Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Actes 8.35
Bible en Swahili de l’est


1 Siku ile kukatukia adha kuu ya kanisa lililokuwa katika Yerusalemu; wote wakatawanyika katika nchi ya Uyahudi na Samaria, isipokuwa hao mitume.
Actes 7.58 Actes 5.40 Actes 5.33 Actes 22.20 Actes 8.4
2 Watu watauwa wakamzika Stefano, wakamfanyia maombolezo makuu.
2 Chroniques 32.33 Deutéronome 34.8 Genèse 23.2 Actes 10.2 1 Samuel 28.3
3 Sauli akaliharibu kanisa, akiingia kila nyumba, na kuwaburuta wanaume na wanawake na kuwatupa gerezani.
1 Corinthiens 15.9 1 Timothée 1.13 Galates 1.13 Philippiens 3.6 Actes 22.19

Témoignage en Judée et environs

L’Évangile en Samarie

4 Lakini wale waliotawanyika wakaenda huko na huko wakilihubiri neno.
Actes 8.1 Actes 15.35 Matthieu 10.23 1 Thessaloniciens 2.2 Actes 11.19
5 Filipo akatelemka akaingia mji wa Samaria, akawahubiri Kristo.
Actes 6.5 Actes 21.8 Actes 8.40 Actes 8.35-8.36 Actes 5.42
6 Na makutano kwa nia moja wakasikiliza maneno yale yaliyosemwa na Filipo walipoyasikia na kuziona ishara alizokuwa akizifanya.
Actes 13.44 Jean 4.41-4.42 2 Chroniques 30.12 Matthieu 20.15-20.16
7 Kwa maana pepo wachafu wakawatoka wengi waliopagawa nao, wakilia kwa sauti kuu; na watu wengi waliopooza, na viwete, wakaponywa.
Marc 16.17-16.18 Actes 5.16 Matthieu 10.1 Luc 10.17 Hébreux 2.4
8 Ikawa furaha kubwa katika mji ule.
Actes 8.39 Psaumes 98.2-98.6 Esaïe 35.1-35.2 Actes 13.52 Romains 15.9-15.12
9 Na mtu mmoja, jina lake Simoni, hapo kwanza alikuwa akifanya uchawi katika mji ule, akiwashangaza watu wa taifa la Wasamaria, akisema ya kuwa yeye ni mtu mkubwa.
Actes 5.36 Actes 13.6 Jean 7.18 Apocalypse 13.13-13.14 2 Timothée 3.5
10 Wote wakamsikiliza tangu mdogo hata mkubwa, wakisema, Mtu huyu ni uweza wa Mungu, ule Mkuu.
Actes 14.11 Actes 28.6 Jérémie 6.13 Apocalypse 13.3 Ephésiens 4.14
11 Wakamsikiliza, kwa maana amewashangaza muda mwingi kwa uchawi wake.
Galates 3.1 Actes 8.9 Esaïe 44.25 Esaïe 47.9-47.13 Esaïe 8.19
12 Lakini walipomwamini Filipo, akizihubiri habari njema za ufalme wa Mungu, na jina lake Yesu Kristo, wakabatizwa, wanaume na wanawake.
Actes 2.38 Actes 1.3 1 Pierre 3.21 Matthieu 28.19 Actes 2.41
13 Na yeye Simoni mwenyewe aliamini akabatizwa, akashikamana na Filipo; akashangaa alipoziona ishara na miujiza mikubwa inayotendeka.
Actes 8.6-8.7 Actes 19.11 Psaumes 106.12-106.13 Luc 8.13 Jean 8.30-8.31
14 Na mitume waliokuwako Yerusalemu, waliposikia ya kwamba Samaria imelikubali neno la Mungu, wakawapelekea Petro na Yohana;
Actes 8.1 Galates 2.9 1 Thessaloniciens 2.13 1 Thessaloniciens 3.2 2 Thessaloniciens 2.10
15 ambao waliposhuka, wakawaombea wampokee Roho Mtakatifu;
Actes 2.38 Philippiens 1.19 Jean 16.23-16.24 Matthieu 18.19 Jean 14.13-14.14
16 kwa maana bado hajawashukia hata mmoja wao, ila wamebatizwa tu kwa jina lake Bwana Yesu.
Matthieu 28.19 Actes 2.38 Actes 19.2 Galates 3.27 Actes 11.15-11.17
17 Ndipo wakaweka mikono yao juu yao, nao wakampokea Roho Mtakatifu.
Actes 6.6 Hébreux 6.2 Actes 9.17 Actes 19.6 Actes 13.3
18 Hata Simoni alipoona ya kuwa watu wanapewa Roho Mtakatifu kwa kuwekewa mikono ya mitume, akataka kuwapa fedha akisema,
Matthieu 10.8 2 Rois 8.9 Ezéchiel 13.19 2 Rois 5.15-5.16 1 Timothée 6.5
19 Nipeni na mimi uwezo huu, ili kila mtu nitakayemweka mikono yangu, apokee Roho Mtakatifu.
Luc 14.7-14.11 3 Jean 1.9 Actes 8.9-8.11 Matthieu 18.1-18.3 1 Corinthiens 15.8-15.9
20 Lakini Petro akamwambia, Fedha yako na ipotelee mbali pamoja nawe, kwa kuwa umedhania ya kuwa karama ya Mungu yapatikana kwa mali.
Daniel 5.17 Actes 2.38 Matthieu 10.8 Apocalypse 18.15 Proverbes 15.26
21 Huna fungu wala huna sehemu katika jambo hili, kwa kuwa moyo wako si mnyofu mbele za Mungu.
Psaumes 36.1 Matthieu 6.22-6.24 Josué 22.25 Hébreux 4.13 Ezéchiel 14.3
22 Basi, tubia uovu wako huu, ukamwombe Bwana, ili kama yamkini, usamehewe fikira hii ya moyo wako.
Daniel 4.27 Apocalypse 2.21 Joël 2.13-2.14 Esaïe 55.6-55.7 2 Timothée 2.25-2.26
23 Kwa maana nakuona u katika uchungu kama nyongo, na tena u katika kifungo cha uovu.
Proverbes 5.22 Esaïe 58.6 Hébreux 12.15 Jean 8.34 Jérémie 9.15
24 Simoni akajibu, akasema, Niombeeni ninyi kwa Bwana, yasinifikilie mambo haya mliyosema hata moja.
Exode 8.8 Nombres 21.7 Jacques 5.16 Exode 10.17 1 Rois 13.6
25 Nao walipokwisha kushuhudia na kulihubiri neno la Bwana wakarudi Yerusalemu, wakaihubiri Injili katika vijiji vingi vya Wasamaria.
Actes 1.8 Actes 28.31 Actes 28.23 Actes 20.21 1 Pierre 5.12

