Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 1.29
Bible en Swahili de l’est


Rappels et encouragements

Rappel des paroles de l’Éternel à Horeb

1 Haya ndiyo maneno Musa aliyowaambia Israeli wote ng’ambo ya Yordani barani, katika Araba lililoelekea Sufu, kati ya Parani, na Tofeli, na Labani, na Hazerothi, na Dizahabu.
1 Samuel 25.1 Deutéronome 33.2 Nombres 32.32 Nombres 34.15 Nombres 13.26
2 Ni mwendo wa siku kumi na moja kutoka Horebu kwa njia ya mlima wa Seiri mpaka Kadesh-barnea.
Nombres 13.26 Nombres 32.8 Deutéronome 9.23 Deutéronome 1.44 Exode 3.1
3 Ikawa mwaka wa arobaini, mwezi wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, Musa akawaambia wana wa Israeli kama yote aliyopewa na Bwana ya kuwaamuru;
Nombres 33.38 Nombres 20.1 Deutéronome 4.1-4.2
4 alipokwisha kumpiga Sihoni mfalme wa Waamori, aliyekuwa akikaa Heshboni, na Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa akikaa Ashtarothi iliyo katika Edrei;
Nombres 21.21-21.35 Néhémie 9.22 Josué 12.2-12.6 Josué 13.10-13.12 Psaumes 135.11
5 ni ng’ambo ya Yordani katika nchi ya Moabu, alipoanza Musa kufunua torati hii, akisema,
Deutéronome 31.9 Deutéronome 17.18-17.19 Deutéronome 4.8 Deutéronome 32.46
6 Bwana, Mungu wetu, alituambia huko Horebu, akasema, Mlivyokaa katika mlima huu vyatosha;
Exode 3.1 Nombres 10.11-10.13 Exode 19.1-19.2 Exode 17.6 Deutéronome 5.2
7 geukeni mshike safari yenu mwende nchi ya milima ya Waamori, na mahali pote palipo karibu ya hapo, katika hiyo Araba, na nchi ya vilima-vilima, na huko Shefela, na Negebu, na pwani-pwani, nchi ya Wakanaani, na Lebanoni, mpaka mto huo mkubwa, mto wa Frati.
Josué 10.40 Deutéronome 11.24 1 Chroniques 18.3 Genèse 15.16-15.21 Exode 23.31
8 Angalieni, nimewawekea nchi mbele yenu, ingieni mkaimiliki nchi Bwana aliyowaapia baba zenu, Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo, kwamba atawapa na uzao wao baada yao.
Genèse 12.7 Genèse 17.7-17.8 Genèse 15.18 Genèse 26.3-26.4 Genèse 28.13-28.14
9 Nami wakati ule niliwaambia, nikasema, Siwezi mimi mwenyewe kuwachukua peke yangu.
Exode 18.18 Nombres 11.11-11.14 Nombres 11.17
10 Bwana, Mungu wenu, amewafanya kuwa wengi, nanyi, angalieni, mmekuwa leo mfano wa nyota za mbinguni kwa wingi.
Genèse 15.5 Deutéronome 10.22 Deutéronome 28.62 Genèse 22.17 Exode 32.13
11 Bwana, Mungu wa baba zenu, na awafanye kuwa wengi mara elfu kuliko mlivyo, na kuwabarikia, kama alivyowaahidi.
Genèse 22.17 Exode 32.13 Psaumes 115.14 2 Samuel 24.3 Nombres 6.27
12 Nitachukuaje peke yangu mimi mwenyewe udhia wenu, na mzigo wenu, na mateto yenu?
2 Corinthiens 2.16 1 Rois 3.7-3.9 Psaumes 89.19 Deutéronome 1.9 Nombres 11.11-11.15
13 Jitwalieni watu wenye akili na fahamu, watu wanaojulikana, kwa kadiri ya kabila zenu, nami nitawafanya wawe vichwa juu yenu.
Exode 18.21 Nombres 11.16-11.17 Actes 6.2-6.6 Actes 1.21-1.23
14 Nanyi mkanijibu, mkaniambia, Jambo ulilonena ni jema la kufanya.
15 Basi nikatwaa vichwa vya kabila zenu wenye akili, waliojulikana, nikawafanya wawe vichwa juu yenu, maakida ya elfu elfu, na maakida ya mia mia, na maakida ya hamsini hamsini, na maakida ya kumi kumi, na wenye amri, kwa kadiri ya kabila zenu.
Nombres 31.14 Exode 18.25-18.26 Deutéronome 16.18 1 Samuel 17.18 1 Samuel 22.7
16 Nikawaagiza wakati ule waamuzi wenu, nikawaambia, Sikizeni ninyi maneno kati ya ndugu zenu, mkaamue kwa haki kati ya mtu na nduguye, na mgeni aliye pamoja naye.
Jean 7.24 Lévitique 24.22 Deutéronome 16.18-16.19 Exode 22.21 Nombres 27.19
17 Msitazame nafsi za watu katika hukumu; mwasikize wadogo na wakubwa sawasawa; msiche uso wa mtu awaye yote; kwa kuwa hukumu ni ya Mungu; na lile neno liwashindalo mniletee mimi, nami nitalisikiza.
Exode 18.26 Lévitique 19.15 Deutéronome 16.19 2 Chroniques 19.6 Proverbes 24.23
18 Nikawaamuru wakati huo mambo yote yaliyowapasa ninyi kuyafanya.
Actes 20.20 Deutéronome 4.40 Deutéronome 4.5 Deutéronome 12.32 Actes 20.27

