Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 68.25
Bible en Swahili de l’est


Chant de triomphe et de gloire

1 Mungu huondoka, adui zake wakatawanyika, Nao wamchukiao huukimbia uso wake.
Nombres 10.35 Esaïe 33.3 Psaumes 89.10 Exode 20.5 Psaumes 78.65-78.68
2 Kama moshi upeperushwavyo, Ndivyo uwapeperushavyo wao; Kama nta iyeyukavyo mbele ya moto, Ndivyo waovu wapoteavyo usoni pa Mungu.
Psaumes 37.20 Michée 1.4 Esaïe 9.18 Osée 13.3 Psaumes 97.5
3 Bali wenye haki hufurahi, Na kuushangilia uso wa Mungu, Naam, hupiga kelele kwa furaha.
Psaumes 64.10 Psaumes 97.12 Psaumes 100.1-100.2 Apocalypse 19.7 Psaumes 21.1
4 Mwimbieni Mungu, lisifuni jina lake, Mtengenezeeni njia ya barabara, Apitaye majangwani kama mpanda farasi; Jina lake ni YAHU; shangilieni mbele zake.
Deutéronome 33.26 Psaumes 18.10 Exode 6.3 Psaumes 68.33 Psaumes 66.4
5 Baba wa yatima na mwamuzi wa wajane, Mungu katika kao lake takatifu.
Psaumes 10.14 Deutéronome 10.18 Jérémie 49.11 Luc 18.2-18.7 Jérémie 5.28
6 Mungu huwakalisha wapweke nyumbani; Huwatoa wafungwa wakae hali ya kufanikiwa; Bali wakaidi hukaa katika nchi kavu.
Psaumes 107.10 Psaumes 113.9 Psaumes 107.34 Psaumes 107.14 Psaumes 146.7
7 Ee Mungu, ulipotoka mbele ya watu wako, Ulipopita nyikani,
Exode 13.21 Juges 4.14 Juges 5.4 Deutéronome 4.34 Psaumes 114.1-114.8
8 Nchi ilitetemeka Naam, mbingu zilidondoka usoni pa Mungu; Hata Sinai usoni pa Mungu; Mungu wa Israeli.
Exode 19.18 Exode 19.16 Juges 5.4-5.5 Psaumes 77.18 Deutéronome 5.23-5.25
9 Ee Mungu, ulinyesha mvua ya neema; Urithi wako ulipochoka uliutia nguvu.
Psaumes 78.24-78.27 Ezéchiel 34.26 Deutéronome 11.14 Psaumes 77.16-77.17 Deutéronome 11.10-11.12
10 Kabila yako ilifanya kao lake huko; Ee Mungu, kwa wema wako uliwaruzuku walioonewa.
Psaumes 74.19 Matthieu 11.5 Deutéronome 32.8-32.14 1 Samuel 2.8 Deutéronome 26.5
11 Bwana analitoa neno lake; Wanawake watangazao habari ni jeshi kubwa;
Exode 15.20 Psaumes 68.25 Exode 14.15 Exode 17.9-17.16 1 Samuel 18.6
12 Wafalme wa majeshi wanakimbia, wanakimbia; Na mwanamke akaaye nyumbani agawa nyara.
Josué 10.16 Juges 5.19 Josué 12.7-12.24 1 Samuel 30.24 Juges 5.30
13 Kwa nini kulala mazizini arukapo hua, Mbawa zake ziking’aa kama fedha Na manyoya yake kama dhahabu?
Genèse 49.14 Exode 1.14 Ephésiens 5.26-5.27 Apocalypse 1.5-1.6 Psaumes 149.4
14 Mwenyezi Mungu alipotawanya wafalme huko, Kulinyesha theluji katika Salmoni.
Esaïe 1.18 Psaumes 51.7 Nombres 21.21-21.35 Juges 2.7 Juges 9.48
15 Ni mlima wa Mungu mlima Bashani, Ni mlima mrefu mlima Bashani.
Psaumes 78.68-78.69 Esaïe 2.2-2.3 Michée 7.14 Psaumes 2.6 Deutéronome 3.10
16 Enyi milima mirefu, kwani kuutazama kwa wivu Mlima alioutamani Mungu akae juu yake? Naam, Bwana atakaa juu yake milele.
Deutéronome 12.5 Psaumes 132.13-132.14 Hébreux 12.22-12.23 1 Rois 9.3 Psaumes 114.4
17 Magari ya Mungu ni ishirini elfu, maelfu maelfu; Bwana yumo kati yao kama katika Sinai, Katika patakatifu.
Daniel 7.10 Deutéronome 33.2 Psaumes 18.10 Apocalypse 5.11 Apocalypse 9.16
