Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Lamentations 3.45
Bible en Swahili de l’est


Souffrance et consolation

1 Mimi ni mtu aliyeona mateso Kwa fimbo ya ghadhabu yake.
Psaumes 88.7 Job 19.21 Psaumes 88.15-88.16 Esaïe 53.3 Jérémie 15.17-15.18
2 Ameniongoza na kuniendesha katika giza Wala si katika nuru.
Job 30.26 Esaïe 59.9 Lamentations 3.53-3.55 Jude 1.6 Jude 1.13
3 Hakika juu yangu augeuza mkono wake Mara kwa mara mchana wote.
Esaïe 1.25 Esaïe 5.25 Lamentations 2.4-2.7 Esaïe 63.10 Deutéronome 29.20
4 Amechakaza nyama yangu na ngozi yangu; Ameivunja mifupa yangu.
Esaïe 38.13 Psaumes 51.8 Jérémie 50.17 Psaumes 102.3-102.5 Psaumes 31.9-31.10
5 Amejenga boma juu yangu, Na kunizungusha uchungu na uchovu.
Lamentations 3.19 Jérémie 23.15 Job 19.8 Jérémie 8.14 Lamentations 3.7-3.9
6 Amenikalisha penye giza, Kama watu waliokufa zamani.
Psaumes 88.5-88.6 Psaumes 143.3 Psaumes 143.7
7 Amenizinga pande zote hata siwezi kutoka; Ameufanya mnyororo wangu mzito.
Job 3.23 Job 19.8 Jérémie 38.6 Psaumes 88.8 Lamentations 3.9
8 Naam, nikilia na kuomba msaada, Huyapinga maombi yangu.
Psaumes 22.2 Job 30.20 Job 19.7 Matthieu 27.46 Lamentations 3.44
9 Ameziziba njia zangu kwa mawe yaliyochongwa; Ameyapotosha mapito yangu.
Esaïe 63.17 Lamentations 3.11 Osée 2.6 Esaïe 30.28
10 Alivyo kwangu ni kama dubu aoteaye, Kama simba aliye mafichoni.
Psaumes 17.12 Amos 5.18-5.20 Job 10.16 Osée 6.1 Psaumes 10.9
11 Amezigeuza njia zangu, na kunirarua-rarua; Amenifanya ukiwa.
Osée 6.1 Job 16.12-16.13 Lamentations 1.13 Jérémie 32.43 Job 16.7
12 Ameupinda upinde wake, Na kunifanya niwe shabaha kwa mshale.
Job 7.20 Psaumes 38.2 Psaumes 7.12-7.13 Lamentations 2.4 Job 6.4
13 Amenichoma viuno Kwa mishale ya podo lake.
Job 6.4 Deutéronome 32.23 Job 41.28
14 Nimekuwa dhihaka kwa watu wangu wote; Wimbo wao mchana kutwa.
Jérémie 20.7 Lamentations 3.63 Psaumes 22.6-22.7 Psaumes 35.15-35.16 Jérémie 48.27
15 Amenijaza uchungu, Amenikinaisha kwa pakanga.
Jérémie 9.15 Jérémie 23.15 Jérémie 25.15-25.18 Jérémie 25.27 Psaumes 60.3
16 Amenivunja meno kwa changarawe; Amenifunika majivu.
Proverbes 20.17 Jérémie 6.26 Psaumes 58.6 Psaumes 3.7 Psaumes 102.9
17 Umeniweka nafsi yangu mbali na amani; Nikasahau kufanikiwa.
Esaïe 59.11 Jérémie 20.14-20.18 Psaumes 119.155 Jérémie 16.5 Jérémie 8.15
18 Nikasema, Nguvu zangu zimepotea, Na tumaini langu kwa Bwana.
Job 17.15 Ezéchiel 37.11 Psaumes 31.22 Job 6.11 1 Samuel 27.1
19 Kumbuka mateso yangu, na msiba wangu, Pakanga na nyongo.
Lamentations 3.15 Lamentations 3.5 Jérémie 9.15 Psaumes 89.50 Néhémie 9.32
20 Nafsi yangu ikali ikiyakumbuka hayo, Nayo imeinama ndani yangu.
Psaumes 42.5-42.6 Psaumes 42.11 Job 21.6 Psaumes 43.5 Psaumes 146.8
21 Najikumbusha neno hili, Kwa hiyo nina matumaini.
Psaumes 130.7 Lamentations 3.24-3.29 Habakuk 2.3 Psaumes 119.81 Psaumes 77.7-77.11
