Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Marc 6.17
Bible en Swahili de l’est


Jésus rejeté à Nazareth

1 Akatoka huko, akafika mpaka nchi ya kwao; wanafunzi wake wakamfuata.
Matthieu 13.54-13.58 Luc 4.16-4.30 Matthieu 13.4 Matthieu 2.23
2 Na ilipokuwa sabato, alianza kufundisha katika sinagogi; wengi waliposikia wakashangaa, wakisema, Huyu ameyapata wapi haya? Na, Ni hekima gani hii aliyopewa huyu? Na, Ni nini miujiza hii mikubwa inayotendeka kwa mikono yake?
Matthieu 4.23 Matthieu 7.28 Luc 4.31-4.32 Jean 6.42 Jean 7.15
3 Huyu si yule seremala, mwana wa Mariamu, na ndugu yao Yakobo, na Yose, na Yuda, na Simoni? Na maumbu yake hawapo hapa petu? Wakajikwaa kwake.
Matthieu 12.46 Matthieu 11.6 Jean 6.42 Marc 15.40 Galates 1.19
4 Yesu akawaambia, Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika nchi yake mwenyewe, na kwa jamaa zake, na nyumbani mwake.
Jean 4.44 Luc 4.24 Jérémie 12.6 Jérémie 11.21 Matthieu 13.57
5 Wala hakuweza kufanya mwujiza wo wote huko, isipokuwa aliweka mikono yake juu ya wagonjwa wachache, akawaponya.
Marc 5.23 Marc 9.23 Matthieu 13.58 Genèse 19.22 Esaïe 59.1-59.2
6 Akastaajabu kwa sababu ya kutokuamini kwao. Akazunguka-zunguka katika vile vijiji, akifundisha.
Luc 13.22 Matthieu 9.35 Matthieu 8.10 Matthieu 4.23 Luc 4.31

Mission des douze apôtres

7 Akawaita wale Thenashara, akaanza kuwatuma wawili wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu;
Marc 3.13-3.14 Luc 10.17-10.20 Luc 10.3-10.12 Matthieu 10.1-10.5 Exode 4.14-4.15
8 akawakataza wasichukue kitu cha njiani isipokuwa fimbo tu; wala mkate, wala mkoba, wala pesa za bindoni;
Luc 22.35 Matthieu 10.9-10.10 Luc 10.4 Luc 9.3
9 lakini wajifungie viatu; akasema, Msivae kanzu mbili.
Actes 12.8 Ephésiens 6.15
10 Akawaambia, Mahali po pote mtakapoingia katika nyumba, kaeni humo hata mtakapotoka mahali pale.
Actes 16.15 Luc 10.7-10.8 Matthieu 10.11-10.13 Actes 17.5-17.7 Luc 9.4
11 Na mahali po pote wasipowakaribisha ninyi wala kuwasikia, mtokapo huko, yakung’uteni mavumbi yaliyo chini ya miguu yenu, kuwa ushuhuda kwao.
Néhémie 5.13 Actes 18.6 Actes 13.50-13.51 Luc 9.5 Luc 10.10-10.15
12 Wakatoka, wakahubiri kwamba watu watubu.
Matthieu 4.17 Matthieu 3.2 Actes 20.21 Luc 24.47 Luc 13.3
13 Wakatoa pepo wengi, wakapaka mafuta watu wengi waliokuwa wagonjwa, wakawapoza.
Jacques 5.14-5.15 Luc 10.17 Marc 6.7

