Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Marc 14.65
Bible en Swahili de l’est


Mort et résurrection de Jésus

Complot contre Jésus

1 Baada ya siku mbili ilikuwa sikukuu ya Pasaka, na mikate isiyochachwa; wakuu wa makuhani na waandishi wakatafuta njia ya kumkamata kwa hila na kumwua.
Luc 22.1-22.2 Exode 12.6-12.20 Jean 13.1 Lévitique 23.5-23.7 Deutéronome 16.1-16.8
2 Kwa maana walisema, Isiwe kwa wakati wa sikukuu, isije ikatokea ghasia katika watu.
Matthieu 26.5 Lamentations 3.27 Proverbes 21.30 Marc 11.32 Marc 11.18

Une femme verse du parfum sur Jésus

3 Naye alipokuwapo Bethania, nyumbani mwa Simoni mkoma, ameketi chakulani, alikuja mwanamke mwenye kibweta cha marhamu ya nardo safi ya thamani nyingi; akakivunja kibweta akaimimina kichwani pake.
Luc 7.37-7.39 Matthieu 21.17 Jean 11.2 Cantique 4.13-4.14 Jean 12.1-12.8
4 Palikuwa na watu waliochukizwa katika nafsi zao wakisema, Kwani kupoteza marhamu namna hii?
Jean 12.4-12.5 Matthieu 26.8-26.9 Malachie 1.12-1.13 Ecclésiaste 4.4 Ecclésiaste 5.4-5.8
5 Maana marhamu hii ingaliweza kuuzwa kwa dinari mia tatu na kuzidi, wakapewa maskini. Wakamnung’unikia sana yule mwanamke.
Jean 13.29 Jean 6.7 Psaumes 106.25 Matthieu 18.28 1 Corinthiens 10.10
6 Yesu akasema, Mwacheni; mbona mnamtaabisha? Amenitendea kazi njema;
Tite 3.8 1 Timothée 5.10 Matthieu 26.10 Ephésiens 2.10 Colossiens 1.10
7 maana sikuzote mnao maskini pamoja nanyi, na kila mpendapo mwaweza kuwatendea mema; lakini mimi hamnami sikuzote.
Deutéronome 15.11 Matthieu 26.11 1 Jean 3.16-3.19 Philémon 1.7 2 Corinthiens 9.13-9.14
8 Ametenda alivyoweza; ametangulia kuupaka mwili wangu marhamu kwa ajili ya maziko.
2 Corinthiens 8.12 2 Chroniques 31.20-31.21 Luc 23.53-24.3 Jean 19.32-19.42 Jean 12.7
9 Amin, nawaambia, Kila ihubiriwapo Injili katika ulimwengu wote, na hili alilotenda huyu litatajwa kwa kumbukumbu lake.
Marc 16.15 Matthieu 26.12-26.13 Psaumes 112.6-112.9 Zacharie 6.14 Matthieu 24.14
10 Yuda Iskariote, yule mmoja katika wale Thenashara, akaenda zake kwa wakuu wa makuhani, apate kumsaliti kwao.
Jean 13.2 Luc 22.3-22.6 Matthieu 26.14-26.16 Jean 13.30 Matthieu 10.4
11 Nao waliposikia walifurahi, wakaahidi kumpa fedha. Akatafuta njia ya kumsaliti wakati wa kufaa.
Proverbes 1.10-1.16 Matthieu 26.15 1 Rois 21.20 2 Pierre 2.14-2.15 Osée 7.3