L’Évangile annoncé à un eunuque éthiopien

26 Malaika wa Bwana akasema na Filipo, akamwambia, Ondoka ukaende upande wa kusini hata njia ile itelemkayo kutoka Yerusalemu kwenda Gaza; nayo ni jangwa.
Actes 5.19 Actes 27.23 Hébreux 1.14 Actes 12.23 2 Rois 1.3
27 Naye akaondoka, akaenda; mara akamwona mtu wa Kushi, towashi, mwenye mamlaka chini ya Kandake malkia wa Kushi, aliyewekwa juu ya hazina yake yote; naye alikuwa amekwenda Yerusalemu kuabudu,
Psaumes 87.4 Psaumes 68.31 Jean 12.20 Sophonie 3.10 1 Rois 8.41-8.43
28 akawa akirejea, ameketi garini mwake akisoma chuo cha nabii Isaya.
Jean 5.39-5.40 Actes 28.25 Deutéronome 17.18-17.19 Esaïe 1.1 Proverbes 8.33-8.34
29 Roho akamwambia Filipo, Sogea karibu na gari hili, ukashikamane nalo.
Actes 10.19 Actes 11.12 Actes 16.6-16.7 Actes 20.22-20.23 1 Timothée 4.1
30 Basi Filipo akaenda mbio, akamsikia anasoma chuo cha nabii Isaya; akanena, Je! Yamekuelea haya unayosoma?
Ecclésiaste 9.10 Matthieu 13.51 Ephésiens 5.17 Matthieu 15.10 Matthieu 13.19
31 Akasema, Nitawezaje kuelewa, mtu asiponiongoza? Akamsihi Filipo apande na kuketi pamoja naye.
Romains 10.14 Jacques 1.21 1 Corinthiens 3.18 Proverbes 30.2-30.3 1 Corinthiens 14.36-14.37
32 Na fungu la Maandiko alilokuwa akilisoma ni hili, Aliongozwa kwenda machinjoni kama kondoo, Na kama vile mwana-kondoo alivyo kimya mbele yake amkataye manyoya, Vivyo hivyo yeye naye hafunui kinywa chake.
Esaïe 53.7-53.8 1 Pierre 2.21-2.24 Jérémie 51.40 Jean 1.29 Psaumes 39.2
33 Katika kujidhili kwake hukumu yake iliondolewa. Ni nani atakayeeleza kizazi chake? Kwa maana uzima wake umeondolewa katika nchi.
Esaïe 53.8 Esaïe 53.12 Job 27.2 Psaumes 22.15 Esaïe 5.23
34 Yule towashi akamjibu Filipo, akasema, Nakuomba, nabii huyu; asema maneno haya kwa habari ya nani; ni habari zake mwenyewe au za mtu mwingine?
Matthieu 13.36 Matthieu 15.15 Matthieu 2.2-2.4
35 Filipo akafunua kinywa chake, naye, akianza kwa andiko lilo hilo, akamhubiri habari njema za Yesu.
Actes 18.28 Luc 24.27 Actes 28.23 Matthieu 5.2 2 Corinthiens 6.11
36 Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe?
Actes 10.47 1 Jean 5.6 Ezéchiel 36.25 Tite 3.5-3.6 Jean 3.23
37 Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba Yesu Kristo ndiye Mwana wa Mungu.]
38 Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza.
Jean 4.1 Jean 3.22-3.23
39 Kisha, walipopanda kutoka majini, Roho wa Bwana akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi.
Ezéchiel 11.24 2 Rois 2.16 Ezéchiel 8.3 1 Rois 18.12 Ezéchiel 43.5
40 Lakini Filipo akaonekana katika Azoto, na alipokuwa akipita akahubiri Injili katika miji yote, hata akafika Kaisaria.
Actes 10.1 Actes 23.23 Actes 21.8 Actes 25.4 Actes 23.33

Cette Bible est dans le domaine public.