Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 27.62
Bible en Swahili de l’est


Jésus devant le gouverneur romain

1 Na ilipokuwa asubuhi, wakuu wa makuhani wote na wazee wa watu wakafanya shauri juu ya Yesu, wapate kumwua;
Marc 15.1 Luc 22.66 Jean 18.28 Proverbes 4.16-4.18 Actes 4.24-4.28
2 wakamfunga, wakamchukua, wakampeleka kwa Pilato aliyekuwa liwali.
Matthieu 20.19 Actes 3.13 1 Timothée 6.13 Luc 13.1 Actes 28.20
3 Kisha Yuda, yule mwenye kumsaliti, alipoona ya kuwa amekwisha kuhukumiwa, alijuta, akawarudishia wakuu wa makuhani na wazee vile vipande thelathini vya fedha, akasema, Nalikosa nilipoisaliti damu isiyo na hatia.
2 Corinthiens 7.10 Matthieu 26.47-26.50 Jean 13.2 Marc 14.43-14.46 Jean 13.27
4 Wakasema, Basi, haya yatupasani sisi? Yaangalie haya wewe mwenyewe.
1 Pierre 1.19 Luc 16.25-16.26 1 Samuel 15.30 Matthieu 27.23-27.25 1 Rois 21.27
5 Akavitupa vile vipande vya fedha katika hekalu, akaondoka; akaenda, akajinyonga.
Job 2.9 2 Samuel 17.23 1 Rois 16.18 Juges 9.54 Job 7.15
6 Wakuu wa makuhani wakavitwaa vile vipande vya fedha, wakasema, Si halali kuviweka katika sanduku ya sadaka, kwa kuwa ni kima cha damu.
Luc 6.7-6.9 Jean 18.28 Matthieu 23.24 Esaïe 61.8 Deutéronome 23.18
7 Wakafanya shauri, wakavitumia kwa kununua konde la mfinyanzi liwe mahali pa kuzika wageni.
8 Kwa hiyo konde lile huitwa konde la damu hata leo.
Actes 1.19 Matthieu 28.15 Josué 4.9 Deutéronome 34.6 2 Chroniques 5.9
9 Ndipo likatimia neno lililonenwa na nabii Yeremia, akisema, Wakavitwaa vipande thelathini vya fedha, kima chake aliyetiwa kima, ambaye baadhi ya Waisraeli walimtia kima;
Zacharie 11.12-11.13 Exode 21.32 Matthieu 26.15 Matthieu 1.22 Lévitique 27.2-27.7
10 wakavitumia kwa kununua konde la mfinyanzi, kama Bwana alivyoniagiza.
Zacharie 11.13
11 Naye Yesu akasimama mbele ya liwali; liwali akamwuliza, akasema, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Yesu akamwambia, Wewe wasema.
Luc 23.2-23.3 Matthieu 2.2 Matthieu 26.25 Marc 15.2-15.5 1 Timothée 6.13
12 Lakini aliposhitakiwa na wakuu wa makuhani na wazee, hakujibu hata neno.
Matthieu 26.63 Esaïe 53.7 Actes 8.32 Matthieu 27.14 Marc 15.3-15.5
13 Ndipo Pilato akamwambia, Husikii ni mambo mangapi wanayokushuhudia?
Matthieu 26.62 Actes 22.24 Jean 18.35
14 Asimjibu hata neno moja, hata liwali akastaajabu sana.
1 Corinthiens 4.9 Psaumes 71.7 Zacharie 3.8 Esaïe 8.18
15 Basi wakati wa siku kuu, liwali desturi yake huwafungulia mkutano mfungwa mmoja waliyemtaka.
Actes 25.9 Jean 18.38-18.40 Actes 24.27 Jean 19.16 Matthieu 26.5
16 Basi palikuwa na mfungwa mashuhuri siku zile, aitwaye Baraba.
