Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jean 8.51
Bible en Swahili de l’est


La femme adultère

1 Walikwenda kila mtu nyumbani kwake; naye Yesu akaenda mpaka mlima wa Mizeituni.
Matthieu 21.1 Marc 11.1 Luc 19.37 Marc 13.3
2 Hata asubuhi kulipokucha akaingia tena hekaluni, na watu wote wakamwendea; naye akaketi, akawa akiwafundisha.
Matthieu 26.55 Luc 4.20 Matthieu 5.1-5.2 Luc 5.3 Luc 21.37
3 Waandishi na Mafarisayo wakamletea mwanamke aliyefumaniwa katika uzinzi, wakamweka katikati.
4 Wakamwambia, Mwalimu, mwanamke huyu amefumaniwa alipokuwa akizini.
5 Basi katika torati, Musa alituamuru kuwapiga kwa mawe wanawake namna hii; nawe wasemaje?
Lévitique 20.10 Deutéronome 22.21-22.24 Matthieu 19.6-19.8 Matthieu 22.16-22.18 Matthieu 5.17
6 Nao wakasema neno hilo wakimjaribu, ili wapate sababu ya kumshitaki. Lakini Yesu akainama, akaandika kwa kidole chake katika nchi.
Jérémie 17.13 Luc 10.25 Matthieu 19.3 Ecclésiaste 3.7 Matthieu 22.18
7 Nao walipozidi kumhoji, alijiinua, akawaambia, Yeye asiye na dhambi miongoni mwenu na awe wa kwanza wa kumtupia jiwe.
Deutéronome 17.6-17.7 Romains 2.1-2.3 Psaumes 50.16-50.20 Proverbes 26.4-26.5 Colossiens 4.6
8 Akainama tena, akaandika kwa kidole chake katika nchi.
9 Nao waliposikia, wakashitakiwa na dhamiri zao, wakatoka mmoja mmoja, wakianzia tangu wazee hata wa mwisho wao; akabaki Yesu peke yake, na yule mwanamke amesimama katikati.
Psaumes 40.14 Ecclésiaste 7.22 Genèse 42.21-42.22 Romains 2.15 Psaumes 9.15-9.16
10 Yesu akajiinua asimwone mtu ila yule mwanamke, akamwambia, Mwanamke, wako wapi wale washitaki wako? Je! Hakuna aliyekuhukumu kuwa na hatia?
Esaïe 41.11-41.12
11 Akamwambia, Hakuna, Bwana. Yesu akamwambia, Wala mimi sikuhukumu. Enenda zako; wala usitende dhambi tena.]
Jean 5.14 Jean 3.17 Jean 8.15 Romains 2.4 Jean 18.36

