Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Actes 13.31
Bible en Swahili de l’est


Premier voyage missionnaire

Envoi de Barnabas et Saul

1 Na huko Antiokia katika kanisa lililokuwako palikuwa na manabii na waalimu, nao ni Barnaba, na Simeoni aitwaye Nigeri, na Lukio Mkirene, na Manaeni aliyekuwa ndugu wa kunyonya wa mfalme Herode, na Sauli.
Actes 11.22-11.27 Actes 4.36 Luc 3.1 Ephésiens 4.11 1 Corinthiens 12.28-12.29
2 Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia.
Galates 1.15 Actes 9.15 2 Timothée 1.11 1 Corinthiens 12.11 Romains 1.1
3 Ndipo wakiisha kufunga na kuomba, wakaweka mikono yao juu yao, wakawaacha waende zao.
Actes 6.6 Actes 14.26 Actes 14.23 1 Timothée 5.22 2 Timothée 2.2
4 Basi watu hao, wakiisha kupelekwa na Roho Mtakatifu wakatelemkia Seleukia, na kutoka huko wakasafiri baharini hata Kipro.
Actes 4.36 Actes 13.2 Actes 27.4 Actes 20.23 Actes 11.19
5 Na walipokuwa katika Salami wakalihubiri neno la Mungu katika masinagogi ya Wayahudi, nao walikuwa naye Yohana kuwa mtumishi wao.
Actes 13.14 Actes 13.46 Actes 17.17 Actes 12.12 Actes 9.20
6 Walipokwisha kupita katikati ya kisiwa chote mpaka Pafo, wakaona mtu mmoja, mchawi, nabii wa uongo, Myahudi jina lake Bar-Yesu;
Matthieu 7.15 Apocalypse 19.20 Esaïe 8.19-8.20 Actes 19.18-19.19 1 Chroniques 10.13
7 mtu huyu alikuwa pamoja na liwali Sergio Paulo, mtu mwenye akili. Yeye liwali akawaita Barnaba na Sauli waje kwake, akataka kulisikia neno la Mungu.
Actes 19.38 Actes 13.12 Actes 18.12 Proverbes 18.15 Actes 13.8
8 Lakini Elima, yule mchawi (maana ndiyo tafsiri ya jina lake), akashindana nao, akitaka kumtia yule liwali moyo wa kuiacha ile imani.
Actes 13.6-13.7 2 Timothée 3.8 1 Rois 22.24 Jean 1.41 Actes 6.7
9 Lakini Sauli, ambaye ndiye Paulo, akijaa Roho Mtakatifu, akamkazia macho,
Actes 4.8 Actes 2.4 Marc 3.5 Luc 20.17 Actes 4.31
10 akasema, Ewe mwenye kujaa hila na uovu wote, mwana wa Ibilisi, adui wa haki yote, huachi kuzipotoa njia za Bwana zilizonyoka?
Matthieu 13.38 Osée 14.9 Jean 8.44 Actes 18.25-18.26 Luc 11.52
11 Basi, angalia, mkono wa Bwana u juu yako, nawe utakuwa kipofu, usilione jua kwa muda. Mara kiwi kikamwangukia na giza, akazunguka-zunguka na kumtafuta mtu wa kumshika mkono na kumwongoza.
Exode 9.3 Psaumes 32.4 Job 19.21 1 Samuel 5.11 Actes 9.8-9.9
12 Ndipo yule liwali, alipoyaona yaliyotendeka, akaamini, akiyastaajabia mafundisho ya Bwana.
Actes 13.7 Actes 13.49 Actes 15.35 2 Corinthiens 10.4-10.5 Actes 19.7
13 Kisha Paulo na wenziwe wakang’oa nanga wakasafiri kutoka Pafo, wakafika Perge katika Pamfilia. Yohana akawaacha akarejea Yerusalemu.
Actes 2.10 Actes 14.24-14.25 Actes 27.5 Actes 13.5-13.6 Actes 15.38

