Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Lamentations 3.54
Bible en Swahili de l’est


Souffrance et consolation

1 Mimi ni mtu aliyeona mateso Kwa fimbo ya ghadhabu yake.
Psaumes 88.7 Job 19.21 Psaumes 88.15-88.16 Jérémie 38.6 Psaumes 71.20
2 Ameniongoza na kuniendesha katika giza Wala si katika nuru.
Job 30.26 Esaïe 59.9 Amos 5.18-5.20 Deutéronome 28.29 Lamentations 2.1
3 Hakika juu yangu augeuza mkono wake Mara kwa mara mchana wote.
Esaïe 63.10 Deutéronome 29.20 Job 31.21 Esaïe 1.25 Esaïe 5.25
4 Amechakaza nyama yangu na ngozi yangu; Ameivunja mifupa yangu.
Esaïe 38.13 Psaumes 51.8 Jérémie 50.17 Psaumes 31.9-31.10 Psaumes 38.2-38.8
5 Amejenga boma juu yangu, Na kunizungusha uchungu na uchovu.
Lamentations 3.19 Jérémie 23.15 Job 19.8 Psaumes 69.21 Jérémie 9.15
6 Amenikalisha penye giza, Kama watu waliokufa zamani.
Psaumes 88.5-88.6 Psaumes 143.3 Psaumes 143.7
7 Amenizinga pande zote hata siwezi kutoka; Ameufanya mnyororo wangu mzito.
Job 19.8 Job 3.23 Psaumes 88.8 Jérémie 38.6 Daniel 9.12
8 Naam, nikilia na kuomba msaada, Huyapinga maombi yangu.
Job 30.20 Psaumes 22.2 Job 19.7 Habakuk 1.2 Matthieu 27.46
9 Ameziziba njia zangu kwa mawe yaliyochongwa; Ameyapotosha mapito yangu.
Esaïe 63.17 Osée 2.6 Esaïe 30.28 Lamentations 3.11
10 Alivyo kwangu ni kama dubu aoteaye, Kama simba aliye mafichoni.
Psaumes 10.9 Osée 13.7-13.8 Esaïe 38.13 Osée 5.14 Psaumes 17.12
11 Amezigeuza njia zangu, na kunirarua-rarua; Amenifanya ukiwa.
Osée 6.1 Job 16.12-16.13 Lamentations 1.13 Jérémie 19.8 Michée 5.8
12 Ameupinda upinde wake, Na kunifanya niwe shabaha kwa mshale.
Job 7.20 Psaumes 38.2 Job 6.4 Psaumes 7.12-7.13 Lamentations 2.4
13 Amenichoma viuno Kwa mishale ya podo lake.
Job 6.4 Deutéronome 32.23 Job 41.28
14 Nimekuwa dhihaka kwa watu wangu wote; Wimbo wao mchana kutwa.
Jérémie 20.7 Lamentations 3.63 Psaumes 22.6-22.7 Psaumes 137.3 Job 30.1-30.9
15 Amenijaza uchungu, Amenikinaisha kwa pakanga.
Jérémie 9.15 Psaumes 60.3 Ruth 1.20 Job 9.18 Esaïe 51.17-51.22
16 Amenivunja meno kwa changarawe; Amenifunika majivu.
Proverbes 20.17 Jérémie 6.26 Psaumes 58.6 Psaumes 3.7 Jonas 3.6
17 Umeniweka nafsi yangu mbali na amani; Nikasahau kufanikiwa.
Esaïe 59.11 Esaïe 54.10 Job 7.7 Lamentations 1.16 Jérémie 14.19
18 Nikasema, Nguvu zangu zimepotea, Na tumaini langu kwa Bwana.
Job 17.15 Ezéchiel 37.11 Psaumes 116.11 Psaumes 31.22 Job 6.11
19 Kumbuka mateso yangu, na msiba wangu, Pakanga na nyongo.
Lamentations 3.15 Lamentations 3.5 Jérémie 9.15 Psaumes 89.47 Job 7.7
20 Nafsi yangu ikali ikiyakumbuka hayo, Nayo imeinama ndani yangu.
Psaumes 42.5-42.6 Psaumes 42.11 Job 21.6 Psaumes 43.5 Psaumes 44.25
21 Najikumbusha neno hili, Kwa hiyo nina matumaini.
Psaumes 130.7 Psaumes 119.81 Psaumes 77.7-77.11 Lamentations 3.24-3.29 Habakuk 2.3
