Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 5.41
Bible en Swahili de l’est


Le sermon sur la montagne

Les béatitudes

1 Naye alipowaona makutano, alipanda mlimani; na alipokwisha kuketi, wanafunzi wake walimjia;
Matthieu 13.2 Matthieu 4.18-4.22 Luc 6.13-6.16 Marc 4.1 Matthieu 10.2-10.4
2 akafumbua kinywa chake, akawafundisha, akisema,
Matthieu 13.35 Actes 8.35 Actes 18.14 Luc 6.20-6.26 Ephésiens 6.19
3 Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.
Esaïe 66.2 Proverbes 29.23 2 Chroniques 7.14 Luc 18.14 Psaumes 51.17
4 Heri wenye huzuni; Maana hao watafarijika.
Apocalypse 21.4 Esaïe 61.2-61.3 2 Corinthiens 7.9-7.10 Jean 16.20-16.22 Esaïe 51.11-51.12
5 Heri wenye upole; Maana hao watairithi nchi.
Psaumes 37.11 Jacques 3.13 Psaumes 149.4 Esaïe 29.19 Psaumes 25.9
6 Heri wenye njaa na kiu ya haki; Maana hao watashibishwa.
Jean 4.14 Psaumes 107.9 Jean 6.27 Jean 6.48-6.58 Psaumes 42.1-42.2
7 Heri wenye rehema; Maana hao watapata rehema.
2 Samuel 22.26 Matthieu 6.14-6.15 Ephésiens 4.32-5.1 Matthieu 18.33-18.35 Hébreux 6.10
8 Heri wenye moyo safi; Maana hao watamwona Mungu.
Psaumes 24.4 Hébreux 12.14 1 Pierre 1.22 Psaumes 51.10 Actes 15.9
9 Heri wapatanishi; Maana hao wataitwa wana wa Mungu.
Hébreux 12.14 Luc 6.35 Romains 8.14 Jacques 3.16-3.18 Colossiens 3.13
10 Heri wenye kuudhiwa kwa ajili ya haki; Maana ufalme wa mbinguni ni wao.
1 Pierre 3.13-3.14 Jacques 1.12 2 Corinthiens 4.17 2 Timothée 3.11 Matthieu 5.3
11 Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo, kwa ajili yangu.
1 Pierre 4.14 Luc 21.17 Matthieu 24.9 1 Pierre 2.23 Marc 13.13
12 Furahini, na kushangilia; kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni; kwa maana ndivyo walivyowaudhi manabii waliokuwa kabla yenu.
Luc 6.23 Jacques 1.2 1 Pierre 4.13 Romains 5.3 2 Chroniques 36.16
13 Ninyi ni chumvi ya dunia; lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu.
Colossiens 4.6 Luc 14.34-14.35 Marc 9.49-9.50 Lévitique 2.13 Hébreux 6.4-6.6
14 Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima.
Philippiens 2.15 Jean 8.12 Jean 12.36 Ephésiens 5.8-5.14 Proverbes 4.18
15 Wala watu hawawashi taa na kuiweka chini ya pishi, bali juu ya kiango; nayo yawaangaza wote waliomo nyumbani.
Luc 8.16 Marc 4.21 Luc 11.33 Nombres 8.2 Exode 25.37
16 Vivyo hivyo nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.
1 Pierre 2.12 Jean 15.8 2 Corinthiens 9.13 1 Pierre 4.14 1 Pierre 3.16

