Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 28.28
Bible en Swahili de l’est


Bénédictions en perspective

1 Itakuwa utakaposikia sauti ya Bwana, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo Bwana, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya duniani;
Lévitique 26.3-26.13 Exode 15.26 Exode 23.22 Esaïe 1.19 Deutéronome 7.12-7.26
2 na baraka hizi zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya Bwana, Mungu wako.
Zacharie 1.6 Deutéronome 28.15 Deutéronome 28.45 1 Timothée 4.8
3 Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani.
Genèse 39.5 Amos 9.13-9.14 Genèse 26.12 Psaumes 107.36-107.37 Aggée 2.19
4 Utabarikiwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako.
Deutéronome 7.13 Genèse 49.25 Proverbes 10.22 Psaumes 128.3 Genèse 22.17
5 Litabarikiwa kapu lako, na chombo chako cha kukandia unga.
6 Utabarikiwa uingiapo, utabarikiwa na utokapo.
Psaumes 121.8 2 Samuel 3.25 2 Chroniques 1.10 Deutéronome 31.2 Nombres 27.17
7 Bwana atawafanya adui zako wainukao juu yako kupigwa mbele yako; watakutokea kwa njia moja, lakini watakimbia mbele yako kwa njia saba.
2 Samuel 22.38-22.41 Deutéronome 28.25 Lévitique 26.7-26.8 2 Chroniques 20.22-20.25 2 Chroniques 14.2-14.6
8 Bwana ataiamuru baraka ije juu yako katika ghala zako, na mambo yote utakayotia mkono wako; naye atakubarikia katika nchi akupayo Bwana, Mungu wako.
Deutéronome 15.10 Lévitique 25.21 Lévitique 26.4-26.5 Malachie 3.10-3.11 Luc 12.18
9 Bwana atakuweka uwe taifa takatifu kwake, kama alivyokuapia; utakaposhika maagizo ya Bwana, Mungu wako, na kutembea katika njia zake.
Exode 19.5-19.6 Deutéronome 13.17 Deutéronome 26.18-26.19 Deutéronome 7.6 1 Pierre 5.10
10 Na mataifa yote ya duniani watakuona umeitwa kwa jina la Bwana, nao watakuwa na hofu kwako.
2 Chroniques 7.14 Deutéronome 11.25 Nombres 6.27 Malachie 3.12 1 Samuel 18.28-18.29
11 Bwana atakufanya uwe na wingi wa uheri, katika uzao wa tumbo lako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo, na uzao wa nchi yako, katika nchi Bwana aliyowaapia baba zako kwamba atakupa.
Deutéronome 30.9 Proverbes 10.22 Deutéronome 28.4 Psaumes 132.11 Lévitique 26.9
12 Atakufunulia Bwana hazina yake nzuri, nayo ni mbingu, kwa kutoa mvua ya nchi yako kwa wakati wake, na kwa kubarikia kazi yote ya mkono wako; nawe utakopesha mataifa mengi, wala hutakopa wewe.
Deutéronome 15.6 Deutéronome 14.29 Deutéronome 11.14 Lévitique 26.4 Joël 2.23-2.24
13 Bwana atakufanya kuwa kichwa, wala si mkia; nawe utakuwa juu tu, wala huwi chini; utakapoyasikiza maagizo ya Bwana, Mungu wako, nikuagizayo hivi leo, kuyaangalia na kufanya;
Deutéronome 28.1 Deutéronome 4.6-4.9 Esaïe 9.14-9.15
14 msipokengeuka katika maneno niwaamuruyo leo kwa lo lote, kwenda mkono wa kuume wala wa kushoto, kwa kuifuata miungu mingine na kuitumikia.
