Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Actes 27.40
Bible en Swahili de l’est


Départ de Paul pour Rome

1 Basi ilipoamriwa tuabiri hata Italia, wakamtia Paulo na wafungwa wengine katika mikono ya akida mmoja, jina lake Yulio, wa kikosi cha Augusto.
Actes 25.25 Actes 10.1 Actes 25.12 Actes 18.2 Actes 27.11
2 Tukapanda katika merikebu ya Adramitio iliyokuwa tayari kusafiri mpaka miji ya pwani za Asia, tukatweka; Aristarko, Mmakedonia wa Thesalonike, akiwa pamoja nasi.
Actes 19.29 Actes 20.4-20.5 Luc 8.22 Actes 21.5 Actes 16.17
3 Siku ya pili tukawasili Sidoni; Yulio akamfadhili sana Paulo akampa ruhusa kwenda kwa rafiki zake, apate kutunzwa.
Actes 24.23 Actes 28.16 Actes 27.43 Esaïe 23.12 Matthieu 11.21
4 Kutoka huko tukatweka, tukasafiri chini ya Kipro ili kuukinga upepo, kwa maana pepo zilikuwa za mbisho.
Actes 4.36 Actes 27.7 Actes 13.4 Actes 11.19-11.20 Matthieu 14.24
5 Tulipopita bahari ya upande wa Kilikia na Pamfilia, tukafika Mira, mji wa Likia.
Actes 6.9 Actes 13.13 Actes 21.39 Actes 2.10 Galates 1.21
6 Na huko yule akida akakuta merikebu ya Iskanderia, tayari kusafiri kwenda Italia, akatupandisha humo.
Actes 28.11 Actes 27.1 Actes 6.9 Actes 18.24
7 Tukasafiri polepole kwa muda wa siku nyingi, tukafika mpaka Nido kwa shida; na kwa sababu upepo ulikuwa ukituzuia tukapita chini ya Krete, tukaikabili Salmone.
Actes 27.21 Tite 1.5 Actes 2.11 Tite 1.12 Actes 27.12-27.13
8 Tukaipita kwa shida, pwani kwa pwani, tukafika mahali paitwapo Bandari Nzuri. Karibu na hapo pana mji uitwao Lasea.
9 Na wakati mwingi ulipokwisha kupita, na safari ikiwa ina hatari sasa, kwa sababu siku za kufunga zilikuwa zimekwisha kupita, Paulo akawaonya,
Nombres 29.7 Lévitique 23.27-23.29 Lévitique 16.29-16.31
10 akawaambia, Wanaume, naona kwamba safari hii itakuwa na madhara na hasara nyingi, si ya shehena na merikebu tu, ila na ya maisha yetu pia.
Actes 27.31 Amos 3.7 Actes 27.20-27.26 Actes 27.41-27.44 Actes 27.34
11 Lakini yule akida akawasikiliza nahodha na mwenye merikebu zaidi ya yale aliyoyasema Paulo.
Actes 27.21 Apocalypse 18.17 2 Rois 6.10 Ezéchiel 3.17-3.18 Exode 9.20-9.21
12 Na kwa sababu bandari ile ilikuwa haifai kukaa wakati wa baridi, wengi wao wakatoa shauri la kutweka kutoka huko ili wapate kufika Foinike, kama ikiwezekana, na kukaa huko wakati wa baridi; nayo ni bandari ya Krete, inaelekea kaskazini-mashariki na kusini-mashariki.
Psaumes 107.30 Actes 27.8
13 Na upepo wa kusi ulipoanza kuvuma kidogo, wakidhani ya kuwa wamepata waliyoazimu kupata, wakang’oa nanga, wakasafiri karibu na Krete pwani kwa pwani.
Psaumes 78.26 Job 37.17 Luc 12.55 Cantique 4.16
14 Baada ya muda mchache ukavuma upepo wa nguvu wa namna ya tufani, uitwao Eurakilo,
Marc 4.37 Jonas 1.3-1.5 Ezéchiel 27.26 Exode 14.21-14.27 Psaumes 107.25-107.27
15 merikebu iliposhikwa, na kutoweza kushindana na upepo, tukaiacha tukachukuliwa.
Actes 27.27 Jacques 3.4
16 Na tukipita upesi karibu na kisiwa kidogo kiitwacho Kauda tukadiriki kuikweza mashua; lakini kwa shida.
17 Walipokwisha kuikweza wakatumia misaada, wakaikaza merikebu kwa kupitisha kamba chini yake, nao wakiogopa wasije wakakwama katika fungu liitwalo Sirti, wakatua matanga wakachukuliwa vivi hivi.
Actes 27.29 Actes 27.26 Actes 27.41
18 Na kwa maana tulikuwa tukipigwa sana na ile tufani, siku ya pili yake wakaanza kuitupa shehena baharini.
Jonas 1.5 Actes 27.38 Actes 27.19 Philippiens 3.7-3.8 Luc 16.8
19 Siku ya tatu wakatupa vyombo vya merikebu kwa mikono yao wenyewe.
Luc 9.24-9.25 Marc 8.35-8.37 Jonas 1.5 Job 2.4
20 Jua wala nyota hazikuonekana kwa muda wa siku nyingi, na tufani kuu ikatushika, basi tukakata tamaa ya kuokoka.
Ephésiens 2.12 Jonas 1.11-1.14 Ezéchiel 37.11 Exode 10.21-10.23 Jonas 1.4
21 Na walipokuwa wamekaa wakati mwingi bila kula chakula, Paulo akasimama katikati yao, akasema, Wanaume, iliwapasa kunisikiliza mimi na kutokung’oa nanga huko Krete, na kupata madhara haya na hasara hii.
