Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 28.45
Bible en Swahili de l’est


Bénédictions en perspective

1 Itakuwa utakaposikia sauti ya Bwana, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo Bwana, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani;
Exode 23.22 Lévitique 26.3-26.13 Exode 15.26 Esaïe 1.19 Deutéronome 7.12-7.26
2 na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya Bwana, Mungu wako.
Zacharie 1.6 Deutéronome 28.15 Deutéronome 28.45 1 Timothée 4.8
3 Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani.
Genèse 39.5 Aggée 2.19 Zacharie 8.3-8.5 Psaumes 144.12-144.15 Esaïe 65.21-65.23
4 Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako.
Deutéronome 7.13 Genèse 49.25 Proverbes 10.22 1 Timothée 4.8 Proverbes 20.7
5 Litabarikiwa kapu lako, na chombo chako cha kukandia unga.
6 Utabarikiwa uingiapo, utabarikiwa na utokapo.
Psaumes 121.8 Nombres 27.17 2 Samuel 3.25 2 Chroniques 1.10 Deutéronome 31.2
7 Bwana atawafanya adui zako wainukao juu yako kupigwa mbele yako; watakutokea kwa njia moja, lakini watakimbia mbele yako kwa njia saba.
2 Samuel 22.38-22.41 Deutéronome 28.25 Lévitique 26.7-26.8 2 Chroniques 20.22-20.25 1 Samuel 7.3-7.4
8 Bwana ataiamuru baraka ije juu yako katika ghala zako, na mambo yote utakayotia mkono wako; naye atakubarikia katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako.
Deutéronome 15.10 Lévitique 25.21 Malachie 3.10-3.11 Luc 12.18 Lévitique 26.10
9 Bwana atakuweka uwe taifa takatifu kwake, kama alivyokuapia; utakaposhika maagizo ya Bwana, Mungu wako, na kutembea katika njia zake.
Exode 19.5-19.6 Deutéronome 26.18-26.19 Deutéronome 7.6 Deutéronome 13.17 1 Pierre 5.10
10 Na mataifa yote ya duniani watakuona umeitwa kwa jina la Bwana, nao watakuwa na hofu kwako.
2 Chroniques 7.14 Nombres 6.27 Deutéronome 11.25 1 Samuel 18.12-18.15 1 Chroniques 14.17
11 Bwana atakufanya uwe na wingi wa uheri, katika uzao wa tumbo lako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, na uzao wa nchi yako, katika nchi Bwana aliyowaapia baba zako kwamba atakupa.
Proverbes 10.22 Deutéronome 30.9 Deutéronome 28.4 Psaumes 132.11 Lévitique 26.9
12 Atakufunulia Bwana hazina yake nzuri, nayo ni mbingu, kwa kutoa mvua ya nchi yako kwa wakati wake, na kwa kubarikia kazi yote ya mkono wako; nawe utakopesha mataifa mengi, wala hutakopa wewe.
Deutéronome 14.29 Deutéronome 15.6 Joël 2.23-2.24 Deutéronome 11.14 Lévitique 26.4
13 Bwana atakufanya kuwa kichwa, wala si mkia; nawe utakuwa juu tu, wala huwi chini; utakapoyasikiza maagizo ya Bwana, Mungu wako, nikuagizayo hivi leo, kuyaangalia na kufanya;
Deutéronome 28.1 Deutéronome 4.6-4.9 Esaïe 9.14-9.15
14 msipokengeuka katika maneno niwaamuruyo leo kwa lo lote, kwenda mkono wa kuume wala wa kushoto, kwa kuifuata miungu mingine na kuitumikia.
