1 Mungu huondoka, adui zake wakatawanyika, Nao wamchukiao huukimbia uso wake.
Esaïe 33.3  Nombres 10.35  Psaumes 89.10  Exode 20.5  Psaumes 68.14  
 2 Kama moshi upeperushwavyo, Ndivyo uwapeperushavyo wao; Kama nta iyeyukavyo mbele ya moto, Ndivyo waovu wapoteavyo usoni pa Mungu.
Psaumes 37.20  Michée 1.4  Osée 13.3  Psaumes 97.5  Esaïe 9.18  
 3 Bali wenye haki hufurahi, Na kuushangilia uso wa Mungu, Naam, hupiga kelele kwa furaha.
Psaumes 64.10  Apocalypse 18.20  1 Thessaloniciens 5.16  Psaumes 43.4  Deutéronome 12.12  
 4 Mwimbieni Mungu, lisifuni jina lake, Mtengenezeeni njia ya barabara, Apitaye majangwani kama mpanda farasi; Jina lake ni YAHU; shangilieni mbele zake.
Exode 6.3  Deutéronome 33.26  Psaumes 18.10  Psaumes 66.4  Psaumes 68.33  
 5 Baba wa yatima na mwamuzi wa wajane, Mungu katika kao lake takatifu.
Psaumes 10.14  Deutéronome 10.18  Jérémie 49.11  Psaumes 72.4  Esaïe 1.23  
 6 Mungu huwakalisha wapweke nyumbani; Huwatoa wafungwa wakae hali ya kufanikiwa; Bali wakaidi hukaa katika nchi kavu.
Psaumes 107.10  Psaumes 113.9  Psaumes 107.34  Psaumes 107.14  Psaumes 146.7  
 7 Ee Mungu, ulipotoka mbele ya watu wako, Ulipopita nyikani,
Exode 13.21  Juges 5.4  Juges 4.14  Psaumes 114.1-114.8  Habakuk 3.12-3.13  
 8 Nchi ilitetemeka Naam, mbingu zilidondoka usoni pa Mungu; Hata Sinai usoni pa Mungu; Mungu wa Israeli.
Exode 19.18  Juges 5.4-5.5  Exode 19.16  Deutéronome 5.23-5.25  Psaumes 77.18  
 9 Ee Mungu, ulinyesha mvua ya neema; Urithi wako ulipochoka uliutia nguvu.
Psaumes 78.24-78.27  Ezéchiel 34.26  Deutéronome 11.10-11.12  Psaumes 65.9-65.13  Deutéronome 11.14  
 10 Kabila yako ilifanya kao lake huko; Ee Mungu, kwa wema wako uliwaruzuku walioonewa.
Psaumes 74.19  1 Pierre 5.3  Psaumes 78.20  Psaumes 74.1-74.2  Nombres 16.3  
 11 Bwana analitoa neno lake; Wanawake watangazao habari ni jeshi kubwa;
Exode 15.20  Psaumes 68.25  Exode 14.15  Exode 17.9-17.16  Ephésiens 4.11  
 12 Wafalme wa majeshi wanakimbia, wanakimbia; Na mwanamke akaaye nyumbani agawa nyara.Josué 10.16  Juges 5.19  1 Samuel 30.24  Josué 12.7-12.24  Apocalypse 19.17-19.20  
 13 Kwa nini kulala mazizini arukapo hua, Mbawa zake ziking’aa kama fedha Na manyoya yake kama dhahabu?
Genèse 49.14  Luc 15.16  Ephésiens 2.1-2.3  Psaumes 105.37  Tite 3.3  
 14 Mwenyezi Mungu alipotawanya wafalme huko, Kulinyesha theluji katika Salmoni.
Esaïe 1.18  Psaumes 51.7  Juges 9.48  Josué 12.1-12.24  Nombres 21.3  
 15 Ni mlima wa Mungu mlima Bashani, Ni mlima mrefu mlima Bashani.
Michée 7.14  Psaumes 2.6  Deutéronome 3.10  Psaumes 87.1-87.2  Psaumes 78.68-78.69  
 16 Enyi milima mirefu, kwani kuutazama kwa wivu Mlima alioutamani Mungu akae juu yake? Naam, Bwana atakaa juu yake milele.