Deutéronome 5.32 Deutéronome 11.16 Proverbes 4.26-4.27 Josué 23.6 Esaïe 30.21

Malédictions en perspective

15 Lakini itakuwa usipotaka kuisikiza sauti ya Bwana, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata.
Malachie 2.2 Deutéronome 28.2 Josué 23.15 Lamentations 2.17 Galates 3.10
16 Utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani.
Lamentations 2.11-2.22 Genèse 8.21-8.22 Jérémie 44.22 1 Rois 17.12 Joël 1.4
17 Litalaaniwa kapu lako na chombo chako cha kukandia.
Deutéronome 28.5 Aggée 1.6 Zacharie 5.3-5.4 Psaumes 69.22 Proverbes 1.32
18 Utalaaniwa uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, maongeo ya ng’ombe wako, na wadogo wa kondoo zako.
Deutéronome 28.4 Luc 23.29-23.30 Psaumes 109.9-109.15 Deutéronome 28.16 Lévitique 26.26
19 Utalaaniwa uingiapo, utalaaniwa na utokapo,
Deutéronome 28.6 Juges 5.6-5.7 2 Chroniques 15.5
20 Bwana atakuletea laana na mashaka, na kukemewa, katika yote utakayotia mkono wako kuyafanya, hata uangamie na kupotea kwa upesi; kwa ule uovu wa matendo yako, uliyoniacha kwayo.
Esaïe 66.15 Malachie 2.2 Esaïe 51.20 Deutéronome 4.26 Esaïe 30.17
21 Bwana atakuambatanisha na tauni, hata atakapokwisha kukuondoa katika nchi uingiayo kwa kuimiliki.
Lévitique 26.25 Jérémie 24.10 Nombres 14.12 Jérémie 16.4 Jérémie 21.6-21.7
22 Bwana atakupiga kwa kifua kikuu, na kwa homa, na kwa kuwashwa, na kwa hari ya moto, na kwa upanga, na kwa ukaufu, na kwa koga; navyo vitakufukuza hata uangamie.
Amos 4.9 Lévitique 26.16 1 Rois 8.37 Aggée 2.17 Jérémie 14.12
23 Na mbingu zako zilizo juu ya kichwa chako zitakuwa shaba, na nchi iliyo chini yako itakuwa chuma.
Lévitique 26.19 Amos 4.7 1 Rois 17.1 Jérémie 14.1-14.6 1 Rois 18.2
24 Bwana atafanya mvua ya nchi yako iwe vumbi na mchanga; itakujilia juu yako kutoka mbinguni hata uangamie.
Deutéronome 28.12 Job 18.15-18.21 Esaïe 5.24 Genèse 19.24 Amos 4.11
25 Bwana atakufanya upigwe mbele ya adui zako; utawatokea juu yao kwa njia moja, lakini utakimbia mbele yao kwa njia saba; nawe utatupwa huko na huko katika falme zote za duniani.
Ezéchiel 23.46 Esaïe 30.17 Jérémie 24.9 Deutéronome 28.7 Lévitique 26.17
26 Na mzoga wako utakuwa chakula cha ndege wote wa angani, na wanyama wote wa duniani, pasiwe na mtu wa kuwafukuza.
Jérémie 7.33 Jérémie 34.20 Jérémie 16.4 Jérémie 19.7 Jérémie 8.1
27 Bwana atakupiga kwa majipu ya Misri, na kwa bawasiri, na kwa pele, na kwa kujikuna, ambayo hupati kupoa.
1 Samuel 5.6 Lévitique 21.20 Exode 9.9 Exode 15.26 Deutéronome 28.35
28 Bwana atakupiga kwa wazimu, na kwa upofu, na kwa bumbuazi la moyoni;
Ezéchiel 4.17 Esaïe 43.19 Actes 13.41 1 Samuel 16.14 Esaïe 6.9-6.10
29 utakwenda kwa kupapasa-papasa mchana, kama apapasavyo kipofu gizani, wala hufanikiwi katika njia zako; nawe sikuzote utaonewa na kutekwa nyara, wala hapatakuwa na mtu wa kukuokoa.
