Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jean 6.13
Bible en Swahili de l’est


Multiplication des pains pour cinq mille hommes

1 Baada ya hayo Yesu alikwenda zake ng’ambo ya Bahari ya Galilaya, nayo ndiyo ya Tiberia.
Luc 9.10-9.17 Matthieu 4.18 Jean 21.1 Luc 5.1 Jean 6.23
2 Na mkutano mkuu wakamfuata, kwa sababu waliziona ishara alizowafanyia wagonjwa.
Matthieu 4.24-4.25 Jean 2.11 Matthieu 12.15
3 Naye Yesu akakwea mlimani, akaketi huko pamoja na wanafunzi wake.
Jean 6.15 Luc 9.28 Matthieu 15.29 Luc 6.12-6.13 Matthieu 14.23
4 Na Pasaka, sikukuu ya Wayahudi, ilikuwa karibu.
Jean 2.13 Jean 11.55 Deutéronome 16.1 Jean 5.1 Exode 12.6-12.14
5 Basi Yesu alipoinua macho yake akaona mkutano mkuu wanakuja kwake, alimwambia Filipo, Tununue wapi mikate, ili hawa wapate kula?
Jean 4.35 Luc 9.12-9.13 Matthieu 15.33 Matthieu 14.14-14.15 Jean 1.43
6 Na hilo alilinena ili kumjaribu; kwa maana alijua mwenyewe atakalotenda.
Genèse 22.1 Deutéronome 8.16 Deutéronome 33.8 Deutéronome 8.2 Deutéronome 13.3
7 Filipo akamjibu, Mikate ya dinari mia mbili haiwatoshi, kila mmoja apate kidogo tu.
Marc 6.37 Nombres 11.21-11.22 Matthieu 18.28 2 Rois 4.43 Jean 12.5
8 Wanafunzi wake mmojawapo, Andrea, nduguye Simoni Petro, akamwambia,
Jean 1.40-1.44 Matthieu 4.18
9 Yupo hapa mtoto, yuna mikate mitano ya shayiri na samaki wawili, lakini hivi ni nini kwa watu wengi kama hawa?
2 Rois 4.42-4.44 Psaumes 78.19 Deutéronome 32.14 2 Corinthiens 8.9 Deutéronome 8.8
10 Yesu akasema, Waketisheni watu. Na mahali pale palikuwa na majani tele. Basi watu waume wakaketi, wapata elfu tano jumla yao.
Matthieu 14.18-14.19 Marc 6.39-6.41 Matthieu 15.35-15.36 Marc 8.6-8.7 Luc 9.14-9.16
11 Basi Yesu akaitwaa ile mikate, akashukuru, akawagawia walioketi; na kadhalika katika wale samaki kwa kadiri walivyotaka.
Jean 6.23 Matthieu 15.36 1 Thessaloniciens 5.18 Luc 24.30 1 Timothée 4.4-4.5
12 Nao waliposhiba, aliwaambia wanafunzi wake, Kusanyeni vipande vilivyobaki, kisipotee cho chote.
Luc 1.53 Marc 8.8-8.9 Proverbes 18.9 Luc 15.13 Matthieu 15.37-15.38
13 Basi wakavikusanya, wakajaza vikapu kumi na viwili, vipande vya mikate mitano ya shayiri vilivyowabakia wale waliokula.
Proverbes 11.24-11.25 2 Corinthiens 9.8-9.9 Philippiens 4.19 2 Chroniques 25.9 2 Rois 4.2-4.7
14 Basi watu wale, walipoiona ishara aliyoifanya, walisema, Hakika huyu ni nabii yule ajaye ulimwenguni.
Matthieu 11.3 Matthieu 21.11 Jean 1.21 Jean 7.40 Jean 4.19
15 Kisha Yesu, hali akitambua ya kuwa walitaka kuja kumshika ili wamfanye mfalme, akajitenga, akaenda tena mlimani yeye peke yake.
Jean 18.36 Jean 7.3-7.4 Jean 6.15-6.21 Matthieu 14.22-14.33 Luc 19.38
16 Hata ilipokuwa jioni wanafunzi wake wakatelemka baharini
17 wakapanda chomboni, wakaanza kuivuka bahari kwenda Kapernaumu. Nako kumekwisha kuwa giza, wala Yesu hajawafikia.
Marc 6.45 Jean 2.12 Jean 4.46 Jean 6.24-6.25
18 Na bahari ikaanza kuchafuka kwa kuvuma upepo mkuu.
Psaumes 107.25 Psaumes 135.7 Matthieu 14.24
19 Basi wakavuta makasia kadiri ya maili tatu nne, wakamwona Yesu anakwenda juu ya bahari na kukikaribia chombo; wakaogopa.
