Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 68.3
Bible en Swahili de l’est


Chant de triomphe et de gloire

1 Mungu huondoka, adui zake wakatawanyika, Nao wamchukiao huukimbia uso wake.
Nombres 10.35 Esaïe 33.3 Psaumes 89.10 Exode 20.5 2 Chroniques 6.41
2 Kama moshi upeperushwavyo, Ndivyo uwapeperushavyo wao; Kama nta iyeyukavyo mbele ya moto, Ndivyo waovu wapoteavyo usoni pa Mungu.
Psaumes 37.20 Michée 1.4 Osée 13.3 Psaumes 97.5 Esaïe 9.18
3 Bali wenye haki hufurahi, Na kuushangilia uso wa Mungu, Naam, hupiga kelele kwa furaha.
Psaumes 64.10 Psaumes 100.1-100.2 Apocalypse 19.7 Psaumes 21.1 Psaumes 32.11-33.1
4 Mwimbieni Mungu, lisifuni jina lake, Mtengenezeeni njia ya barabara, Apitaye majangwani kama mpanda farasi; Jina lake ni YAHU; shangilieni mbele zake.
Deutéronome 33.26 Psaumes 18.10 Exode 6.3 Psaumes 68.33 Psaumes 66.4
5 Baba wa yatima na mwamuzi wa wajane, Mungu katika kao lake takatifu.
Psaumes 10.14 Deutéronome 10.18 Jérémie 49.11 Luc 18.2-18.7 Jérémie 5.28
6 Mungu huwakalisha wapweke nyumbani; Huwatoa wafungwa wakae hali ya kufanikiwa; Bali wakaidi hukaa katika nchi kavu.
Psaumes 107.10 Psaumes 113.9 Psaumes 107.34 Psaumes 107.14 Psaumes 146.7
7 Ee Mungu, ulipotoka mbele ya watu wako, Ulipopita nyikani,
Exode 13.21 Juges 4.14 Juges 5.4 Deutéronome 4.34 Psaumes 114.1-114.8
8 Nchi ilitetemeka Naam, mbingu zilidondoka usoni pa Mungu; Hata Sinai usoni pa Mungu; Mungu wa Israeli.
Exode 19.18 Exode 19.16 Juges 5.4-5.5 Psaumes 77.18 Deutéronome 5.23-5.25
9 Ee Mungu, ulinyesha mvua ya neema; Urithi wako ulipochoka uliutia nguvu.
Psaumes 78.24-78.27 Ezéchiel 34.26 Deutéronome 11.14 Psaumes 77.16-77.17 Deutéronome 11.10-11.12
10 Kabila yako ilifanya kao lake huko; Ee Mungu, kwa wema wako uliwaruzuku walioonewa.
Psaumes 74.19 Deutéronome 32.8-32.14 1 Samuel 2.8 Deutéronome 26.5 Deutéronome 26.9-26.10
11 Bwana analitoa neno lake; Wanawake watangazao habari ni jeshi kubwa;
Exode 15.20 Psaumes 68.25 Exode 14.15 Exode 17.9-17.16 1 Samuel 18.6
12 Wafalme wa majeshi wanakimbia, wanakimbia; Na mwanamke akaaye nyumbani agawa nyara.
Josué 10.16 Juges 5.19 1 Samuel 30.24 Josué 12.7-12.24 Juges 5.30
13 Kwa nini kulala mazizini arukapo hua, Mbawa zake ziking’aa kama fedha Na manyoya yake kama dhahabu?
Genèse 49.14 Ephésiens 5.26-5.27 Apocalypse 1.5-1.6 Psaumes 149.4 1 Corinthiens 6.9-6.11
14 Mwenyezi Mungu alipotawanya wafalme huko, Kulinyesha theluji katika Salmoni.
Esaïe 1.18 Psaumes 51.7 Nombres 21.21-21.35 Juges 2.7 Juges 9.48
15 Ni mlima wa Mungu mlima Bashani, Ni mlima mrefu mlima Bashani.
Psaumes 78.68-78.69 Esaïe 2.2-2.3 Michée 7.14 Psaumes 2.6 Deutéronome 3.10
16 Enyi milima mirefu, kwani kuutazama kwa wivu Mlima alioutamani Mungu akae juu yake? Naam, Bwana atakaa juu yake milele.
Deutéronome 12.5 Psaumes 132.13-132.14 Hébreux 12.22-12.23 1 Rois 9.3 Psaumes 114.4
17 Magari ya Mungu ni ishirini elfu, maelfu maelfu; Bwana yumo kati yao kama katika Sinai, Katika patakatifu.
Daniel 7.10 Deutéronome 33.2 Apocalypse 5.11 Apocalypse 9.16 Ezéchiel 1.15-1.28