Esaïe 59.10 Job 5.14 Juges 6.1-6.6 Juges 10.8 Psaumes 106.40-106.42
30 Utaposa mke na mume mwingine atalala naye; utajenga nyumba usiikae; utapanda mizabibu usitumie matunda yake.
Amos 5.11 Jérémie 8.10 Job 31.10 Jérémie 12.13 Sophonie 1.13
31 Ng’ombe wako atachinjwa mbele ya macho yako, usile nyama yake; utanyang’anywa punda wako mbele ya uso wako kwa jeuri, usirudishiwe; kondoo zako watapewa adui zako, usipate mtu wa kukuokoa.
Job 1.14-1.15 Juges 6.1
32 Wanao na binti zako litapewa taifa lingine, na macho yako yataangalia, na kuzimia kwa kuwatamani mchana kutwa; wala hapatakuwa na kitu katika uwezo wa mkono wako.
Deutéronome 28.41 Joël 3.6 2 Chroniques 29.9 Lamentations 2.11 Michée 4.10
33 Matunda ya nchi yako, na taabu yako yote, vitaliwa na taifa usilolijua; utaonewa tu, na kupondwa chini daima;
Jérémie 5.17 Deutéronome 28.29-28.30 Deutéronome 28.51 Jérémie 8.16 Lévitique 26.16
34 hata uwe mwenye wazimu kwa yaonwayo na macho yako, utakayoyaona.
Apocalypse 16.10-16.11 Esaïe 33.14 Deutéronome 28.28 Jérémie 25.15-25.16 Deutéronome 28.68
35 Bwana atakupiga magoti na miguu kwa jipu lililo zito, usilopata kupozwa, tokea wayo wa mguu mpaka utosi wa kichwa.
Deutéronome 28.27 Esaïe 3.17 Job 2.6-2.7 Esaïe 1.6 Esaïe 3.24
36 Bwana atakupeleka wewe, na mfalme wako utakayemweka juu yako, kwa taifa usilolijua wewe wala baba zako; nawe huko utatumikia miungu mingine ya miti na mawe.