Deutéronome 5.32 Deutéronome 11.16 2 Rois 22.2 Deutéronome 11.26-11.28 Proverbes 4.26-4.27

Malédictions en perspective

15 Lakini itakuwa usipotaka kuisikiza sauti ya Bwana, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata.
Malachie 2.2 Deutéronome 28.2 Lamentations 2.17 Galates 3.10 Romains 2.8-2.9
16 Utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani.
Lamentations 4.1-4.13 Malachie 4.6 Jérémie 26.6 Jérémie 14.2-14.5 Jérémie 14.18
17 Litalaaniwa kapu lako na chombo chako cha kukandia.
Deutéronome 28.5 Malachie 2.2 Luc 16.25 Aggée 1.6 Zacharie 5.3-5.4
18 Utalaaniwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako.
Deutéronome 28.4 Job 18.16-18.19 Malachie 2.3 Osée 9.11-9.14 Lamentations 2.20
19 Utalaaniwa uingiapo, utalaaniwa na utokapo,
Deutéronome 28.6 Juges 5.6-5.7 2 Chroniques 15.5
20 Bwana atakuletea laana na mashaka, na kukemewa, katika yote utakayotia mkono wako kuyafanya, hata uangamie na kupotea kwa upesi; kwa ule uovu wa matendo yako, uliyoniacha kwayo.
Esaïe 66.15 Malachie 2.2 Esaïe 51.20 Deutéronome 4.26 Josué 23.16
21 Bwana atakuambatanisha na tauni, hata atakapokwisha kukuondoa katika nchi uingiayo kwa kuimiliki.
Lévitique 26.25 Jérémie 24.10 Nombres 14.12 2 Samuel 24.15 Nombres 16.46-16.49
22 Bwana atakupiga kwa kifua kikuu, na kwa homa, na kwa kuwashwa, na kwa hari ya moto, na kwa upanga, na kwa ukaufu, na kwa koga; navyo vitakufukuza hata uangamie.
Lévitique 26.16 Amos 4.9 1 Rois 8.37 Aggée 2.17 2 Chroniques 6.28
23 Na mbingu zako zilizo juu ya kichwa chako zitakuwa shaba, na nchi iliyo chini yako itakuwa chuma.
Lévitique 26.19 1 Rois 18.2 Amos 4.7 1 Rois 17.1 Jérémie 14.1-14.6
24 Bwana atafanya mvua ya nchi yako iwe vumbi na mchanga; itakujilia juu yako kutoka mbinguni hata uangamie.
Deutéronome 28.12 Amos 4.11 Job 18.15-18.21 Esaïe 5.24 Genèse 19.24
25 Bwana atakufanya upigwe mbele ya adui zako; utawatokea juu yao kwa njia moja, lakini utakimbia mbele yao kwa njia saba; nawe utatupwa huko na huko katika falme zote za duniani.
Esaïe 30.17 Ezéchiel 23.46 Jérémie 24.9 Deutéronome 28.7 Lévitique 26.17
26 Na mzoga wako utakuwa chakula cha ndege wote wa angani, na wanyama wote wa duniani, pasiwe na mtu wa kuwafukuza.
Jérémie 16.4 Jérémie 7.33 Jérémie 34.20 Jérémie 19.7 1 Samuel 17.44-17.46
27 Bwana atakupiga kwa majipu ya Misri, na kwa bawasiri, na kwa pele, na kwa kujikuna, ambayo hupati kupoa.
1 Samuel 5.6 Exode 15.26 Deutéronome 28.35 Lévitique 21.20 Exode 9.9
28 Bwana atakupiga kwa wazimu, na kwa upofu, na kwa bumbuazi la moyoni;
Esaïe 6.9-6.10 Esaïe 19.11-19.17 Psaumes 60.3 Jérémie 4.9 Luc 21.25-21.26
29 utakwenda kwa kupapasa-papasa mchana, kama apapasavyo kipofu gizani, wala hufanikiwi katika njia zako; nawe sikuzote utaonewa na kutekwa nyara, wala hapatakuwa na mtu wa kukuokoa.
Esaïe 59.10 Job 5.14 Juges 10.8 Psaumes 106.40-106.42 Juges 3.14
30 Utaposa mke na mume mwingine atalala naye; utajenga nyumba usiikae; utapanda mizabibu usitumie matunda yake.
Amos 5.11 Jérémie 8.10 Job 31.10 Sophonie 1.13 Deutéronome 20.6-20.7
31 Ng’ombe wako atachinjwa mbele ya macho yako, usile nyama yake; utanyang’anywa punda wako mbele ya uso wako kwa jeuri, usirudishiwe; kondoo zako watapewa adui zako, usipate mtu wa kukuokoa.
