Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Luc 8.12
Bible en Swahili de l’est


1 Ikawa baada ya hayo alikuwa akizunguka-zunguka katika miji na vijiji akihubiri na kuitangaza habari njema ya ufalme wa Mungu; na wale Thenashara walikuwa pamoja naye,
Matthieu 4.23 Matthieu 9.35 Matthieu 13.19 Matthieu 10.2-10.4 Luc 4.43-4.44
2 na wanawake kadha wa kadha ambao walikuwa na pepo wabaya na magonjwa wakaponywa; nao ni Mariamu aitwaye Magdalene aliyetokwa na pepo saba,
Matthieu 27.55-27.56 Marc 15.40-15.41 Marc 16.9 Actes 1.14 Jean 19.25
3 na Yoana mkewe Kuza, wakili wake Herode, na Susana, na wengine wengi, waliokuwa wakimhudumia kwa mali zao.
Luc 24.10 1 Timothée 5.10 Matthieu 25.40 Matthieu 2.11 Actes 13.1

Le semeur et les terrains

4 Mkutano mkuu ulipokutanika, na wale waliotoka kila mji wakimjia, alisema kwa mfano;
Marc 4.1-4.9 Matthieu 13.2-13.9
5 Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake; naye alipokuwa akizipanda, nyingine zilianguka karibu na njia, zikakanyagwa, ndege wa angani wakazila.
Jacques 1.23-1.24 Matthieu 13.37 Marc 4.15 Psaumes 119.118 Matthieu 13.3-13.4
6 Nyingine zikaanguka penye mwamba; zilipoanza kumea zikakauka kwa kukosa rutuba.
Marc 4.5-4.6 Hébreux 3.7-3.8 Luc 8.13 Romains 2.4-2.5 Hébreux 3.15
7 Nyingine zikaanguka kati ya miiba, na miiba ikamea pamoja nazo ikazisonga.
Jérémie 4.3 Marc 4.7 Luc 21.34 Matthieu 13.22 Genèse 3.18
8 Nyingine zikaanguka penye udongo mzuri; zikamea, zikazaa moja kwa mia. Alipokuwa akinena hayo alipaza sauti akisema, Mwenye masikio ya kusikilia, na asikie.
Matthieu 11.15 Apocalypse 2.7 Apocalypse 2.11 Genèse 26.12 Marc 4.8
9 Wanafunzi wake wakamwuliza, Maana yake nini mfano huo?
Marc 4.10 Matthieu 13.10 Matthieu 13.18 Jean 15.15 Marc 4.34
10 Akasema, Ninyi mmepewa kuzijua siri za ufalme wa Mungu; bali wengine kwa mifano, ili wakiona wasione, na wakisikia wasielewe.
Esaïe 6.9 Marc 4.11 Matthieu 11.25 Matthieu 13.11-13.17 Esaïe 44.18
11 Na huo mfano, maana yake ni hii; Mbegu ni neno la Mungu.