Marc 6.47-6.49 Psaumes 93.4 Job 9.8 Luc 24.36-24.39 Matthieu 14.25-14.26
20 Naye akawaambia, Ni mimi, msiogope.
Esaïe 41.10 Esaïe 44.8 Marc 6.50 Marc 16.6 Esaïe 41.14
21 Basi wakataka kumpokea chomboni; na mara hiyo chombo kikaifikilia nchi waliyokuwa wakiiendea.
Marc 6.51 Psaumes 24.7-24.10 Matthieu 14.32-14.33 Apocalypse 3.20 Cantique 3.4

Jésus, le pain de vie

22 Siku ya pili yake mkutano waliosimama ng’ambo ya bahari waliona ya kuwa hakuna mashua nyingine huko ila moja, tena ya kuwa Yesu hakuingia katika mashua ile pamoja na wanafunzi wake, bali wanafunzi wake walikwenda peke yao.
Matthieu 14.22 Jean 6.15-6.21 Marc 6.45 Jean 6.2
23 (Walakini zikaja mashua nyingine kutoka Tiberia mpaka karibu na mahali pale walipokula mikate, wakati Bwana aliposhukuru.)
Jean 6.11-6.12 Jean 6.1
24 Basi mkutano, walipoona ya kuwa Yesu hayuko huko wala wanafunzi wake, waliingia mashuani wenyewe, wakaenda Kapernaumu wakimtafuta Yesu.
Jean 6.17 Jean 7.11 Jean 18.4-18.5 Jean 6.59 Jean 20.15
25 Hata walipomwona ng’ambo ya bahari, walimwambia, Rabi, wewe umekuja lini hapa?
Jean 1.38-1.39 Matthieu 23.7
26 Yesu akawajibu, akasema, Amin, amin, nawaambieni, Ninyi mnanitafuta, si kwa sababu mliona ishara, bali kwa sababu mlikula ile mikate mkashiba.
Jacques 4.3-4.4 Philippiens 2.21 Philippiens 3.19 Psaumes 78.37 Romains 16.18
27 Msikitendee kazi chakula chenye kuharibika, bali chakula kidumucho hata uzima wa milele; ambacho Mwana wa Adamu atawapa, kwa sababu huyo ndiye aliyetiwa muhuri na Baba, yaani, Mungu.
Esaïe 55.2 Jean 6.54 Romains 6.23 Jean 17.2 Jean 10.28
28 Basi wakamwambia, Tufanyeje ili tupate kuzitenda kazi za Mungu?
Luc 10.25 Deutéronome 5.27 Actes 9.6 Matthieu 19.16 Michée 6.7-6.8
29 Yesu akajibu, akawaambia, Hii ndiyo kazi ya Mungu, mmwamini yeye aliyetumwa na yeye.
1 Jean 3.23 Hébreux 5.9 Romains 4.4-4.5 Actes 16.31 Jean 3.36
30 Wakamwambia, Unafanya ishara gani basi, ili tuione tukakuamini? Unatenda kazi gani?
Jean 12.37 Matthieu 16.1-16.4 Hébreux 2.4 Exode 4.8 1 Rois 13.5
31 Baba zetu waliila mana jangwani kama vile ilivyoandikwa, Aliwapa chakula cha mbinguni ili wale.
Psaumes 105.40 Néhémie 9.15 Jean 6.49 1 Corinthiens 10.3 Apocalypse 2.17
32 Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Siye Musa aliyewapa chakula kile cha mbinguni, bali Baba yangu anawapa ninyi chakula cha kweli kitokacho mbinguni.
1 Jean 5.20 Exode 16.8 Jean 15.1 Jean 6.33 Jean 6.35
33 Kwa maana chakula cha Mungu ni kile kishukacho kutoka mbinguni na kuupa ulimwengu uzima.
1 Jean 1.1-1.2 Jean 3.13 Jean 6.50 1 Timothée 1.15 Jean 6.48
34 Basi wakamwambia, Bwana, sikuzote utupe chakula hiki.
Jean 4.15 Jean 6.26 Psaumes 4.6
35 Yesu akawaambia, Mimi ndimi chakula cha uzima; yeye ajaye kwangu hataona njaa kabisa, naye aniaminiye hataona kiu kamwe.