Luc 23.18-23.19 Luc 23.25 Jean 18.40 Marc 15.7 Romains 1.32
17 Basi walipokutanika, Pilato akawaambia, Mnataka niwafungulie yupi? Yule Baraba, au Yesu aitwaye Kristo?
1 Rois 18.21 Josué 24.15 Jean 19.15 Marc 15.9-15.12 Matthieu 1.16
18 Kwa maana alijua ya kuwa wamemtoa kwa husuda.
Proverbes 27.4 Genèse 37.11 Actes 13.45 Esaïe 26.11 Jacques 4.5
19 Na alipokuwa ameketi juu ya kiti cha hukumu, mkewe alimpelekea mjumbe, kumwambia, Usiwe na neno na yule mwenye haki; kwa sababu nimeteswa mengi leo katika ndoto kwa ajili yake.
Matthieu 27.24 1 Pierre 2.22 Luc 23.47 Jean 19.13 Job 33.14-33.17
20 Nao wakuu wa makuhani na wazee wakawashawishi makutano ili wamtake Baraba, na kumwangamiza Yesu.
Marc 15.11 Jean 19.15-19.16 Luc 23.18-23.20 Actes 19.23-19.29 Jean 18.40
21 Basi liwali akajibu, akawaambia, Mnataka niwafungulie yupi katika hawa wawili? Wakasema, Baraba.
22 Pilato akawaambia, Basi, nimtendeje Yesu aitwaye Kristo? Wakasema wote, Asulibiwe.
Jean 19.14-19.15 Matthieu 1.16 Marc 14.55 Matthieu 27.17 Esaïe 53.2-53.3
23 Akasema, Kwani? Ni ubaya gani alioutenda? Wakazidi sana kupiga kelele, wakisema, Na asulibiwe.
Actes 21.28-21.31 1 Samuel 19.3-19.15 1 Samuel 20.31-20.33 Actes 22.22-22.23 Matthieu 21.38-21.39
24 Basi Pilato alipoona ya kuwa hafai lo lote, bali ghasia inazidi tu, akatwaa maji, akanawa mikono yake mbele ya mkutano, akasema, Mimi sina hatia katika damu ya mtu huyu mwenye haki; yaangalieni haya ninyi wenyewe.
Matthieu 27.4 Psaumes 26.6 Deutéronome 21.6-21.8 Matthieu 26.5 Job 9.30-9.31
25 Watu wote wakajibu wakasema, Damu yake na iwe juu yetu, na juu ya watoto wetu.
Actes 5.28 Josué 2.19 Actes 7.52 1 Thessaloniciens 2.15-2.16 Exode 20.5
26 Ndipo akawafungulia Baraba; na baada ya kumpiga Yesu mijeledi, akamtoa ili asulibiwe.
Jean 19.1 Luc 23.16 Esaïe 53.5 Marc 15.15 Matthieu 20.19
27 Ndipo askari wa liwali wakamchukua Yesu ndani ya Praitorio, wakamkusanyikia kikosi kizima.
Jean 18.28 Jean 18.33 Actes 10.1 Actes 23.35 Jean 19.8-19.9
28 Wakamvua nguo, wakamvika vazi jekundu.
Luc 23.11 Marc 15.17 Jean 19.2-19.5
29 Wakasokota taji ya miiba, wakaiweka juu ya kichwa chake, na mwanzi katika mkono wake wa kuume; wakapiga magoti mbele yake, wakamdhihaki, wakisema, Salamu, Mfalme wa Wayahudi!
Marc 15.18 Esaïe 53.3 Matthieu 20.19 Esaïe 49.7 Jérémie 20.7
30 Kisha wakamtemea mate, wakautwaa ule mwanzi, wakampiga-piga kichwani.
Matthieu 26.67 Marc 15.19 Job 30.8-30.10 Esaïe 50.6 Esaïe 53.3
31 Walipokwisha kumdhihaki, wakalivua lile vazi, wakamvika mavazi yake, wakamchukua kumsulibisha.
Esaïe 53.7 Jean 19.16 Jean 19.27 Hébreux 13.12 1 Rois 21.13