Deutéronome 12.5  Psaumes 132.13-132.14  Hébreux 12.22-12.23  Psaumes 114.6  Apocalypse 21.2-21.3  
 17 Magari ya Mungu ni ishirini elfu, maelfu maelfu; Bwana yumo kati yao kama katika Sinai, Katika patakatifu.
Daniel 7.10  Deutéronome 33.2  Matthieu 26.53  2 Rois 6.16-6.17  Habakuk 3.8  
 18 Wewe umepaa juu, umeteka mateka, Umepewa vipawa katikati ya wanadamu; Naam, hata na wakaidi, Bwana Mungu akae nao.
Juges 5.12  Psaumes 47.5  Psaumes 78.60  Apocalypse 21.3  Jean 14.23  
 19 Na ahimidiwe Bwana, Siku kwa siku hutuchukulia mzigo wetu; Mungu ndiye wokovu wetu.
Esaïe 46.4  Ephésiens 1.3  Psaumes 72.17-72.19  Psaumes 55.22  Psaumes 103.1-103.22  
 20 Mungu kwetu sisi ni Mungu wa kuokoa; Na njia za kutoka mautini zina YEHOVA Bwana.
Deutéronome 32.39  Apocalypse 1.18  Apocalypse 20.1  Esaïe 45.17-45.22  Jean 5.23  
 21 Naam, Mungu atakipasua kichwa cha adui zake, Utosi wenye nywele wa mtu afulizaye kukosa.
Habakuk 3.13  Ezéchiel 18.27-18.30  Psaumes 110.6  Psaumes 7.12  Luc 13.5  
 22 Bwana alisema, Kutoka Bashani nitawarudisha, Nitawarudisha kutoka vilindi vya bahari;
Nombres 21.33  Osée 1.10-1.11  Jérémie 23.5-23.8  Amos 9.2-9.3  Exode 14.22  
 23 Uuchovye mguu wako katika damu ya adui zako, Na ulimi wa mbwa zako upate sehemu yake.
1 Rois 21.19  Psaumes 58.10  1 Rois 22.38  Apocalypse 19.17-19.21  2 Rois 9.33-9.37  
 24 Ee Mungu, wameiona miendo yako; Miendo ya Mungu wangu, Mfalme wangu, katika patakatifu
2 Samuel 6.12-6.17  Psaumes 24.7-24.10  Psaumes 47.5-47.7  1 Chroniques 13.8  Psaumes 63.2  
 25 Waimbaji hutangulia, nyuma yao wapigao vinanda, Kati ya wanawali wapiga matari.
Juges 11.34  Exode 15.20  1 Chroniques 13.8  Apocalypse 14.2-14.3  Apocalypse 15.2-15.3  
 26 Mhimidini Mungu katika mikutano, Bwana katika makusanyiko ya Israeli.
Esaïe 48.1  Deutéronome 33.28  Psaumes 26.12  1 Chroniques 16.7-16.36  Psaumes 111.1  
 27 Yuko Benyamini mdogo, mtawala wao; Wakuu wa Yuda, kundi lao; Wakuu wa Zabuloni; Wakuu wa Naftali.
1 Samuel 9.21  Juges 20.35  Juges 21.6-21.25  Psaumes 60.7  1 Chroniques 15.3  
 28 Ee Mungu, uziamuru nguvu zako; Ee Mungu, uwe hodari uliyetufanyia makuu.
Psaumes 42.8  Psaumes 44.4  2 Thessaloniciens 1.11  Ephésiens 3.17-3.20  2 Corinthiens 12.9-12.10  
 29 Kwa ajili ya hekalu lako Yerusalemu Wafalme watakuletea hedaya.
1 Rois 10.10  Psaumes 76.11  2 Chroniques 32.33  Néhémie 2.8  Esdras 7.13-7.28  
 30 Mkemee mnyama wa manyasini; Kundi la mafahali, na ndama za watu; Hata wanyenyekee na kuleta vipande vya fedha, Uwatawanye watu wapendao vita.
2 Samuel 10.1-10.19  Esaïe 37.1-37.38  Psaumes 18.44  Psaumes 89.10  Romains 7.22  
 31 Masheki watakuja kutoka Misri, Kushi itamnyoshea Mungu mikono yake mara.
Esaïe 45.14  Sophonie 3.10  Psaumes 44.20  Psaumes 143.6  Esaïe 60.6-60.7  
 32 Enyi falme za dunia, mwimbieni Mungu, Msifuni Bwana kwa nyimbo.
Romains 15.10-15.11  Deutéronome 32.43  Psaumes 67.2-67.5  Psaumes 117.1-117.2  Apocalypse 15.4  
 33 Apandaye mbingu za mbingu za tangu milele; Aitoa sauti yake, sauti ya nguvu.
Psaumes 18.10  Psaumes 104.3  Ezéchiel 10.5  1 Rois 8.27  Psaumes 68.4  
 34 Mhesabieni Mungu nguvu; Enzi yake i juu ya Israeli; Na nguvu zake zi mawinguni.
Psaumes 96.6-96.8  Psaumes 150.1  2 Pierre 1.17  Deutéronome 33.26  Apocalypse 19.6  
 35 Mungu ni mwenye kutisha Kutoka patakatifu pako. Ndiye Mungu wa Israeli; Yeye huwapa watu wake nguvu na uwezo. Na ahimidiwe Mungu.
Psaumes 29.11  Psaumes 65.5  Psaumes 66.5  Ephésiens 3.16  Esaïe 40.29