Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Hébreux 11.7
Bible en Swahili de l’est


Exemples de foi

1 Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.
2 Corinthiens 5.7 2 Corinthiens 4.18 Romains 8.24-8.25 Hébreux 11.7 Hébreux 6.18-6.19
2 Maana kwa hiyo wazee wetu walishuhudiwa.
Hébreux 11.39 Hébreux 11.4
3 Kwa imani twafahamu ya kuwa ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu, hata vitu vinavyoonekana havikufanywa kwa vitu vilivyo dhahiri.
Romains 4.17 Apocalypse 4.11 Psaumes 33.6 Jean 1.3 2 Pierre 3.5
4 Kwa imani Habili alimtolea Mungu dhabihu iliyo bora kuliko Kaini; kwa hiyo alishuhudiwa kuwa ana haki; Mungu akazishuhudia sadaka zake, na kwa hiyo, ijapokuwa amekufa, angali akinena.
Matthieu 23.35 Genèse 4.3-4.5 Genèse 4.10 Hébreux 12.24 Jude 1.11
5 Kwa imani Henoko alihamishwa, asije akaona mauti, wala hakuonekana, kwa sababu Mungu alimhamisha; maana kabla ya kuhamishwa alikuwa ameshuhudiwa kwamba amempendeza Mungu.
2 Rois 2.11 Genèse 5.21-5.24 Jude 1.14 Psaumes 89.48 Luc 3.37
6 Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.
Proverbes 8.17 Jérémie 29.13-29.14 1 Chroniques 28.9 Luc 12.31 Matthieu 6.33
7 Kwa imani Nuhu akiisha kuonywa na Mungu katika habari za mambo yasiyoonekana bado, kwa jinsi alivyomcha Mungu, aliunda safina, apate kuokoa nyumba yake. Na hivyo akauhukumu makosa ulimwengu, akawa mrithi wa haki ipatikanayo kwa imani.
1 Pierre 3.20 Romains 4.13 Ezéchiel 14.20 Ezéchiel 14.14 Hébreux 5.7
8 Kwa imani Ibrahimu alipoitwa aliitika, atoke aende mahali pale atakapopapata kuwa urithi; akatoka asijue aendako.
Genèse 12.1-12.4 Actes 7.2-7.4 Genèse 12.7 Matthieu 7.24-7.25 1 Pierre 1.22
9 Kwa imani alikaa ugenini katika ile nchi ya ahadi, kama katika nchi isiyo yake, akikaa katika hema pamoja na Isaka na Yakobo, warithi pamoja naye wa ahadi ile ile.
Genèse 12.8 Genèse 13.18 Genèse 18.9 Hébreux 6.17 Genèse 13.3
10 Maana alikuwa akiutazamia mji wenye misingi, ambao mwenye kuubuni na kuujenga ni Mungu.
Hébreux 13.14 Hébreux 12.22 Apocalypse 21.2 2 Corinthiens 5.1 Philippiens 3.20
11 Kwa imani hata Sara mwenyewe alipokea uwezo wa kuwa na mimba; alipokuwa amepita wakati wake; kwa kuwa alimhesabu yeye aliyeahidi kuwa mwaminifu.
Genèse 18.11-18.14 Hébreux 10.23 Romains 4.20-4.21 Genèse 17.17-17.19 Luc 1.36
12 Na kwa ajili ya hayo wakazaliwa na mtu mmoja, naye alikuwa kama mfu, watu wengi kama nyota za mbinguni wingi wao, na kama mchanga ulio ufuoni, usioweza kuhesabika.
Genèse 22.17 Genèse 32.12 Genèse 15.5 Osée 1.10 Esaïe 10.22
13 Hawa wote wakafa katika imani, wasijazipokea zile ahadi, bali wakaziona tokea mbali na kuzishangilia, na kukiri kwamba walikuwa wageni, na wasafiri juu ya nchi.