L’Évangile à Antioche de Pisidie

14 Lakini wao wakatoka Perge, wakapita kati ya nchi, wakafika Antiokia, mji wa Pisidia, wakaingia katika sinagogi siku ya sabato, wakaketi.
Actes 16.13 Actes 17.2 Actes 13.5 Actes 14.19 Actes 18.4
15 Kisha, baada ya kusomwa torati na chuo cha manabii, wakuu wa sinagogi wakatuma mtu kwao, na kuwaambia, Ndugu, kama mkiwa na neno la kuwafaa watu hawa, lisemeni.
Actes 15.21 Hébreux 13.22 Marc 5.22 Actes 13.27 Luc 4.16-4.18
16 Paulo akasimama, akawapungia mkono, akasema, Enyi waume wa Israeli, nanyi mnaomcha Mungu, sikilizeni.
Actes 12.17 Actes 13.26 Actes 10.2 Actes 2.14 Luc 1.50
17 Mungu wa watu hawa Israeli aliwachagua baba zetu, akawatukuza watu hao, walipokuwa wakikaa kama wageni katika nchi ya Misri, na kwa mkono ulioinuliwa akawatoa, akawaongoza.
Deutéronome 7.6-7.8 Psaumes 105.23-105.24 Deutéronome 9.5 Genèse 17.7-17.8 Deutéronome 4.34
18 Na kwa muda wa miaka kama arobaini akawavumilia katika jangwa.
Actes 7.36 Deutéronome 9.7 Deutéronome 9.21-9.24 Deutéronome 1.31 Exode 16.2
19 Na alipokwisha kuwaharibu mataifa saba katika nchi ya Kanaani akawapa nchi yao iwe urithi kwa muda wa miaka kama mia nne na hamsini;
Psaumes 78.55 Deutéronome 7.1 Actes 7.45 Josué 14.1 Josué 19.51
20 baada ya hayo akawapa waamuzi hata zamani za nabii Samweli.
Juges 2.16 1 Samuel 3.20 Actes 3.24 Ruth 1.1 1 Chroniques 17.6
21 Hatimaye wakaomba kupewa mfalme; Mungu akawapa Sauli mwana wa Kishi, mtu wa kabila ya Benyamini, kwa muda wa miaka arobaini.
1 Samuel 10.1 1 Samuel 8.5-9.2 1 Samuel 12.12-12.19 1 Samuel 11.15 1 Samuel 10.21-10.26
22 Na alipokwisha kumwondoa huyo, akamwinua Daudi awe mfalme wao ambaye alimshuhudia, akisema, Nimemwona Daudi, mwana wa Yese, mtu anayeupendeza moyo wangu, atakayefanya mapenzi yangu yote.
1 Samuel 16.1 1 Samuel 16.13 1 Samuel 15.23 1 Samuel 15.26 Actes 7.46
23 Katika uzao wake mtu huyo Mungu amewaletea Israeli Mwokozi, yaani, Yesu, kama alivyoahidi;
Matthieu 1.1 Psaumes 132.11 Actes 13.32 2 Samuel 7.12 Jérémie 23.5-23.6
24 Yohana alipokuwa amekwisha kuwahubiri watu wote wa Israeli habari za ubatizo wa toba, kabla ya kuja kwake.
Actes 1.22 Jean 5.33-5.36 Matthieu 3.1-3.11 Jean 1.6-1.8 Luc 3.2-3.20
25 Naye Yohana alipokuwa akimaliza mwendo wake alinena, Mwanidhani mimi kuwa nani? Mimi siye. Lakini, angalieni, anakuja mmoja nyuma yangu ambaye mimi sistahili kumlegezea viatu vya miguu yake.
Matthieu 3.11 Marc 1.7 Actes 20.24 Jean 1.36 Actes 13.36
26 Ndugu zangu, wana wa ukoo wa Ibrahimu, na hao miongoni mwenu wanaomcha Mungu, kwetu sisi neno la wokovu huu limepelekwa.
Ephésiens 1.13 Actes 13.46 Actes 28.28 Actes 4.12 Matthieu 10.6
27 Kwa maana wakaao Yerusalemu, na wakuu wao, kwa kuwa hawakumjua yeye, wala maneno ya manabii yanayosomwa kila sabato, wameyatimiza kwa kumhukumu.
Actes 3.17 Actes 15.21 Actes 26.22-26.23 Luc 24.20 2 Corinthiens 3.14
28 Na ijapokuwa hawakuona sababu ya kumfisha wakamwomba Pilato auawe.
Matthieu 27.22-27.25 Luc 23.21-23.25 Actes 3.13-3.14 Jean 18.38 Luc 23.4-23.5
29 Hata walipokwisha kumaliza yote aliyoandikiwa, wakamtelemsha katika ule mti, wakamweka kaburini.
Luc 23.53 Actes 5.30 Jean 19.30 Luc 24.44 Marc 15.45-15.46
30 Lakini Mungu akamfufua katika wafu;
Actes 2.24 Matthieu 28.6 Hébreux 13.20 Actes 2.32 Actes 17.31
31 akaonekana siku nyingi na wale waliopanda naye kutoka Galilaya hata Yerusalemu, ambao sasa ndio walio mashahidi wake mbele ya watu.
Luc 24.48 Actes 1.3 Actes 1.11 Actes 1.8 Matthieu 28.16
32 Na sisi tunawahubiri habari njema ya ahadi ile waliyopewa mababa,
Actes 26.6 Romains 4.13 Zacharie 6.12 Jérémie 23.5 Michée 5.2
