Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 21.26
Bible en Swahili de l’est


Entrée triomphale de Jésus à Jérusalem

1 Hata walipokaribia Yerusalemu, na kufika Bethfage, katika mlima wa Mizeituni, ndipo Yesu alipotuma wanafunzi wawili akiwaambia,
Matthieu 24.3 Jean 8.1 Actes 1.12 Matthieu 26.30 Zacharie 14.4
2 Enendeni mpaka kijiji kile kinachowakabili, na mara mtaona punda amefungwa, na mwana-punda pamoja naye; wafungueni mniletee.
Jean 2.5-2.8 Marc 14.13-14.16 Marc 11.2-11.3 Matthieu 26.18 Luc 19.30-19.32
3 Na kama mtu akiwaambia neno, semeni, Bwana anawahitaji; na mara huyo atawapeleka.
Aggée 2.8-2.9 Jean 17.2 Jacques 1.17 1 Rois 17.9 Psaumes 50.10-50.11
4 Haya yote yamekuwa, ili litimie neno lililonenwa na nabii, akisema,
Zacharie 9.9 Jean 19.36-19.37 Matthieu 1.22 Jean 12.15 Matthieu 26.56
5 Mwambieni binti Sayuni Tazama, mfalme wako anakuja kwako, Mpole, naye amepanda punda, Na mwana-punda, mtoto wa punda.
Zacharie 9.9-9.10 Esaïe 62.11 Genèse 49.10 Matthieu 11.29 Esaïe 40.9
6 Wale wanafunzi wakaenda zao, wakafanya kama Yesu alivyowaamuru,
Genèse 6.22 Exode 40.16 Jean 15.14 Genèse 12.4 Exode 39.43
7 wakamleta yule punda na mwana-punda, wakaweka nguo zao juu yao, naye akaketi juu yake.
Luc 19.32-19.35 2 Rois 9.13 Marc 11.4-11.8
8 Watu wengi katika ule mkutano wakatandaza nguo zao njiani; na wengine wakakata matawi ya miti, wakayatandaza njiani.
Jean 12.13 2 Rois 9.13 Lévitique 23.40
9 Na makutano waliotangulia, na wale waliofuata, wakapaza sauti, wakisema, Hosana, Mwana wa Daudi; ndiye mbarikiwa, yeye ajaye kwa jina la Bwana; Hosana juu mbinguni.
Matthieu 23.39 Psaumes 118.24-118.26 Luc 2.14 Matthieu 21.15 Jean 12.13-12.15
10 Hata alipoingia Yerusalemu, mji wote ukataharuki, watu wakisema, Ni nani huyu?
Luc 20.2 Esaïe 63.1 Jean 12.16-12.19 Luc 5.21 Luc 7.49
11 Makutano wakasema, Huyu ni yule nabii, Yesu, wa Nazareti ya Galilaya.
Jean 6.14 Jean 9.17 Matthieu 2.23 Jean 7.40 Luc 7.16