18 Wewe umepaa juu, umeteka mateka, Umepewa vipawa katikati ya wanadamu; Naam, hata na wakaidi, Bwana Mungu akae nao.
Juges 5.12 Psaumes 47.5 Psaumes 78.60 Psaumes 110.1 Jean 16.7
19 Na ahimidiwe Bwana, Siku kwa siku hutuchukulia mzigo wetu; Mungu ndiye wokovu wetu.
Esaïe 46.4 Ephésiens 1.3 Psaumes 139.17 Psaumes 72.17-72.19 Psaumes 55.22
20 Mungu kwetu sisi ni Mungu wa kuokoa; Na njia za kutoka mautini zina YEHOVA Bwana.
Deutéronome 32.39 Apocalypse 20.1 Apocalypse 1.18 Esaïe 12.2 Psaumes 56.13
21 Naam, Mungu atakipasua kichwa cha adui zake, Utosi wenye nywele wa mtu afulizaye kukosa.
Habakuk 3.13 Psaumes 7.12 Luc 13.5 Ezéchiel 18.27-18.30 Psaumes 110.6
22 Bwana alisema, Kutoka Bashani nitawarudisha, Nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari;
Nombres 21.33 Esaïe 49.22 Esaïe 11.11-11.16 Osée 1.10-1.11 Jérémie 23.5-23.8
23 Uuchovye mguu wako katika damu ya adui zako, Na ulimi wa mbwa zako upate sehemu yake.
Psaumes 58.10 1 Rois 21.19 1 Rois 22.38 Esaïe 63.1-63.6 Apocalypse 19.17-19.21
24 Ee Mungu, wameiona miendo yako; Miendo ya Mungu wangu, Mfalme wangu, katika patakatifu
Psaumes 63.2 1 Chroniques 15.16-15.24 2 Samuel 6.12-6.17 Psaumes 24.7-24.10 Psaumes 47.5-47.7
25 Waimbaji hutangulia, nyuma yao wapigao vinanda, Kati ya wanawali wapiga matari.
Juges 11.34 Exode 15.20 1 Chroniques 13.8 Psaumes 87.7 Jérémie 31.4
26 Mhimidini Mungu katika mikutano, Bwana katika makusanyiko ya Israeli.
Esaïe 48.1 Deutéronome 33.28 Psaumes 26.12 Psaumes 107.32 1 Chroniques 16.7-16.36
27 Yuko Benyamini mdogo, mtawala wao; Wakuu wa Yuda, kundi lao; Wakuu wa Zabuloni; Wakuu wa Naftali.
1 Samuel 9.21 Genèse 42.32 1 Chroniques 12.29 Psaumes 47.9 1 Chroniques 27.12
28 Ee Mungu, uziamuru nguvu zako; Ee Mungu, uwe hodari uliyetufanyia makuu.
Psaumes 42.8 Psaumes 44.4 Psaumes 138.8 Jean 5.8-5.9 Psaumes 71.3
29 Kwa ajili ya hekalu lako Yerusalemu Wafalme watakuletea hedaya.
1 Rois 10.10 Psaumes 76.11 Esaïe 60.16-60.17 Esaïe 18.7 1 Chroniques 17.4-17.12
30 Mkemee mnyama wa manyasini; Kundi la mafahali, na ndama za watu; Hata wanyenyekee na kuleta vipande vya fedha, Uwatawanye watu wapendao vita.
Psaumes 120.7 Jacques 4.1 Psaumes 2.12 2 Chroniques 20.1-20.37 2 Samuel 8.1-8.18
31 Masheki watakuja kutoka Misri, Kushi itamnyoshea Mungu mikono yake mara.
Esaïe 45.14 Sophonie 3.10 Psaumes 44.20 Esaïe 66.19 Actes 8.27-8.40
32 Enyi falme za dunia, mwimbieni Mungu, Msifuni Bwana kwa nyimbo.
Psaumes 102.22 Psaumes 100.1 Romains 15.10-15.11 Deutéronome 32.43 Psaumes 67.2-67.5
33 Apandaye mbingu za mbingu za tangu milele; Aitoa sauti yake, sauti ya nguvu.
Psaumes 18.10 Psaumes 104.3 Deutéronome 10.14 Apocalypse 11.19 Psaumes 102.25
34 Mhesabieni Mungu nguvu; Enzi yake i juu ya Israeli; Na nguvu zake zi mawinguni.
Psaumes 29.1-29.2 1 Chroniques 16.28-16.29 Psaumes 96.6-96.8 Psaumes 150.1 2 Pierre 1.17
35 Mungu ni mwenye kutisha Kutoka patakatifu pako. Ndiye Mungu wa Israeli; Yeye huwapa watu wake nguvu na uwezo. Na ahimidiwe Mungu.
Psaumes 29.11 Psaumes 65.5 Psaumes 66.5 Néhémie 1.5 Hébreux 12.24-12.29

Cette Bible est dans le domaine public.