Jésus, la lumière du monde

12 Basi Yesu akawaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.
Jean 12.46 Jean 9.5 Jean 12.35 Matthieu 5.14 Jean 3.19
13 Basi Mafarisayo wakamwambia, Wewe unajishuhudia mwenyewe; ushuhuda wako si kweli.
Jean 5.31-5.47
14 Yesu akajibu, akawaambia, Mimi ningawa ninajishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu ndio kweli; kwa sababu najua nilikotoka na niendako; lakini ninyi hamjui nilikotoka wala niendako.
Jean 13.3 Jean 16.28 Jean 8.42 Jean 14.10 2 Corinthiens 11.31
15 Ninyi mwahukumu kwa kufuata mambo ya mwili; mimi simhukumu mtu.
Jean 7.24 1 Samuel 16.7 Jean 12.47 Jean 3.17 Jean 8.11
16 Nami nijapohukumu, hukumu yangu ni kweli; kwa kuwa mimi si peke yangu, bali ni mimi na yeye aliyenipeleka.
Jean 16.32 Jean 8.29 Esaïe 32.1-32.2 Psaumes 45.6-45.7 Psaumes 99.4
17 Tena katika torati yenu imeandikwa kwamba, Ushuhuda wa watu wawili ni kweli.
Matthieu 18.16 Deutéronome 19.15 Deutéronome 17.6 Galates 4.21 Hébreux 10.28
18 Mimi ndimi ninayejishuhudia mwenyewe, naye Baba aliyenipeleka ananishuhudia.
Hébreux 2.4 Jean 14.6 Jean 8.58 Jean 8.12 1 Jean 5.6-5.12
19 Basi wakamwambia, Yuko wapi Baba yako? Yesu akajibu, Mimi hamnijui, wala Baba yangu hammjui; kama mngalinijua mimi, mngalimjua na Baba yangu.
Jean 16.3 Jean 7.28 2 Corinthiens 4.4-4.6 Jean 8.54-8.55 1 Corinthiens 15.34
20 Maneno hayo aliyasema alipokuwa akifundisha hekaluni, katika chumba cha hazina; wala hakuna mtu aliyemkamata, kwa sababu saa yake ilikuwa haijaja bado.
Jean 7.30 Marc 12.41 Jean 7.8 Matthieu 27.6 Marc 12.43
21 Basi akawaambia tena, Mimi naondoka, nanyi mtanitafuta; nanyi mtakufa katika dhambi yenu; mimi niendako ninyi hamwezi kuja.
Jean 7.34 Jean 8.24 Jean 13.33 Matthieu 23.39 Jean 12.33
22 Basi Wayahudi wakasema, Je! Atajiua! Kwa kuwa asema, Mimi niendako ninyi hamwezi kuja?
Jean 8.52 Jean 8.48 Hébreux 12.3 Jean 7.20 Jean 7.35
23 Akawaambia, Ninyi ni wa chini, mimi ni wa juu; ninyi ni wa ulimwengu huu, mimi si wa ulimwengu huu.
Jean 3.31 Jean 17.14 1 Jean 2.15-2.16 Jean 17.16 Jean 1.14
24 Kwa hiyo naliwaambieni ya kwamba mtakufa katika dhambi zenu; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye, mtakufa katika dhambi zenu.
Hébreux 12.25 Jean 3.36 Hébreux 10.26-10.29 Marc 16.16 Jean 3.18
25 Basi wakamwambia, U nani wewe? Yesu akawaambia, Hasa neno lilo hilo ninalowaambia.
Jean 1.19 Jean 19.9 Jean 8.12 Jean 10.24 Jean 5.17-5.29
26 Ninayo mengi ya kusema na kuhukumu juu yenu; lakini yeye aliyenipeleka ni kweli, nami niliyoyasikia kwake, ndiyo ninenayo katika ulimwengu.
Jean 15.15 Jean 7.28 Jean 8.40 Jean 5.42-5.43 Jean 9.39-9.41
27 Wala hawakutambua ya kuwa anawatajia Baba.
Esaïe 6.9 Romains 11.7-11.10 2 Corinthiens 4.3-4.4 Esaïe 42.18-42.20 Jean 8.43
28 Basi Yesu akawaambia, Mtakapokuwa mmekwisha kumwinua Mwana wa Adamu, ndipo mtakapofahamu ya kuwa mimi ndiye; na ya kuwa sifanyi neno kwa nafsi yangu, ila kama Baba alivyonifundisha ndivyo ninenavyo.
Jean 5.30 Jean 5.19 Jean 3.14 Romains 1.4 Jean 6.38
29 Naye aliyenipeleka yu pamoja nami, hakuniacha peke yangu; kwa sababu nafanya sikuzote yale yampendezayo.
Jean 6.38 Jean 16.32 Jean 4.34 Jean 8.16 Esaïe 42.1
30 Naye alipokuwa akisema hayo, wengi walimwamini.
Jean 7.31 Jean 6.14 Jean 11.45 Jean 10.42 Jean 2.23
31 Basi Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini, Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli;
2 Jean 1.9 2 Timothée 3.14 Jean 15.4-15.9 Jean 6.55 Matthieu 24.13
32 tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli itawaweka huru.
Jean 8.36 Romains 8.2 Jacques 2.12 Jean 14.6 Jean 17.17
33 Wakamjibu, Sisi tu uzao wake Ibrahimu, wala hatujawa watumwa wa mtu wakati wo wote; nawe wasemaje, Mtawekwa huru?
Matthieu 3.9 Jean 8.39 Jean 8.37 Lévitique 25.42 Néhémie 9.36-9.37
34 Yesu akawajibu, Amin, amin, nawaambia, Kila atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi.
2 Pierre 2.19 Romains 6.16 Tite 3.3 Proverbes 5.22 Romains 6.6
35 Wala mtumwa hakai nyumbani sikuzote; mwana hukaa sikuzote.