Crucifixion et mort de Jésus

32 Hata walipokuwa wakitoka, wakamwona mtu Mkirene, jina lake Simoni; huyu wakamshurutisha auchukue msalaba wake.
Luc 23.26 Marc 15.21 Actes 2.10 Actes 6.9 Actes 13.1
33 Na walipofika mahali paitwapo Golgotha, yaani, Fuvu la kichwa,
Marc 15.34 Marc 15.22-15.32 Jean 19.17-19.19 Jean 19.23-19.24 Luc 23.44
34 wakampa kunywa divai iliyochanganyika na nyongo; lakini yeye alipoionja hakutaka kunywa.
Psaumes 69.21 Marc 15.23 Matthieu 27.48 Jean 19.28-19.30
35 Walipokwisha kumsulibisha, waligawa mavazi yake, wakipiga kura; [ili litimie neno lililonenwa na nabii, Waligawa nguo zangu kati yao, na juu ya vazi langu walipiga kura.]
Psaumes 22.18 Luc 23.34 Jean 20.27 Jean 19.23-19.24 Psaumes 22.16
36 Wakaketi, wakamlinda huko.
Matthieu 27.54 Marc 15.39 Marc 15.44
37 Wakaweka juu ya kichwa chake mashitaka yake, yaliyoandikwa HUYU NI YESU, MFALME WA WAYAHUDI.
Marc 15.26 Luc 23.38 Jean 19.19-19.22
38 Wakati uo huo wanyang’anyi wawili wakasulibiwa pamoja naye, mmoja mkono wake wa kuume, na mmoja mkono wake wa kushoto.
Esaïe 53.12 Luc 23.39-23.43 Marc 15.27 Luc 23.32-23.33 Jean 19.31-19.35
39 Nao waliokuwa wakipita njiani wakamtukana, wakitikisa-tikisa vichwa vyao, wakisema,
Psaumes 109.25 Lamentations 1.12 Psaumes 69.20 1 Pierre 2.22-2.24 Psaumes 109.2
40 Ewe mwenye kulivunja hekalu na kulijenga kwa siku tatu, jiokoe nafsi yako; ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, shuka msalabani.
Matthieu 26.61 Matthieu 4.3 Matthieu 4.6 Matthieu 26.63-26.64 Jean 2.19-2.22
41 Kadhalika na wale wakuu wa makuhani wakamdhihaki pamoja na waandishi na wazee, wakisema, Aliokoa wengine, hawezi kujiokoa mwenyewe.
Marc 15.31-15.32 Luc 22.52 Psaumes 35.26 Luc 18.32 Luc 23.35
42 Yeye ni mfalme wa Israeli; na ashuke sasa msalabani, nasi tutamwamini.
Jean 1.49 Matthieu 27.37 Jean 12.13 Actes 4.14 Luc 19.38
43 Amemtegemea Mungu; na amwokoe sasa, kama anamtaka; kwa maana alisema, Mimi ni Mwana wa Mungu.
Psaumes 22.8 Jean 19.7 Jean 10.36 Psaumes 14.6 Esaïe 36.15
44 Pia wale wanyang’anyi waliosulibiwa pamoja naye walimshutumu vile vile.
Luc 23.39-23.43 Job 30.7-30.9 Marc 15.32 Matthieu 27.38 Psaumes 35.15
45 Basi tangu saa sita palikuwa na giza juu ya nchi yote hata saa tisa.
Luc 23.44-23.45 Amos 8.9 Marc 15.25 Marc 15.33-15.34 Esaïe 50.3
46 Na kama saa tisa, Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu akisema, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Yaani, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?
Psaumes 22.1 Hébreux 5.7 Psaumes 71.11 Lamentations 1.12 Esaïe 53.10
47 Na baadhi yao waliohudhuria, waliposikia, walisema, Huyu anamwita Eliya.
Matthieu 11.14 Malachie 4.5 Marc 15.35-15.36
48 Mara mmoja wao akaenda mbio, akatwaa sifongo, akaijaza siki, akaitia juu ya mwanzi, akamnywesha.
Psaumes 69.21 Matthieu 27.34 Luc 23.36 Jean 19.29-19.30
49 Wale wengine wakasema, Acha; na tuone kama Eliya anakuja kumwokoa.
50 Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake.
Jean 19.30 Marc 15.37 Luc 23.46 Psaumes 22.14-22.15 Matthieu 20.28
51 Na tazama, pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini; nchi ikatetemeka; miamba ikapasuka;
Marc 15.38 Hébreux 10.19-10.22 Exode 26.31-26.37 Luc 23.45 Matthieu 27.54
52 makaburi yakafunuka; ikainuka miili mingi ya watakatifu waliolala;
1 Corinthiens 15.20 Daniel 12.2 Jean 5.25-5.29 Esaïe 26.19 1 Thessaloniciens 4.14
53 nao wakiisha kutoka makaburini mwao, baada ya kufufuka kwake, wakauingia mji mtakatifu, wakawatokea wengi.
Apocalypse 11.2 Matthieu 4.5 Esaïe 48.2 Apocalypse 22.19 Daniel 9.24
54 Basi yule akida, na hao waliokuwa pamoja naye wakimlinda Yesu, walipoliona tetemeko la nchi na mambo yaliyofanyika, wakaogopa sana, wakisema, Hakika huyu alikuwa Mwana wa Mungu.
Matthieu 27.36 Marc 15.39 Matthieu 27.43 Actes 23.23 Matthieu 8.5
55 Palikuwa na wanawake wengi pale wakitazama kwa mbali, hao ndio waliomfuata Yesu toka Galilaya, na kumtumikia.
Luc 8.2-8.3 Luc 23.27-23.28 Luc 23.48-23.49 Jean 19.25-19.27
56 Miongoni mwao alikuwamo Mariamu Magdalene, na Mariamu mama yao Yakobo na Yusufu, na mama yao wana wa Zebedayo.
Jean 19.25 Marc 16.9 Matthieu 28.1 Marc 15.47-16.1 Matthieu 13.55

