Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jean 11.19
Bible en Swahili de l’est


Jésus ressuscite Lazare

1 Basi mtu mmoja alikuwa hawezi, Lazaro wa Bethania, mwenyeji wa mji wa Mariamu na Martha, dada yake.
Jean 12.17 Matthieu 21.17 Jean 12.9 Jean 12.1-12.2 Luc 16.20-16.25
2 Ndiye Mariamu yule aliyempaka Bwana marhamu, akamfuta miguu kwa nywele zake, ambaye Lazaro nduguye alikuwa hawezi.
Jean 12.3 Marc 14.3 Luc 7.37-7.38 Matthieu 26.6-26.7
3 Basi wale maumbu wakatuma ujumbe kwake wakisema, Bwana, yeye umpendaye hawezi.
Jean 11.5 Jean 11.36 Psaumes 16.3 Jacques 5.14-5.15 Jean 11.1
4 Naye Yesu aliposikia, alisema, Ugonjwa huu si wa mauti, bali ni kwa ajili ya utukufu wa Mungu, ili Mwana wa Mungu atukuzwe kwa huo.
Jean 11.40 Jean 9.3 Jean 13.31-13.32 Jean 5.23 Marc 5.39-5.42
5 Naye Yesu alimpenda Martha na umbu lake na Lazaro.
Jean 11.36 Jean 15.9-15.13 Jean 17.26 Jean 16.27 Jean 11.8
6 Basi aliposikia ya kwamba hawezi, alikaa bado siku mbili pale pale alipokuwapo.
Esaïe 30.18 Esaïe 55.8-55.9 Genèse 44.1-44.5 Genèse 43.29-43.31 Genèse 22.14
7 Kisha, baada ya hayo, akawaambia wanafunzi wake, Twendeni Uyahudi tena.
Actes 20.22-20.24 Luc 9.51 Actes 15.36 Jean 10.40-10.42
8 Wale wanafunzi wakamwambia, Rabi, juzijuzi tu Wayahudi walikuwa wakitafuta kukupiga kwa mawe, nawe unakwenda huko tena?
Jean 10.31 Jean 8.59 Matthieu 16.21-16.23 Matthieu 23.7 Actes 20.24
9 Yesu akajibu, Je! Saa za mchana si kumi na mbili? Mtu akienda mchana hajikwai; kwa sababu aiona nuru ya ulimwengu huu.
Jean 9.4 Jean 12.35 Jérémie 31.9 Proverbes 3.23 Luc 13.31-13.33
10 Bali akienda usiku hujikwaa; kwa sababu nuru haimo ndani yake.
Jérémie 20.11 Jérémie 13.16 1 Jean 2.10-2.11 Psaumes 27.2 Proverbes 4.18-4.19
11 Aliyasema hayo; kisha, baada ya hayo, akawaambia, Rafiki yetu, Lazaro, amelala; lakini ninakwenda nipate kumwamsha.
Daniel 12.2 Actes 7.60 Marc 5.39 1 Thessaloniciens 5.10 1 Corinthiens 15.51
12 Basi wale wanafunzi wakamwambia, Bwana, ikiwa amelala, atapona.
13 Lakini Yesu alikuwa amenena habari ya mauti yake; nao walidhania ya kuwa ananena habari ya kulala usingizi.
Matthieu 9.24
14 Basi hapo Yesu akawaambia waziwazi, Lazaro amekufa.
Jean 10.24 Jean 16.25 Jean 16.29
15 Nami nafurahi kwa ajili yenu kwamba sikuwako huko, ili mpate kuamini; lakini na twendeni kwake.
2 Timothée 2.10 Jean 2.11 Esaïe 54.15 Genèse 26.24 Jean 17.19
16 Basi Tomaso, aitwaye Pacha, akawaambia wanafunzi wenziwe, Twendeni na sisi, ili tufe pamoja naye.
Matthieu 10.3 Jean 21.2 Luc 6.15 Marc 3.18 Matthieu 26.35
17 Basi Yesu alipofika, alimkuta amekwisha kuwamo kaburini yapata siku nne.
Jean 11.39 Actes 2.27-2.31 Osée 6.2 Jean 2.19
18 Na Bethania ilikuwa karibu na Yerusalemu, kadiri ya maili mbili hivi;
Apocalypse 21.16 Jean 6.19 Apocalypse 14.20 Luc 24.13 Jean 11.1
19 na watu wengi katika Wayahudi walikuwa wamekuja kwa Martha na Mariamu, ili kuwafariji kwa habari ya ndugu yao.