Institution de la cène

12 Hata siku ya kwanza ya mikate isiyochachwa, walipoichinja pasaka, wanafunzi wake wakamwambia, Ni wapi utakapo tuende tukuandalie uile pasaka?
Exode 12.6 Exode 12.18 Exode 12.8 Deutéronome 16.1-16.4 Luc 22.7-22.13
13 Akatuma wawili katika wanafunzi wake, akawaambia, Nendeni zenu mjini; atakutana nanyi mwanamume amechukua mtungi wa maji; mfuateni;
Hébreux 4.13 Matthieu 26.18-26.19 Jean 2.5 Matthieu 8.9 Hébreux 5.9
14 na po pote atakapoingia, mwambieni mwenye nyumba, Mwalimu asema, Ki wapi chumba changu cha wageni, niile pasaka humo, pamoja na wanafunzi wangu?
Jean 13.13 Apocalypse 3.20 Marc 11.3 Jean 11.28 Marc 10.17
15 Naye mwenyewe atawaonyesha orofa kubwa, imeandikwa tayari; humo tuandalieni.
Actes 1.13 Psaumes 110.3 Actes 20.8 Jean 21.17 Proverbes 16.1
16 Wanafunzi wakatoka, wakaenda mjini, wakaona kama alivyowaambia, wakaiandaa pasaka.
Luc 22.13 Luc 22.35 Jean 16.4
17 Basi ilipokuwa jioni yuaja pamoja na wale Thenashara.
Luc 22.14 Matthieu 26.20-26.24 Jean 13.21-13.26 Luc 22.21-22.23
18 Nao walipokuwa wameketi chakulani, wakila, Yesu alisema, Amin, nawaambia, Mmoja wenu, naye anakula pamoja nami, atanisaliti.
Jean 6.70 Psaumes 41.9 Jean 3.3 Jean 13.21 Jean 3.11
19 Wakaanza kuhuzunika, wakamwambia mmoja mmoja, Je! Ni mimi?
Jean 13.22 Matthieu 26.22 Luc 22.21-22.23
20 Akawaambia, Ni mmoja wa hao Thenashara, ambaye achovya pamoja nami katika kombe.
Jean 13.26 Matthieu 26.47 Matthieu 26.23 Luc 22.47 Jean 6.71
21 Kwa maana Mwana wa Adamu aenda zake kama alivyoandikiwa; lakini ole wake mtu yule ambaye amsaliti Mwana wa Adamu; ingekuwa heri kwake mtu yule kama asingalizaliwa.
Zacharie 13.7 Psaumes 22.1-22.31 Jean 19.36-19.37 Esaïe 53.1-53.12 Actes 13.27-13.29
22 Nao walipokuwa wakila, alitwaa mkate, akabariki, akaumega, akawapa, akasema, Twaeni; huu ndio mwili wangu.
Matthieu 26.26-26.29 Luc 24.30 Marc 14.24 Marc 6.41 Jean 6.48-6.58
23 Akatwaa kikombe, akashukuru, akawapa; wakakinywea wote.
1 Corinthiens 10.16 Luc 22.17 Marc 14.22 Matthieu 26.27 Romains 14.6
24 Akawaambia, Hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi.
Exode 24.8 Zacharie 9.11 1 Corinthiens 10.16 Hébreux 13.20-13.21 Hébreux 9.15-9.23
25 Amin, nawaambia ninyi, Sitakunywa tena kabisa uzao wa mzabibu, hata siku ile nitakapounywa mpya katika ufalme wa Mungu.
Psaumes 104.15 Matthieu 26.29 Amos 9.13-9.14 Luc 22.29-22.30 Joël 3.18
26 Nao walipokwisha kuimba walitoka kwenda mlima wa Mizeituni.
Matthieu 26.30 Luc 22.39 Matthieu 21.1 Psaumes 47.6-47.7 1 Corinthiens 14.15
27 Yesu akawaambia, Mtakunguwazwa ninyi nyote kwa ajili yangu usiku huu; kwa kuwa imeandikwa, Nitampiga mchungaji, na kondoo watatawanyika.
Zacharie 13.7 Jean 16.32 Matthieu 26.31 2 Timothée 4.16 Luc 22.31-22.32
28 Lakini baada ya kufufuka kwangu, nitawatangulia kwenda Galilaya.
Matthieu 28.16 Marc 16.7 Matthieu 28.10 Matthieu 28.7 Matthieu 16.21
29 Petro akamwambia, Hata wajapokunguwazwa wote, lakini siyo mimi.
Luc 22.33-22.34 Jean 21.15 Matthieu 26.33-26.35 Jean 13.36-13.38
30 Yesu akamwambia, Amin, nakuambia wewe, Leo, usiku huu, kabla ya kuwika jogoo mara mbili, utanikana mara tatu.
Jean 13.38 Marc 14.66-14.72 Luc 22.34 Genèse 1.8 Genèse 1.5
31 Naye akazidi sana kusema, Ijaponipasa kufa nawe, hata hivyo sitakukana kamwe. Na wote wakasema vile vile.
Job 40.4-40.5 Exode 19.8 Deutéronome 5.27-5.29 Jérémie 17.9 2 Rois 8.13