Juges 6.1 Job 1.14-1.15
32 Wanao na binti zako litapewa taifa lingine, na macho yako yataangalia, na kuzimia kwa kuwatamani mchana kutwa; wala hapatakuwa na kitu katika uwezo wa mkono wako.
Deutéronome 28.41 2 Chroniques 29.9 Joël 3.6 Néhémie 5.2-5.5 Nombres 21.29
33 Matunda ya nchi yako, na taabu yako yote, vitaliwa na taifa usilolijua; utaonewa tu, na kupondwa chini daima;
Jérémie 5.17 Lévitique 26.16 Jérémie 4.17 Esaïe 1.7 Néhémie 9.36-9.37
34 hata uwe mwenye wazimu kwa yaonwayo na macho yako, utakayoyaona.
Deutéronome 28.68 Apocalypse 16.10-16.11 Esaïe 33.14 Deutéronome 28.28 Jérémie 25.15-25.16
35 Bwana atakupiga magoti na miguu kwa jipu lililo zito, usilopata kupozwa, tokea wayo wa mguu mpaka utosi wa kichwa.
Deutéronome 28.27 Esaïe 3.24 Esaïe 3.17 Job 2.6-2.7 Esaïe 1.6
36 Bwana atakupeleka wewe, na mfalme wako utakayemweka juu yako, kwa taifa usilolijua wewe wala baba zako; nawe huko utatumikia miungu mingine ya miti na mawe.
