Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Luc 10.34
Bible en Swahili de l’est


Mission des soixante dix disciples

1 Basi, baada ya hayo Bwana aliweka na wengine, sabini, akawatuma wawili wawili wamtangulie kwenda kila mji na kila mahali alipokusudia kwenda mwenyewe.
Luc 9.52 Marc 6.7-6.13 Matthieu 10.1-10.4 Luc 9.1-9.2 Nombres 11.16
2 Akawaambia, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache; basi mwombeni Bwana wa mavuno apeleke watenda kazi katika mavuno yake.
Matthieu 9.36-9.38 1 Timothée 4.10 1 Timothée 4.15-4.16 2 Thessaloniciens 3.1 1 Timothée 1.12-1.14
3 Enendeni, angalieni, nawatuma kama wana kondoo kati ya mbwa-mwitu.
Matthieu 10.16 Actes 20.29 Jean 15.20 Ezéchiel 2.3-2.6 Sophonie 3.3
4 Msichukue mfuko, wala mkoba, wala viatu; wala msimwamkie mtu njiani.
2 Rois 4.29 Luc 22.35 2 Rois 4.24 1 Samuel 21.8 Luc 10.4-10.12
5 Na nyumba yo yote mtakayoingia, semeni kwanza, Amani iwemo nyumbani humu;
1 Samuel 25.6 2 Corinthiens 5.18-5.20 Luc 19.9 Matthieu 10.12-10.13 Ephésiens 2.17
6 na akiwamo mwana wa amani, amani yenu itamkalia; la, hayumo, amani yenu itarudi kwenu.
2 Corinthiens 2.15-2.16 Psaumes 35.13 2 Thessaloniciens 3.16 Ephésiens 5.6 1 Samuel 25.17
7 Basi, kaeni katika nyumba iyo hiyo, mkila na kunywa vya kwao; maana, mtenda kazi amestahili kupewa ujira wake. Msihame-hame kutoka nyumba hii kwenda nyumba hii.
Actes 16.40 2 Timothée 2.6 Deutéronome 12.12 1 Timothée 5.17-5.18 3 Jean 1.5-1.8
8 Na mji wo wote mtakaouingia, wakiwakaribisha, vileni vyakula viwekwavyo mbele yenu;
1 Corinthiens 10.27 Luc 10.10 Luc 9.48 Jean 13.20 Matthieu 10.40
9 waponyeni wagonjwa waliomo, waambieni, Ufalme wa Mungu umewakaribia.
Matthieu 3.2 Actes 28.7-28.10 Luc 10.11 Jean 3.5 Marc 4.30
10 Na mji wo wote mtakaouingia, nao hawawakaribishi, tokeni humo, nanyi mkipita katika njia zake semeni,
Matthieu 10.14 Luc 9.5 Actes 18.6 Actes 13.51
11 Hata mavumbi ya mji wenu yaliyogandamana na miguu yetu tunayakung’uta juu yenu. Lakini jueni hili, ya kuwa Ufalme wa Mungu umekaribia.
Luc 10.9 Actes 13.51 Romains 10.8 Actes 13.26 Actes 13.46
12 Nawaambia ya kwamba siku ile itakuwa rahisi zaidi Sodoma kuistahimili adhabu yake kuliko mji huo.
Matthieu 10.15 Matthieu 11.24 Lamentations 4.6 Ezéchiel 16.48-16.50 Marc 6.11
13 Ole wako Korazini! Ole wako, Bethsaida! Kwa kuwa kama miujiza hiyo iliyofanyika kwenu ingalifanyika katika Tiro na Sidoni, wangalitubu tangu hapo, huku wakiketi katika nguo za kigunia na majivu.
Esaïe 23.1-23.18 Ezéchiel 26.1-28.26 Romains 11.8-11.11 Joël 3.4-3.8 Actes 28.25-28.28
14 Lakini, siku ya hukumu itakuwa rahisi Tiro na Sidoni kustahimili adhabu zake kuliko ninyi.
Jean 15.22-15.25 Luc 12.47-12.48 Romains 2.1 Jean 3.19 Romains 2.27
15 Nawe Kapernaumu, je! Utakuzwa hata mbinguni? Utashushwa hata kuzimu.
Esaïe 14.13-14.15 Matthieu 4.13 Matthieu 11.23 Matthieu 10.28 2 Pierre 2.4
16 Awasikilizaye ninyi anisikiliza mimi, naye awakataaye ninyi anikataa mimi; naye anikataaye mimi amkataa yeye aliyenituma.
Matthieu 10.40 1 Thessaloniciens 4.8 Jean 13.20 Jean 12.48 Luc 9.48
17 Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako.
Marc 16.17 Luc 10.1 Luc 9.1 Luc 10.9 Romains 16.20
18 Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme.
Esaïe 14.12 Apocalypse 9.1 Jean 16.11 Matthieu 4.10 Apocalypse 20.2
19 Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.
Marc 16.18 Psaumes 91.13 Romains 16.20 Actes 28.5 Luc 21.17-21.18
20 Lakini, msifurahi kwa vile pepo wanavyowatii; bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni.
Philippiens 4.3 Exode 32.32 Hébreux 12.23 Daniel 12.1 Apocalypse 21.27
21 Saa ile ile alishangilia kwa Roho Mtakatifu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya umewaficha wenye hekima na akili; umewafunulia watoto wachanga; Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo ilivyokupendeza.
2 Corinthiens 4.3 1 Corinthiens 2.6-2.8 Ephésiens 1.5 Matthieu 16.17 Ephésiens 1.11
22 Akasema, Nimekabidhiwa vyote na Baba yangu, wala hakuna amjuaye Mwana ila Baba; wala hakuna amjuaye Baba ila Mwana, na ye yote ambaye Mwana apenda kumfunulia.
Jean 10.15 Jean 1.18 Jean 6.44-6.46 Matthieu 11.27 Matthieu 28.18
23 Akawageukia wanafunzi wake, akasema nao kwa faragha, Heri macho yaonayo mnayoyaona ninyi.
Matthieu 13.16-13.17
24 Kwa kuwa nawaambia ya kwamba manabii wengi na wafalme walitamani kuyaona mnayoyaona ninyi wasiyaone; na kuyasikia mnayoyasikia ninyi wasiyasikie.
Hébreux 11.13 1 Pierre 1.10-1.12 Jean 8.56 Hébreux 11.39