22 Ni huruma za Bwana kwamba hatuangamii, Kwa kuwa rehema zake hazikomi.
Psaumes 86.15 Psaumes 78.38 Psaumes 106.45 Néhémie 9.31 Luc 1.50
23 Ni mpya kila siku asubuhi; Uaminifu wako ni mkuu.
Psaumes 30.5 Esaïe 33.2 Sophonie 3.5 Hébreux 10.23 Psaumes 36.5
24 Bwana ndiye fungu langu, husema nafsi yangu, Kwa hiyo nitamtumaini yeye.
Psaumes 16.5 Psaumes 73.26 Lamentations 3.21 Psaumes 33.18 1 Pierre 1.21
25 Bwana ni mwema kwa hao wamngojeao, Kwa hiyo nafsi imtafutayo.
Psaumes 27.8 Psaumes 27.14 2 Chroniques 19.3 Psaumes 37.7 Psaumes 37.34
26 Ni vema mtu autarajie wokovu wa Bwana Na kumngojea kwa utulivu.
Psaumes 37.7 Hébreux 10.35 Hébreux 3.14 Psaumes 130.5 Psaumes 119.174
27 Ni vema mwanadamu aichukue nira Wakati wa ujana wake.
Ecclésiaste 12.1 Psaumes 90.12 Psaumes 94.12 Psaumes 119.71 Hébreux 12.5-12.12
28 Na akae peke yake na kunyamaza kimya; Kwa sababu Bwana ameweka hayo juu yake.
Jérémie 15.17 Lamentations 2.10 Psaumes 102.7 Psaumes 39.9
29 Na atie kinywa chake mavumbini; Ikiwa yamkini liko tumaini.
Job 40.4 2 Chroniques 33.12 Ezéchiel 16.63 Luc 18.13 Jérémie 31.17
30 Na amwelekezee yule ampigaye shavu lake; Ashibishwe mashutumu.
Esaïe 50.6 Job 16.10 Matthieu 5.39 Psaumes 123.3 Matthieu 26.67
31 Kwa kuwa Bwana hatamtupa mtu Hata milele.
Psaumes 94.14 Psaumes 77.7 Esaïe 54.7-54.10 Esaïe 57.16 Jérémie 31.37
32 Maana ajapomhuzunisha atamrehemu, Kwa kadiri ya wingi wa huruma zake.
Osée 11.8 Psaumes 78.38 Psaumes 106.43-106.45 Jérémie 31.20 Psaumes 103.11
33 Maana moyo wake hapendi kuwatesa wanadamu. Wala kuwahuzunisha.
Ezéchiel 33.11 Ezéchiel 18.32 Hébreux 12.9-12.10 Esaïe 28.21
34 Kuwaseta chini kwa miguu Wafungwa wote wa duniani,
Jérémie 50.33-50.34 Jérémie 50.17 Psaumes 79.11 Esaïe 49.9 Esaïe 14.17
35 Kuipotosha hukumu ya mtu Mbele zake Aliye juu,
36 Na kumnyima mtu haki yake, Hayo Bwana hayaridhii kabisa.
Habakuk 1.13 2 Samuel 11.27 Esaïe 59.15 Jérémie 22.3
37 Ni nani asemaye neno nalo likafanyika, Ikiwa Bwana hakuliagiza?
Psaumes 33.9-33.11 Esaïe 46.10 Proverbes 21.30 Proverbes 16.9 Daniel 4.35
38 Je! Katika kinywa chake Aliye juu Hayatoki maovu na mema?
Esaïe 45.7 Job 2.10 Amos 3.6 Jérémie 32.42 Proverbes 29.26
39 Mbona anung’unika mwanadamu aliye hai Mtu akiadhibiwa kwa dhambi zake?
Michée 7.9 Proverbes 19.3 Jonas 4.8-4.9 2 Rois 3.13 Josué 7.6-7.13
40 Na tuchunguze njia zetu na kuzijaribu, Na kumrudia Bwana tena.
Psaumes 119.59 2 Corinthiens 13.5 2 Chroniques 30.6 Psaumes 139.23-139.24 Job 11.13-11.15
41 Na tumwinulie Mungu aliye mbinguni Mioyo yetu na mikono.
Psaumes 25.1 Psaumes 28.2 Psaumes 141.2 1 Thessaloniciens 2.8 Psaumes 143.6-143.8