Job 2.11 1 Thessaloniciens 5.11 Jean 11.31 Ecclésiaste 7.2 1 Thessaloniciens 4.18
20 Basi Martha aliposikia kwamba Yesu anakuja, alikwenda kumlaki; na Mariamu alikuwa akikaa nyumbani.
Luc 10.38-10.42 Matthieu 25.1 Matthieu 25.6 Actes 10.25 1 Thessaloniciens 4.17
21 Basi Martha akamwambia Yesu, Bwana, kama ungalikuwapo hapa, ndugu yangu hangalikufa.
Jean 11.32 Jean 11.37 Luc 8.49-8.55 Luc 7.6-7.10 Psaumes 78.19
22 Lakini hata sasa najua ya kuwa yo yote utakayomwomba Mungu, Mungu atakupa.
Jean 9.31 Jean 11.41-11.42 Matthieu 28.18 Marc 9.23 Jean 3.35
23 Yesu akamwambia, Ndugu yako atafufuka.
Jean 11.43-11.44
24 Martha akamwambia, Najua ya kuwa atafufuka katika ufufuo siku ya mwisho.
Actes 24.15 Jean 5.28-5.29 Luc 14.14 Esaïe 26.19 Ezéchiel 37.1-37.10
25 Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi;
1 Thessaloniciens 4.14 Jean 3.36 Jean 1.4 Jean 6.39-6.40 Jean 6.44
26 naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele. Je! Unayasadiki hayo?
Jean 10.28 Jean 14.10 Matthieu 9.28 Jean 6.54-6.58 Jean 8.51-8.53
27 Akamwambia, Naam, Bwana, mimi nimesadiki ya kwamba wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu, yule ajaye ulimwenguni.
Matthieu 16.16 Jean 6.14 Malachie 3.1 Matthieu 11.3 Jean 6.69
28 Naye alipokwisha kusema hayo, alikwenda zake; akamwita umbu lake Mariamu faraghani, akisema, Mwalimu yupo anakuita.
Jean 13.13 Hébreux 12.12 Marc 10.49 Jean 11.20 Matthieu 26.18
29 Naye aliposikia, aliondoka upesi, akamwendea.
Proverbes 15.23 Psaumes 27.8 Cantique 3.1-3.4 Psaumes 119.59-119.60 Proverbes 27.17
30 Na Yesu alikuwa hajafika ndani ya kijiji; lakini alikuwa akalipo pale pale alipomlaki Martha.
Jean 11.20
31 Basi wale Wayahudi waliokuwapo na Mariamu nyumbani, wakimfariji, walipomwona jinsi alivyoondoka upesi na kutoka, walimfuata; huku wakidhania ya kuwa anakwenda kaburini ili alie huko.
Jean 11.19 Genèse 37.35 1 Corinthiens 2.15 2 Samuel 12.16-12.18
32 Basi Mariamu alipofika pale alipokuwapo Yesu, na kumwona, alianguka miguuni pake, akamwambia, Bwana, kama ungalikuwapo hapa, ndugu yangu hangalikufa.
Jean 11.21 Apocalypse 5.14 Apocalypse 22.8 Jean 11.37 Jean 4.49
33 Basi Yesu alipomwona analia, na wale Wayahudi waliofuatana naye wanalia, aliugua rohoni, akafadhaika roho yake,
Jean 12.27 Jean 11.38 Genèse 43.30-43.31 Marc 3.5 Hébreux 5.7-5.8
34 akasema, Mmemweka wapi? Wakamwambia, Bwana, njoo utazame.
Jean 20.2 Jean 1.39 Marc 15.47 Matthieu 28.6 Marc 16.6
35 Yesu akalia machozi.
Luc 19.41 Jean 11.33 Jérémie 13.17 Hébreux 4.15 Psaumes 35.13-35.15
36 Basi Wayahudi wakasema, Angalieni jinsi alivyompenda.
Jean 11.3 Jean 21.15-21.17 1 Jean 4.9-4.10 1 Jean 3.1 2 Corinthiens 8.8-8.9
37 Bali wengine wao wakasema, Je! Huyu aliyemfumbua macho yule kipofu, hakuweza kumfanya na huyu asife?
Jean 9.6-9.7 Luc 23.39 Luc 23.35 Jean 11.32 Jean 11.21
38 Basi Yesu, hali akiugua tena nafsini mwake, akafika kwenye kaburi. Nalo lilikuwa ni pango, na jiwe limewekwa juu yake.
Matthieu 27.60 Jean 11.33 Luc 24.2 Esaïe 22.16 Jean 20.1
39 Yesu akasema, Liondoeni jiwe. Martha, dada yake yule aliyefariki, akamwambia, Bwana, ananuka sasa; maana amekuwa maiti siku nne.
