Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Luc 17.17
Bible en Swahili de l’est


Le pardon et la foi

1 Akawaambia wanafunzi wake, Makwazo hayana budi kuja, lakini ole wake mtu yule ambaye yaja kwa sababu yake!
Matthieu 18.7 1 Corinthiens 11.19 Romains 14.20-14.21 Romains 16.17 1 Corinthiens 8.13
2 Ingemfaa zaidi mtu huyo jiwe la kusagia lifungwe shingoni mwake, akatupwe baharini, kuliko kumkosesha mmojawapo wa wadogo hawa.
Marc 9.42 Matthieu 18.3-18.6 Matthieu 18.10 Matthieu 18.14 1 Corinthiens 9.22
3 Jilindeni; kama ndugu yako akikosa, mwonye; akitubu msamehe.
Lévitique 19.17 Matthieu 18.21 Matthieu 18.15-18.17 2 Chroniques 19.6-19.7 Psaumes 141.5
4 Na kama akikukosa mara saba katika siku moja, na kurudi kwako mara saba, akisema, Nimetubu, msamehe.
Matthieu 18.21-18.22 Colossiens 3.12-3.13 Romains 12.20 Matthieu 18.35 2 Thessaloniciens 3.13-3.14
5 Mitume wakamwambia Bwana, Tuongezee imani.
Marc 9.24 Hébreux 12.2 2 Thessaloniciens 1.3 Marc 6.30 1 Pierre 1.22-1.23
6 Bwana akasema, Kama mngekuwa na imani kiasi cha chembe ya haradali, mngeuambia mkuyu huu, Ng’oka, ukapandwe baharini, nao ungewatii.
Matthieu 17.20 Marc 9.23 Matthieu 21.21 Marc 11.22-11.23 1 Corinthiens 13.2
7 Lakini, ni nani kwenu mwenye mtumwa alimaye au achungaye ng’ombe, atakayemwambia mara arudipo kutoka shambani, Njoo upesi, keti, ule chakula?
8 Je! Hatamwambia, Nifanyie tayari chakula, nile; jifunge unitumikie, hata niishe kula na kunywa, ndipo nawe utakapokula na kunywa?
Luc 12.37 Genèse 43.16 2 Samuel 12.20
9 Je! Atampa asante yule mtumwa, kwa sababu ameyafanya aliyoagizwa?
10 Vivyo hivyo nanyi, mtakapokwisha kuyafanya yote mliyoagizwa, semeni, Sisi tu watumwa wasio na faida; tumefanya tu yaliyotupasa kufanya.
1 Pierre 5.5-5.6 Psaumes 16.2-16.3 Romains 11.35 Romains 3.12 Esaïe 6.5

Guérison de dix lépreux

11 Ikawa walipokuwa njiani kwenda Yerusalemu, alikuwa akipita katikati ya Samaria na Galilaya.
Luc 9.51-9.52 Jean 4.3-4.4
12 Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali,
Lévitique 13.45-13.46 2 Rois 5.27 Luc 18.13 2 Rois 7.3 2 Chroniques 26.20-26.21
13 wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu!
Marc 9.22 Matthieu 20.30-20.31 Matthieu 9.27 Luc 18.38-18.39 Matthieu 15.22
14 Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika.
Luc 5.14 Matthieu 3.15 Jean 11.10 Jean 2.5 Lévitique 13.1-13.46
15 Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, huku akimtukuza Mungu kwa sauti kuu;
Luc 17.17-17.18 Psaumes 107.20-107.22 Jean 9.38 Psaumes 103.1-103.4 Jean 5.14
16 akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria.
Matthieu 10.5 Actes 1.8 Apocalypse 5.14 Jean 5.23 Actes 8.5-8.25
17 Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi?
Romains 1.21 Jean 8.7-8.10 Psaumes 106.13 Genèse 3.9
18 Je! Hawakuonekana waliorudi kumpa Mungu utukufu ila mgeni huyu?
Psaumes 106.13 Psaumes 50.23 Matthieu 8.10 Apocalypse 14.7 Matthieu 19.30
19 Akamwambia, Inuka, enenda zako, imani yako imekuokoa.
Matthieu 9.22 Marc 5.34 Marc 10.52 Luc 18.42 Luc 8.48