42 Sisi tumekosa na kuasi; Wewe hukusamehe.
Néhémie 9.26 2 Rois 24.4 Job 33.27-33.28 Ezéchiel 24.13 Zacharie 1.5
43 Umetufunika kwa hasira na kutufuatia; Umeua, wala hukuona huruma.
Lamentations 2.21 Lamentations 2.17 Psaumes 83.15 Lamentations 3.66 Ezéchiel 7.9
44 Umejifunika nafsi yako kwa wingu, Maombi yetu yasipite.
Lamentations 3.8 Zacharie 7.13 Psaumes 97.2 Jérémie 15.1 Jérémie 14.11
45 Umetufanya kuwa takataka, na vifusi Katikati ya mataifa.
1 Corinthiens 4.13 Deutéronome 28.37 Lamentations 2.15 Deutéronome 28.13 Lamentations 4.14-4.15
46 Juu yetu adui zetu wote Wametupanulia vinywa vyao.
Lamentations 2.16 Psaumes 22.6-22.8 Matthieu 27.38-27.45 Psaumes 79.4 Job 30.9-30.11
47 Hofu imetujilia na shimo, Ukiwa na uharibifu.
Esaïe 24.17-24.18 Esaïe 51.19 Jérémie 48.43-48.44 Lamentations 1.4 Luc 21.35
48 Jicho langu lachuruzika mito ya maji Kwa ajili ya uvunjifu wa binti ya watu wangu.
Jérémie 9.1 Lamentations 2.11 Psaumes 119.136 Jérémie 13.17 Lamentations 1.16
49 Jicho langu latoka machozi lisikome, Wala haliachi;
Jérémie 14.17 Psaumes 77.2 Lamentations 1.16
50 Hata Bwana atakapoangalia Na kutazama toka mbinguni.
Esaïe 63.15 Lamentations 5.1 Esaïe 62.6-62.7 Psaumes 80.14-80.16 Daniel 9.16-9.19
51 Jicho langu lanitia huzuni nafsini mwangu, Kwa sababu ya binti zote za mji wangu.
Jérémie 11.22 1 Samuel 30.3-30.4 Jérémie 4.19-4.21 Lamentations 2.21 Jérémie 14.18
52 Walio adui zangu bila sababu Wameniwinda sana kama ndege;
Psaumes 35.19 Psaumes 35.7 Jérémie 38.4-38.6 1 Samuel 24.10-24.15 Psaumes 109.3
53 Wameukatilia mbali uhai wangu gerezani, Na kutupa jiwe juu yangu.
Jérémie 38.9 Daniel 6.17 Jérémie 38.6 Jérémie 37.16 Matthieu 27.60
54 Maji mengi yalipita juu ya kichwa changu, Nikasema, Nimekatiliwa mbali.
Jonas 2.3-2.5 Ezéchiel 37.11 Psaumes 18.4 Psaumes 31.22 Esaïe 38.10-38.13
55 Naliliitia jina lako, Bwana, kutoka lile shimo Liendalo chini kabisa.
Jérémie 38.6 Psaumes 69.13-69.18 Psaumes 130.1-130.2 Psaumes 40.1-40.2 2 Chroniques 33.11-33.12
56 Ukaisikia sauti yangu; usifiche sikio lako Ili usisikie pumzi yangu, kwa kilio changu.
Psaumes 55.1 Job 34.28 Psaumes 116.1-116.2 Psaumes 88.13-88.14 Psaumes 3.4
57 Ulinikaribia siku ile nilipokulilia; Ukasema, Usiogope.
Esaïe 41.10 Esaïe 41.14 Jacques 4.8 Actes 18.9 Esaïe 43.1-43.2
58 Ee Bwana umenitetea mateto ya nafsi yangu; Umeukomboa uhai wangu.
Jérémie 50.34 Psaumes 71.23 1 Samuel 25.39 Jérémie 51.36 Psaumes 103.4
59 Umekuona kudhulumiwa kwangu, Ee Bwana; Unihukumie neno langu.
Psaumes 26.1 Psaumes 43.1 Psaumes 35.23 Jérémie 37.1-37.21 Jérémie 18.18-18.23
60 Umekiona kisasi chao chote, Na mashauri yao yote juu yangu.
Jérémie 11.19-11.20 Lamentations 3.59 Psaumes 10.14
61 Ee Bwana, umeyasikia matukano yao, Na mashauri yao yote juu yangu;
Lamentations 5.1 Psaumes 89.50 Psaumes 74.18 Sophonie 2.8 Lamentations 3.30
62 Midomo yao walioinuka juu yangu Na maazimio yao juu yangu mchana kutwa.
Ezéchiel 36.3 Psaumes 140.3 Psaumes 59.12 Psaumes 59.7 Jérémie 18.18
63 Uangalie kuketi kwao, na kuinuka kwao; Wimbo wao ndio mimi.
Lamentations 3.14 Psaumes 139.2 Job 30.9
64 Utawalipa malipo, Ee Bwana, Sawasawa na kazi ya mikono yao.
Psaumes 28.4 2 Timothée 4.14 Jérémie 11.20 Jérémie 50.29 Apocalypse 18.6
65 Utawapa ushupavu wa moyo; Laana yako juu yao.
Esaïe 6.10 Deutéronome 2.30 Psaumes 109.17-109.18 Deutéronome 27.15-27.26 1 Corinthiens 16.22
66 Utawafuatia kwa hasira, na kuwaangamiza Wasiwe tena chini ya mbingu za Bwana.
Psaumes 8.3 Jérémie 10.11 Lamentations 3.43 Deutéronome 25.19 Psaumes 73.15

Cette Bible est dans le domaine public.