Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 24.41
Bible en Swahili de l’est


Discours sur le mont des Oliviers

Destruction de Jérusalem et retour du Fils de l’homme

1 Yesu akaenda zake, akatoka hekaluni; wanafunzi wake wakamwendea ili kumwonyesha majengo ya hekalu.
Marc 13.1-13.37 Matthieu 23.39 Luc 21.5-21.36 Matthieu 21.23 Jean 2.20
2 Naye akajibu akawaambia, Hamyaoni haya yote? Amin, nawaambieni, Halitasalia hapa jiwe juu ya jiwe ambalo halitabomoshwa.
Luc 19.44 Daniel 9.26-9.27 1 Rois 9.7-9.8 2 Pierre 3.11 Michée 3.12
3 Hata alipokuwa ameketi katika mlima wa Mizeituni, wanafunzi wake wakamwendea kwa faragha, wakisema, Tuambie, mambo hayo yatakuwa lini? Nayo ni nini dalili ya kuja kwako, na ya mwisho wa dunia?
Matthieu 21.1 Actes 1.7 Matthieu 28.20 Matthieu 17.19 Luc 21.7
4 Yesu akajibu, akawaambia, Angalieni, mtu asiwadanganye.
Jérémie 29.8 2 Thessaloniciens 2.3 Marc 13.5-13.6 Luc 21.8 1 Jean 4.1
5 Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, Mimi ni Kristo; nao watadanganya wengi.
Matthieu 24.24 Matthieu 24.11 1 Jean 2.18 Jérémie 14.14 Actes 8.9-8.10
6 Nanyi mtasikia habari za vita na matetesi ya vita; angalieni, msitishwe; maana hayo hayana budi kutukia; lakini ule mwisho bado.
Marc 13.7-13.8 Luc 21.9 Esaïe 8.12-8.14 1 Pierre 3.14-3.15 Ezéchiel 21.28
7 Kwa maana taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme; kutakuwa na njaa, na matetemeko ya nchi mahali mahali.
2 Chroniques 15.6 Joël 2.30-2.31 Actes 11.28 Esaïe 19.2 Luc 21.11
8 Hayo yote ndiyo mwanzo wa utungu.
1 Pierre 4.17-4.18 1 Thessaloniciens 5.3 Esaïe 9.12 Esaïe 10.4 Esaïe 9.17
9 Wakati huo watawasaliti ninyi mpate dhiki, nao watawaua; nanyi mtakuwa watu wa kuchukiwa na mataifa yote kwa ajili ya jina langu.
Jean 15.19-15.20 Jean 16.2 Apocalypse 2.10 Luc 21.16-21.17 Marc 13.9-13.13
10 Ndipo wengi watakapojikwaa, nao watasalitiana, na kuchukiana.
Matthieu 11.6 Marc 13.12 Matthieu 10.35-10.36 Matthieu 13.21 2 Timothée 4.16
11 Na manabii wengi wa uongo watatokea, na kudanganya wengi.
Matthieu 7.15 Matthieu 24.24 Matthieu 24.5 Actes 20.30 1 Timothée 4.1
12 Na kwa sababu ya kuongezeka maasi, upendo wa wengi utapoa.
Apocalypse 2.4-2.5 Apocalypse 3.15 Jacques 4.1-4.4 Jacques 5.1-5.6 Apocalypse 2.10
13 Lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka.
Matthieu 10.22 Marc 13.13 Romains 2.7 Hébreux 3.14 Matthieu 24.6
14 Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja.
Colossiens 1.6 Apocalypse 14.6 Romains 10.18 Matthieu 9.35 Colossiens 1.23
15 Basi hapo mtakapoliona chukizo la uharibifu, lile lililonenwa na nabii Danieli, limesimama katika patakatifu (asomaye na afahamu),
Daniel 9.27 Daniel 12.11 Marc 13.14 Daniel 9.25 Apocalypse 1.3
16 ndipo walio katika Uyahudi na wakimbilie milimani;
Hébreux 11.7 Genèse 19.15-19.17 Luc 21.21-21.22 Jérémie 37.11-37.12 Proverbes 22.3
17 naye aliye juu ya dari asishuke kuvichukua vitu vilivyomo nyumbani mwake;
Luc 17.31-17.33 Matthieu 10.27 1 Samuel 9.25 Matthieu 6.25 Actes 10.9