Christ et la loi

17 Msidhani ya kuwa nalikuja kuitangua torati au manabii; la, sikuja kutangua, bali kutimiliza.
Romains 8.4 Romains 10.4 Galates 3.17-3.24 Esaïe 42.21 Romains 3.31
18 Kwa maana, amin, nawaambia ,Mpaka mbingu na nchi zitakapoondoka,yodi moja wala nukta moja ya torati haitaoondoka ,hata yote yatimie.
Luc 16.17 Esaïe 40.8 Psaumes 119.89-119.90 1 Pierre 1.25 Esaïe 51.6
19 Basi mtu ye yote atakayevunja amri moja katika hizi zilizo ndogo, na kuwafundisha watu hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika ufalme wa mbinguni; bali mtu atakayezitenda na kuzifundisha, huyo ataitwa mkubwa katika ufalme wa mbinguni.
Jacques 2.10-2.11 Matthieu 28.20 Matthieu 11.11 1 Timothée 4.11-4.12 Galates 5.14-5.24
20 Maana nawaambia ya kwamba, Haki yenu isipozidi hiyo haki ya waandishi na Mafarisayo, hamtaingia kamwe katika ufalme wa mbinguni.
Jean 3.3-3.5 Philippiens 3.9 Romains 10.2-10.3 Hébreux 12.14 Luc 16.14-16.15
21 Mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiue, na mtu akiua, itampasa hukumu.
Deutéronome 5.17 Exode 20.13 Matthieu 5.27 Nombres 35.30-35.34 Matthieu 5.43
22 Bali mimi nawaambieni, Kila amwoneaye ndugu yake hasira itampasa hukumu; na mtu akimfyolea ndugu yake, itampasa baraza; na mtu akimwapiza, itampasa jehanum ya moto.
1 Jean 4.20-4.21 1 Jean 3.14-3.15 Jacques 3.6 Matthieu 26.59 1 Jean 2.9
23 Basi ukileta sadaka yako madhabahuni, na huku ukikumbuka ya kuwa ndugu yako ana neno juu yako,
Marc 11.25 Matthieu 23.19 1 Samuel 15.22 Matthieu 8.4 Lamentations 3.20
24 iache sadaka yako mbele ya madhabahu, uende zako, upatane kwanza na ndugu yako, kisha urudi uitoe sadaka yako.
Romains 12.17-12.18 Jacques 5.16 Jacques 3.13-3.18 1 Corinthiens 6.7-6.8 Matthieu 23.23
25 Patana na mshitaki wako upesi, wakati uwapo pamoja naye njiani; yule mshitaki asije akakupeleka kwa kadhi, na kadhi akakupeleka kwa askari, ukatupwa gerezani.
Luc 12.58-12.59 Proverbes 25.8 Job 22.21 Esaïe 55.6-55.7 Hébreux 12.17
26 Amin, nakuambia, Hutoki humo kamwe hata uishe kulipa senti ya mwisho.
Matthieu 18.34 Luc 12.59 2 Thessaloniciens 1.9 Matthieu 25.46 Jacques 2.13
27 Mmesikia kwamba imenenwa, Usizini;
Deutéronome 5.18 Exode 20.14 Deutéronome 22.22-22.24 Matthieu 5.21 Proverbes 6.32
28 lakini mimi nawaambia, Kila mtu atazamaye mwanamke kwa kumtamani, amekwisha kuzini naye moyoni mwake.
Jacques 1.14-1.15 Job 31.1 Proverbes 6.25 2 Samuel 11.2 1 Jean 2.16
29 Jicho lako la kuume likikukosesha, ling’oe ulitupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum.
Marc 9.43-9.48 Romains 6.6 Galates 5.24 Romains 8.13 Colossiens 3.5
30 Na mkono wako wa kuume ukikukosesha, ukate uutupe mbali nawe; kwa maana yakufaa kiungo chako kimoja kipotee wala mwili wako mzima usitupwe katika jehanum.
Matthieu 5.29 Marc 9.43 Matthieu 22.13 1 Pierre 2.8 Romains 14.20-14.21
