Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 68.33
Bible en Swahili de l’est


Chant de triomphe et de gloire

1 Mungu huondoka, adui zake wakatawanyika, Nao wamchukiao huukimbia uso wake.
Esaïe 33.3 Nombres 10.35 Exode 20.5 Psaumes 89.10 Jean 14.23-14.24
2 Kama moshi upeperushwavyo, Ndivyo uwapeperushavyo wao; Kama nta iyeyukavyo mbele ya moto, Ndivyo waovu wapoteavyo usoni pa Mungu.
Psaumes 37.20 Michée 1.4 Osée 13.3 Psaumes 97.5 Esaïe 9.18
3 Bali wenye haki hufurahi, Na kuushangilia uso wa Mungu, Naam, hupiga kelele kwa furaha.
Psaumes 64.10 1 Thessaloniciens 5.16 Psaumes 43.4 Deutéronome 12.12 Psaumes 95.1-95.2
4 Mwimbieni Mungu, lisifuni jina lake, Mtengenezeeni njia ya barabara, Apitaye majangwani kama mpanda farasi; Jina lake ni YAHU; shangilieni mbele zake.
Exode 6.3 Deutéronome 33.26 Psaumes 18.10 Psaumes 66.4 Psaumes 68.33
5 Baba wa yatima na mwamuzi wa wajane, Mungu katika kao lake takatifu.
Psaumes 10.14 Deutéronome 10.18 Jérémie 49.11 Esaïe 1.23 2 Chroniques 6.2
6 Mungu huwakalisha wapweke nyumbani; Huwatoa wafungwa wakae hali ya kufanikiwa; Bali wakaidi hukaa katika nchi kavu.
Psaumes 107.10 Psaumes 113.9 Psaumes 107.34 Psaumes 146.7 Psaumes 107.14
7 Ee Mungu, ulipotoka mbele ya watu wako, Ulipopita nyikani,
Exode 13.21 Juges 5.4 Juges 4.14 Michée 2.13 Deutéronome 4.34
8 Nchi ilitetemeka Naam, mbingu zilidondoka usoni pa Mungu; Hata Sinai usoni pa Mungu; Mungu wa Israeli.
Exode 19.18 Juges 5.4-5.5 Exode 19.16 Psaumes 77.18 Deutéronome 5.23-5.25
9 Ee Mungu, ulinyesha mvua ya neema; Urithi wako ulipochoka uliutia nguvu.
Ezéchiel 34.26 Psaumes 78.24-78.27 Psaumes 65.9-65.13 Deutéronome 11.14 Psaumes 77.16-77.17
10 Kabila yako ilifanya kao lake huko; Ee Mungu, kwa wema wako uliwaruzuku walioonewa.
Psaumes 74.19 Psaumes 74.1-74.2 Nombres 16.3 Job 5.10-5.11 Exode 19.5-19.6
11 Bwana analitoa neno lake; Wanawake watangazao habari ni jeshi kubwa;
Exode 15.20 Psaumes 68.25 Exode 14.15 Exode 17.9-17.16 Juges 4.6-5.31
12 Wafalme wa majeshi wanakimbia, wanakimbia; Na mwanamke akaaye nyumbani agawa nyara.
Josué 10.16 Juges 5.19 1 Samuel 30.24 Josué 12.7-12.24 Nombres 31.27
13 Kwa nini kulala mazizini arukapo hua, Mbawa zake ziking’aa kama fedha Na manyoya yake kama dhahabu?
Genèse 49.14 Psaumes 105.37 Tite 3.3 Ezéchiel 16.6-16.14 Juges 5.16
14 Mwenyezi Mungu alipotawanya wafalme huko, Kulinyesha theluji katika Salmoni.
Psaumes 51.7 Esaïe 1.18 Josué 12.1-12.24 Nombres 21.3 Josué 10.10-10.43
15 Ni mlima wa Mungu mlima Bashani, Ni mlima mrefu mlima Bashani.
Deutéronome 3.10 Psaumes 87.1-87.2 Psaumes 78.68-78.69 Esaïe 2.2-2.3 Michée 7.14
16 Enyi milima mirefu, kwani kuutazama kwa wivu Mlima alioutamani Mungu akae juu yake? Naam, Bwana atakaa juu yake milele.
Deutéronome 12.5 Psaumes 132.13-132.14 Hébreux 12.22-12.23 Psaumes 87.1-87.2 Esaïe 2.2
17 Magari ya Mungu ni ishirini elfu, maelfu maelfu; Bwana yumo kati yao kama katika Sinai, Katika patakatifu.
Daniel 7.10 Deutéronome 33.2 Habakuk 3.8 Exode 3.5 2 Rois 2.11
