Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Josué 19.10
Bible en Swahili de l’est


Territoires accordés aux six dernières tribus

1 Kisha kura ya pili ilitokea kwa ajili ya Simeoni, maana, kwa ajili ya hiyo kabila ya wana wa Simeoni, kwa kuandama jamaa zao; na urithi wao ulikuwa katikati ya urithi wa wana wa Yuda.
Josué 19.9 Josué 18.6-18.11 Genèse 49.5-49.7
2 Miji waliyokuwa nayo katika urithi wao ni Beer-sheba, na Sheba, na Molada;
1 Chroniques 4.28-4.30 Néhémie 11.26-11.30 Josué 15.28 Genèse 21.31
3 na Hasarshuali, na Bala, na Esemu;
Josué 15.28-15.29
4 na Eltoladi, na Bethuli, na Horma;
Juges 1.17 Josué 15.30
5 na Siklagi, na Bethmarkabothi, na Hasarsusa;
Josué 15.31 1 Chroniques 4.31 1 Samuel 27.6 1 Samuel 30.1
6 na Bethlebaothi, na Sharuheni; miji kumi na mitatu, pamoja na vijiji vyake;
Josué 15.32
7 na Aini, na Rimoni, na Etheri, na Ashani; miji minne, pamoja na vijiji vyake;
Josué 15.42 Josué 15.32 Nombres 33.19-33.20 1 Chroniques 4.32
8 tena vijiji vyote vilivyozunguka miji hiyo kote kote mpaka Baalath-beeri, Rama wa Kusini. Huo ndio urithi wa kabila ya wana wa Simeoni kwa kuandama jamaa zao.
1 Samuel 30.27 1 Chroniques 4.33
9 Huo urithi wa hao wana wa Simeoni ulitoka katika fungu la wana wa Yuda; kwa maana hilo fungu la wana wa Yuda lilikuwa ni kubwa mno kwao; kwa hiyo wana wa Simeoni walikuwa na urithi katikati ya urithi wao.
2 Corinthiens 8.14-8.15 Exode 16.18
10 Kisha kura ya tatu ilitokea kwa ajili ya wana wa Zabuloni kwa kuandama jamaa zao; na mpaka wa urithi wao ulifikilia hata Saridi;
Genèse 49.13 Josué 18.6 Josué 18.11 Deutéronome 33.18-33.19
11 kisha mpaka wao ukakwea kwendelea upande wa magharibi, hata kufikilia Marala, nao ukafikilia hata Dabeshethi; nao ukafikilia kijito cha maji kilicho mkabala wa Yokneamu;
Josué 12.22 1 Chroniques 6.68 1 Rois 4.12
12 kisha ukazunguka kutoka Saridi kwendelea upande wa mashariki kwa kuelekea maawio ya jua hata kufikilia mpaka wa Kisiloth-ubori; kisha ukatokea hata Daberathi, kisha ukakwea kwendelea Yafia;
1 Chroniques 6.72 Josué 21.28 Josué 19.22 Juges 4.12 Juges 4.6
13 kutoka hapo ukaendelea kuelekea mashariki mpaka Gath-heferi, hata kufikilia Ethkasini; kisha ukatokea huko Rimoni ufikiliao hata Nea;
2 Rois 14.25
14 kisha mpaka uliizunguka nchi hiyo kwa upande wa kaskazini hata Hanathoni; kisha matokeo yake yalikuwa katika bonde la Iftaeli;
15 na Katathi, na Nahalali, na Shimroni, na Idala, na Bethlehemu; miji kumi na miwili, pamoja na vijiji vyake.
Josué 11.1 Josué 12.20 2 Samuel 23.15 Juges 1.30 2 Chroniques 11.6
16 Huu ndio urithi wa wana wa Zabuloni kwa kuandama jamaa zao; miji hii pamoja na vijiji vyake.
17 Kisha kura ya nne ilitokea kwa ajili ya Isakari, maana, ni kwa ajili ya wana wa Isakari kwa kuandama jamaa zao.
18 Na mpaka wao ulifikilia Yezreeli, na Kesulothi, na Shunemu;
1 Samuel 28.4 2 Rois 4.8 1 Rois 2.21 1 Rois 1.3 2 Rois 4.12
19 na Hafaraimu, na Shioni, na Anaharathi;
20 na Rabithu, na Kishioni, na Ebesi;
21 na Remethi, na Enganimu, na Enhada, na Bethpasesi;
Josué 21.29
22 na mpaka ukafikilia hata Tabori, na Shahasuma na Bethshemeshi; na matokeo ya mpaka wao yalikuwa katika mto wa Yordani; miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
Juges 4.6 Josué 19.38 1 Chroniques 6.77 1 Rois 4.9 1 Samuel 6.9-6.19
23 Huu ndio urithi wa kabila ya wana wa Isakari kwa kuandama jamaa zao; miji hiyo pamoja na vijiji vyake.
24 Kisha kura ya tano ilitokea kwa ajili ya kabila ya wana wa Asheri kwa kuandama jamaa zao.
Luc 2.26-2.38
25 Na mpaka wao ulikuwa ni Helkathi, na Hali, na Beteni, na Akishafu;
Josué 11.1 Josué 12.20 2 Samuel 2.16
26 na Alameleki, na Amadi, na Mishali; nao ukafikilia hata Karmeli upande wa magharibi, tena ulifikilia hata Shihor-libnathi;
Esaïe 33.9 1 Rois 18.42 1 Rois 18.20 Cantique 7.5 Esaïe 37.24