22 Ni huruma za Bwana kwamba hatuangamii, Kwa kuwa rehema zake hazikomi.
Psaumes 86.15 Psaumes 78.38 Luc 1.50 Malachie 3.6 Psaumes 106.45
23 Ni mpya kila siku asubuhi; Uaminifu wako ni mkuu.
Psaumes 30.5 Hébreux 10.23 Esaïe 33.2 Sophonie 3.5 Psaumes 36.5
24 Bwana ndiye fungu langu, husema nafsi yangu, Kwa hiyo nitamtumaini yeye.
Psaumes 16.5 Psaumes 73.26 Psaumes 33.18 Lamentations 3.21 Jérémie 10.16
25 Bwana ni mwema kwa hao wamngojeao, Kwa hiyo nafsi imtafutayo.
2 Chroniques 15.2 Psaumes 39.7 Psaumes 40.1-40.5 Genèse 49.18 Michée 7.7-7.8
26 Ni vema mtu autarajie wokovu wa Bwana Na kumngojea kwa utulivu.
Psaumes 37.7 Hébreux 10.35 Psaumes 130.5 Psaumes 119.174 Psaumes 119.166
27 Ni vema mwanadamu aichukue nira Wakati wa ujana wake.
Ecclésiaste 12.1 Hébreux 12.5-12.12 Matthieu 11.29-11.30 Psaumes 90.12 Psaumes 94.12
28 Na akae peke yake na kunyamaza kimya; Kwa sababu Bwana ameweka hayo juu yake.
Jérémie 15.17 Lamentations 2.10 Psaumes 39.9 Psaumes 102.7
29 Na atie kinywa chake mavumbini; Ikiwa yamkini liko tumaini.
Job 40.4 Sophonie 2.3 Romains 3.19 Jonas 3.9 Luc 15.18-15.19
30 Na amwelekezee yule ampigaye shavu lake; Ashibishwe mashutumu.
Esaïe 50.6 Job 16.10 Matthieu 5.39 Luc 6.29 Psaumes 69.9
31 Kwa kuwa Bwana hatamtupa mtu Hata milele.
Psaumes 94.14 Esaïe 54.7-54.10 Psaumes 77.7 Romains 11.1-11.6 Jérémie 32.40
32 Maana ajapomhuzunisha atamrehemu, Kwa kadiri ya wingi wa huruma zake.
Osée 11.8 Psaumes 78.38 Psaumes 106.43-106.45 Lamentations 3.22 Luc 15.20
33 Maana moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu. Wala kuwahuzunisha.
Ezéchiel 33.11 Ezéchiel 18.32 Hébreux 12.9-12.10 Esaïe 28.21
34 Kuwaseta chini kwa miguu Wafungwa wote wa duniani,
Esaïe 14.17 Jérémie 51.33-51.36 Zacharie 9.11-9.12 Esaïe 51.22-51.23 Psaumes 69.33
35 Kuipotosha hukumu ya mtu Mbele zake Aliye juu,
36 Na kumnyima mtu haki yake, Hayo Bwana hayaridhii kabisa.
Habakuk 1.13 Esaïe 59.15 Jérémie 22.3 2 Samuel 11.27
37 Ni nani asemaye neno nalo likafanyika, Ikiwa Bwana hakuliagiza?
Psaumes 33.9-33.11 Esaïe 46.10 Proverbes 16.9 Daniel 4.35 Proverbes 19.21
38 Je! Katika kinywa chake Aliye juu Hayatoki maovu na mema?
Esaïe 45.7 Job 2.10 Amos 3.6 Jérémie 32.42 Psaumes 75.7
39 Mbona anung’unika mwanadamu aliye hai Mtu akiadhibiwa kwa dhambi zake?
Michée 7.9 Proverbes 19.3 Jérémie 30.15 Nombres 17.12 2 Rois 6.32
40 Na tuchunguze njia zetu na kuzijaribu, Na kumrudia Bwana tena.
Psaumes 119.59 2 Corinthiens 13.5 Job 11.13-11.15 2 Chroniques 30.6 Psaumes 139.23-139.24
41 Na tumwinulie Mungu aliye mbinguni Mioyo yetu na mikono.
Psaumes 25.1 Psaumes 28.2 Psaumes 141.2 Psaumes 86.4 1 Thessaloniciens 2.8
42 Sisi tumekosa na kuasi; Wewe hukusamehe.
Néhémie 9.26 2 Rois 24.4 Lamentations 5.16 Luc 15.18-15.19 Lamentations 1.18
43 Umetufunika kwa hasira na kutufuatia; Umeua, wala hukuona huruma.
Lamentations 2.21 Lamentations 2.17 Lamentations 3.66 Psaumes 83.15 Psaumes 44.19