La venue du royaume de Dieu

20 Na alipoulizwa na Mafarisayo, Ufalme wa Mungu utakuja lini? Aliwajibu akawaambia, ufalme wa Mungu hauji kwa kuuchunguza;
Luc 19.11 Luc 17.23-17.24 Jean 18.36 Actes 1.6-1.7 Luc 16.16
21 wala hawatasema, Tazama, upo huku, au, kule, kwa maana, tazama, ufalme wa Mungu umo ndani yenu.
Matthieu 12.28 Romains 14.17 Luc 10.9-10.11 Matthieu 24.23-24.28 Colossiens 1.27
22 Akawaambia wanafunzi, Siku zitakuja mtakapotamani kuona siku moja katika siku zake Mwana wa Adamu, msiione.
Luc 5.35 Matthieu 9.15 Luc 13.35 Jean 17.11-17.13 Jean 16.16-16.22
23 Tena watawaambia, Tazama, kule! Tazama, huku! Msiondoke mahali mlipo, wala msiwafuate;
Luc 21.8 Luc 17.21 Matthieu 24.23-24.26 Marc 13.21-13.23
24 kwa kuwa, kama vile umeme umulikavyo toka upande huu chini ya mbingu hata upande huu chini ya mbingu, ndivyo atakavyokuwa Mwana wa Adamu katika siku yake.
Matthieu 24.27 2 Thessaloniciens 2.2 Matthieu 24.30 2 Pierre 3.10 Malachie 3.1-3.2
25 Lakini kwanza, hana budi kupata mateso mengi, na kukataliwa na kizazi hiki.
Matthieu 16.21 Luc 9.22 Marc 8.31 Marc 12.10 Matthieu 17.22-17.23
26 Na kama ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa katika siku zake Mwana wa Adamu.
2 Pierre 2.5 Genèse 7.7-7.23 Hébreux 11.7 Matthieu 24.37-24.39 Luc 17.22
27 Walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakioa na kuolewa, hata siku ile Nuhu aliyoingia katika safina, gharika ikashuka ikawaangamiza wote.
Deutéronome 6.10-6.12 Deutéronome 8.12-8.14 Esaïe 21.4 Esaïe 22.12-22.14 1 Samuel 25.36-25.38
28 Na kadhalika, kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakinunua na kuuza, wakipanda na kujenga;
Genèse 18.20-18.21 Genèse 13.13 Genèse 19.1-19.28 Ezéchiel 16.49-16.50 Jacques 5.1-5.5
29 lakini siku ile Lutu aliyotoka Sodoma kulinyesha moto na kibiriti kutoka mbinguni vikawaangamiza wote.
2 Pierre 2.6 Esaïe 13.19 Apocalypse 11.8 Sophonie 2.9 Matthieu 11.23-11.24
30 Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku ile atakayofunuliwa Mwana wa Adamu.
Apocalypse 1.7 2 Thessaloniciens 1.7 Matthieu 24.3 1 Corinthiens 1.7 1 Pierre 1.13
31 Katika siku ile, aliye juu ya dari, na vyombo vyake vimo ndani ya nyumba, asishuke ili kuvitwaa; na kadhalika, aliye shambani asirejee nyuma.
Jérémie 45.5 Marc 13.14-13.16 Matthieu 6.25 Matthieu 16.26 Philippiens 3.7-3.8
32 Mkumbukeni mkewe Lutu.
Genèse 19.26 Hébreux 10.38-10.39 2 Pierre 2.18-2.22 Genèse 19.17 1 Corinthiens 10.6-10.12
33 Mtu ye yote atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza; na ye yote atakayeiangamiza ataiponya.
Jean 12.25 Matthieu 10.39 Marc 8.35-8.37 Luc 9.24-9.25 Matthieu 16.25
34 Nawaambia, usiku huo watu wawili watakuwa katika kitanda kimoja; mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.
Matthieu 24.40-24.41 Ezéchiel 9.4-9.6 Matthieu 24.25 Malachie 3.16-3.18 Luc 13.24
35 Wanawake wawili watakuwa wakisaga pamoja; mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.
Matthieu 24.41 Exode 11.5 Juges 16.21
36 Watu wawili watakuwa shambani, mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.]
37 Wakajibu, wakamwuliza, Wapi, Bwana? Akawaambia, Ulipo mzoga, ndipo watakapokutanika tai.
Matthieu 24.28 Zacharie 14.2 Daniel 9.26-9.27 Zacharie 13.8-13.9 Apocalypse 19.17-19.18

Cette Bible est dans le domaine public.