Jésus dans le temple

12 Yesu akaingia ndani ya hekalu, akawafukuza wote waliokuwa wakiuza na kununua hekaluni, akazipindua meza za wabadili fedha, na viti vyao waliokuwa wakiuza njiwa;
Jean 2.14-2.17 Lévitique 1.14 Luc 19.45-19.47 Marc 11.15-11.18 Lévitique 12.8
13 akawaambia, Imeandikwa, Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala; bali ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi.
Jérémie 7.11 Esaïe 56.7 Luc 19.46 Marc 11.17 Psaumes 93.5
14 Na vipofu na viwete wakamwendea mle hekaluni, akawaponya.
Matthieu 4.23 Esaïe 35.5 Actes 10.38 Matthieu 9.35 Matthieu 11.4-11.5
15 Lakini wakuu wa makuhani na waandishi walipoyaona maajabu aliyoyafanya, na watoto waliopaza sauti zao hekaluni, wakisema, Hosana, Mwana wa Daudi! Walikasirika,
Matthieu 21.9 Luc 19.39-19.40 Matthieu 27.1 Matthieu 26.59 Luc 22.66
16 wakamwambia, Wasikia hawa wasemavyo? Yesu akawaambia, Naam; hamkupata kusoma, Kwa vinywa vya watoto wachanga na wanyonyao umekamilisha sifa?
Psaumes 8.2 Matthieu 11.25 Matthieu 19.4 Matthieu 12.3 Matthieu 22.31
17 Akawaacha, akatoka nje ya mji mpaka Bethania, akalala huko.
Jean 11.18 Marc 11.11 Jean 11.1 Marc 11.19 Luc 24.50
18 Hata asubuhi alipokuwa akienda mjini, aliona njaa.
Matthieu 4.2 Marc 11.12-11.14 Marc 11.20-11.24 Matthieu 12.1 Hébreux 4.15
19 Akaona mtini mmoja kando ya njia, akauendea, asione kitu juu yake ila majani tu; akauambia, Yasipatikane matunda kwako tangu leo hata milele. Mtini ukanyauka mara.
Marc 11.14 Luc 13.6-13.9 Tite 1.16 2 Pierre 2.20-2.22 Jean 15.6
20 Wanafunzi walipoona, walistaajabu, wakisema, Jinsi gani mtini umenyauka mara?
Jacques 1.10-1.11 Marc 11.20-11.21 Esaïe 40.6-40.8
21 Yesu akajibu, akawaambia, Amin, nawaambia Mkiwa na imani, msipokuwa na shaka, mtafanya si hilo la mtini tu, lakini hata mkiuambia mlima huu, Ng’oka, ukatupwe baharini, litatendeka.
Matthieu 17.20 Jacques 1.6 1 Corinthiens 13.2 Romains 4.19-4.20 Matthieu 8.12
22 Na yo yote mtakayoyaomba katika sala mkiamini, mtapokea.
Matthieu 7.7 1 Jean 3.22 Jean 15.7 Jean 16.24 Jacques 5.16
23 Hata alipokwisha kuingia hekaluni, wakuu wa makuhani na wazee wa watu wakamwendea alipokuwa akifundisha, wakasema, Ni kwa amri gani unatenda mambo haya? Naye ni nani aliyekupa amri hii?
Actes 4.7 Actes 7.27 Exode 2.14 Matthieu 26.55 1 Chroniques 24.1-24.19
24 Yesu akajibu akawaambia, Na mimi nitawauliza neno moja; ambalo mkinijibu, nami nitawaambia ni kwa amri gani ninatenda haya.
Colossiens 4.6 Luc 6.9 Matthieu 10.16 Proverbes 26.4-26.5
25 Ubatizo wa Yohana ulitoka wapi? Ulitoka mbinguni, au kwa wanadamu? Wakahojiana wao kwa wao, wakisema, Tukisema, Ulitoka mbinguni, atatuambia, Mbona basi hamkumwamini?
1 Jean 3.20 Matthieu 3.1-3.12 Jean 10.25-10.26 Jean 1.25-1.34 Jean 5.44-5.47
26 Na tukisema, Ulitoka kwa wanadamu, twaogopa mkutano; maana watu wote wamwona Yohana kuwa ni nabii.
Marc 6.20 Matthieu 21.46 Matthieu 14.5 Jean 5.35 Matthieu 11.9
27 Wakamjibu Yesu wakasema, Hatujui. Naye akawaambia, Wala mimi siwaambii ninyi ni kwa amri gani ninatenda haya.
Jean 9.40-9.41 Malachie 2.6-2.9 Romains 1.28 Esaïe 28.9 Esaïe 29.10-29.12

Parabole des deux fils

28 Lakini mwaonaje? Mtu mmoja alikuwa na wana wawili; akamwendea yule wa kwanza, akasema, Mwanangu, leo nenda kafanye kazi katika shamba la mizabibu.
Matthieu 20.1 Matthieu 21.33 1 Corinthiens 10.15 Matthieu 17.25 Luc 15.11-15.32
29 Akajibu akasema, Naenda, Bwana; asiende.
Matthieu 3.2-3.8 2 Chroniques 33.10-33.19 Matthieu 21.31 Jérémie 44.16 Jonas 3.8-3.10
30 Akamwendea yule wa pili, akasema vile vile. Naye akajibu akasema, Sitaki; baadaye akatubu, akaenda.
Tite 1.16 Romains 2.17-2.25 Ezéchiel 33.31 Matthieu 23.3
31 Je! Katika hao wawili ni yupi aliyefanya mapenzi ya babaye? Wakamwambia, Ni yule wa pili. Basi Yesu akawaambia, Amin nawaambia, watoza ushuru na makahaba wanatangulia mbele yenu kuingia katika ufalme wa Mungu.
Luc 7.37-7.50 Luc 7.29 2 Pierre 3.9 Matthieu 12.50 Matthieu 7.21
32 Kwa sababu Yohana alikuja kwenu kwa njia ya haki, ninyi msimwamini; lakini watoza ushuru na makahaba walimwamini, nanyi hata mlipoona, hamkutubu baadaye, ili kumwamini.
Luc 7.37-7.50 2 Pierre 2.21 Matthieu 11.18 Matthieu 21.25 Luc 7.29-7.30