Incrédulité à Kadès-Barnéa

19 Tukasafiri kutoka Horebu, tukapita katikati ya jangwa lile kubwa la kutisha mliloliona, njia ile ya kuiendea nchi ya vilima vya Waamori, kama Bwana, Mungu wetu, alivyotuamuru, tukafika Kadesh-barnea.
Deutéronome 1.2 Jérémie 2.6 Deutéronome 8.15 Deutéronome 32.10 Nombres 10.12
20 Nami nikawaambia, Mmefika nchi ya vilima ya Waamori, anayotupa sisi Bwana, Mungu wetu.
Deutéronome 1.7-1.8
21 Tazama, Bwana, Mungu wako, ameiweka nchi mbele yako; haya panda, itamalaki, kama Bwana, Mungu wa baba zako, alivyokuambia; usiogope wala usifadhaike.
Josué 1.9 Hébreux 13.6 Psaumes 46.1 Josué 1.6 Nombres 13.30
22 Nanyi mkanikaribia kila mmoja wenu, mkasema, Na tupeleke watu mbele yetu, ili watupelelezee nchi na kutuletea habari za njia itupasayo kuipandia, na za miji tutakayoifikia.
Nombres 13.1-13.20
23 Neno hili likanipendeza sana; nikatwaa watu kumi na wawili, mtu mmoja wa kila kabila.
Nombres 13.3-13.33
24 Nao wakageuka, wakapanda mlimani wakafika bonde la Eshkoli, wakalipeleleza.
Nombres 13.21-13.27 Josué 2.1-2.2
25 Wakatwaa baadhi ya matunda ya nchi ile mikononi mwao, wakatuletea huku chini, wakatuletea habari tena, wakasema, Nchi hii anayotupa Bwana, Mungu wetu, ni nchi njema.
26 Lakini hamkukubali kukwea huko, mlihalifu neno la Bwana, Mungu wenu;
Nombres 14.1-14.4 Actes 7.51 Psaumes 106.24-106.25 Esaïe 63.10
27 mkanung’unika hemani mwenu, mkasema, Ni kwa sababu Bwana ametuchukia, ndipo akatutoa katika nchi ya Misri, apate kututia katika mikono ya Waamori, ili kutuangamiza.
Deutéronome 9.28 Psaumes 106.25 Nombres 14.3 Exode 16.3 Matthieu 25.24
28 Twakwea kwenda wapi? Ndugu zetu wameiyeyusha mioyo yetu, wakituambia, Wale watu ni wengi, ni warefu kuliko sisi; miji nayo ni mikubwa, imejengewa kuta hata mbinguni; na zaidi ya hayo huko tumewaona Waanaki.
Deutéronome 9.1-9.2 Josué 14.8 Nombres 13.28-13.33 Exode 15.15 Esaïe 13.7
29 Ndipo nikawaambieni, Msifanye hofu, wala msiwache.
30 Bwana, Mungu wenu, anayetangulia mbele yenu, ndiye atakayewapigania, kwa mfano wa yote aliyowafanyia huko Misri mbele ya macho yenu;
Exode 14.14 Néhémie 4.20 Exode 14.25 Josué 10.42 Deutéronome 3.22
31 na huko jangwani, ulipoona alivyokuchukua Bwana, Mungu wako, kama mtu amchukuavyo mwanawe, njia yote mliyoiendea, hata mkafikilia mahali hapa.
Esaïe 46.3-46.4 Esaïe 63.9 Actes 13.18 Nombres 11.11-11.12 Esaïe 40.11
32 Lakini katika jambo hili hamkumwamini Bwana, Mungu wenu,
Psaumes 106.24 Jude 1.5 2 Chroniques 20.20 Hébreux 3.12 Hébreux 3.18-3.19