2 Rois 25.11 Jérémie 16.13 Deutéronome 4.28 2 Chroniques 36.20 2 Chroniques 36.6
37 Nawe utakuwa ushangao, na mithali, na dharau, kati ya mataifa yote huko atakakokuongoza Bwana.
1 Rois 9.7-9.8 Jérémie 24.9 Jérémie 25.9 2 Chroniques 7.20 Joël 2.17
38 Mbegu nyingi utazichukua nje shambani, lakini utavuna haba, kwa kuwa nzige watazila.
Aggée 1.6 Michée 6.15 Joël 1.4 Joël 2.25 Joël 2.3
39 Utapanda mizabibu na kuitengeza, wala hutakunywa katika divai yake, wala kuichuma kwani italiwa na mabuu.
Esaïe 5.10 Esaïe 17.10-17.11 Joël 1.4-1.7 Joël 2.2-2.4 Jonas 4.7
40 Utakuwa na mizeituni katika mipaka yako yote usijipake mafuta yake; kwa kuwa mzeituni wako utapukutika.
Michée 6.15 Psaumes 23.5 Psaumes 104.15
41 Utazaa wana na binti, lakini hawatakuwa wako wewe; kwa sababu watakwenda utumwani.
Deutéronome 28.32 Lamentations 1.5 2 Rois 24.14
42 Miti yako yote, na mazao ya nchi yako, nzige watakuwa nayo.
Amos 7.1-7.2 Deutéronome 28.38-28.39
43 Mgeni aliye kati yako atazidi kupaa juu yako; nawe utazidi kushuka chini.
Deutéronome 28.13 1 Samuel 13.19-13.23 Juges 15.11-15.12 Juges 14.4 Jean 18.31
44 Yeye atakukopesha, wala wewe usimkopeshe; yeye atakuwa ni kichwa, wewe utakuwa mkia.
Deutéronome 28.12-28.13 Lamentations 1.5
45 Na laana hizi zote zitakujilia juu yako, zitakuandama na kukupata, hata uangamizwe, kwa kuwa hukuisikiza sauti ya Bwana, Mungu wako, kushika maagizo yake na amri zake alizokuagiza;
Deutéronome 28.15 Jérémie 7.22-7.25 Ezéchiel 14.21 Esaïe 1.20 Deutéronome 28.5
46 nazo zitakuwa juu yako kwa ishara na ajabu, na juu ya uzao wako milele;
Esaïe 8.18 Ezéchiel 14.8 1 Corinthiens 10.11 Ezéchiel 23.32-23.33 Deutéronome 28.59
47 kwa kuwa hukumtumikia Bwana, Mungu wako, kwa furaha na moyo wa kushukuru, kwa ajili ya ule wingi wa vitu vyote;
Deutéronome 16.11 Deutéronome 32.13-32.15 1 Timothée 6.17-6.19 Néhémie 9.35-9.37 Deutéronome 12.7-12.12
48 kwa hiyo utawatumikia adui zako atakaowaleta Bwana juu yako, kwa njaa, na kwa kiu, na kwa uchi, na kwa uhitaji wa vitu vyote; naye atakuvika kongwa la chuma shingoni mwako, hata atakapokwisha kukuangamiza.
Jérémie 28.13-28.14 Ezéchiel 17.12 Matthieu 11.29 Jérémie 27.12-27.13 Jérémie 17.4
49 Bwana atakuletea taifa juu yako kutoka mbali, kutoka ncha ya dunia, kama arukavyo tai; taifa usiloufahamu ulimi wake;
Lamentations 4.19 Osée 8.1 Esaïe 5.26-5.30 Jérémie 48.40 Jérémie 49.22
50 taifa lenye uso mkali, ambalo haliangalii uso wa mzee, wala halipendelei kijana;
Esaïe 47.6 2 Chroniques 36.17 Proverbes 7.13 Daniel 8.23 Luc 21.23-21.24
51 naye atakula uzao wa ng’ombe wako wa mifugo, na uzao wa nchi yako mpaka utakapokwisha kuangamizwa; wala hatakuachia nafaka, wala divai, wala mafuta, wala maongeo ya ng’ombe wako, wala wana-kondoo wako, hata atakapokwisha kukuangamiza.
Deutéronome 28.33 Esaïe 62.8 Jérémie 15.13 Ezéchiel 12.19 Jérémie 17.3
52 Naye atakuhusuru katika malango yako yote, hata kuta zako ndefu, zenye maboma, ulizokuwa ukiziamini, zishuke, katika nchi yako yote kila upande; naye atakuhusuru katika malango yako yote kila upande, katika nchi yako yote aliyokupa Bwana, Mungu wako.
Luc 19.43-19.44 2 Rois 18.13 Luc 21.20-21.24 Daniel 9.26 2 Rois 17.1-17.6
53 Nawe utakula uzao wa tumbo lako mwenyewe, nyama ya wana wako na binti zako aliokupa Bwana, Mungu wako; katika mazingirwa na katika mkazo utakaokazwa na adui zako.
Lamentations 2.20 Lamentations 4.10 Lévitique 26.29 Jérémie 19.9 2 Rois 6.28-6.29
54 Mtu mume kati yenu aliye mwororo na laini sana, jicho lake litakuwa ovu juu ya nduguye, na juu ya mke wa kifuani mwake, na juu ya masalio ya wanawe waliosalia naye;
Deutéronome 13.6 Deutéronome 15.9 Proverbes 28.22 Matthieu 7.9-7.11 Esaïe 49.15
55 hata asitake wao mmojawapo apewe katika nyama ya wanawe atakaowala, kwa kuwa hana kitu kilichomsalia kwake; katika mazingirwa na mkazo utakaokazwa na adui yako katika malango yako yote.
Jérémie 52.6 Jérémie 5.10 Jérémie 34.2
56 Mwanamke kati yenu aliye mwororo na laini, ambaye hangehatirisha kuweka wayo wa mguu wake nchi kwa umalidadi na ulaini, jicho lake huyu litakuwa ovu juu ya mume wa kifuani mwake, na juu ya mwanawe, na juu ya binti yake,
Deutéronome 28.54 Esaïe 3.16 Lamentations 4.3-4.6
57 na juu ya mchanga wake atokaye katikati ya miguu yake, na juu ya wanawe atakaowazaa; kwa kuwa atawala kwa siri, kwa uhitaji wa vitu vyote; katika mazingirwa na mkazo utakaokazwa na adui yako katika malango yako.