Jacques 1.21 Matthieu 13.19 Marc 4.14-4.20 1 Corinthiens 3.6-3.7 1 Pierre 1.23-1.25
12 Wale wa karibu na njia ndio wasikiao, kisha huja Ibilisi akaliondoa hilo neno mioyoni mwao, wasije wakaamini na kuokoka.
Apocalypse 12.9 2 Thessaloniciens 2.9-2.14 Marc 4.15 Proverbes 1.24-1.26 Luc 8.5
13 Na wale penye mwamba ndio wale ambao wasikiapo hulipokea lile neno kwa furaha; nao hawana mizizi, huamini kitambo kidogo, na wakati wa kujaribiwa hujitenga.
Osée 6.4 Marc 6.20 Esaïe 58.2 Ezéchiel 33.32 Proverbes 12.12
14 Na zilizoanguka penye miiba ni wale waliosikia, na katika kuenenda kwao husongwa na shughuli na mali, na anasa za maisha haya, wasiivishe lo lote.
1 Timothée 6.17 Matthieu 13.22 1 Timothée 6.9-6.10 Marc 4.19 Matthieu 6.24-6.25
15 Na zile penye udongo mzuri, ndio wale ambao kwa unyofu na wema wa mioyo yao hulisikia neno, na kulishika; kisha huzaa matunda kwa kuvumilia.
Colossiens 1.10 Colossiens 1.6 Hébreux 10.36 1 Jean 2.3 Romains 6.22
16 Hakuna mtu ambaye akiisha washa taa huifunika kwa chombo, au kuiweka mvunguni, bali huiweka juu ya kiango, ili waingiao wapate kuona nuru yake.
Luc 11.33 Marc 4.21-4.22 Philippiens 2.15-2.16 Matthieu 5.15-5.16 Apocalypse 11.4
17 Kwa maana hakuna neno lililositirika ambalo halitafunuliwa; wala lililofichwa ambalo halitajulikana na kutokea wazi.
Matthieu 10.26 Luc 12.2-12.3 Ecclésiaste 12.14 1 Corinthiens 4.5 Marc 4.22
18 Jiangalieni basi jinsi msikiavyo; kwa kuwa mwenye kitu atapewa, na yule asiye na kitu atanyang’anywa hata kile ambacho anadhaniwa kuwa nacho.
Matthieu 13.12 Luc 19.26 Matthieu 25.29 1 Corinthiens 14.37 Luc 9.44
19 Wakamwendea mama yake na ndugu zake, wasiweze kumkaribia kwa sababu ya mkutano.
Matthieu 12.46-12.50 Marc 3.31-3.35 Marc 3.21
20 Akaletewa habari akiambiwa, Mama yako na ndugu zako wamesimama nje wakitaka kuonana nawe.
1 Corinthiens 9.5 Actes 1.14 Jean 7.3-7.6 Marc 6.3 Matthieu 13.55-13.56
21 Akawajibu akasema, Mama yangu na ndugu zangu ndio hao walisikiao neno la Mungu na kulifanya.
Jean 13.17 Jacques 1.22 Luc 8.15 Matthieu 25.40 Matthieu 7.21-7.26