Parabole du bon Samaritain

25 Na tazama, mwana-sheria mmoja alisimama amjaribu; akisema, Mwalimu, nifanye nini ili niurithi uzima wa milele?
Luc 18.18 Matthieu 22.34-22.39 Luc 7.30 Luc 11.45-11.46 Matthieu 19.16-19.19
26 Akamwambia, Imeandikwa nini katika torati? Wasomaje?
Galates 3.21-3.22 Romains 4.14-4.16 Esaïe 8.20 Romains 10.5 Romains 3.19
27 Akajibu akasema, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako.
Matthieu 22.37-22.40 Marc 12.30-12.31 Deutéronome 6.5 Deutéronome 30.6 Romains 13.9
28 Akamwambia, Umejibu vema; fanya hivi nawe utaishi.
Lévitique 18.5 Ezéchiel 20.11 Matthieu 19.17 Néhémie 9.29 Galates 3.12
29 Naye akitaka kujidai haki, alimwuliza Yesu, Na jirani yangu ni nani?
Luc 16.15 Jacques 2.24 Lévitique 19.34 Galates 3.11 Luc 10.36
30 Yesu akajibu akasema, Mtu mmoja alishuka toka Yerusalemu kwenda Yeriko, akaangukia kati ya wanyang’anyi; wakamvua nguo, wakamtia jeraha, wakaenda zao, wakimwacha karibu ya kufa.
Luc 19.28 Luc 18.31 Lamentations 2.12 Psaumes 88.4 Ezéchiel 30.24
31 Kwa nasibu kuhani mmoja alishuka kwa njia ile; na alipomwona alipita kando.
Psaumes 142.4 Jérémie 5.31 Osée 6.9 Psaumes 69.20 1 Jean 3.16-3.18
32 Na Mlawi vivyo hivyo, alipofika pale akamwona, akapita kando.
Actes 18.17 Psaumes 109.25 Proverbes 27.10 2 Timothée 3.2
33 Lakini, Msamaria mmoja katika kusafiri kwake alifika hapo alipo; na alipomwona alimhurumia,
Proverbes 27.10 Matthieu 10.5 1 Rois 8.50 Exode 2.6 Luc 9.52-9.53
34 akakaribia, akamfunga jeraha zake, akizitia mafuta na divai; akampandisha juu ya mnyama wake, akampeleka mpaka nyumba ya wageni, akamtunza.
Proverbes 24.17-24.18 Genèse 42.27 Psaumes 147.3 Romains 12.20 Exode 23.4-23.5
35 Hata siku ya pili akatoa dinari mbili, akampa mwenye nyumba ya wageni, akisema, Mtunze huyu, na cho chote utakachogharimiwa zaidi, mimi nitakaporudi nitakulipa.
Luc 14.13 Proverbes 19.17 Matthieu 20.2 Romains 16.23
36 Waonaje wewe, katika hao watatu, ni yupi aliyekuwa jirani yake yule aliyeangukia kati ya wanyang’anyi?
Matthieu 22.42 Matthieu 17.25 Matthieu 21.28-21.31 Luc 7.42
37 Akasema, Ni huyo aliyemwonea huruma. Yesu akamwambia, Enenda zako, nawe ukafanye vivyo hivyo.
1 Jean 3.16-3.18 Matthieu 23.23 Jean 13.15-13.17 1 Pierre 2.21 2 Corinthiens 8.9

Marthe et Marie

38 Ikawa katika kuenenda kwao aliingia katika kijiji kimoja; mwanamke mmoja jina lake Martha akamkaribisha nyumbani kwake.
Actes 16.15 Jean 11.19-11.20 Jean 11.1-11.5 Jean 12.1-12.3 Luc 8.2-8.3
39 Naye alikuwa na umbu lake aitwaye Mariamu, aliyeketi miguuni pake Yesu, akasikiliza maneno yake.
Luc 8.35 Proverbes 8.34 Actes 22.3 Jean 12.3 Deutéronome 33.3
40 Lakini Martha alikuwa akihangaika kwa utumishi mwingi; akamwendea, akasema, Bwana, huoni vibaya hivyo ndugu yangu alivyoniacha nitumike peke yangu? Basi mwambie anisaidie.
Jean 6.27 Luc 12.29 Jonas 4.1-4.4 Matthieu 14.15 Matthieu 16.22
41 Bwana akajibu akamwambia, Martha, Martha, unasumbuka na kufadhaika kwa ajili ya vitu vingi;
Matthieu 6.25-6.34 Philippiens 4.6 Marc 4.19 Luc 21.34 Luc 12.22
42 lakini kinatakiwa kitu kimoja tu; na Mariamu amelichagua fungu lililo jema, ambalo hataondolewa.
Psaumes 27.4 Jean 5.24 Jean 10.27-10.28 Psaumes 16.5-16.6 Luc 18.22

Cette Bible est dans le domaine public.