44 Umejifunika nafsi yako kwa wingu, Maombi yetu yasipite.
Lamentations 3.8 Zacharie 7.13 Psaumes 97.2 Jérémie 15.1 Jérémie 14.11
45 Umetufanya kuwa takataka, na vifusi Katikati ya mataifa.
1 Corinthiens 4.13 Lamentations 4.14-4.15 Lamentations 3.14 Deutéronome 28.44 Deutéronome 28.37
46 Juu yetu adui zetu wote Wametupanulia vinywa vyao.
Lamentations 2.16 Psaumes 22.6-22.8 Psaumes 79.10 Exode 11.7 Matthieu 27.38-27.45
47 Hofu imetujilia na shimo, Ukiwa na uharibifu.
Esaïe 51.19 Esaïe 24.17-24.18 Jérémie 48.43-48.44 Lamentations 1.13 Lamentations 1.4
48 Jicho langu lachuruzika mito ya maji Kwa ajili ya uvunjifu wa binti ya watu wangu.
Lamentations 2.11 Jérémie 9.1 Lamentations 2.18 Jérémie 9.18 Psaumes 119.136
49 Jicho langu latoka machozi lisikome, Wala haliachi;
Jérémie 14.17 Psaumes 77.2 Lamentations 1.16
50 Hata Bwana atakapoangalia Na kutazama toka mbinguni.
Esaïe 63.15 Lamentations 5.1 Esaïe 64.1 Lamentations 2.20 Esaïe 62.6-62.7
51 Jicho langu lanitia huzuni nafsini mwangu, Kwa sababu ya binti zote za mji wangu.
Jérémie 14.18 Luc 19.41-19.44 Jérémie 14.16 Genèse 44.34 Jérémie 19.9
52 Walio adui zangu bila sababu Wameniwinda sana kama ndege;
Psaumes 35.19 Psaumes 35.7 1 Samuel 26.18-26.20 Jérémie 37.15-37.16 1 Samuel 25.28-25.29
53 Wameukatilia mbali uhai wangu gerezani, Na kutupa jiwe juu yangu.
Jérémie 38.6 Jérémie 38.9 Daniel 6.17 Jérémie 37.16 Jérémie 37.20
54 Maji mengi yalipita juu ya kichwa changu, Nikasema, Nimekatiliwa mbali.
Jonas 2.3-2.5 Ezéchiel 37.11 Psaumes 69.1-69.2 Job 17.11-17.16 Lamentations 3.18
55 Naliliitia jina lako, Bwana, kutoka lile shimo Liendalo chini kabisa.
2 Chroniques 33.11-33.12 Psaumes 142.3-142.7 Psaumes 18.5-18.6 Actes 16.24-16.28 Psaumes 116.3-116.4
56 Ukaisikia sauti yangu; usifiche sikio lako Ili usisikie pumzi yangu, kwa kilio changu.
Psaumes 55.1 Job 34.28 Psaumes 66.19 Esaïe 38.5 2 Chroniques 33.19
57 Ulinikaribia siku ile nilipokulilia; Ukasema, Usiogope.
Esaïe 41.10 Esaïe 41.14 Jacques 4.8 Jérémie 1.17 Esaïe 58.9
58 Ee Bwana umenitetea mateto ya nafsi yangu; Umeukomboa uhai wangu.
Psaumes 103.4 Genèse 48.16 Psaumes 34.22-35.1 Jérémie 50.34 Psaumes 71.23
59 Umekuona kudhulumiwa kwangu, Ee Bwana; Unihukumie neno langu.
Psaumes 43.1 Psaumes 35.23 Psaumes 26.1 Jérémie 11.19-11.21 1 Pierre 2.23
60 Umekiona kisasi chao chote, Na mashauri yao yote juu yangu.
Jérémie 11.19-11.20 Lamentations 3.59 Psaumes 10.14
61 Ee Bwana, umeyasikia matukano yao, Na mashauri yao yote juu yangu;
Lamentations 5.1 Sophonie 2.8 Psaumes 89.50 Psaumes 74.18 Lamentations 3.30
62 Midomo yao walioinuka juu yangu Na maazimio yao juu yangu mchana kutwa.
Ezéchiel 36.3 Psaumes 140.3 Psaumes 59.12 Psaumes 59.7 Jérémie 18.18
63 Uangalie kuketi kwao, na kuinuka kwao; Wimbo wao ndio mimi.
Lamentations 3.14 Psaumes 139.2 Job 30.9
64 Utawalipa malipo, Ee Bwana, Sawasawa na kazi ya mikono yao.
Psaumes 28.4 Jérémie 11.20 2 Timothée 4.14 Apocalypse 18.6 Apocalypse 6.10
65 Utawapa ushupavu wa moyo; Laana yako juu yao.
Esaïe 6.10 Deutéronome 2.30 Deutéronome 27.15-27.26 1 Corinthiens 16.22 Psaumes 109.17-109.18
66 Utawafuatia kwa hasira, na kuwaangamiza Wasiwe tena chini ya mbingu za Bwana.
Psaumes 8.3 Jérémie 10.11 Lamentations 3.43 Deutéronome 25.19 Deutéronome 7.24

Cette Bible est dans le domaine public.