Genèse 21.10 Hébreux 3.5-3.6 Romains 8.29-8.30 Matthieu 21.41-21.43 Galates 4.4-4.7
36 Basi Mwana akiwaweka huru, mtakuwa huru kweli kweli.
Galates 5.1 Romains 8.2 2 Corinthiens 3.17 Jean 8.31-8.32 Zacharie 9.11-9.12
37 Najua ya kuwa ninyi ni uzao wa Ibrahimu lakini mnatafuta kuniua kwa sababu neno langu halimo ndani yenu.
Jean 7.1 1 Corinthiens 2.14 Jean 7.25 Matthieu 13.15 Actes 13.26
38 Niliyoyaona kwa Baba ndiyo niyanenayo; nanyi vivyo hivyo mliyoyasikia kwa baba yenu ndiyo myatendayo.
Jean 5.19 Jean 8.44 Jean 8.41 Jean 14.10 Jean 14.24
39 Wakajibu, wakamwambia, Baba yetu ndiye Ibrahimu! Yesu akawaambia, Kama mngekuwa watoto wa Ibrahimu, mngezitenda kazi zake Ibrahimu.
Galates 3.7 Romains 9.7 Jean 8.37 Matthieu 3.9 Galates 3.29
40 Lakini sasa mnatafuta kuniua mimi, mtu ambaye nimewaambia iliyo kweli, niliyoisikia kwa Mungu. Ibrahimu hakufanya hivyo.
Jean 8.26 Apocalypse 12.12-12.13 Galates 4.29 Apocalypse 12.17 Apocalypse 12.4
41 Ninyi mnazitenda kazi za baba yenu. Ndipo walipomwambia, Sisi hatukuzaliwa kwa zinaa; sisi tunaye Baba mmoja, yaani, Mungu.
Esaïe 63.16 Esaïe 64.8 Jean 8.44 Jean 8.38 Deutéronome 32.6
42 Yesu akawaambia, Kama Mungu angekuwa baba yenu, mngenipenda mimi; kwa maana nalitoka kwa Mungu, nami nimekuja; wala sikuja kwa nafsi yangu, bali yeye ndiye aliyenituma.
Jean 17.8 Jean 12.49 Jean 14.10 Jean 17.25 Jean 3.17
43 Mbona hamyafahamu hayo niyasemayo? Ni kwa sababu ninyi hamwezi kulisikia neno langu.
Jérémie 6.10 Jean 7.17 Jean 5.43 Jean 6.60 Michée 4.12
44 Ninyi ni wa baba yenu, Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo.
Apocalypse 12.9 1 Jean 3.12 1 Jean 3.8-3.10 2 Corinthiens 11.3 Actes 13.10
45 Nami, kwa sababu nasema iliyo kweli, hamnisadiki.
2 Timothée 4.3-4.4 Jean 3.19-3.20 2 Thessaloniciens 2.10 Jean 18.37 Jean 7.7
46 Ni nani miongoni mwenu anishuhudiaye ya kuwa nina dhambi? Nami nikisema kweli, mbona ninyi hamnisadiki?
Hébreux 4.15 Marc 11.31 Jean 8.7 Matthieu 21.25 Jean 14.30
47 Yeye aliye wa Mungu huyasikia maneno ya Mungu; hivyo ninyi hamsikii kwa sababu ninyi si wa Mungu.
Jean 1.12-1.13 Jean 6.45-6.46 1 Jean 3.10 Jean 8.37 Jean 18.37
48 Wayahudi wakajibu, wakamwambia, Je! Sisi hatusemi vema ya kwamba wewe u Msamaria, nawe una pepo?
Jean 7.20 Jean 8.52 Jean 4.9 Matthieu 10.25 Jean 10.20
49 Yesu akajibu, Mimi sina pepo; lakini mimi namheshimu Baba yangu, na ninyi mwanivunjia heshima yangu.
Jean 14.13 Matthieu 3.15-3.17 Jean 13.31-13.32 Jean 17.4 Proverbes 26.4-26.5
50 Wala mimi siutafuti utukufu wangu; yuko mwenye kutafuta na kuhukumu.
Jean 5.41 Jean 8.54 Jean 12.47-12.48 Jean 5.20-5.23 Jean 5.45
51 Amin, amin, nawaambia, Mtu akilishika neno langu, hataona mauti milele.
Jean 5.24 Jean 11.25-11.26 Jean 3.15-3.16 Luc 2.26 Hébreux 11.5
52 Basi Wayahudi wakamwambia, Sasa tumeng’amua ya kuwa una pepo. Ibrahimu amekufa, na manabii wamekufa; nawe wasema, Mtu akilishika neno langu, hataonja mauti milele.
Hébreux 2.9 Jean 8.48 Zacharie 1.5-1.6 Jean 8.51 Hébreux 11.13
53 Wewe u mkuu kuliko baba yetu Ibrahimu, ambaye amekufa? Nao manabii wamekufa. Wajifanya u nani?
Jean 4.12 Jean 8.58 Jean 12.34 Jean 19.7 Jean 5.18
54 Yesu akajibu, Nikijitukuza mwenyewe, utukufu wangu si kitu; anitukuzaye ni Baba yangu, ambaye ninyi mwanena kuwa ni Mungu wenu.
Jean 8.50 Jean 17.1 Jean 7.39 2 Pierre 1.17 Actes 3.13
55 Wala ninyi hamkumjua; lakini mimi namjua. Nikisema ya kwamba simjui, nitakuwa mwongo kama ninyi; lakini namjua, na neno lake nalishika.
Jean 8.19 Jean 8.44 Jean 7.28-7.29 Jean 8.51 Matthieu 11.27
56 Ibrahimu, baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu; naye akaiona, akafurahi.
Hébreux 11.13 Jean 8.39 Matthieu 13.17 Luc 2.28-2.30 Galates 3.7-3.9
57 Basi Wayahudi wakamwambia, Wewe hujapata bado miaka hamsini, nawe umemwona Ibrahimu?
58 Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.
Exode 3.14 Jean 17.5 Jean 17.24 Colossiens 1.17 Esaïe 44.6
59 Basi wakaokota mawe ili wamtupie; lakini Yesu akajificha, akatoka hekaluni.
Jean 11.8 Lévitique 24.16 Jean 10.30-10.33 Jean 5.13 Genèse 19.11

Cette Bible est dans le domaine public.