona basi hamkumwamini?
1 Jean 3.20 Luc 3.2-3.20 Jean 3.18 Jean 12.37-12.43 Luc 1.11-1.17
26 Na tukisema, Ulitoka kwa wanadamu, twaogopa mkutano; maana watu wote wamwona Yohana kuwa ni nabii.
Marc 6.20 Matthieu 14.5 Jean 5.35 Matthieu 11.9 Matthieu 21.46
27 Wakamjibu Yesu wakasema, Hatujui. Naye akawaambia, Wala mimi siwaambii ninyi ni kwa amri gani ninatenda haya.
Matthieu 23.16-23.28 Esaïe 6.10 Jean 9.30 Romains 1.18-1.22 Jérémie 8.7-8.9

Parabole des deux fils

28 Lakini mwaonaje? Mtu mmoja alikuwa na wana wawili; akamwendea yule wa kwanza, akasema, Mwanangu, leo nenda kafanye kazi katika shamba la mizabibu.
Matthieu 21.33 1 Corinthiens 10.15 Matthieu 17.25 Matthieu 20.1 Luc 13.4
29 Akajibu akasema, Naenda, Bwana; asiende.
Esaïe 55.6-55.7 Esaïe 1.16-1.19 1 Corinthiens 6.11 Ezéchiel 18.28-18.32 Ephésiens 2.1-2.13
30 Akamwendea yule wa pili, akasema vile vile. Naye akajibu akasema, Sitaki; baadaye akatubu, akaenda.
Tite 1.16 Romains 2.17-2.25 Ezéchiel 33.31 Matthieu 23.3
31 Je! Katika hao wawili ni yupi aliyefanya mapenzi ya babaye? Wakamwambia, Ni yule wa pili. Basi Yesu akawaambia, Amin nawaambia, watoza ushuru na makahaba wanatangulia mbele yenu kuingia katika ufalme wa Mungu.
Luc 7.37-7.50 Luc 7.29 2 Pierre 3.9 Romains 5.20 Matthieu 18.3
32 Kwa sababu Yohana alikuja kwenu kwa njia ya haki, ninyi msimwamini; lakini watoza ushuru na makahaba walimwamini, nanyi hata mlipoona, hamkutubu baadaye, ili kumwamini.
2 Pierre 2.21 Matthieu 11.18 Matthieu 21.25 Luc 7.29-7.30 Luc 7.37-7.50

Parabole des vignerons

33 Sikilizeni mfano mwingine. Kulikuwa na mtu mwenye nyumba, naye alipanda shamba la mizabibu, akalizungusha ugo, akachimba shimo la shinikizo ndani yake, akajenga mnara, akapangisha wakulima, akasafiri.
Matthieu 25.14-25.15 Cantique 8.11-8.12 Esaïe 5.1-5.4 Marc 12.1-12.12 Luc 20.9-20.19
34 Wakati wa matunda ulipokuwa karibu, akawatuma watumwa wake kwa wale wakulima, wapokee matunda yake.
Marc 12.2-12.5 Zacharie 7.9-7.13 Cantique 8.11-8.12 Esaïe 5.4 Jérémie 35.15
35 Wale wakulima wakawakamata watumwa wake, huyu wakampiga, na huyu wakamwua, na huyu wakampiga kwa mawe.
Hébreux 11.36-11.37 Matthieu 5.12 2 Chroniques 36.15-36.16 Actes 7.52 Néhémie 9.26
36 Akawatuma tena watumwa wengine wengi kuliko wa kwanza wakawatenda vile vile.
Matthieu 22.4
37 Mwishowe akamtuma mwanawe kwao, akisema, Watamstahi mwanangu.
Jean 1.34 Luc 20.13 Jean 3.16 Esaïe 5.4 Jean 3.35-3.36
38 Lakini wale wakulima walipomwona yule mwana, wakasemezana wao kwa wao, Huyu ni mrithi; haya na tumwue, tuutwae urithi wake.
Actes 4.27-4.28 Actes 5.24-5.28 Genèse 37.18-37.20 Psaumes 2.2-2.8 Matthieu 27.1-27.2
39 Wakamkamata, wakamtupa nje ya shamba la mizabibu, wakamwua.
Actes 2.23 Jean 18.12 Actes 4.10 Jacques 5.6 Actes 7.52
40 Basi atakapokuja yule bwana wa shamba la mizabibu, atawatendaje wale wakulima?
Marc 12.9 Luc 20.15-20.16 Hébreux 10.29
41 Wakamwambia, Atawaangamiza vibaya wale wabaya; na shamba la mizabibu atawapangisha wakulima wengine, watakaomlipa matunda kwa wakati wake.
Actes 18.6 Matthieu 21.43 Actes 28.28 Psaumes 2.9 Luc 13.28-13.29
42 Yesu akawaambia, Hamkupata kusoma katika maandiko, Jiwe walilolikataa waashi, Hilo limekuwa jiwe kuu la pembeni; Neno hili limetoka kwa Bwana, Nalo ni ajabu machoni petu?
Psaumes 118.22-118.23 Esaïe 28.16 Actes 4.11 1 Pierre 2.4-2.8 Romains 9.33
43 Kwa sababu hiyo nawaambia, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu, nao watapewa taifa lingine lenye kuzaa matunda yake.
Luc 17.20-17.21 Jean 3.3 Esaïe 26.2 Esaïe 28.2 Matthieu 21.41
44 Naye aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika-vunjika; naye ye yote ambaye litamwangukia, litamsaga tikitiki.
Esaïe 8.14-8.15 Daniel 2.44-2.45 Luc 20.18 Romains 9.33 Daniel 2.34-2.35
45 Wakuu wa makuhani na Mafarisayo, waliposikia mifano yake, walitambua ya kuwa anawanenea wao.
Luc 11.45 Luc 20.19 Matthieu 12.12
46 Nao walipotafuta kumkamata, waliwaogopa makutano, kwa maana wao walimwona kuwa nabii.
Matthieu 21.11 Matthieu 21.26 Proverbes 9.7-9.9 Luc 7.39 2 Samuel 12.7-12.13

Cette Bible est dans le domaine public.