Deutéronome 4.28 2 Rois 25.11 Jérémie 16.13 2 Chroniques 36.6 2 Chroniques 36.20
37 Nawe utakuwa ushangao, na mithali, na dharau, kati ya mataifa yote huko atakakokuongoza Bwana.
1 Rois 9.7-9.8 Jérémie 24.9 Jérémie 25.9 2 Chroniques 7.20 Psaumes 44.13-44.14
38 Mbegu nyingi utazichukua nje shambani, lakini utavuna haba, kwa kuwa nzige watazila.
Aggée 1.6 Michée 6.15 Joël 1.4 Joël 2.25 Amos 4.9
39 Utapanda mizabibu na kuitengeza, wala hutakunywa katika divai yake, wala kuichuma kwani italiwa na mabuu.
Esaïe 17.10-17.11 Joël 1.4-1.7 Joël 2.2-2.4 Jonas 4.7 Esaïe 5.10
40 Utakuwa na mizeituni katika mipaka yako yote usijipake mafuta yake; kwa kuwa mzeituni wako utapukutika.
Michée 6.15 Psaumes 104.15 Psaumes 23.5
41 Utazaa wana na binti, lakini hawatakuwa wako wewe; kwa sababu watakwenda utumwani.
Deutéronome 28.32 Lamentations 1.5 2 Rois 24.14
42 Miti yako yote, na mazao ya nchi yako, nzige watakuwa nayo.
Deutéronome 28.38-28.39 Amos 7.1-7.2
43 Mgeni aliye kati yako atazidi kupaa juu yako; nawe utazidi kushuka chini.
Deutéronome 28.13 2 Rois 17.23 Juges 4.2-4.3 2 Rois 17.20 Juges 2.3
44 Yeye atakukopesha, wala wewe usimkopeshe; yeye atakuwa ni kichwa, wewe utakuwa mkia.
Deutéronome 28.12-28.13 Lamentations 1.5
45 Na laana hizi zote zitakujilia juu yako, zitakuandama na kukupata, hata uangamizwe, kwa kuwa hukuisikiza sauti ya Bwana, Mungu wako, kushika maagizo yake na amri zake alizokuagiza;
Deutéronome 28.15 Deutéronome 11.27-11.28 Esaïe 65.14-65.15 Proverbes 13.21 Psaumes 119.21
46 nazo zitakuwa juu yako kwa ishara na ajabu, na juu ya uzao wako milele;
Esaïe 8.18 Ezéchiel 14.8 Jérémie 25.18 Jérémie 19.8 Deutéronome 28.37
47 kwa kuwa hukumtumikia Bwana, Mungu wako, kwa furaha na moyo wa kushukuru, kwa ajili ya ule wingi wa vitu vyote;
Deutéronome 32.13-32.15 1 Timothée 6.17-6.19 Néhémie 9.35-9.37 Deutéronome 12.7-12.12 Deutéronome 16.11
48 kwa hiyo utawatumikia adui zako atakaowaleta Bwana juu yako, kwa njaa, na kwa kiu, na kwa uchi, na kwa uhitaji wa vitu vyote; naye atakuvika kongwa la chuma shingoni mwako, hata atakapokwisha kukuangamiza.
Jérémie 28.13-28.14 Ezéchiel 4.16-4.17 Ezéchiel 17.3 Jérémie 44.17-44.18 Ezéchiel 17.12
49 Bwana atakuletea taifa juu yako kutoka mbali, kutoka ncha ya dunia, kama arukavyo tai; taifa usiloufahamu ulimi wake;
Lamentations 4.19 Osée 8.1 Jérémie 49.22 Esaïe 5.26-5.30 Jérémie 48.40
50 taifa lenye uso mkali, ambalo haliangalii uso wa mzee, wala halipendelei kijana;
Esaïe 47.6 2 Chroniques 36.17 Osée 13.16 Ecclésiaste 8.1 Daniel 7.7
51 naye atakula uzao wa ng’ombe wako wa mifugo, na uzao wa nchi yako mpaka utakapokwisha kuangamizwa; wala hatakuachia nafaka, wala divai, wala mafuta, wala maongeo ya ng’ombe wako, wala wana-kondoo wako, hata atakapokwisha kukuangamiza.
Deutéronome 28.33 Esaïe 62.8 Esaïe 1.7 Lévitique 26.26 Habakuk 3.16-3.17
52 Naye atakuhusuru katika malango yako yote, hata kuta zako ndefu, zenye maboma, ulizokuwa ukiziamini, zishuke, katika nchi yako yote kila upande; naye atakuhusuru katika malango yako yote kila upande, katika nchi yako yote aliyokupa Bwana, Mungu wako.
Ezéchiel 4.1-4.8 2 Rois 25.1-25.4 Zacharie 12.2 Matthieu 24.15-24.16 Zacharie 14.2
53 Nawe utakula uzao wa tumbo lako mwenyewe, nyama ya wana wako na binti zako aliokupa Bwana, Mungu wako; katika mazingirwa na katika mkazo utakaokazwa na adui zako.
Lamentations 2.20 2 Rois 6.28-6.29 Lamentations 4.10 Lévitique 26.29 Jérémie 19.9
54 Mtu mume kati yenu aliye mwororo na laini sana, jicho lake litakuwa ovu juu ya nduguye, na juu ya mke wa kifuani mwake, na juu ya masalio ya wanawe waliosalia naye;
Deutéronome 15.9 Deutéronome 13.6 Michée 7.5 Psaumes 103.13 Luc 11.11-11.13
55 hata asitake wao mmojawapo apewe katika nyama ya wanawe atakaowala, kwa kuwa hana kitu kilichomsalia kwake; katika mazingirwa na mkazo utakaokazwa na adui yako katika malango yako yote.
Jérémie 5.10 Jérémie 34.2 Jérémie 52.6
56 Mwanamke kati yenu aliye mwororo na laini, ambaye hangehatirisha kuweka wayo wa mguu wake nchi kwa umalidadi na ulaini, jicho lake huyu litakuwa ovu juu ya mume wa kifuani mwake, na juu ya mwanawe, na juu ya binti yake,
Esaïe 3.16 Lamentations 4.3-4.6 Deutéronome 28.54
57 na juu ya mchanga wake atokaye katikati ya miguu yake, na juu ya wanawe atakaowazaa; kwa kuwa atawala kwa siri, kwa uhitaji wa vitu vyote; katika mazingirwa na mkazo utakaokazwa na adui yako katika malango yako.