Genèse 42.22 Actes 27.33-27.35 Actes 27.9-27.10 Actes 27.7 Psaumes 107.5-107.6
22 Sasa nawapeni shauri, iweni na moyo mkuu, kwa maana hapana hata nafsi mmoja miongoni mwenu atakayepotea, ila merikebu tu.
Actes 27.25 Actes 27.36 Actes 27.34 Actes 27.44 2 Corinthiens 4.8-4.9
23 Kwa maana usiku huu wa leo malaika wa Mungu yule ambaye mimi ni wake, naye ndiye nimwabuduye, alisimama karibu nami,
Actes 23.11 Actes 5.19 Romains 1.9 Hébreux 1.14 2 Timothée 4.17
24 akaniambia, Usiogope, Paulo, huna budi kusimama mbele ya Kaisari; tena, tazama, Mungu amekupa watu wote wanaosafiri pamoja nawe.
Actes 23.11 Genèse 18.23-18.32 Matthieu 10.28 Actes 9.15 Actes 27.37
25 Basi, wanaume, changamkeni; kwa sababu namwamini Mungu, ya kwamba yatakuwa vile vile kama nilivyoambiwa.
Romains 4.20-4.21 2 Timothée 1.12 Actes 27.21-27.22 Nombres 23.19 Luc 1.45
26 Lakini hatuna budi kupwelewa katika kisiwa kimoja.
Actes 28.1 Actes 27.17 Actes 27.29
27 Hata usiku wa kumi na nne ulipofika, tulipokuwa tukichukuliwa huko na huko katika bahari ya Adria, kama usiku wa manane baharia wakadhani ya kuwa wanaikaribia nchi kavu.
1 Rois 9.27 Jonas 1.6 Actes 27.30 Apocalypse 18.17
28 Wakatupa bildi wakapata pima ishirini, wakaendelea kidogo wakatupa bildi tena, wakapata pima kumi na tano.
29 Wakachelea tusije tukapwelewa mahali penye miamba, wakatupa nanga nne za tezi, wakaomba kuche.
Actes 27.17 Hébreux 6.19 Actes 27.26 Actes 27.30 Psaumes 130.6
30 Na baharia walipotaka kukimbia na kuiacha merikebu, wakiishusha mashua baharini kana kwamba wanataka kutupa nanga za omo,
Actes 27.16 Actes 27.32
31 Paulo akawaambia akida na askari, Hawa wasipokaa ndani ya merikebu hamtaweza kuokoka.
2 Thessaloniciens 2.13-2.14 Actes 27.21-27.24 Actes 27.11 Jérémie 29.11-29.13 Actes 27.42-27.43
32 Basi askari wakazikata kamba za mashua, wakaiacha ianguke.
Philippiens 3.7-3.9 Luc 16.8
33 Na kulipokuwa kukipambauka Paulo akawasihi wote wale chakula, akisema, Leo ni siku ya kumi na nne kungoja na kufunga, hamkula kitu cho chote.
34 Basi nawasihi mle chakula, maana itakuwa kwa wokovu wenu; kwa maana hapana hata unywele wa kichwa cha mmoja wenu utakaopotea.
Matthieu 10.30 1 Rois 1.52 Luc 21.18 Marc 8.2-8.3 1 Timothée 5.23
35 Alipokwisha kusema hayo akatwaa mkate, akamshukuru Mungu mbele yao wote akaumega akaanza kula.
Matthieu 15.36 2 Timothée 1.8 Luc 24.30 Jean 6.11 1 Pierre 4.16
36 Ndipo wakachangamka wote, wakala chakula wenyewe.
Actes 27.22 2 Corinthiens 1.4-1.6 Actes 27.25 Psaumes 27.14
37 Na sisi tuliokuwa ndani ya merikebu tulipata watu mia mbili na sabini na sita.
Actes 2.41 Romains 13.1 Actes 7.14 1 Pierre 3.20
38 Walipokwisha kushiba wakaipunguza shehena ya merikebu, wakiitupa ngano baharini.
Jonas 1.5 Matthieu 6.25 Hébreux 12.1 Matthieu 16.26 Job 2.4
39 Kulipokucha hawakuitambua ile nchi, ila waliona hori yenye ufuo, wakashauriana kuiegesha merikebu huko, kama ikiwezekana.
Actes 28.1
40 Wakazitupilia mbali zile nanga, na kuziacha baharini, pamoja na kuzilegeza kamba za sukani, wakalitweka tanga dogo ili liushike upepo, wakauendea ule ufuo.
Esaïe 33.23 Actes 27.29-27.30
41 Lakini wakafikia mahali palipokutana bahari mbili, wakaiegesha merikebu, omo ikakwama ikakaa isitikiswe, bali tezi ilikuwa imefumuliwa kwa nguvu za mawimbi.
Ezéchiel 27.26 1 Rois 22.48 2 Chroniques 20.37 Actes 27.26-27.29 2 Corinthiens 11.25-11.26
42 Shauri la askari lilikuwa kuwaua wafungwa, mtu asiogelee na kukimbia.
Proverbes 12.10 Marc 15.15-15.20 Luc 23.40-23.41 Ecclésiaste 9.3 Psaumes 74.20
43 Bali akida, akitaka kumponya Paulo, akawazuia, wasifanye kama walivyokusudia, akawaamuru wale wawezao kuogelea wajitupe kwanza baharini, wafike nchi kavu;
Actes 27.3 Proverbes 16.7 Actes 23.24 Actes 23.10 Actes 27.31
44 nao waliosalia, hawa juu ya mbao na hawa juu ya vitu vingine vya merikebu. Na hivyo watu wote wakapata kuifikilia nchi kavu salama.
Actes 27.22 Actes 27.24 1 Pierre 4.18 Amos 9.9 Actes 27.31

Cette Bible est dans le domaine public.