Parabole des vignerons

33 Sikilizeni mfano mwingine. Kulikuwa na mtu mwenye nyumba, naye alipanda shamba la mizabibu, akalizungusha ugo, akachimba shimo la shinikizo ndani yake, akajenga mnara, akapangisha wakulima, akasafiri.
Esaïe 5.1-5.4 Matthieu 25.14-25.15 Cantique 8.11-8.12 Marc 13.34 Marc 12.1-12.12
34 Wakati wa matunda ulipokuwa karibu, akawatuma watumwa wake kwa wale wakulima, wapokee matunda yake.
Néhémie 9.29-9.30 Luc 20.10-20.19 2 Chroniques 36.15-36.16 2 Rois 17.13-17.23 Jérémie 25.3-25.7
35 Wale wakulima wakawakamata watumwa wake, huyu wakampiga, na huyu wakamwua, na huyu wakampiga kwa mawe.
Hébreux 11.36-11.37 Actes 7.52 Néhémie 9.26 Matthieu 5.12 2 Chroniques 36.15-36.16
36 Akawatuma tena watumwa wengine wengi kuliko wa kwanza wakawatenda vile vile.
Matthieu 22.4
37 Mwishowe akamtuma mwanawe kwao, akisema, Watamstahi mwanangu.
Marc 12.6 Matthieu 3.17 Hébreux 1.1-1.2 Jean 1.18 Jérémie 36.3
38 Lakini wale wakulima walipomwona yule mwana, wakasemezana wao kwa wao, Huyu ni mrithi; haya na tumwue, tuutwae urithi wake.
Hébreux 1.2 Matthieu 2.13-2.16 Luc 20.14 Matthieu 26.3-26.4 Jean 11.47-11.53
39 Wakamkamata, wakamtupa nje ya shamba la mizabibu, wakamwua.
Actes 2.23 Actes 4.25-4.27 Matthieu 26.57 Matthieu 26.50 Luc 22.52-22.54
40 Basi atakapokuja yule bwana wa shamba la mizabibu, atawatendaje wale wakulima?
Marc 12.9 Luc 20.15-20.16 Hébreux 10.29
41 Wakamwambia, Atawaangamiza vibaya wale wabaya; na shamba la mizabibu atawapangisha wakulima wengine, watakaomlipa matunda kwa wakati wake.
Actes 18.6 Actes 28.28 Matthieu 21.43 Malachie 4.1-4.6 Deutéronome 28.59-28.68
42 Yesu akawaambia, Hamkupata kusoma katika maandiko, Jiwe walilolikataa waashi, Hilo limekuwa jiwe kuu la pembeni; Neno hili limetoka kwa Bwana, Nalo ni ajabu machoni petu?
Psaumes 118.22-118.23 Actes 4.11 Esaïe 28.16 1 Pierre 2.4-2.8 Romains 9.33
43 Kwa sababu hiyo nawaambia, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu, nao watapewa taifa lingine lenye kuzaa matunda yake.
Matthieu 12.28 1 Pierre 2.9 1 Corinthiens 13.2 Exode 19.6 Matthieu 8.11-8.12
44 Naye aangukaye juu ya jiwe hilo atavunjika-vunjika; naye ye yote ambaye litamwangukia, litamsaga tikitiki.
Esaïe 8.14-8.15 Daniel 2.44-2.45 Luc 20.18 Romains 9.33 Daniel 2.34-2.35
45 Wakuu wa makuhani na Mafarisayo, waliposikia mifano yake, walitambua ya kuwa anawanenea wao.
Luc 11.45 Luc 20.19 Matthieu 12.12
46 Nao walipotafuta kumkamata, waliwaogopa makutano, kwa maana wao walimwona kuwa nabii.
Matthieu 21.11 Matthieu 21.26 Esaïe 29.1 Actes 2.22 Proverbes 15.12

Cette Bible est dans le domaine public.