Jean 11.17 Psaumes 49.7 Psaumes 49.14 Genèse 23.4 Marc 16.3
40 Yesu akamwambia, Mimi sikukuambia ya kwamba ukiamini utauona utukufu wa Mungu?
Jean 11.4 Jean 11.23-11.26 Romains 4.17-4.25 Jean 1.14 Psaumes 63.2
41 Basi wakaliondoa lile jiwe. Yesu akainua macho yake juu, akasema, Baba, nakushukuru kwa kuwa umenisikia.
Matthieu 11.25 Jean 17.1 Psaumes 123.1 Luc 10.21 Luc 18.13
42 Nami nalijua ya kuwa wewe wanisikia sikuzote; lakini kwa ajili ya mkutano huu wanaohudhuria nalisema haya, ili wapate kusadiki kwamba ndiwe uliyenituma.
Jean 3.17 Jean 17.21 Jean 11.22 Jean 17.8 Matthieu 26.53
43 Naye akiisha kusema hayo, akalia kwa sauti kuu, Lazaro, njoo huku nje.
Luc 7.14-7.15 2 Rois 4.33-4.36 Actes 9.40 1 Rois 17.21-17.22 Actes 3.6
44 Akatoka nje yule aliyekufa, amefungwa sanda miguuni na mikononi, na uso wake amefungwa leso. Naye Yesu akawaambia, Mfungueni, mkamwache aende zake.
Jean 20.7 Jean 19.40 Philippiens 3.21 Jean 10.30 Genèse 1.3
45 Basi wengi katika Wayahudi waliokuja kwa Mariamu, na kuyaona yale aliyoyafanya, wakamwamini.
Jean 2.23 Jean 11.19 Jean 12.9-12.11 Jean 12.17-12.19 Jean 12.42
46 Lakini wengine wakaenda zao kwa Mafarisayo, wakawaambia aliyoyafanya Yesu.
Jean 9.13 Luc 16.30-16.31 Jean 5.15-5.16 Jean 12.37 Actes 5.25
47 Basi wakuu wa makuhani na Mafarisayo wakakusanya baraza, wakasema, Tunafanya nini? Maana mtu huyu afanya ishara nyingi.
Matthieu 26.3 Matthieu 5.22 Jean 12.19 Matthieu 27.1-27.2 Actes 4.16-4.17
48 Tukimwacha hivi, watu wote watamwamini; na Warumi watakuja, watatuondolea mahali petu na taifa letu.
Matthieu 21.40-21.42 Jean 1.7 Deutéronome 28.50-28.68 Matthieu 22.7 Zacharie 14.1-14.2
49 Mtu mmoja miongoni mwao, Kayafa, aliyekuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, akawaambia, Ninyi hamjui neno lo lote;
Jean 11.51 Proverbes 26.12 Jean 18.13-18.14 Matthieu 26.3 Esaïe 5.20-5.23
50 wala hamfikiri ya kwamba yafaa mtu mmoja afe kwa ajili ya watu, wala lisiangamie taifa zima.
Jean 18.14 Luc 24.46 Jean 19.12 Romains 3.8 Jean 11.48
51 Na neno hilo yeye hakulisema kwa nafsi yake; bali kwa kuwa alikuwa Kuhani Mkuu mwaka ule, alitabiri ya kwamba Yesu atakufa kwa ajili ya taifa hilo.
1 Samuel 23.9 Exode 28.30 Matthieu 20.28 Romains 3.25-3.26 Esaïe 53.5-53.8
52 Wala si kwa ajili ya taifa hilo tu; lakini pamoja na hayo awakusanye watoto wa Mungu waliotawanyika, ili wawe wamoja.
Jean 10.16 Esaïe 49.6 1 Jean 2.2 Esaïe 60.4 Psaumes 72.19
53 Basi tangu siku ile walifanya shauri la kumwua.
Jean 11.47 Psaumes 113.2 Néhémie 13.21 Marc 3.6 Jérémie 38.4
54 Kwa hiyo Yesu hakutembea tena kwa wazi katikati ya Wayahudi; bali alitoka huko, akaenda mahali karibu na jangwa, mpaka mji uitwao Efraimu; akakaa huko pamoja na wanafunzi wake.
Jean 7.1 2 Chroniques 13.19 Jean 7.4 Jean 4.1-4.3 Jean 7.10
55 Na Pasaka ya Wayahudi ilikuwa karibu; na wengi wakakwea toka mashambani kwenda Yerusalemu kabla ya Pasaka, ili wajitakase.
Jean 6.4 Jean 2.13 Exode 19.10 Jean 12.1 2 Chroniques 30.17-30.20
56 Basi wao wakamtafuta Yesu, wakasemezana hali wamesimama hekaluni, Mwaonaje? Haji kabisa sikukuu hii?
Jean 7.11 Jean 11.7-11.8
57 Na wakuu wa makuhani na Mafarisayo walikuwa wametoa amri ya kwamba mtu akimjua alipo, alete habari, ili wapate kumkamata.
Psaumes 109.4 Jean 8.59 Jean 9.22 Jean 5.16-5.18 Jean 10.39

Cette Bible est dans le domaine public.