Arrestation de Jésus

32 Kisha wakaja mpaka bustani iitwayo Gethsemane; akawaambia wanafunzi wake, Ketini hapa muda niombapo.
Marc 14.36 Marc 14.39 Matthieu 26.36-26.46 Jean 18.1-18.11 Psaumes 22.1-22.2
33 Akamtwaa Petro na Yakobo na Yohana pamoja naye, akaanza kufadhaika sana na kuhangaika.
Luc 22.44 Marc 5.37 Esaïe 53.10 Hébreux 5.7 Psaumes 38.11
34 Akawaambia, Roho yangu ina huzuni nyingi kiasi cha kufa; kaeni hapa mkeshe.
Jean 12.27 Marc 13.35-13.37 Ephésiens 6.18-6.19 Lamentations 1.12 Esaïe 53.12
35 Akaendelea mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akiomba ya kuwa, ikiwezekana, saa hiyo imwepuke.
Hébreux 5.7 Marc 14.41 Deutéronome 9.18 Matthieu 26.39 Luc 17.15-17.16
36 Akasema, Aba, Baba, yote yawezekana kwako; uniondolee kikombe hiki; walakini, si kama nitakavyo mimi, bali utakavyo wewe.
Philippiens 2.8 Jean 5.30 Galates 4.6 Jean 18.11 Jean 12.27
37 Akaja akawakuta wamelala usingizi, akamwambia Petro, Je! Simoni, umelala? Hukuweza kukesha saa moja?
Luc 9.31-9.32 Marc 14.29-14.31 Matthieu 25.5 Matthieu 26.40 Hébreux 12.3
38 Kesheni mwombe, msije mkaingia majaribuni, roho i radhi ila mwili ni dhaifu.
Matthieu 26.41 Romains 7.18-7.25 Luc 22.46 Luc 22.40 Matthieu 24.42
39 Akaenda zake tena, akaomba, akisema neno lilo hilo.
Matthieu 6.7 Matthieu 26.42-26.44 Luc 18.1 2 Corinthiens 12.8
40 Akaja tena akawakuta wamelala, maana macho yao yamekuwa mazito, wala hawakujua la kumjibu.
Marc 9.33-9.34 Romains 3.19 Genèse 44.16
41 Akaja mara ya tatu, akawaambia, Laleni sasa, mpumzike; yatosha, saa imekuja; tazama, Mwana wa Adamu anatiwa mikononi mwao wenye dhambi.
Marc 9.31 Marc 14.35 Marc 10.33-10.34 1 Rois 22.15 1 Rois 18.27
42 Ondokeni, twendeni zetu; tazama, yule anayenisaliti amekaribia.
Jean 18.1-18.2 Matthieu 26.46
43 Basi alipokuwa katika kusema, mara Yuda alifika, mmoja wa wale Thenashara, na pamoja naye mkutano, wana panga na marungu, wametoka kwa wakuu wa makuhani, na waandishi, na wazee.
Actes 1.16 Matthieu 26.47-26.56 Jean 18.3-18.11 Psaumes 3.1-3.2 Luc 22.47-22.53
44 Na yule anayemsaliti alikuwa amewapa ishara, akisema, Nitakayembusu, huyo ndiye; mkamateni, mkamchukue salama.
2 Samuel 20.9-20.10 1 Samuel 23.22-23.23 Proverbes 27.6 Josué 2.12 Actes 16.23
45 Basi alipokuja, mara akamwendea, akasema, Rabi, akambusu.
Malachie 1.6 Jean 20.16 Jean 13.13-13.14 Marc 12.14 Matthieu 23.7-23.10
46 Wakanyosha mikono yao wakamkamata.
Lamentations 4.20 Juges 16.21 Actes 2.23 Jean 18.12
47 Na mmoja wao waliokuwapo akafuta upanga, akampiga mtumwa wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.
Matthieu 26.51-26.54 Luc 22.49-22.51 Jean 18.10-18.11
48 Yesu akajibu, akawaambia, Je! Ni kama juu ya mnyang’anyi mmetoka wenye panga na marungu, kunitwaa mimi?
1 Samuel 26.18 Luc 22.52-22.53 Matthieu 26.55 1 Samuel 24.14-24.15
49 Kila siku nalikuwa mbele yenu hekaluni nikifundisha, msinikamate; lakini haya yamekuwa ili maandiko yapate kutimia.
Jean 18.20 Matthieu 26.56 Matthieu 26.54 Marc 12.35 Matthieu 1.22
50 Ndipo wakamwacha, wakakimbia wote.
Marc 14.27 Psaumes 38.11 Psaumes 88.18 Jean 16.32 Job 19.13-19.14
51 Na kijana mmoja alimfuata, amejitanda mwili wake nguo ya kitani; wakamkamata;
52 naye akaiacha ile nguo ya kitani, akakimbia yu uchi.
Marc 13.14-13.16 Genèse 39.12 Job 2.4

