Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jean 16.9
Bible en Swahili de l’est


1 Maneno hayo nimewaambia, msije mkachukizwa.
Matthieu 13.21 Matthieu 26.31-26.33 1 Pierre 2.8 Romains 14.21 Jean 15.18-15.27
2 Watawatenga na masinagogi; naam, saa yaja atakapodhania kila mtu awauaye ya kuwa anamtolea Mungu ibada.
Actes 26.9-26.11 Jean 9.22 Jean 12.42 1 Corinthiens 4.13 Actes 22.3-22.4
3 Na hayo watawatenda kwa sababu hawakumjua Baba wala mimi.
Jean 15.21 Jean 17.25 Jean 8.55 1 Jean 3.1 Jean 8.19
4 Lakini nimewaambia hayo, ili makusudi saa ile itakapokuja myakumbuke ya kuwa mimi naliwaambia. Sikuwaambia hayo tangu mwanzo, kwa sababu nalikuwapo pamoja nanyi.
Matthieu 9.15 Jean 14.29 Jean 13.19 Jean 17.12-17.13 Marc 13.23
5 Lakini sasa mimi naenda zangu kwake yeye aliyenipeleka, wala hakuna mmoja wenu aniulizaye, Unakwendapi?
Jean 13.36 Jean 7.33 Jean 16.28 Jean 16.10 Ephésiens 4.7-4.11
6 Ila kwa sababu nimewaambia hayo huzuni imejaa mioyoni mwenu.
Jean 14.1 Jean 16.20-16.22 Jean 20.11-20.15 Luc 24.17 Luc 22.45
7 Lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu.
Jean 14.26 Jean 15.26 Jean 14.16-14.17 Romains 8.28 Jean 7.39
8 Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu.
Jean 8.46 Jude 1.15 1 Corinthiens 14.24 Actes 2.37 Actes 16.29-16.30
9 Kwa habari ya dhambi, kwa sababu hawaniamini mimi;
Actes 2.22-2.38 Jean 8.23-8.24 Actes 3.14-3.19 Marc 16.16 Jean 12.47-12.48
10 kwa habari ya haki, kwa sababu mimi naenda zangu kwa Baba, wala hamnioni tena;
1 Pierre 3.18 1 Corinthiens 1.30 Jérémie 23.5-23.6 Actes 3.14 Jean 5.32
11 kwa habari ya hukumu, kwa sababu yule mkuu wa ulimwengu huu amekwisha kuhukumiwa.
Jean 12.31 Colossiens 2.15 Hébreux 2.14 1 Jean 3.8 Jean 14.30
12 Hata bado nikali ninayo mengi ya kuwaambia, lakini hamwezi kuyastahimili hivi sasa.
Marc 4.33 Jean 15.15 Hébreux 5.11-5.14 Actes 1.3 Jean 14.30
13 Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.
Jean 14.26 1 Corinthiens 2.10-2.13 Jean 14.17 Jean 15.26 Jean 7.16-7.18
14 Yeye atanitukuza mimi, kwa kuwa atatwaa katika yaliyo yangu na kuwapasha habari.
1 Jean 4.13-4.14 1 Jean 5.6 Actes 2.32-2.36 1 Jean 3.23-4.3 1 Pierre 1.10-1.12
15 Na yote aliyo nayo Baba ni yangu; kwa hiyo nalisema ya kwamba atatwaa katika yaliyo yangu, na kuwapasheni habari.
Jean 17.10 Jean 13.3 Matthieu 11.27 Jean 10.29-10.30 Jean 3.35
16 Bado kitambo kidogo nanyi hamnioni; na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona.
Jean 7.33 Jean 16.22 Jean 16.17-16.19 Jean 16.10 Actes 10.40-10.41
17 Basi baadhi ya wanafunzi wake wakasemezana, Neno gani hilo asemalo, Bado kitambo kidogo nanyi hamnioni, na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona? Na hilo, Kwa sababu naenda zangu kwa Baba?
