Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 14.29
Bible en Swahili de l’est


Exécution de Jean-Baptiste

1 Wakati ule mfalme Herode alisikia habari za Yesu, akawaambia watumishi wake,
Luc 3.1 Marc 8.15 Actes 4.27 Luc 9.7-9.9 Luc 23.7-23.12
2 Huyo ndiye Yohana Mbatizaji; amefufuka katika wafu; na kwa hiyo nguvu hizo zinatenda kazi ndani yake.
Matthieu 16.14 Jean 10.41 Matthieu 11.11 Marc 8.28
3 Maana Herode alikuwa amemkamata Yohana, akamfunga, akamtia gerezani, kwa ajili ya Herodia, mke wa Filipo nduguye.
Marc 6.17 Luc 3.19-3.20 Matthieu 4.12 Matthieu 11.2 Jean 3.23-3.24
4 Kwa sababu Yohana alimwambia, Si halali kwako kuwa naye.
Lévitique 18.16 Lévitique 20.21 Actes 24.24-24.25 2 Samuel 12.7 Esaïe 8.20
5 Naye alipotaka kumwua, aliwaogopa watu, maana walimwona Yohana kuwa nabii.
Matthieu 11.9 Matthieu 21.26 Luc 20.6 Matthieu 21.32 Marc 6.19-6.20
6 Hata ilipofika sikukuu ya kuzaliwa kwake Herode, binti Herodia alicheza mbele ya watu, akampendeza Herode.
Marc 6.21-6.23 Genèse 40.20 Esther 1.2-1.12 Matthieu 22.24 Osée 1.5-1.6
7 Hata akaahidi kwa kiapo ya kwamba atampa lo lote atakaloliomba.
Esther 7.2 Esther 5.6 Esther 5.3
8 Naye, huku akichochewa na mamaye, akasema, Nipe hapa katika kombe kichwa cha Yohana Mbatizaji.
Proverbes 29.10 1 Rois 18.4 2 Rois 11.1 Marc 6.24 2 Chroniques 22.2-22.3
9 Naye mfalme akasikitika; lakini kwa ajili ya viapo vyake, na kwa ajili ya wale walioketi chakulani pamoja naye, akaamuru apewe;
Matthieu 27.17-27.26 1 Samuel 14.24 Jean 19.12-19.16 Juges 21.7-21.23 2 Rois 6.31-6.33
10 akatuma mtu, akamkata kichwa Yohana mle gerezani.
Matthieu 17.12 Luc 9.9 Jérémie 2.30 Matthieu 21.35-21.36 2 Chroniques 36.16
11 Kichwa chake kikaletwa katika kombe, akapewa yule kijana; akakichukua kwa mamaye.
Proverbes 27.4 Ezéchiel 16.3-16.4 Proverbes 29.10 Apocalypse 17.6 Ezéchiel 19.2-19.3
12 Wanafunzi wake wakaenda, wakamchukua yule maiti, wakamzika; kisha wakaenda wakampasha Yesu habari.
Actes 8.2 Matthieu 27.58-27.61