Jean 6.41 Luc 6.25 Jean 6.48-6.58 Apocalypse 22.17 Jean 7.37-7.38
36 Lakini naliwaambia ya kwamba mmeniona wala hamwamini.
Jean 6.26 Jean 12.37 Jean 6.40 Luc 16.31 1 Pierre 1.8-1.9
37 Wote anipao Baba watakuja kwangu; wala ye yote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe.
Jean 6.39 Jean 17.24 Jean 17.2 Jean 10.28-10.29 Jean 17.6
38 Kwa kuwa mimi sikushuka kutoka mbinguni ili niyafanye mapenzi yangu, bali mapenzi yake aliyenipeleka.
Jean 5.30 Jean 4.34 Jean 3.13 Jean 3.31 Jean 6.33
39 Na mapenzi yake aliyenipeleka ni haya, ya kwamba katika wote alionipa nisimpoteze hata mmoja, bali nimfufue siku ya mwisho.
Jean 6.40 Jean 6.54 Jean 6.44 Jean 17.12 Jean 18.9
40 Kwa kuwa mapenzi yake Baba yangu ni haya, ya kwamba kila amtazamaye Mwana na kumwamini yeye, awe na uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho.
Romains 6.23 Jean 6.54 Jean 1.14 Jean 6.27 Esaïe 45.21-45.22
41 Basi Wayahudi wakamnung’unikia, kwa sababu alisema, Mimi ni chakula kilichoshuka kutoka mbinguni.
Jean 6.33 Jean 6.58 Jean 6.51-6.52 Jean 6.60 Jean 6.43
42 Wakasema, Je! Huyu siye Yesu, mwana wa Yusufu, ambaye twamjua babaye na mamaye? Sasa asemaje huyu, Nimeshuka kutoka mbinguni?
Luc 4.22 Matthieu 13.55-13.56 Romains 9.5 Galates 4.4 Marc 6.3
43 Basi Yesu akajibu, akawaambia, Msinung’unike ninyi kwa ninyi.
Jean 6.64 Hébreux 4.13 Jean 16.19 Matthieu 16.8 Marc 9.33
44 Hakuna mtu awezaye kuja kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka; nami nitamfufua siku ya mwisho.
Jean 6.65 Matthieu 11.25-11.27 Jean 12.32 Ephésiens 2.4-2.10 Osée 11.4
45 Imeandikwa katika manabii, Na wote watakuwa wamefundishwa na Mungu. Basi kila aliyesikia na kujifunza kwa Baba huja kwangu.
Esaïe 54.13 Jérémie 31.33-31.34 Hébreux 8.10-8.11 Hébreux 10.16 Jean 6.65
46 Si kwamba mtu amemwona Baba, ila yeye atokaye kwa Mungu; huyo ndiye aliyemwona Baba.
Jean 1.18 Jean 7.29 1 Jean 4.12 Luc 10.22 Jean 5.37
47 Amin, amin, nawaambia, Yeye aaminiye yuna uzima wa milele.
Jean 3.36 Jean 5.24 Romains 5.9-5.10 Jean 6.54 Jean 3.16
48 Mimi ndimi chakula cha uzima.
Jean 6.51 Jean 6.33-6.35 Jean 6.41 1 Corinthiens 11.24-11.25 1 Corinthiens 10.16-10.17
49 Baba zenu waliila mana jangwani; wakafa.
Jean 6.58 Jean 6.31 Zacharie 1.5 1 Corinthiens 10.3-10.5 Hébreux 3.17-3.19
50 Hiki ni chakula kishukacho kutoka mbinguni, kwamba mtu akile wala asife.
Jean 6.33 Jean 6.51 Jean 6.58 Jean 6.42 Jean 8.51
51 Mimi ndimi chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka mbinguni; mtu akila chakula hiki, ataishi milele. Na chakula nitakachotoa mimi ni mwili wangu, kwa ajili ya uzima wa ulimwengu.
Ephésiens 5.2 Luc 22.19 Jean 3.13 2 Corinthiens 5.21 1 Jean 4.14
52 Basi Wayahudi walishindana wao kwa wao wakisema, Awezaje mtu huyu kutupa sisi mwili wake ili tuule?
Jean 10.19 Jean 9.16 Jean 3.9 Jean 6.41 Actes 17.32
53 Basi Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambieni, Msipoula mwili wake Mwana wa Adamu na kuinywa damu yake, hamna uzima ndani yenu.
1 Jean 5.12 Matthieu 26.26-26.28 Jean 15.4 Jean 6.55 Jean 3.3
54 Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu anao uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho.