Jean 16.16 Marc 9.32 Jean 16.5 Marc 9.10 Jean 14.22
18 Basi walisema, Neno gani hilo asemalo; hilo, Bado kitambo kidogo? Hatujui asemalo.
Luc 24.25 Matthieu 16.9-16.11 Hébreux 5.12
19 Yesu alifahamu ya kwamba wanataka kumwuliza, akawaambia, Ndilo hilo mnaloulizana, ya kuwa nalisema, Bado kitambo kidogo nanyi hamnioni, na tena bado kitambo kidogo nanyi mtaniona?
Jean 16.30 Jean 2.24-2.25 Jean 13.33 Jean 16.16 Matthieu 9.4
20 Amin, amin, nawaambia, Ninyi mtalia na kuomboleza, bali ulimwengu utafurahi; ninyi mtahuzunishwa, lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.
Marc 16.10 Luc 23.27 Matthieu 5.4 Apocalypse 11.10 Luc 6.21
21 Mwanamke azaapo, yuna huzuni kwa kuwa saa yake imefika; lakini akiisha kuzaa mwana, haikumbuki tena ile dhiki, kwa sababu ya furaha ya kuzaliwa mtu ulimwenguni.
1 Thessaloniciens 5.3 Jérémie 30.6-30.7 Luc 1.57-1.58 Galates 4.27 Genèse 3.16
22 Basi ninyi hivi sasa mna huzuni; lakini mimi nitawaona tena; na mioyo yenu itafurahi, na furaha yenu hakuna awaondoleaye.
Jean 16.6 1 Pierre 1.8 Actes 13.52 Hébreux 6.18 Actes 2.46
23 Tena siku ile hamtaniuliza neno lo lote. Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa jina langu.
1 Jean 5.14-5.16 Esaïe 65.24 Matthieu 21.22 Jean 15.7 Jean 14.20
24 Hata sasa hamkuomba neno kwa jina langu; ombeni, nanyi mtapata; furaha yenu iwe timilifu.
Matthieu 7.7-7.8 Jean 15.11 Jacques 4.2-4.3 Ephésiens 1.16-1.17 2 Thessaloniciens 2.16-2.17
25 Hayo nimesema nanyi kwa mithali; saa yaja ambapo sitasema nanyi tena kwa mithali, lakini nitawapa waziwazi habari ya Baba.
Jean 16.2 Matthieu 13.10-13.11 Psaumes 49.4 Marc 4.13 Jean 10.6
26 Na siku ile mtaomba kwa jina langu, wala siwaambii ya kwamba mimi nitawaombea kwa Baba;
Jean 17.19 Romains 8.34 Jean 14.16 Jean 17.24 Jean 16.23
27 kwa maana Baba mwenyewe awapenda kwa kuwa ninyi mmenipenda mimi, na kusadiki ya kwamba mimi nalitoka kwa Baba.
Jean 14.21 Jean 14.23 Jean 8.42 Jean 21.15-21.17 1 Corinthiens 16.22
28 Nalitoka kwa Baba, nami nimekuja hapa ulimwenguni; tena nauacha ulimwengu; na kwenda kwa Baba.
Jean 13.3 Jean 13.1 Jean 8.14 Jean 16.5 Jean 17.13
29 Basi wanafunzi wake wakasema, Tazama, sasa wasema waziwazi, wala huneni mithali yo yote.
Jean 16.25
30 Sasa tumejua ya kuwa wewe wafahamu mambo yote, wala huna haja ya mtu akuulize; kwa hiyo twasadiki ya kwamba ulitoka kwa Mungu.
Jean 21.17 Jean 5.20 Jean 16.17 Jean 17.8 Jean 16.27-16.28
31 Yesu akawajibu, Je! Mnasadiki sasa?
Jean 13.38 Luc 9.44-9.45
32 Tazama, saa yaja, naam, imekwisha kuja, ambapo mtatawanyika kila mmoja kwao kwao, na kuniacha mimi peke yangu; walakini mimi si peke yangu, kwa kuwa Baba yupo pamoja nami.
Jean 8.29 Matthieu 26.31 Jean 8.16 Zacharie 13.7 Marc 14.27
33 Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu.
Jean 14.27 1 Jean 4.4 1 Jean 5.4 Jean 14.1 Jean 15.18-15.21

Cette Bible est dans le domaine public.