Multiplication des pains pour cinq mille hommes

13 Naye Yesu aliposikia; hayo, aliondoka huko katika chombo, akaenda mahali pasipo watu, faraghani. Na makutano waliposikia, walimfuata kwa miguu kutoka mijini mwao.
Luc 9.10-9.17 Jean 6.1-6.15 Marc 6.30-6.44 Matthieu 15.32-15.38 Matthieu 12.15
14 Yesu akatoka, akaona mkutano mkuu, akawahurumia, akawaponya wagonjwa wao.
Matthieu 9.36 Hébreux 4.15 Matthieu 4.23 Marc 8.1-8.2 Luc 19.41
15 Hata kulipokuwa jioni, wanafunzi wake walimwendea, wakasema, Mahali hapa ni nyika tupu, na saa imekwisha pita; uwaage makutano, waende zao vijijini, wakajinunulie vyakula.
Matthieu 15.23 Marc 8.3 Marc 6.35-6.36 Luc 9.12
16 Yesu akawaambia, Hawana haja kwenda zao, wapeni ninyi vyakula.
2 Rois 4.42-4.44 Ecclésiaste 11.2 Proverbes 11.24 Jean 13.29 Luc 3.11
17 Wakamwambia, Hamna kitu hapa ila mikate mitano na samaki wawili.
Nombres 11.21-11.23 Jean 6.5-6.9 Matthieu 15.33-15.34 Matthieu 16.9 Luc 9.13
18 Akasema, Nileteeni hapa.
19 Akawaagiza makutano waketi katika majani; akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama juu mbinguni, akabariki, akaimega ile mikate, akawapa wanafunzi, wanafunzi wakawapa makutano.
Luc 24.30 1 Samuel 9.13 Actes 27.35 1 Timothée 4.4-4.5 Romains 14.6
20 Wakala wote wakashiba; wakayaokota masazo ya vipande vya mikate, vikapu kumi na viwili, vimejaa.
Matthieu 16.8-16.10 Marc 8.8-8.9 Luc 1.53 Luc 9.17 Marc 6.42-6.44
21 Nao waliokula walikuwa wanaume wapata elfu tano, bila wanawake na watoto.
Actes 4.4 2 Corinthiens 9.8-9.11 Philippiens 4.19 Actes 4.34 Jean 6.10
22 Mara akawalazimisha wanafunzi wake wapande chomboni na kutangulia mbele yake kwenda ng’ambo, wakati yeye alipokuwa akiwaaga mkutano.
Jean 6.15-6.21 Marc 6.45-6.51 Matthieu 15.39 Matthieu 13.36
23 Naye alipokwisha kuwaaga makutano, alipanda mlimani faraghani, kwenda kuomba. Na kulipokuwa jioni, alikuwako huko peke yake.
Luc 6.12 Marc 6.46 Jean 6.15-6.17 Matthieu 26.36 Matthieu 6.6
24 Na kile chombo kimekwisha kufika katikati ya bahari, kinataabika sana na mawimbi; maana upepo ulikuwa wa mbisho.
Marc 6.48 Jean 6.18 Matthieu 8.24 Esaïe 54.11
25 Hata wakati wa zamu ya nne ya usiku Yesu akawaendea, akienda kwa miguu juu ya bahari.
Job 9.8 Matthieu 24.43 Apocalypse 10.8 Marc 6.48 Jean 6.19
26 Wanafunzi walipomwona akienda juu ya bahari, wakafadhaika, wakisema, Ni kivuli; wakapiga yowe kwa hofu.
Marc 6.49-6.50 Job 4.14-4.16 Luc 24.37 Apocalypse 1.17 Luc 24.5
27 Mara Yesu alinena, akawaambia, Jipeni moyo ni mimi; msiogope.
Actes 23.11 Matthieu 9.2 Jean 6.20 Jean 16.33 Apocalypse 1.17-1.18
28 Petro akamjibu, akasema, Bwana, ikiwa ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji.
Romains 12.3 Luc 22.31-22.34 Matthieu 19.27 Jean 13.36-13.38 Luc 22.49-22.50
29 Akasema, Njoo. Petro akashuka chomboni, akaenda kwa miguu juu ya maji, ili kumwendea Yesu.
Philippiens 4.13 Actes 3.16 Romains 4.19 Matthieu 17.20 Luc 17.6
30 Lakini alipouona upepo, akaogopa; akaanza kuzama, akapiga yowe, akisema, Bwana, niokoe.
2 Timothée 4.16-4.17 Lamentations 3.54-3.57 Jean 18.25-18.27 Luc 22.54-22.61 Psaumes 116.3-116.4
31 Mara Yesu akanyosha mkono wake, akamshika, akamwambia, Ewe mwenye imani haba, mbona uliona shaka?
Genèse 22.14 Jacques 1.6-1.8 Matthieu 16.8 1 Pierre 1.5 Romains 4.18-4.20
32 Nao walipopanda chomboni, upepo ulikoma.
Jean 6.21 Psaumes 107.29-107.30 Marc 6.51 Marc 4.41
33 Nao waliokuwamo ndani ya chombo wakamsujudia, wakisema, Hakika wewe u Mwana wa Mungu.
Psaumes 2.7 Jean 1.49 Jean 11.27 Marc 15.39 Matthieu 28.9
34 Na walipokwisha kuvuka, walifika nchi ya Genesareti.
Marc 6.53-6.56 Luc 5.1 Jean 6.24-6.25
35 Na watu wa mahali pale walipomtambua, walituma watu kwenda nchi zile zilizo kandokando, wakamletea wote waliokuwa hawawezi;
Marc 3.8-3.10 Marc 2.1-2.12 Matthieu 4.24-4.25 Marc 1.28-1.34 Marc 6.55
36 nao wakamsihi waguse hata pindo la vazi lake tu; na wote waliogusa wakaponywa kabisa.
Luc 6.19 Marc 3.10 Matthieu 9.20-9.21 Jean 6.37 Matthieu 23.5

Cette Bible est dans le domaine public.