Mise au tombeau du corps de Jésus

57 Hata ilipokuwa jioni akafika mtu tajiri wa Arimathaya, jina lake Yusufu, naye mwenyewe alikuwa mwanafunzi wa Yesu;
Jean 19.38-19.42 Luc 23.50-23.56 Marc 15.42-15.47 1 Samuel 7.17 1 Samuel 1.1
58 mtu huyu alimwendea Pilato akauomba mwili wa Yesu. Ndipo Pilato akaamuru apewe.
Marc 15.44-15.46 Luc 23.52-23.53
59 Yusufu akautwaa mwili, akauzonga-zonga katika sanda ya kitani safi,
60 akauweka katika kaburi lake jipya, alilokuwa amelichonga mwambani; akavingirisha jiwe kubwa mbele ya mlango wa kaburi, akaenda zake.
Matthieu 27.66 Matthieu 28.2 Esaïe 53.9 Luc 24.2 Jean 20.1
61 Na pale walikuwapo Mariamu Magdalene, na Mariamu yule wa pili, wameketi kulielekea kaburi.
Matthieu 27.56 Matthieu 28.1
62 Hata siku ya pili, ndiyo iliyo baada ya Maandalio, wakuu wa makuhani, na Mafarisayo wakamkusanyikia Pilato,
Jean 19.14 Marc 15.42 Jean 19.42 Matthieu 27.1-27.2 Psaumes 2.1-2.6
63 wakasema, Bwana, tumekumbuka kwamba yule mjanja alisema, alipokuwa akali hai, Baada ya siku tatu nitafufuka.
Luc 9.22 Matthieu 16.21 Luc 18.33 Matthieu 20.19 Matthieu 17.23
64 Basi amuru kwamba kaburi lilindwe salama hata siku ya tatu; wasije wanafunzi wake wakamwiba, na kuwaambia watu, Amefufuka katika wafu; na udanganyifu wa mwisho utapita ule wa kwanza.
Matthieu 28.13 Matthieu 12.45
65 Pilato akawaambia, Mna askari; nendeni mkalilinde salama kadiri mjuavyo.
Matthieu 27.66 Matthieu 28.11-28.15 Psaumes 76.10 Proverbes 21.30
66 Wakaenda, wakalilinda kaburi salama, kwa kulitia lile jiwe muhuri, pamoja na wale askari walinzi.
Daniel 6.17 2 Timothée 2.19 Matthieu 28.2 Matthieu 28.11 Matthieu 27.60

Cette Bible est dans le domaine public.