Jésus, plus fort que la nature et les démons

22 Ikawa siku zile mojawapo alipanda chomboni yeye na wanafunzi wake, akawaambia, Na tuvuke mpaka ng’ambo ya ziwa. Wakatweka matanga.
Matthieu 8.23-8.27 Luc 5.1 Jean 6.1 Luc 8.23 Marc 5.21
23 Nao walipokuwa wakienda, alilala usingizi. Ikashuka tufani juu ya ziwa, chombo kikaanza kujaa maji, wakawa katika hatari.
Psaumes 124.2-124.4 Hébreux 4.15 Psaumes 44.23 Luc 8.22 Esaïe 54.11
24 Wakamwendea, wakamwamsha, wakisema, Bwana mkubwa, Bwana mkubwa, tunaangamia. Akaamka, akaukemea upepo na msukosuko wa maji, vikakoma; kukawa shwari.
Psaumes 65.7 Luc 4.39 2 Corinthiens 1.9-1.10 Psaumes 69.1-69.2 Luc 5.5
25 Akawaambia, Imani yenu iko wapi? Wakaogopa, wakamaka, wakisema wao kwa wao, Ni nani huyu basi hata anaamuru upepo na maji, navyo vyamtii?
Matthieu 6.30 Job 38.8-38.10 Matthieu 17.20 Proverbes 30.4 Marc 4.40-4.41
26 Wakafika pwani ya nchi ya Wagerasi, inayoelekea Galilaya.
Matthieu 8.28-8.34 Marc 5.1-5.20
27 Naye aliposhuka pwani, alikutana na mtu mmoja wa mji ule, mwenye pepo, hakuvaa nguo siku nyingi, wala hakukaa nyumbani, ila makaburini.
Marc 5.2-5.5 Nombres 19.16 1 Samuel 19.24 Esaïe 65.4
28 Alipomwona Yesu alipiga kelele, akaanguka mbele yake, akasema kwa sauti kuu, Nina nini nawe, Yesu, Mwana wa Mungu aliye juu? Nakusihi usinitese.
Matthieu 8.29 Esaïe 27.1 1 Jean 3.8 Marc 5.6-5.8 Marc 1.24-1.27
29 Kwa kuwa amemwamuru yule pepo mchafu amtoke mtu yule. Maana amepagawa naye mara nyingi, hata alilindwa kifungoni na kufungwa minyororo na pingu; akavikata vile vifungo, akakimbizwa jangwani kwa nguvu za yule pepo.
2 Timothée 2.25-2.26 Marc 5.3-5.5 Luc 9.39 Luc 9.42 Actes 19.12-19.16
30 Yesu akamwuliza, Jina lako nani? Akasema, Jina langu ni Jeshi; kwa sababu pepo wengi wamemwingia.
Matthieu 26.53 Marc 16.9 Marc 5.9 Luc 8.2 Matthieu 8.29
31 Wakamsihi asiwaamuru watoke kwenda shimoni.
Apocalypse 9.1-9.2 Job 2.5 Apocalypse 11.7 Apocalypse 19.20 Job 1.11
32 Basi, hapo palikuwa na kundi la nguruwe wengi wakilisha mlimani; wakamsihi awape ruhusa kuwaingia wale. Akawapa ruhusa.
Esaïe 65.4 Esaïe 66.3 Job 1.10 1 Jean 4.4 Psaumes 62.11
33 Pepo wakamtoka mtu yule wakawaingia nguruwe, nalo kundi lilitelemka gengeni kwa kasi, wakaingia ziwani, wakafa maji.
Luc 8.22-8.23 Jean 8.44 Apocalypse 9.11 1 Pierre 5.8
34 Wachungaji walipoona lililotokea walikimbia, wakaieneza habari mjini na mashambani.
Matthieu 8.33 Matthieu 28.11 Actes 19.16-19.17 Marc 5.14
35 Watu wakatoka kwenda kuliona lililotokea, wakamwendea Yesu, wakamwona mtu yule aliyetokwa na pepo ameketi miguuni pa Yesu, amevaa nguo, ana akili zake; wakaogopa.
Luc 10.39 Psaumes 51.10 Luc 8.27 Esaïe 53.12 Luc 15.17
36 Na wale waliokuwa wameona waliwaeleza jinsi alivyoponywa yule aliyepagawa na pepo.
Matthieu 4.24
37 Na jamii ya watu wa nchi ya Wagerasi iliyo kando kando walimwomba aondoke kwao, kwa kuwa walishikwa na hofu nyingi; basi akapanda chomboni, akarudi.
Actes 16.39 Luc 5.8 1 Rois 17.18 Matthieu 8.34 Marc 5.17
38 Na mtu yule aliyetokwa na pepo alimwomba ruhusa afuatane naye; lakini yeye alimwaga akisema,
Marc 5.18-5.20 Philippiens 1.23 Psaumes 107.31-107.32 Psaumes 145.3-145.12 Psaumes 32.7
39 Rudi nyumbani kwako, ukahubiri yalivyo makuu Mungu aliyokutendea. Akaenda zake, akihubiri katika mji wote, yalivyo makuu mambo aliyotendewa na Yesu.
Psaumes 66.16 Daniel 4.1-4.3 Marc 1.45 Daniel 4.34-4.37 Psaumes 126.2-126.3