18 Wewe umepaa juu, umeteka mateka, Umepewa vipawa katikati ya wanadamu; Naam, hata na wakaidi, Bwana Mungu akae nao.
Juges 5.12 Psaumes 78.60 Psaumes 47.5 Psaumes 24.3 Actes 2.4
19 Na ahimidiwe Bwana, Siku kwa siku hutuchukulia mzigo wetu; Mungu ndiye wokovu wetu.
Esaïe 46.4 Ephésiens 1.3 Psaumes 103.1-103.22 Psaumes 32.7 Lamentations 3.23
20 Mungu kwetu sisi ni Mungu wa kuokoa; Na njia za kutoka mautini zina YEHOVA Bwana.
Deutéronome 32.39 Apocalypse 1.18 Apocalypse 20.1 1 Samuel 2.6 Psaumes 118.17-118.18
21 Naam, Mungu atakipasua kichwa cha adui zake, Utosi wenye nywele wa mtu afulizaye kukosa.
Habakuk 3.13 Psaumes 110.6 Psaumes 7.12 Luc 13.5 Ezéchiel 18.27-18.30
22 Bwana alisema, Kutoka Bashani nitawarudisha, Nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari;
Nombres 21.33 Jérémie 23.5-23.8 Amos 9.2-9.3 Exode 14.22 Ezéchiel 36.24
23 Uuchovye mguu wako katika damu ya adui zako, Na ulimi wa mbwa zako upate sehemu yake.
1 Rois 21.19 Psaumes 58.10 1 Rois 22.38 Esaïe 63.1-63.6 Apocalypse 19.17-19.21
24 Ee Mungu, wameiona miendo yako; Miendo ya Mungu wangu, Mfalme wangu, katika patakatifu
Psaumes 47.5-47.7 1 Chroniques 13.8 Psaumes 63.2 1 Chroniques 15.16-15.24 2 Samuel 6.12-6.17
25 Waimbaji hutangulia, nyuma yao wapigao vinanda, Kati ya wanawali wapiga matari.
Juges 11.34 Exode 15.20 1 Chroniques 13.8 Jérémie 31.13 1 Samuel 18.6
26 Mhimidini Mungu katika mikutano, Bwana katika makusanyiko ya Israeli.
Esaïe 48.1 Deutéronome 33.28 Psaumes 26.12 Proverbes 5.16 Psaumes 135.19-135.21
27 Yuko Benyamini mdogo, mtawala wao; Wakuu wa Yuda, kundi lao; Wakuu wa Zabuloni; Wakuu wa Naftali.
1 Samuel 9.21 Psaumes 60.7 1 Chroniques 15.3 Esaïe 11.13 1 Chroniques 12.16
28 Ee Mungu, uziamuru nguvu zako; Ee Mungu, uwe hodari uliyetufanyia makuu.
Psaumes 44.4 Psaumes 42.8 Ephésiens 3.17-3.20 2 Corinthiens 12.9-12.10 Esaïe 40.31
29 Kwa ajili ya hekalu lako Yerusalemu Wafalme watakuletea hedaya.
1 Rois 10.10 Psaumes 76.11 Néhémie 2.8 Esdras 7.13-7.28 Psaumes 72.10-72.11
30 Mkemee mnyama wa manyasini; Kundi la mafahali, na ndama za watu; Hata wanyenyekee na kuleta vipande vya fedha, Uwatawanye watu wapendao vita.
Psaumes 18.44 Psaumes 89.10 Romains 7.22 Esaïe 34.7 Ezéchiel 29.3
31 Masheki watakuja kutoka Misri, Kushi itamnyoshea Mungu mikono yake mara.
Esaïe 45.14 Sophonie 3.10 Psaumes 44.20 Esaïe 19.18-19.25 Psaumes 72.8-72.11
32 Enyi falme za dunia, mwimbieni Mungu, Msifuni Bwana kwa nyimbo.
Psaumes 67.2-67.5 Psaumes 117.1-117.2 Apocalypse 15.4 Psaumes 102.22 Psaumes 100.1
33 Apandaye mbingu za mbingu za tangu milele; Aitoa sauti yake, sauti ya nguvu.
Psaumes 18.10 Psaumes 104.3 Psaumes 68.4 Apocalypse 11.12 Psaumes 46.6
34 Mhesabieni Mungu nguvu; Enzi yake i juu ya Israeli; Na nguvu zake zi mawinguni.
2 Pierre 1.17 Deutéronome 33.26 Apocalypse 19.6 Psaumes 29.1-29.2 1 Chroniques 16.28-16.29
35 Mungu ni mwenye kutisha Kutoka patakatifu pako. Ndiye Mungu wa Israeli; Yeye huwapa watu wake nguvu na uwezo. Na ahimidiwe Mungu.
Psaumes 29.11 Psaumes 65.5 Psaumes 66.5 Psaumes 45.4 Psaumes 47.2

Cette Bible est dans le domaine public.