Jean 6.39-6.40 Philippiens 3.7-3.10 Jean 4.14 Esaïe 55.1-55.3 Jean 6.63
55 Kwa maana mwili wangu ni chakula cha kweli, na damu yangu ni kinywaji cha kweli.
Jean 1.47 Jean 15.1 Jean 6.32 1 Jean 5.20 Jean 8.31
56 Aulaye mwili wangu na kuinywa damu yangu hukaa ndani yangu, nami hukaa ndani yake.
1 Jean 3.24 Jean 15.4-15.5 1 Jean 4.15-4.16 Jean 14.20 Jean 17.21-17.23
57 Kama vile Baba aliye hai alivyonituma mimi, nami ni hai kwa Baba; kadhalika naye mwenye kunila atakuwa hai kwa mimi.
Jean 5.26 Galates 2.20 Jean 3.17 1 Thessaloniciens 1.9 Jean 17.21
58 Hiki ndicho chakula kishukacho kutoka mbinguni; si kama mababa walivyokula, wakafa; bali akilaye chakula hicho ataishi milele.
Jean 6.47-6.51 Jean 6.41 Jean 6.31-6.34 Jean 3.36
59 Maneno hayo aliyasema katika sinagogi, alipokuwa akifundisha, huko Kapernaumu.
Jean 6.24 Proverbes 8.1-8.3 Psaumes 40.9-40.10 Jean 18.20 Luc 4.31
60 Basi watu wengi miongoni mwa wanafunzi wake waliposikia, walisema, Neno hili ni gumu, ni nani awezaye kulisikia?
Jean 6.66 Matthieu 11.6 Jean 8.31 Jean 6.41-6.42 Jean 8.43
61 Naye Yesu akafahamu nafsini mwake ya kuwa wanafunzi wake wanalinung’unikia neno hilo, akawaambia, Je! Neno hili linawakwaza?
Jean 2.24-2.25 Jean 6.64 Apocalypse 2.23 Matthieu 11.6 Jean 21.17
62 Itakuwaje basi, mmwonapo Mwana wa Adamu akipaa huko alikokuwako kwanza?
Marc 16.19 Jean 3.13 Luc 24.51 Jean 17.4-17.5 Ephésiens 4.8-4.10
63 Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu; maneno hayo niliyowaambia ni roho, tena ni uzima.
Jean 6.68 Psaumes 119.93 1 Corinthiens 15.45 Romains 10.17 Psaumes 119.50
64 Lakini kuna wengine miongoni mwenu wasioamini. Kwa maana Yesu alijua tangu mwanzo ni nani wasioamini, naye ni nani atakayemsaliti.
2 Timothée 2.19 Hébreux 4.13 Jean 13.10-13.11 Jean 10.26 Jean 6.61
65 Akasema, Kwa sababu hiyo nimewaambia ya kwamba hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba yangu.
Jean 6.44-6.45 Jean 6.37 2 Timothée 2.25 Ephésiens 2.8-2.9 Jean 12.37-12.41
66 Kwa ajili ya hayo wengi miongoni mwa wanafunzi wake wakarejea nyuma, wasiandamane naye tena.
Jean 6.60 1 Jean 2.19 Luc 9.62 Hébreux 10.38 2 Timothée 4.10
67 Basi Yesu akawaambia wale Thenashara, Je! Ninyi nanyi mwataka kuondoka?
Matthieu 10.2 Jean 6.70 Ruth 1.11-1.18 Luc 14.25-14.33 2 Samuel 15.19-15.20
68 Basi Simoni Petro akamjibu, Bwana! Twende kwa nani? Wewe unayo maneno ya uzima wa milele.
Jean 5.24 Jean 6.63 Psaumes 73.25 Actes 4.12 1 Jean 5.11-5.13
69 Nasi tumesadiki, tena tumejua, ya kuwa wewe ndiwe Mtakatifu wa Mungu.
Luc 9.20 Marc 8.29 Jean 11.27 Jean 1.41 Jean 20.31
70 Yesu akawajibu, Je! Mimi sikuwachagua ninyi Thenashara, na mmoja wenu ni shetani?
Jean 17.12 Jean 13.27 Jean 13.2 Jean 13.18 Jean 6.64
71 Alimnena Yuda, mwana wa Simoni Iskariote; maana huyo ndiye atakayemsaliti; naye ni mmojawapo wa wale Thenashara.
Matthieu 26.14-26.16 Jude 1.4 Jean 13.26 Jean 18.2-18.6 Psaumes 41.9

Cette Bible est dans le domaine public.