Guérison d’une femme et résurrection d’une fillette

40 Basi Yesu aliporudi mkutano ulimkaribisha kwa furaha, maana walikuwa wakimngojea wote.
Marc 5.21 Matthieu 9.1 Jean 5.35 Proverbes 8.34 Actes 10.33
41 Na tazama, mtu mmoja akaja, jina lake Yairo, naye ni mtu mkuu wa sinagogi, akaanguka miguuni pa Yesu, akamsihi aingie nyumbani kwake;
Marc 5.22-5.43 Actes 18.8 Actes 13.15 Actes 18.17 Luc 13.14
42 kwa kuwa binti yake yu katika kufa, ambaye ni mwana pekee, umri wake amepata miaka kumi na miwili. Na alipokuwa akienda makutano walimsonga.
Luc 7.12 Luc 8.45 Psaumes 103.15-103.16 Job 1.18-1.19 Job 4.20
43 Na mwanamke mmoja, ambaye ametokwa na damu muda wa miaka kumi na miwili, [aliyekuwa amegharimiwa mali zake zote kwa kuwapa waganga] asipate kuponywa na mtu ye yote,
Matthieu 9.20-9.22 Actes 3.2 Marc 5.25-5.26 Job 13.4 Psaumes 108.12
44 alikwenda nyuma yake, akaugusa upindo wa vazi lake; na mara hiyo kutoka damu kwake kulikoma.
Deutéronome 22.12 Marc 5.27-5.28 Actes 5.15 Exode 15.26 Malachie 4.2
45 Yesu akasema, Ni nani aliyenigusa? Basi, watu wote walipokana, Petro alimwambia, Bwana mkubwa, makutano haya wanakuzunguka na kukusonga.
Luc 5.5 Marc 5.30-5.32 Luc 9.13
46 Yesu akasema, Mtu alinigusa, maana naona ya kuwa nguvu zimenitoka.
Luc 6.19 Luc 5.17 1 Pierre 2.9
47 Yule mwanamke, alipoona ya kwamba hawezi kusitirika akaja akitetemeka, akaanguka mbele yake, akamweleza mbele ya watu wote sababu yake ya kumgusa, na jinsi alivyoponywa mara.
Marc 5.33 1 Corinthiens 2.3 Hébreux 12.28 2 Corinthiens 7.15 Habakuk 3.16
48 Akamwambia Binti, imani yako imekuponya; enenda zako na amani.
Matthieu 9.22 Hébreux 4.2 Luc 7.50 Marc 5.34 Luc 17.19
49 Alipokuwa akinena hayo, alikuja mtu kutoka nyumbani kwa yule mkuu wa sinagogi, akamwambia, Binti yako amekwisha kufa; usimsumbue mwalimu.
Luc 7.6 Esaïe 7.12 Luc 8.41-8.43 Marc 5.35-5.43 Matthieu 9.23-9.26
50 Lakini Yesu aliposikia hayo, alimjibu, Usiwe na hofu, amini tu, naye ataponywa.
Marc 5.36 Jean 11.40 Romains 4.20 Jean 11.25 Luc 8.48
51 Alipofika nyumbani hakuacha mtu kuingia pamoja naye ila Petro, na Yohana, na Yakobo, na babaye yule mtoto na mamaye.
Esaïe 42.2 Luc 9.28 Matthieu 6.5-6.6 2 Rois 4.4-4.6 Marc 14.33
52 Na watu wote walikuwa wakilia na kumwombolezea; akasema, Msilie, hakufa huyu, bali amelala usingizi tu.
Luc 23.27 Jean 11.4 Genèse 27.34-27.35 Matthieu 11.17 Genèse 23.2
53 Wakamcheka sana, maana walijua ya kuwa amekwisha kufa.
Jean 11.39 Marc 15.44-15.45 Job 17.2 Luc 16.14 Psaumes 22.7
54 Akamshika mkono, akapaza sauti, akisema Kijana, inuka.
Marc 1.31 Jean 11.43 Romains 4.17 Luc 8.51 Marc 8.23
55 Roho yake ikamrejea, naye mara hiyo akasimama. Akaamuru apewe chakula.
Jean 11.44 1 Rois 17.21-17.23 Marc 5.43 Luc 24.41-24.43
56 Wazazi wake wakastaajabu sana, lakini akawakataza wasimwambie mtu lililotukia.
Matthieu 8.4 Marc 5.42-5.43 Luc 5.14 Matthieu 9.30

Cette Bible est dans le domaine public.