27 kisha ukazunguka kuelekea maawio ya jua mpaka Beth-dagoni, nao ukafikilia hata Zabuloni, tena mpaka bonde la Iftaeli upande wa kaskazini hata Bethemeki na Neyeli; kisha ukatokea hata Kabuli upande wa kushoto;
1 Rois 9.13 1 Samuel 5.2
28 na Ebroni, na Rehobu, na Hamoni, na Kana, hata kufikilia Sidoni mkuu;
Juges 1.31 Josué 11.8 Esaïe 23.4 Esaïe 23.2 Jean 2.1
29 kisha mpaka ulizunguka kuelekea Rama, na mji wa Tiro ulio na boma; kisha mpaka ulizunguka kuelekea Hosa; na matokeo yake yalikuwa baharini katika nchi ya Akzibu;
Juges 1.31 2 Samuel 5.11 Michée 1.14 Genèse 38.5 Ezéchiel 26.1-26.21
30 na Uma pia, na Afeka, na Rehobu; miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
1 Samuel 4.1 Nombres 13.11 Josué 21.31 Josué 12.18 Josué 19.28
31 Huu ndio urithi wa kabila ya wana wa Asheri kwa kuandama jamaa zao; miji hii pamoja na vijiji vyake.
Genèse 49.20 Deutéronome 33.24-33.25
32 Kisha kura ya sita ikatokea kwa ajili ya wana wa Naftali, maana, ni kwa ajili ya wana wa Naftali kwa kuandama jamaa zao.
33 Na mpaka wao ulikuwa kutoka Helefu, tokea ule mwaloni ulio katika Saananimu, na Adami-nekebu, na Yabineeli, hata kufikilia Lakumu; na matokeo yake yalikuwa katika mto wa Yordani;
Juges 4.11
34 tena mpaka ulizunguka kwendelea upande wa magharibi hata Aznoth-tabori, tena kutoka hapo ukaendelea mpaka Hukoki; kisha ukafikilia hata Zabuloni upande wa kusini, tena ulifikilia hata Asheri upande wa magharibi, tena ulifikilia hata Yuda hapo katika mto wa Yordani kwa upande wa kuelekea maawio ya jua.
Deutéronome 33.23 Josué 19.22 Josué 19.12
35 Na miji yenye boma ilikuwa ni hii, Sidimu, na Seri, na Hamathi, na Rakathi, na Kinerethi;
Josué 11.2 1 Rois 8.65 Genèse 10.18 Nombres 13.21 Josué 13.27
36 na Adama, na Rama, na Hazori;
Josué 11.1 Josué 12.19 Josué 11.20
37 na Kedeshi, na Edrei, na Enhasori;
Josué 12.22 Josué 20.7
38 na Ironi, na Migdal-eli, na Horemu, na Bethanathi, na Bethshemeshi; miji kumi na kenda, pamoja na vijiji vyake.
39 Huu ndio urithi wa kabila ya wana wa Naftali kwa kuandama jamaa zao; miji hiyo pamoja na vijiji vyake.
40 Kisha kura ya saba ilitokea kwa ajili ya kabila ya wana wa Dani kwa kuandama jamaa zao.
41 Na mpaka wa urithi wao ulikuwa ni Sora, na Eshtaoli, na Irishemeshi;
1 Chroniques 2.53 2 Chroniques 11.10 Josué 15.33 Juges 16.31 Juges 13.2
42 na Shaalabini, na Aiyaloni, na Ithla;
Juges 1.35 Josué 10.12 1 Samuel 14.31 Josué 21.24
43 na Eloni, na Timna, na Ekroni;
Genèse 38.12 Amos 1.8 Josué 15.45 Juges 14.1-14.2 1 Samuel 5.10
44 na Elteka, na Gibethoni, na Baalathi;
Josué 21.23 1 Rois 16.15 1 Rois 15.27 1 Rois 9.18
45 na Yehudi, na Bene-beraki, na Gathrimoni;
Josué 21.24
46 na Meyarkoni, na Rakoni, pamoja na huo mpaka uliokuwa mkabala wa Yafa.
Jonas 1.3 2 Chroniques 2.16 Actes 9.43 Actes 10.8 Actes 9.36
47 Kisha mpaka wa wana wa Dani ulitokea kuwapita wao; kwa kuwa hao wana wa Dani wakakwea na kupigana na Leshemu, na kuutwaa, na kuupiga kwa makali ya upanga, na kuumiliki, nao wakakaa humo, wakauita Dani, kwa kuliandama jina la huyo Dani mzee wao.
Juges 1.34-1.35 Juges 18.1-18.29
48 Huu ndio urithi wa kabila ya wana wa Dani kwa kuandama jamaa zao; miji hii pamoja na vijiji vyake.

Territoire accordé à Josué

49 Basi wakamaliza hiyo kazi yao ya kuigawanya nchi iwe urithi kwa kuandama mipaka yake; kisha wana wa Israeli wakampa Yoshua, mwana wa Nuni, urithi katikati yao;
Ezéchiel 45.7-45.8
50 sawasawa na ile amri ya Bwana wakampa mji alioutaka, maana, ni Timnath-sera katika nchi ya vilima ya Efraimu; naye akaujenga huo mji na kukaa mumo.
Josué 24.30 Juges 2.9 1 Chroniques 7.24
51 Hizi ndizo nchi, ambazo Eleazari kuhani, na Yoshua huyo mwana wa Nuni, pamoja na hao vichwa vya nyumba za mababa ya kabila za wana wa Israeli, walizigawanya kwa njia ya kupiga kura, ziwe urithi, huko Shilo mbele ya Bwana, hapo mlangoni mwa hema ya kukutania. Basi hivyo wakamaliza kazi ya kuigawanya hiyo nchi.
Josué 18.10 Josué 14.1 Josué 18.1 Hébreux 4.8-4.9 Psaumes 78.60

Cette Bible est dans le domaine public.