Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Luc 17.13
Bible en Swahili de l’est


Le pardon et la foi

1 Akawaambia wanafunzi wake, Makwazo hayana budi kuja, lakini ole wake mtu yule ambaye yaja kwa sababu yake!
Matthieu 18.7 1 Corinthiens 11.19 1 Corinthiens 8.13 1 Corinthiens 10.32 Apocalypse 13.14-13.18
2 Ingemfaa zaidi mtu huyo jiwe la kusagia lifungwe shingoni mwake, akatupwe baharini, kuliko kumkosesha mmojawapo wa wadogo hawa.
Marc 9.42 Matthieu 18.10 Matthieu 18.14 Matthieu 18.3-18.6 Matthieu 26.24
3 Jilindeni; kama ndugu yako akikosa, mwonye; akitubu msamehe.
Matthieu 18.21 Lévitique 19.17 Matthieu 18.15-18.17 Ephésiens 5.15 Proverbes 27.5
4 Na kama akikukosa mara saba katika siku moja, na kurudi kwako mara saba, akisema, Nimetubu, msamehe.
Matthieu 18.21-18.22 2 Thessaloniciens 3.13-3.14 Ephésiens 4.31-4.32 Matthieu 6.14-6.15 Matthieu 6.12
5 Mitume wakamwambia Bwana, Tuongezee imani.
Marc 9.24 Hébreux 12.2 2 Thessaloniciens 1.3 1 Pierre 1.22-1.23 Philippiens 4.13
6 Bwana akasema, Kama mngekuwa na imani kiasi cha chembe ya haradali, mngeuambia mkuyu huu, Ng’oka, ukapandwe baharini, nao ungewatii.
Matthieu 17.20 Matthieu 21.21 Marc 9.23 Matthieu 13.31-13.32 Marc 11.22-11.23
7 Lakini, ni nani kwenu mwenye mtumwa alimaye au achungaye ng’ombe, atakayemwambia mara arudipo kutoka shambani, Njoo upesi, keti, ule chakula?
8 Je! Hatamwambia, Nifanyie tayari chakula, nile; jifunge unitumikie, hata niishe kula na kunywa, ndipo nawe utakapokula na kunywa?
Luc 12.37 Genèse 43.16 2 Samuel 12.20
9 Je! Atampa asante yule mtumwa, kwa sababu ameyafanya aliyoagizwa?
10 Vivyo hivyo nanyi, mtakapokwisha kuyafanya yote mliyoagizwa, semeni, Sisi tu watumwa wasio na faida; tumefanya tu yaliyotupasa kufanya.
Esaïe 6.5 1 Corinthiens 9.16-9.17 Job 35.6-35.7 Matthieu 25.30 1 Pierre 5.5-5.6

Guérison de dix lépreux

11 Ikawa walipokuwa njiani kwenda Yerusalemu, alikuwa akipita katikati ya Samaria na Galilaya.
Luc 9.51-9.52 Jean 4.3-4.4
12 Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali,
Lévitique 13.45-13.46 Luc 5.12 2 Rois 5.27 Luc 18.13 2 Rois 7.3
13 wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu!
Matthieu 15.22 Marc 9.22 Matthieu 20.30-20.31 Matthieu 9.27 Luc 18.38-18.39
14 Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika.
Luc 5.14 Matthieu 3.15 Jean 11.10 Lévitique 14.1-14.32 Matthieu 8.3-8.4
15 Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, huku akimtukuza Mungu kwa sauti kuu;
Luc 17.17-17.18 Jean 9.38 Psaumes 103.1-103.4 Jean 5.14 Psaumes 118.18-118.19
16 akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria.
Matthieu 10.5 Apocalypse 19.10 Apocalypse 4.10 Apocalypse 19.4-19.5 Actes 1.8
17 Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi?
Romains 1.21 Jean 8.7-8.10 Psaumes 106.13 Genèse 3.9
18 Je! Hawakuonekana waliorudi kumpa Mungu utukufu ila mgeni huyu?
Psaumes 106.13 Matthieu 19.30 Psaumes 29.1-29.2 Matthieu 8.12 Matthieu 15.24-15.28
19 Akamwambia, Inuka, enenda zako, imani yako imekuokoa.
Matthieu 9.22 Luc 18.42 Marc 5.34 Marc 10.52 Luc 7.50