18 wala aliye shambani asirudi nyuma kuichukua nguo yake.
19 Ole wao wenye mimba na wanyonyeshao siku hizo!
Deutéronome 28.53-28.56 Marc 13.17-13.18 Luc 21.23 2 Rois 15.16 Lamentations 4.3-4.4
20 Ombeni, ili kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi, wala siku ya sabato.
Exode 16.29 Actes 1.12
21 Kwa kuwa wakati huo kutakuwapo dhiki kubwa, ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu hata sasa, wala haitakuwapo kamwe.
Daniel 12.1 Joël 2.2 Zacharie 14.2-14.3 Luc 21.24 Matthieu 24.29
22 Na kama siku hizo zisingalifupizwa, asingeokoka mtu ye yote; lakini kwa ajili ya wateule zitafupizwa siku hizo.
Marc 13.20 Esaïe 65.8-65.9 Matthieu 24.24 Matthieu 24.31 Zacharie 13.8
23 Wakati huo mtu akiwaambia, Tazama, Kristo yupo hapa, au yuko kule msisadiki.
Luc 21.8 Marc 13.21 Luc 17.23-17.24 Deutéronome 13.1-13.3 Jean 5.43
24 Kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini, hata walio wateule.
2 Thessaloniciens 2.9-2.11 Matthieu 24.11 Apocalypse 13.13-13.14 Apocalypse 19.20 Matthieu 7.15
25 Tazama, nimekwisha kuwaonya mbele.
Esaïe 48.5-48.6 Esaïe 46.10-46.11 Jean 16.1 Esaïe 44.7-44.8 Luc 21.13
26 Basi wakiwaambia, Yuko jangwani, msitoke; yumo nyumbani, msisadiki.
Actes 21.38 Luc 3.2-3.3 Esaïe 40.3 Matthieu 3.1
27 Kwa maana kama vile umeme utokavyo mashariki ukaonekana hata magharibi, hivyo ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.
Zacharie 9.14 Jacques 5.8 Malachie 3.2 Matthieu 24.39 Luc 17.24-17.37
28 Kwa kuwa po pote ulipo mzoga, ndipo watakapokusanyika tai.
Luc 17.37 Amos 9.1-9.4 Jérémie 16.16 Deutéronome 28.49 Job 39.27-39.30
29 Lakini mara, baada ya dhiki ya siku zile, jua litatiwa giza, na mwezi hautatoa mwanga wake, na nyota zitaanguka mbinguni, na nguvu za mbinguni zitatikisika;
Amos 8.9 Esaïe 24.23 Esaïe 13.10 Joël 3.15 Apocalypse 6.12-6.17
30 ndipo itakapoonekana ishara yake Mwana wa Adamu mbinguni; ndipo mataifa yote ya ulimwengu watakapoomboleza, nao watamwona Mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya mbinguni pamoja na nguvu na utukufu mwingi.
Apocalypse 1.7 Daniel 7.13 Matthieu 16.27-16.28 Matthieu 26.64 Luc 21.27
31 Naye atawatuma malaika zake pamoja na sauti kuu ya parapanda, nao watawakusanya wateule wake toka pepo nne, toka mwisho huu wa mbingu mpaka mwisho huu.
Esaïe 27.13 1 Thessaloniciens 4.16 1 Corinthiens 15.52 Marc 13.27 Matthieu 13.41
32 Basi kwa mtini jifunzeni mfano; tawi lake likiisha kuchipuka na kuchanua majani, mwatambua ya kuwa wakati wa mavuno u karibu;
Luc 21.29-21.30 Marc 13.28-13.29
33 nanyi kadhalika, myaonapo hayo yote, tambueni ya kuwa yu karibu, milangoni.
Jacques 5.9 1 Pierre 4.7 Hébreux 10.37 Ezéchiel 7.2-7.14 Apocalypse 3.20
34 Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia.
Matthieu 16.28 Matthieu 23.36 Luc 11.50 Marc 13.30-13.31 Luc 21.32-21.33
35 Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
Esaïe 40.8 1 Pierre 1.25 Nombres 23.19 Matthieu 5.18 Esaïe 54.10