33 aliyewatangulia njiani, usiku kwa moto, kuwaonyesha njia mtakayoiendea, na mchana kwa hilo wingu, ili apate kuwatafutia mahali pa kusimamisha hema zenu.
Nombres 10.33 Psaumes 78.14 Nombres 9.15-9.22 Néhémie 9.12 Exode 13.21-13.22
34 Bwana akaisikia sauti ya maneno yenu, akaghadhibika, akaapa, akasema,
Psaumes 95.11 Hébreux 3.8-3.11 Deutéronome 2.14-2.15 Nombres 32.8-32.13 Nombres 14.22-14.30
35 Hakika yangu hapana mmoja miongoni mwa watu hawa wa kizazi hiki kibaya atakayeiona nchi hiyo nzuri, niliyowaapia baba zenu kuwapa,
Psaumes 95.11
36 isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune, huyo ataiona; nami nitampa yeye na watoto wake nchi hiyo aliyoikanyaga; kwa kuwa amemfuata Bwana kwa kila neno.
Nombres 14.24 Nombres 13.6 Nombres 32.12 Josué 14.6-14.14 Nombres 13.30
37 Na Bwana alinikasirikia mimi kwa ajili yenu, akasema, Wala wewe hutaingia humo;
Deutéronome 4.21 Nombres 20.12 Deutéronome 34.4 Nombres 27.13-27.14 Psaumes 106.32-106.33
38 Yoshua mwana wa Nuni asimamaye mbele yako ndiye atakayeingia; mtie moyo; kwa kuwa yeye atawarithisha Israeli.
Deutéronome 3.28 Deutéronome 31.7-31.8 Nombres 14.30 1 Samuel 16.22 Nombres 13.16
39 Tena, wadogo wenu, mliosema watakuwa mateka, na wana wenu, wasiokuwa leo na maarifa ya mabaya wala mema, ndio watakaoingia, nao ndio nitakaowapa, nao wataimiliki.
Esaïe 7.15-7.16 Nombres 14.3 Nombres 14.31 Jonas 4.11 Ephésiens 2.3
40 Na ninyi basi geukeni, mshike safari yenu, mwende jangwani kwa njia ya Bahari ya Shamu.
Nombres 14.25
41 Ndipo mkanijibu, mkaniambia, Sisi tumefanya dhambi juu ya Bwana, tutakwea kupigana kwa mfano wa yote tuliyoamriwa na Bwana. Mkajifunga kila mtu silaha zake za vita, mkafanya wepesi kukwea mlimani.
Nombres 22.34 Nombres 14.39-14.45 Proverbes 19.3
42 Bwana akaniambia, Uwaambie, Msiende, wala msipigane; kwani mimi si kati yenu; msije mkapigwa mbele ya adui zenu.
Esaïe 59.1-59.2 Esaïe 30.17 Lévitique 26.17 Osée 9.12 1 Samuel 4.2
43 Basi niliwaambia, msinisikize, bali mliasi amri ya Bwana, mkajikinai, na kukwea mlimani.
Nombres 14.44 Esaïe 63.10 Actes 7.51 Romains 8.7-8.8
44 Na Waamori waliokuwa wakikaa katika mlima huo, waliwatokea juu yenu, wakawafukuza, kama wafukuzwao na nyuki, wakawapomoshea Seiri mpaka Horma.
Psaumes 118.12 Nombres 14.45 Nombres 21.3 Esaïe 7.18 Deutéronome 28.25
45 Mkarudi mkalia mbele za Bwana; Bwana asiisikize sauti yenu, wala hakuelekeza masikio yake kwenu.
Psaumes 78.34 Hébreux 12.17
46 Ndipo mkakaa Kadeshi siku nyingi, kwa kadiri ya hizo siku mlizokaa.
Nombres 20.1 Nombres 20.22 Nombres 14.34 Nombres 14.25 Juges 11.16-11.17

Cette Bible est dans le domaine public.