Hébreux 11.39 Genèse 23.4 Jean 8.56 Psaumes 39.12 Genèse 47.9
14 Maana hao wasemao maneno kama hayo waonyesha wazi kwamba wanatafuta nchi yao wenyewe.
2 Corinthiens 4.18-5.7 Philippiens 1.23 Romains 8.23-8.25 Hébreux 11.16 Hébreux 13.14
15 Na kama wangaliikumbuka nchi ile waliyotoka, wangalipata nafasi ya kurejea.
Genèse 24.6-24.8 Genèse 12.10 Genèse 32.9-32.11 Genèse 31.18 Genèse 11.31
16 Lakini sasa waitamani nchi iliyo bora, yaani, ya mbinguni. Kwa hiyo Mungu haoni haya kuitwa Mungu wao; maana amewatengenezea mji.
Exode 3.6 Hébreux 11.10 Hébreux 2.11 Hébreux 13.14 Exode 3.15
17 Kwa imani Ibrahimu alipojaribiwa, akamtoa Isaka awe dhabihu; na yeye aliyezipokea hizo ahadi alikuwa akimtoa mwanawe, mzaliwa pekee;
Genèse 22.16 Genèse 22.1-22.12 Job 1.11-1.12 Proverbes 17.3 Zacharie 13.9
18 naam, yeye aliyeambiwa, Katika Isaka uzao wako utaitwa,
Genèse 21.12 Romains 9.7 Genèse 17.19
19 akihesabu ya kuwa Mungu aweza kumfufua hata kutoka kuzimu; akampata tena toka huko kwa mfano.
Romains 4.17-4.21 Genèse 22.13 Ephésiens 3.20 Genèse 22.4-22.5 Hébreux 11.11-11.12
20 Kwa imani Isaka akawabariki Yakobo na Esau, hata katika habari ya mambo yatakayokuwa baadaye.
Genèse 27.27-27.40 Genèse 28.2-28.3
21 Kwa imani Yakobo, alipokuwa katika kufa, akambariki kila mmoja wa wana wa Yusufu, akaabudu akiegemea kichwa cha fimbo yake.
Genèse 48.5-48.22 Genèse 47.31-48.1
22 Kwa imani Yusufu, alipokuwa amekaribia mwisho wake, alitaja habari za kutoka kwao wana wa Israeli, akaagiza kwa habari ya mifupa yake.
Exode 13.19 Genèse 50.24-50.25 Actes 7.16 Josué 24.32
23 Kwa imani Musa, alipozaliwa, akafichwa miezi mitatu na wazazi wake, kwa sababu waliona kwamba ni mtoto mzuri; wala hawakuiogopa amri ya mfalme.
Exode 1.22 Exode 1.16 Exode 2.2-2.10 Actes 7.20 Hébreux 13.6
24 Kwa imani Musa alipokuwa mtu mzima, akakataa kuitwa mwana wa binti Farao;
Exode 2.10-2.11 Actes 7.21-7.24
25 akaona ni afadhali kupata mateso pamoja na watu wa Mungu kuliko kujifurahisha katika dhambi kwa kitambo;
Psaumes 84.10 Job 20.5 Job 36.21 2 Corinthiens 5.17 Romains 8.17-8.18
26 akihesabu ya kuwa kushutumiwa kwake Kristo ni utajiri mkuu kuliko hazina za Misri; kwa kuwa aliyatazamia hayo malipo.