Appel à la vigilance

36 Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba peke yake.
Actes 1.7 Marc 13.32 2 Pierre 3.10 Matthieu 24.44 Matthieu 24.42
37 Kwa maana kama vile ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.
Luc 17.26-17.27 Hébreux 11.7 Genèse 7.6-7.23 2 Pierre 3.6 1 Pierre 3.20-3.21
38 Kwa kuwa kama vile siku zile zilizokuwa kabla ya Gharika watu walivyokuwa wakila, na kunywa, wakioa na kuolewa, hata siku ile aliyoingia Nuhu katika safina,
Romains 13.13-13.14 Esaïe 22.12-22.14 Amos 6.3-6.6 1 Samuel 25.36-25.38 1 Samuel 30.16-30.17
39 wasitambue, hata Gharika ikaja, ikawachukua wote, ndivyo kutakavyokuwa kuja kwake Mwana wa Adamu.
Jean 3.20 Matthieu 24.37 Actes 13.41 Proverbes 24.12 Esaïe 44.18-44.19
40 Wakati ule watu wawili watakuwako kondeni; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa;
Luc 17.34-17.37 2 Pierre 2.5 2 Pierre 2.7-2.9 1 Corinthiens 4.7 Luc 23.39-23.43
41 wanawake wawili watakuwa wakisaga; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa.
Esaïe 47.2 Exode 11.5 Luc 17.35
42 Kesheni basi; kwa maana hamjui ni siku ipi atakayokuja Bwana wenu.
Luc 21.36 Matthieu 25.13 1 Corinthiens 16.13 1 Thessaloniciens 5.6 Apocalypse 16.15
43 Lakini fahamuni neno hili; kama mwenye nyumba angaliijua ile zamu mwivi atakayokuja, angalikesha, wala asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa.
Luc 12.39 1 Thessaloniciens 5.2-5.6 Proverbes 7.19 Exode 22.2-22.3 2 Pierre 3.10-3.11
44 Kwa sababu hiyo ninyi nanyi jiwekeni tayari; kwa kuwa katika saa msiyodhani Mwana wa Adamu yuaja.
Matthieu 25.10 Matthieu 25.13 Apocalypse 19.7 Luc 12.40 Jacques 5.9
45 Ni nani basi yule mtumwa mwaminifu mwenye akili, ambaye bwana wake alimweka juu ya nyumba yake, awape watu chakula kwa wakati wake?
Matthieu 25.21 Matthieu 25.23 2 Timothée 2.2 Hébreux 3.5 1 Corinthiens 4.1-4.2
46 Heri mtumwa yule, ambaye bwana wake ajapo atamkuta akifanya hivyo.
Apocalypse 16.15 Philippiens 1.21-1.23 Luc 12.43 Luc 12.37 Apocalypse 2.19
47 Amin, nawaambieni, atamweka juu ya vitu vyake vyote.
Matthieu 25.21 Matthieu 25.23 2 Timothée 2.12 Luc 12.37 Daniel 12.3
48 Lakini mtumwa yule mbaya akisema moyoni mwake, Bwana wangu anakawia;
2 Pierre 3.3-3.5 Matthieu 18.32 Esaïe 32.6 Marc 7.21 Jean 13.2
49 akaanza kuwapiga wajoli wake, na kula na kunywa pamoja na walevi;
2 Pierre 2.13-2.14 Apocalypse 13.7 Philippiens 3.19 Apocalypse 17.6 Esaïe 66.5
50 bwana wake mtumwa huyo atakuja siku asiyodhani, na saa asiyojua,
Apocalypse 3.3 1 Thessaloniciens 5.2-5.3 Matthieu 24.42-24.44 Proverbes 29.1
51 atamkata vipande viwili, na kumwekea fungu lake pamoja na wanafiki; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.
Matthieu 8.12 Luc 13.28 Esaïe 33.14 Luc 12.46 Matthieu 25.30

Cette Bible est dans le domaine public.