La venue du royaume de Dieu

20 Na alipoulizwa na Mafarisayo, Ufalme wa Mungu utakuja lini? Aliwajibu akawaambia, ufalme wa Mungu hauji kwa kuuchunguza;
Luc 19.11 Luc 17.23-17.24 Actes 1.6-1.7 Luc 16.16 Jean 18.36
21 wala hawatasema, Tazama, upo huku, au, kule, kwa maana, tazama, ufalme wa Mungu umo ndani yenu.
Romains 14.17 Matthieu 12.28 Luc 10.9-10.11 Colossiens 1.27 Matthieu 24.23-24.28
22 Akawaambia wanafunzi, Siku zitakuja mtakapotamani kuona siku moja katika siku zake Mwana wa Adamu, msiione.
Luc 5.35 Matthieu 9.15 Jean 8.21-8.24 Jean 7.33-7.36 Jean 13.33
23 Tena watawaambia, Tazama, kule! Tazama, huku! Msiondoke mahali mlipo, wala msiwafuate;
Luc 21.8 Luc 17.21 Matthieu 24.23-24.26 Marc 13.21-13.23
24 kwa kuwa, kama vile umeme umulikavyo toka upande huu chini ya mbingu hata upande huu chini ya mbingu, ndivyo atakavyokuwa Mwana wa Adamu katika siku yake.
Matthieu 24.27 Jacques 5.8 Malachie 4.1-4.2 1 Thessaloniciens 5.2 Zacharie 9.14
25 Lakini kwanza, hana budi kupata mateso mengi, na kukataliwa na kizazi hiki.
Matthieu 16.21 Luc 9.22 Marc 8.31 Luc 18.33 Matthieu 21.42
26 Na kama ilivyokuwa siku za Nuhu, ndivyo itakavyokuwa katika siku zake Mwana wa Adamu.
Hébreux 11.7 Matthieu 24.37-24.39 2 Pierre 2.5 Genèse 7.7-7.23 Luc 17.24
27 Walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakioa na kuolewa, hata siku ile Nuhu aliyoingia katika safina, gharika ikashuka ikawaangamiza wote.
1 Samuel 25.36-25.38 Luc 16.19-16.23 Job 21.9-21.13 1 Thessaloniciens 5.1-5.3 Luc 12.19-12.20
28 Na kadhalika, kama ilivyokuwa katika siku za Lutu, walikuwa wakila na kunywa, walikuwa wakinunua na kuuza, wakipanda na kujenga;
Jacques 5.1-5.5 Genèse 18.20-18.21 Genèse 13.13 Genèse 19.1-19.28 Ezéchiel 16.49-16.50
29 lakini siku ile Lutu aliyotoka Sodoma kulinyesha moto na kibiriti kutoka mbinguni vikawaangamiza wote.
2 Pierre 2.6 Apocalypse 11.8 Sophonie 2.9 Matthieu 11.23-11.24 Jude 1.7
30 Hivyo ndivyo itakavyokuwa siku ile atakayofunuliwa Mwana wa Adamu.
Matthieu 24.3 1 Corinthiens 1.7 1 Pierre 1.13 Apocalypse 1.7 2 Thessaloniciens 1.7
31 Katika siku ile, aliye juu ya dari, na vyombo vyake vimo ndani ya nyumba, asishuke ili kuvitwaa; na kadhalika, aliye shambani asirejee nyuma.
Marc 13.14-13.16 Jérémie 45.5 Job 2.4 Matthieu 24.17-24.21 Luc 21.21
32 Mkumbukeni mkewe Lutu.
Genèse 19.26 Hébreux 10.38-10.39 2 Pierre 2.18-2.22 1 Corinthiens 10.6-10.12 Genèse 19.17
33 Mtu ye yote atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza; na ye yote atakayeiangamiza ataiponya.
Jean 12.25 Matthieu 10.39 Marc 8.35-8.37 Matthieu 16.25 Luc 9.24-9.25
34 Nawaambia, usiku huo watu wawili watakuwa katika kitanda kimoja; mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.
Matthieu 24.40-24.41 Matthieu 24.25 Malachie 3.16-3.18 Ezéchiel 9.4-9.6 Marc 13.23
35 Wanawake wawili watakuwa wakisaga pamoja; mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.
Matthieu 24.41 Exode 11.5 Juges 16.21
36 Watu wawili watakuwa shambani, mmoja atatwaliwa, mmoja ataachwa.]
37 Wakajibu, wakamwuliza, Wapi, Bwana? Akawaambia, Ulipo mzoga, ndipo watakapokutanika tai.
Matthieu 24.28 Job 39.29-39.30 Amos 9.1-9.4 Zacharie 14.2 Daniel 9.26-9.27

Cette Bible est dans le domaine public.