Hébreux 13.13 Hébreux 10.35 Hébreux 2.2 Philippiens 3.7 1 Pierre 4.14
27 Kwa imani akatoka Misri, asiogope ghadhabu ya mfalme; maana alistahimili kama amwonaye yeye asiyeonekana.
Hébreux 11.13 Exode 2.14-2.15 Exode 14.10-14.13 Exode 10.28-10.29 1 Timothée 1.17
28 Kwa imani akaifanya Pasaka, na kule kunyunyiza damu, ili yule mwenye kuwaangamiza wazaliwa wa kwanza asiwaguse wao.
Exode 12.21-12.30 Exode 12.3-12.14 Hébreux 9.19 1 Pierre 1.2 Hébreux 12.24
29 Kwa imani wakapita kati ya Bahari ya Shamu, kama katika nchi kavu; Wamisri walipojaribu kufanya vivyo wakatoswa.
Psaumes 106.9-106.11 Esaïe 63.11-63.16 Psaumes 114.1-114.5 Psaumes 136.13-136.15 Néhémie 9.11
30 Kwa imani kuta za Yeriko zikaanguka, zilipokwisha kuzungukwa siku saba.
Josué 6.3-6.20 2 Corinthiens 10.4-10.5
31 Kwa imani Rahabu, yule kahaba, hakuangamia pamoja na hao walioasi; kwa kuwa aliwakaribisha wale wapelelezi kwa amani.
Jacques 2.25 Josué 6.22-6.25 Matthieu 1.5 Hébreux 3.18 Matthieu 1.1
32 Nami niseme nini tena? Maana wakati usingenitosha kuleta habari za Gideoni na Baraka na Samsoni na Yeftha na Daudi na Samweli na za manabii;
1 Samuel 1.20 1 Samuel 16.13 1 Samuel 16.1 Juges 13.1-13.16 Juges 11.1-11.12
33 ambao kwa imani walishinda milki za wafalme, walitenda haki, walipata ahadi, walifunga vinywa vya simba,
Juges 14.5-14.6 Psaumes 144.1-144.2 1 Samuel 17.33-17.36 Psaumes 44.2-44.6 1 Pierre 5.8
34 walizima nguvu za moto, waliokoka na makali ya upanga. Walitiwa nguvu baada ya kuwa dhaifu, walikuwa hodari katika vita, walikimbiza majeshi ya wageni.
Juges 7.19-7.25 Juges 15.8 1 Rois 19.3 2 Rois 6.32 2 Rois 6.16-6.18
35 Wanawake walipokea wafu wao waliofufuliwa. Lakini wengine waliumizwa vibaya hata kuuawa, wasikubali ukombozi, ili wapate ufufuo ulio bora;
1 Rois 17.22-17.24 2 Rois 4.27-4.37 Matthieu 22.30 Actes 9.41 Actes 22.29
36 wengine walijaribiwa kwa dhihaka na mapigo, naam, kwa mafungo, na kwa kutiwa gerezani;
Jérémie 20.2 Genèse 39.20 2 Chroniques 16.10 Jérémie 20.7 2 Chroniques 30.10
37 walipigwa kwa mawe, walikatwa kwa misumeno, walijaribiwa, waliuawa kwa upanga; walizunguka-zunguka wakivaa ngozi za kondoo na ngozi za mbuzi; walikuwa wahitaji, wakiteswa, wakitendwa mabaya;
2 Chroniques 24.21 1 Rois 19.10 Jérémie 26.23 2 Rois 1.8 1 Rois 21.13-21.15
38 (watu ambao ulimwengu haukustahili kuwa nao), walikuwa wakizunguka-zunguka katika nyika na katika milima na katika mapango na katika mashimo ya nchi.
1 Rois 18.4 1 Rois 19.9 1 Samuel 22.1 1 Rois 18.13 1 Samuel 24.1-24.3
39 Na watu hao wote wakiisha kushuhudiwa kwa sababu ya imani yao, hawakuipokea ahadi;
Hébreux 11.13 Hébreux 11.2 1 Pierre 1.12 Luc 10.23-10.24
40 kwa kuwa Mungu alikuwa ametangulia kutuwekea sisi kitu kilicho bora, ili wao wasikamilishwe pasipo sisi.
Apocalypse 6.11 Hébreux 5.9 Hébreux 10.11-10.14 Hébreux 7.22 Hébreux 9.23

Cette Bible est dans le domaine public.