Esaïe 49.15 Genèse 49.10
58 Kama hutaki kutunza kufanya maneno yote ya torati hii yaliyoandikwa katika kitabu hiki, upate kulicha jina hili la fahari na utisho, Bwana, MUNGU WAKO;
Esaïe 42.8 Deutéronome 28.15 Exode 6.2-6.3 Jérémie 7.9-7.10 Psaumes 72.19
59 ndipo atakapofanya Bwana mapigo yako yawe ya ajabu, na mapigo ya uzao wako, mapigo makubwa kwa kweli, ya kudumu sana, na magonjwa mazito ya kudumu sana.
Osée 3.4 Lamentations 4.12 Deutéronome 29.20-29.28 1 Rois 9.7-9.9 Lamentations 1.12
60 Naye atakurejezea maradhi yote ya Misri juu yako uliyokuwa ukiyaogopa, nayo yataambatana nawe.
Deutéronome 7.15 Deutéronome 28.27 Exode 15.26
61 Tena kila ugonjwa, na kila pigo yasiyoandikwa katika kitabu cha torati hii, atakutia nayo Bwana juu yako, hata utakapokwisha kuangamizwa.
Deutéronome 4.25-4.26
62 Nanyi mtasalia wachache kwa hesabu, ninyi mliokuwa mfano wa nyota za mbinguni kwa wingi; kwa kuwa hukuisikiza sauti ya Bwana, Mungu wako.
Néhémie 9.23 Deutéronome 4.27 Deutéronome 10.22 Jérémie 42.2 Néhémie 7.4
63 Tena itakuwa, kama vile alivyokuwa akifurahi Bwana juu yenu kwa kuwatendea mema na kuwafanya kuwa wengi, ndivyo atakavyofurahi Bwana juu yenu kwa kuwapoteza na kuwaangamiza; nanyi mtanyakuliwa katika hiyo nchi mwingiayo kuimiliki.
Proverbes 1.26 Jérémie 32.41 Deutéronome 30.9 Esaïe 1.24 Ezéchiel 5.13
64 Bwana atakutawanya katika mataifa yote, tokea ncha hii ya dunia hata ncha hii ya dunia; nawe huko utatumikia miungu mingine usiyoijua wewe wala baba zako, nayo ni miti na mawe.
Lévitique 26.33 Néhémie 1.8 Jérémie 16.13 Deutéronome 4.27-4.28 Deutéronome 28.36
65 Wala katika mataifa hayo hutapata raha iwayo yote, wala hutakuwa na kituo cha wayo wa mguu wako; lakini Bwana atakupa huko moyo wa kutetema, na macho ya kuzimia, na roho ya kudhoofika;
Lévitique 26.36 Lévitique 26.16 Amos 9.4 Esaïe 51.17 Matthieu 24.8
66 na uzima wako utakuwa na wasiwasi mbele yako; nawe utakuwa na woga usiku na mchana, wala hutaamini kamwe maisha yako;
Apocalypse 6.15-6.17 Deutéronome 28.67 Lamentations 1.13 Hébreux 10.27
67 asubuhi utasema, Laiti ingekuwa jioni! Na jioni utasema, Laiti ingekuwa asubuhi! Kwa kicho cha moyo wako utakavyokucha, na kuona kwa macho yako utakavyoona.
Deutéronome 28.34 Job 7.3-7.4 Apocalypse 9.6
68 Bwana atakurudisha tena Misri kwa merikebu, kwa njia ambayo nilikuambia, Hutaiona tena po pote; nanyi huko mtajiuza nafsi zenu kwa adui zenu kuwa watumwa na wajakazi, wala hapana atakayewanunua.
Osée 9.3 Jérémie 44.12 Jérémie 43.7 Osée 8.13 Deutéronome 17.16

Cette Bible est dans le domaine public.