Jésus devant le conseil juif

53 Nao wakamchukua Yesu kwa Kuhani Mkuu; wakamkusanyikia wote, wakuu wa makuhani na wazee na waandishi.
Matthieu 26.57-26.68 Jean 18.12-18.14 Luc 22.54-22.62 Actes 4.5-4.6 Jean 18.19-18.24
54 Naye Petro akamfuata kwa mbali, hata ndani katika behewa ya Kuhani Mkuu; akawa ameketi pamoja na watumishi, anakota moto mwangani.
Jean 18.18 Matthieu 26.3 Marc 14.29-14.31 Marc 14.38 Luc 22.55-22.56
55 Basi wakuu wa makuhani na baraza yote wakatafuta ushuhuda juu ya Yesu wapate kumwua; wasione.
Actes 6.11-6.13 Daniel 6.4 1 Rois 21.10 Actes 24.1-24.13 1 Pierre 3.16-3.18
56 Kwa maana wengi walimshuhudia uongo, walakini ushuhuda wao haukupatana.
57 Hata wengine wakasimama, wakamshuhudia uongo, wakisema,
Matthieu 26.60-26.61 Actes 6.13-6.14 Jean 2.18-2.21 Marc 15.29 Jérémie 26.18
58 Sisi tulimsikia akisema, Mimi nitalivunja hekalu hili lililofanyika kwa mikono, na katika siku tatu nitajenga jingine lisilofanyika kwa mikono.
Hébreux 9.24 Jean 2.19 2 Corinthiens 5.1 Marc 15.29 Hébreux 9.11
59 Wala hata hivi ushuhuda wao haukupatana.
60 Kisha Kuhani Mkuu akasimama katikati, akamwuliza Yesu, akisema, Hujibu neno? Hawa wanakushuhudia nini?
Matthieu 26.62-26.63 Marc 15.3-15.5 Jean 19.9-19.10
61 Lakini akanyamaza, wala hakujibu neno. Kuhani Mkuu akamwuliza tena, akamwambia, Wewe ndiwe Kristo, Mwana wake Mtukufu?
Esaïe 53.7 Marc 15.2 Matthieu 16.16 Matthieu 26.63-26.64 Luc 22.67-22.71
62 Yesu akasema, Mimi ndiye, nanyi mtamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kuume wa nguvu, akija na mawingu ya mbinguni.
Psaumes 110.1 Daniel 7.13-7.14 Matthieu 24.30 Hébreux 1.3 Marc 13.26
63 Kuhani Mkuu akararua nguo zake, akisema, Tuna haja gani tena ya mashahidi?
Lévitique 21.10 Nombres 14.6 Matthieu 26.65 Jérémie 36.23-36.24 Actes 14.13-14.14
64 Mmesikia kufuru yake; mwaonaje ninyi? Wote wakamhukumu kuwa imempasa kuuawa.
Lévitique 24.16 Luc 22.71 Jean 10.31-10.33 Jean 8.58-8.59 1 Rois 21.9-21.13
65 Wengine wakaanza kumtemea mate, wakamfunika uso, na kumpiga makonde, na kumwambia, tabiri. Hata watumishi nao wakampiga makofi.
Actes 23.2 Marc 15.19 Luc 22.63-22.64 Esaïe 50.6 Matthieu 26.67-26.68
66 Na Petro alikuwa chini behewani; akaja mmoja wa vijakazi wa Kuhani Mkuu,
Marc 14.54 Luc 22.55-22.62 Jean 18.15-18.18 Jean 18.25-18.27 Matthieu 26.69-26.75
67 akamwona Petro akikota moto; akamkazia macho, akasema, Wewe nawe ulikuwapo pamoja na yule Mnazareti, Yesu.
Marc 14.54 Jean 1.45-1.49 Marc 10.47 Jean 19.19 Matthieu 21.11
68 Akakana, akasema, Sijui wala sisikii unayoyasema wewe. Akatoka nje hata ukumbini; jogoo akawika.
Jean 13.36-13.38 Marc 14.29-14.31 2 Timothée 2.12-2.13 Marc 14.72 Matthieu 26.71-26.72
69 Na yule kijakazi akamwona tena, akaanza tena kuwaambia waliosimama pale, Huyu ni mmoja wao.
Jean 18.17 Galates 6.1 Marc 14.38 Jean 18.25 Luc 22.58
70 Akakana tena. Kitambo kidogo tena wale waliosimama pale wakamwambia Petro, Hakika u mmoja wao, kwa sababu u Mgalilaya wewe.
Actes 2.7 Matthieu 26.73-26.74 Jean 18.26-18.27 Luc 22.59-22.60 Marc 14.68
71 Akaanza kulaani na kuapiza, Simjui mtu huyu mnayemnena.
Jérémie 17.9 2 Rois 10.32 1 Corinthiens 10.12 2 Rois 8.12-8.15
72 Na mara jogoo akawika mara ya pili. Petro akalikumbuka lile neno aliloambiwa na Yesu, Kabla ya kuwika jogoo mara mbili, utanikana mara tatu. Na alipolifikiri, akalia.
Marc 14.68 Marc 14.30 2 Samuel 24.10 Ezéchiel 16.63 Psaumes 119.59-119.60

Cette Bible est dans le domaine public.