31 Imenenwa pia, Mtu akimwacha mkewe, na ampe hati ya talaka;
Deutéronome 24.1-24.4 Jérémie 3.1 Matthieu 19.7 Marc 10.2-10.9 Matthieu 19.3
32 lakini mimi nawaambia, Kila mtu amwachaye mkewe, isipokuwa kwa habari ya uasherati, amfanya kuwa mzinzi; na mtu akimwoa yule aliyeachwa, azini.
Luc 16.18 1 Corinthiens 7.10-7.11 Matthieu 5.28 Romains 7.3 Matthieu 19.8-19.9
33 Tena mmesikia watu wa kale walivyoambiwa, Usiape uongo, ila mtimizie Bwana nyapo zako;
Lévitique 19.12 Deutéronome 23.21 Deutéronome 23.23 Nombres 30.2-30.16 Psaumes 76.11
34 lakini mimi nawaambia, Usiape kabisa; hata kwa mbingu, kwa maana ndicho kiti cha enzi cha Mungu;
Jacques 5.12 Esaïe 66.1 Matthieu 23.16-23.22 Deutéronome 23.21-23.23 Esaïe 57.15
35 wala kwa nchi, kwa maana ndiyo pa kuwekea miguu yake; wala kwa Yerusalemu, kwa maana ndio mji wa Mfalme mkuu.
Psaumes 48.2 Malachie 1.14 Apocalypse 21.10 Apocalypse 21.2 Psaumes 99.5
36 Wala usiape kwa kichwa chako, maana huwezi kufanya unywele mmoja kuwa mweupe au mweusi.
Luc 12.25 Matthieu 6.27 Matthieu 23.16-23.21
37 Bali maneno yenu yawe Ndiyo, ndiyo; Siyo, siyo; kwa kuwa yazidiyo hayo yatoka kwa yule mwovu.
Jacques 5.12 Matthieu 13.19 Colossiens 4.6 Colossiens 3.9 Matthieu 13.38
38 Mmesikia kwamba imenenwa, Jicho kwa jicho, na jino kwa jino;
Exode 21.22-21.27 Deutéronome 19.21 Lévitique 24.19-24.20 Matthieu 5.27 Deutéronome 19.19
39 Lakini mimi nawaambia, Msishindane na mtu mwovu; lakini mtu akupigaye shavu la kuume, mgeuzie na la pili.
1 Corinthiens 6.7 Esaïe 50.6 Lamentations 3.30 Proverbes 24.29 1 Samuel 26.8-26.10
40 Na mtu atakaye kukushitaki na kuitwaa kanzu yako, mwachie na joho pia.
1 Corinthiens 6.7 Luc 6.29
41 Na mtu atakayekulazimisha mwendo wa maili moja, nenda naye mbili.
Matthieu 27.32 Luc 23.26 Marc 15.21
42 Akuombaye, mpe; naye atakaye kukopa kwako, usimpe kisogo.
Proverbes 19.17 Psaumes 112.5-112.9 Hébreux 13.16 Psaumes 37.21 Romains 12.20
43 Mmesikia kwamba imenenwa, Umpende jirani yako, na, Umchukie adui yako;
Lévitique 19.18 Deutéronome 23.6 Matthieu 19.19 Galates 5.13-5.14 Luc 10.27-10.29
44 lakini mimi nawaambia, Wapendeni adui zenu, waombeeni wanaowaudhi,
Romains 12.14 Luc 6.27-6.28 1 Pierre 3.9 Romains 12.20-12.21 Luc 23.34
45 ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio haki.
Psaumes 145.9 Luc 6.35 Actes 14.17 Job 25.3 Matthieu 5.9
46 Maana mkiwapenda wanaowapenda ninyi mwapata thawabu gani? Hata watoza ushuru, je! Nao hawafanyi yayo hayo?
Luc 6.32-6.35 Matthieu 18.17 Luc 18.13 Luc 19.2 1 Pierre 2.20-2.23
47 Tena mkiwaamkia ndugu zenu tu, mnatenda tendo gani la ziada? Hata watu wa mataifa, je! Nao hawafanyi kama hayo?
Matthieu 5.20 1 Pierre 2.20 Luc 10.4-10.5 Luc 6.32 Matthieu 10.12
48 Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.
Lévitique 19.2 Jacques 1.4 1 Pierre 1.15-1.16 Colossiens 1.28 Deutéronome 18.13

Cette Bible est dans le domaine public.