33 ya kwamba Mungu amewatimizia watoto wetu ahadi hiyo, kwa kumfufua Yesu; kama ilivyoandikwa katika Zaburi ya pili, Wewe ndiwe Mwanangu, mimi leo nimekuzaa.
Psaumes 2.7 Hébreux 5.5 Hébreux 1.5-1.6
34 Tena ya kuwa alimfufua katika wafu, asipate kurudia uharibifu, amenena hivi, Nitawapa ninyi mambo matakatifu ya Daudi yaliyo amini.
Esaïe 55.3 Romains 6.9 Psaumes 89.2-89.4 Amos 9.11 Jérémie 33.15-33.17
35 Kwa hiyo anena na pengine, Hutamwachia Mtakatifu wako kuona uharibifu,
Psaumes 16.10 Actes 2.27-2.31 Jean 3.36 Actes 13.36-13.37 Psaumes 49.9
36 Kwa maana Daudi, akiisha kulitumikia shauri la Mungu katika kizazi chake, alilala, akawekwa pamoja na baba zake, akaona uharibifu.
1 Rois 2.10 Actes 2.29 Actes 13.22 2 Samuel 7.12 1 Chroniques 15.25-15.29
37 Bali huyu aliyefufuliwa na Mungu hakuona uharibifu.
Actes 13.30 Actes 2.24
38 Basi, na ijulikane kwenu, ndugu zangu, ya kuwa kwa huyo mnahubiriwa msamaha wa dhambi;
Luc 24.47 2 Corinthiens 5.18-5.21 Actes 5.31 1 Jean 2.12 Actes 2.38
39 na kwa yeye kila amwaminiye huhesabiwa haki katika mambo yale yote asiyoweza kuhesabiwa haki kwa torati ya Musa.
Galates 2.16 Romains 8.3 Romains 10.4 Hébreux 7.19 Romains 10.10
40 Angalieni, basi, isiwajilie habari ile iliyonenwa katika manabii.
Habakuk 1.5 Malachie 4.1 Malachie 3.2 Hébreux 3.12 Esaïe 29.14
41 Tazameni, enyi mnaodharau, kastaajabuni, mkatoweke; kwa kuwa natenda kazi mimi siku zenu, kazi ambayo msingeisadiki kabisa, ijapo mtu akiwasimulia sana.
Habakuk 1.5 Actes 13.47 Hébreux 10.28-10.30 Romains 11.7-11.14 1 Pierre 4.17
42 Na walipokuwa wakitoka, wakawasihi waambiwe maneno haya sabato ya pili.
Actes 10.33 Actes 13.14 Actes 28.28 Matthieu 19.30 Ezéchiel 3.6
43 Sinagogi ilipofumukana, Wayahudi na waongofu watauwa wengi wakashikamana na Paulo na Barnaba; ambao, wakisema nao, wakawatia moyo kudumu katika neema ya Mungu.
Actes 11.23 Actes 14.22 Actes 6.5 Hébreux 12.15 Philippiens 3.16
44 Hata sabato ya pili, watu wengi, karibu mji wote, wakakusanyika walisikie neno la Mungu.
Esaïe 60.8 Genèse 49.10 Psaumes 110.3 Esaïe 11.10
45 Bali Wayahudi, walipowaona makutano, wakajaa wivu, wakayakanusha maneno yaliyonenwa na Paulo, wakibisha na kutukana.
Jude 1.10 Actes 18.6 Actes 19.9 Actes 5.17 1 Thessaloniciens 2.16
46 Paulo na Barnaba wakanena kwa ushujaa wakasema, Ilikuwa lazima neno la Mungu linenwe kwenu kwanza; lakini kwa kuwa mnalisukumia mbali, na kujiona nafsi zenu kuwa hamkustahili uzima wa milele, angalieni, twawageukia Mataifa.
Actes 28.28 Actes 3.26 Actes 26.20 Actes 22.21 Actes 13.26
47 Kwa sababu ndivyo tulivyoamriwa na Bwana, Nimekuweka uwe nuru ya Mataifa, Upate kuwa wokovu hata mwisho wa dunia.
Esaïe 49.6 Esaïe 42.6 Luc 2.32 Esaïe 45.22 Actes 1.8
48 Mataifa waliposikia hayo wakafurahi, wakalitukuza neno la Bwana, nao waliokuwa wamekusudiwa uzima wa milele wakaamini.
Romains 8.29-8.30 Romains 11.7 Jean 10.16 Jean 11.52 Romains 15.9-15.12
49 Neno la Bwana likaenea katika nchi ile yote.
Actes 19.26 Actes 9.42 Actes 12.24 Actes 19.10 Philippiens 1.13-1.14
50 Lakini Wayahudi wakawafitinisha wanawake watauwa wenye cheo na wakuu wa mji, wakawataharakisha watu wawaudhi Paulo na Barnaba; wakawatoa katika mipaka yao.
Actes 14.2 Actes 14.19 Actes 21.27 Actes 13.45 2 Timothée 3.11
51 Nao wakawakung’utia mavumbi ya miguu yao, wakaenda Ikonio.
Matthieu 10.14 Actes 14.21 Actes 18.6 Actes 14.19 Luc 9.5
52 Na wanafunzi walijaa furaha na Roho Mtakatifu.
Actes 2.4 1 Thessaloniciens 1.6 Matthieu 5.12 Romains 5.3 1 Pierre 4.13

Cette Bible est dans le domaine public.