18 Wewe umepaa juu, umeteka mateka, Umepewa vipawa katikati ya wanadamu; Naam, hata na wakaidi, Bwana Mungu akae nao.
Juges 5.12 Psaumes 47.5 Psaumes 78.60 Actes 1.2-1.9 Apocalypse 21.3
19 Na ahimidiwe Bwana, Siku kwa siku hutuchukulia mzigo wetu; Mungu ndiye wokovu wetu.
Esaïe 46.4 Ephésiens 1.3 Psaumes 139.17 Psaumes 72.17-72.19 Psaumes 55.22
20 Mungu kwetu sisi ni Mungu wa kuokoa; Na njia za kutoka mautini zina YEHOVA Bwana.
Deutéronome 32.39 Apocalypse 20.1 Apocalypse 1.18 Psaumes 56.13 Jean 5.28-5.29
21 Naam, Mungu atakipasua kichwa cha adui zake, Utosi wenye nywele wa mtu afulizaye kukosa.
Habakuk 3.13 Luc 13.5 Ezéchiel 18.27-18.30 Psaumes 110.6 Psaumes 7.12
22 Bwana alisema, Kutoka Bashani nitawarudisha, Nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari;
Nombres 21.33 Esaïe 49.22 Esaïe 11.11-11.16 Osée 1.10-1.11 Jérémie 23.5-23.8
23 Uuchovye mguu wako katika damu ya adui zako, Na ulimi wa mbwa zako upate sehemu yake.
Psaumes 58.10 1 Rois 21.19 1 Rois 22.38 Esaïe 63.1-63.6 Apocalypse 19.17-19.21
24 Ee Mungu, wameiona miendo yako; Miendo ya Mungu wangu, Mfalme wangu, katika patakatifu
Psaumes 63.2 1 Chroniques 15.16-15.24 2 Samuel 6.12-6.17 Psaumes 24.7-24.10 Psaumes 47.5-47.7
25 Waimbaji hutangulia, nyuma yao wapigao vinanda, Kati ya wanawali wapiga matari.
Juges 11.34 Exode 15.20 1 Chroniques 13.8 Jérémie 31.4 Psaumes 150.3-150.5
26 Mhimidini Mungu katika mikutano, Bwana katika makusanyiko ya Israeli.
Esaïe 48.1 Deutéronome 33.28 Psaumes 26.12 Psaumes 107.32 1 Chroniques 16.7-16.36
27 Yuko Benyamini mdogo, mtawala wao; Wakuu wa Yuda, kundi lao; Wakuu wa Zabuloni; Wakuu wa Naftali.
1 Samuel 9.21 1 Chroniques 12.29 Psaumes 47.9 1 Chroniques 27.12 Ezéchiel 37.19-37.27
28 Ee Mungu, uziamuru nguvu zako; Ee Mungu, uwe hodari uliyetufanyia makuu.
Psaumes 42.8 Psaumes 44.4 Jean 5.8-5.9 Psaumes 71.3 2 Thessaloniciens 1.11
29 Kwa ajili ya hekalu lako Yerusalemu Wafalme watakuletea hedaya.
1 Rois 10.10 Psaumes 76.11 Esaïe 18.7 1 Chroniques 17.4-17.12 2 Chroniques 32.23
30 Mkemee mnyama wa manyasini; Kundi la mafahali, na ndama za watu; Hata wanyenyekee na kuleta vipande vya fedha, Uwatawanye watu wapendao vita.
Jacques 4.1 Psaumes 2.12 2 Chroniques 20.1-20.37 2 Samuel 8.1-8.18 2 Chroniques 14.1-14.15
31 Masheki watakuja kutoka Misri, Kushi itamnyoshea Mungu mikono yake mara.
Esaïe 45.14 Sophonie 3.10 Psaumes 44.20 Actes 8.27-8.40 Psaumes 143.6
32 Enyi falme za dunia, mwimbieni Mungu, Msifuni Bwana kwa nyimbo.
Psaumes 102.22 Psaumes 100.1 Romains 15.10-15.11 Deutéronome 32.43 Psaumes 67.2-67.5
33 Apandaye mbingu za mbingu za tangu milele; Aitoa sauti yake, sauti ya nguvu.
Psaumes 18.10 Psaumes 104.3 Apocalypse 11.19 Psaumes 102.25 Psaumes 29.3-29.9
34 Mhesabieni Mungu nguvu; Enzi yake i juu ya Israeli; Na nguvu zake zi mawinguni.
Psaumes 29.1-29.2 1 Chroniques 16.28-16.29 Psaumes 96.6-96.8 Psaumes 150.1 2 Pierre 1.17
35 Mungu ni mwenye kutisha Kutoka patakatifu pako. Ndiye Mungu wa Israeli; Yeye huwapa watu wake nguvu na uwezo. Na ahimidiwe Mungu.
Psaumes 29.11 Psaumes 65.5 Psaumes 66.5 Néhémie 1.5 Hébreux 12.24-12.29

Cette Bible est dans le domaine public.