Genèse 49.10 Esaïe 49.15
58 Kama hutaki kutunza kufanya maneno yote ya torati hii yaliyoandikwa katika kitabu hiki, upate kulicha jina hili la fahari na utisho, Bwana, MUNGU WAKO;
Esaïe 42.8 Exode 20.2 Néhémie 9.5 Jérémie 7.26-7.28 Exode 34.5-34.7
59 ndipo atakapofanya Bwana mapigo yako yawe ya ajabu, na mapigo ya uzao wako, mapigo makubwa kwa kweli, ya kudumu sana, na magonjwa mazito ya kudumu sana.
Lamentations 1.12 Deutéronome 32.22 1 Rois 16.3-16.4 Daniel 9.12 Marc 13.19
60 Naye atakurejezea maradhi yote ya Misri juu yako uliyokuwa ukiyaogopa, nayo yataambatana nawe.
Deutéronome 7.15 Exode 15.26 Deutéronome 28.27
61 Tena kila ugonjwa, na kila pigo yasiyoandikwa katika kitabu cha torati hii, atakutia nayo Bwana juu yako, hata utakapokwisha kuangamizwa.
Deutéronome 4.25-4.26
62 Nanyi mtasalia wachache kwa hesabu, ninyi mliokuwa mfano wa nyota za mbinguni kwa wingi; kwa kuwa hukuisikiza sauti ya Bwana, Mungu wako.
Deutéronome 4.27 Deutéronome 10.22 Néhémie 9.23 Jérémie 42.2 Néhémie 7.4
63 Tena itakuwa, kama vile alivyokuwa akifurahi Bwana juu yenu kwa kuwatendea mema na kuwafanya kuwa wengi, ndivyo atakavyofurahi Bwana juu yenu kwa kuwapoteza na kuwaangamiza; nanyi mtanyakuliwa katika hiyo nchi mwingiayo kuimiliki.
Proverbes 1.26 Jérémie 32.41 Esaïe 1.24 Ezéchiel 5.13 Sophonie 3.17
64 Bwana atakutawanya katika mataifa yote, tokea ncha hii ya dunia hata ncha hii ya dunia; nawe huko utatumikia miungu mingine usiyoijua wewe wala baba zako, nayo ni miti na mawe.
Lévitique 26.33 Deutéronome 4.27-4.28 Néhémie 1.8 Jérémie 16.13 Deutéronome 28.36
65 Wala katika mataifa hayo hutapata raha iwayo yote, wala hutakuwa na kituo cha wayo wa mguu wako; lakini Bwana atakupa huko moyo wa kutetema, na macho ya kuzimia, na roho ya kudhoofika;
Lévitique 26.36 Lévitique 26.16 Amos 9.4 Habakuk 3.16 Ezéchiel 20.32-20.35
66 na uzima wako utakuwa na wasiwasi mbele yako; nawe utakuwa na woga usiku na mchana, wala hutaamini kamwe maisha yako;
Hébreux 10.27 Apocalypse 6.15-6.17 Deutéronome 28.67 Lamentations 1.13
67 asubuhi utasema, Laiti ingekuwa jioni! Na jioni utasema, Laiti ingekuwa asubuhi! Kwa kicho cha moyo wako utakavyokucha, na kuona kwa macho yako utakavyoona.
Deutéronome 28.34 Job 7.3-7.4 Apocalypse 9.6
68 Bwana atakurudisha tena Misri kwa merikebu, kwa njia ambayo nilikuambia, Hutaiona tena po pote; nanyi huko mtajiuza nafsi zenu kwa adui zenu kuwa watumwa na wajakazi, wala hapana atakayewanunua.
Osée 9.3 Jérémie 43.7 Jérémie 44.12 Deutéronome 17.16 Osée 8.13

Cette Bible est dans le domaine public.