Exécution de Jean-Baptiste

14 Naye Mfalme Herode akasikia habari; kwa maana jina lake lilikuwa kutangaa, akasema, Yohana Mbatizaji amefufuka katika wafu, na kwa hiyo nguvu hizi zinatenda kazi ndani yake.
Luc 9.7-9.9 Marc 6.14-6.29 Matthieu 14.1-14.12 Luc 23.7-23.12 1 Thessaloniciens 1.8
15 Wengine walisema, Ni Eliya. Wengine walisema, Huyu ni nabii, au ni kama mmoja wa manabii.
Matthieu 21.11 Marc 8.28 Matthieu 16.14 Malachie 4.5 Luc 9.8
16 Lakini Herode aliposikia, alisema, Yohana, niliyemkata kichwa, amefufuka.
Genèse 40.10-40.11 Apocalypse 11.10-11.13 Psaumes 53.5 Matthieu 14.2 Luc 9.9
17 Kwa maana Herode mwenyewe alikuwa ametuma watu, akamkamata Yohana, akamfunga gerezani, kwa ajili ya Herodia, mkewe Filipo ndugu yake, kwa kuwa amemwoa;
Luc 3.19-3.20 Matthieu 11.2 Matthieu 4.12 Matthieu 14.3-14.12 Luc 3.1
18 kwa sababu Yohana alimwambia Herode, Si halali kwako kuwa na mke wa nduguyo.
Lévitique 20.21 Lévitique 18.16 Matthieu 14.3-14.4 Ezéchiel 3.18-3.19 1 Rois 22.14
19 Naye yule Herodia akawa akimvizia, akataka kumwua, asipate.
Ecclésiaste 7.9 Genèse 39.17-39.20 1 Rois 21.20 Ephésiens 4.26-4.27
20 Maana Herode alimwogopa Yohana; akimjua kuwa ni mtu wa haki, mtakatifu, akamlinda; na alipokwisha kumsikiliza alifadhaika sana; naye alikuwa akimsikiliza kwa furaha.
Matthieu 21.26 Matthieu 14.5 Marc 4.16 1 Rois 21.20 Daniel 4.18
21 Hata ilipotokea siku ya kufaa, na Herode, sikukuu ya kuzaliwa kwake, alipowafanyia karamu wakubwa wake, na majemadari, na watu wenye cheo wa Galilaya;
Esther 2.18 Genèse 40.20 Esther 1.3-1.7 Osée 7.5 Daniel 5.1-5.4
22 ndipo binti yake yule Herodia alipoingia, akacheza, akampendeza Herode na wale walioketi pamoja naye karamuni. Mfalme akamwambia yule kijana, Niombe lo lote utakalo, nitakupa.
Esther 1.10-1.12 Matthieu 14.6 Esaïe 3.16-3.26 Daniel 5.2
23 Akamwapia, Lo lote utakaloniomba nitakupa, hata nusu ya ufalme wangu.
Esther 7.2 Esther 5.3 Esther 5.6 Matthieu 5.34-5.37 Proverbes 6.2
24 Basi akatoka, akamwuliza mamaye, Niombe nini? Naye akasema, Kichwa cha Yohana Mbatizaji.
Ezéchiel 19.2-19.3 Psaumes 37.12 Job 31.31 Psaumes 37.14 Matthieu 14.8
25 Mara akaingia kwa haraka mbele ya mfalme, akaomba akisema, Nataka unipe sasa hivi katika kombe kichwa cha Yohana Mbatizaji.
Nombres 7.19-7.89 Romains 3.15 Nombres 7.13 Proverbes 1.16
26 Mfalme akafanya huzuni sana, lakini kwa ajili ya viapo vyake, na kwa ajili ya hao walioketi karamuni, hakutaka kumkatalia.
Matthieu 14.9 Matthieu 27.24-27.25 Matthieu 27.3-27.5
27 Mara mfalme akatuma askari, akaamuru kuleta kichwa chake. Basi akaenda, akamkata kichwa mle gerezani,
Matthieu 14.10-14.11
28 akakileta kichwa chake katika kombe, akampa yule kijana, naye yule kijana akampa mamaye.
29 Wanafunzi wake waliposikia habari, walikwenda, wakauchukua mwili wake, wakauzika kaburini.
Actes 8.2 2 Chroniques 24.16 Matthieu 27.57-27.60 1 Rois 13.29-13.30 Matthieu 14.12

Multiplication des pains pour cinq mille hommes

30 Na mitume wakakusanyika mbele ya Yesu; wakampa habari za mambo yote waliyoyafanya, na mambo yote waliyoyafundisha.
Luc 9.10 Marc 6.7-6.13 Luc 17.5 Luc 24.10 Luc 22.14
31 Akawaambia, Njoni ninyi peke yenu kwa faragha, mahali pasipokuwa na watu, mkapumzike kidogo. Kwa sababu walikuwako watu wengi, wakija, wakienda, hata haikuwapo nafasi ya kula.
Marc 3.20 Marc 1.45 Marc 3.7 Jean 6.1 Matthieu 14.13
32 Wakaenda zao faragha mashuani, mahali pasipokuwa na watu.
Matthieu 14.13-14.21 Jean 6.5-6.13 Marc 6.45 Marc 8.2-8.9 Marc 3.9
33 Watu wakawaona wakienda zao, na wengi wakatambua, wakaenda huko mbio kwa miguu, toka miji yote, wakatangulia kufika.
Matthieu 15.29-15.31 Marc 6.54-6.55 Jacques 1.19 Jean 6.2
34 Naye aliposhuka mashuani, akaona mkutano mkuu, akawahurumia; kwa sababu walikuwa kama kondoo wasio na mchungaji; akaanza kuwafundisha mambo mengi.
Matthieu 9.36 Nombres 27.17 Zacharie 10.2 2 Chroniques 18.16 1 Rois 22.17
35 Hata zilipopita saa nyingi za mchana, wanafunzi wake walimwendea, wakasema, Mahali hapa ni nyika tupu, na sasa kunakuchwa;
Matthieu 14.15-14.21 Luc 9.12-9.17 Jean 6.5-6.15
36 uwaage watu hawa, ili waende zao mashambani na vijijini kandokando, wakajinunulie chakula.
Matthieu 15.23 Marc 5.31 Matthieu 16.22 Marc 3.21
37 Akajibu, akawaambia, Wapeni ninyi chakula. Wakamwambia, Je! Twende tukanunue mikate ya dinari mia mbili ili tuwape kula?
2 Rois 4.42-4.44 Nombres 11.13 Matthieu 14.16 Jean 6.4-6.10 Marc 8.2-8.3
38 Akawaambia, Mnayo mikate mingapi? Nendeni mkatazame. Walipokwisha kujua wakasema, Mitano, na samaki wawili.
Marc 8.5 Matthieu 15.34 Jean 6.9 Luc 9.13 Matthieu 14.17-14.18
39 Akawaagiza wawaketishe wote, vikao vikao, penye majani mabichi.
1 Corinthiens 14.40 Matthieu 15.35 1 Corinthiens 14.33 1 Rois 10.5 Esther 1.5-1.6
40 Wakaketi safu safu, hapa mia hapa hamsini.
Luc 9.14-9.15
41 Akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama mbinguni, akashukuru, akaimega ile mikate, akawapa wanafunzi wake wawaandikie; na wale samaki wawili akawagawia wote.
Matthieu 14.19 Marc 7.34 1 Samuel 9.13 Luc 24.30 Jean 17.1
42 Wakala wote wakashiba.
Marc 8.8-8.9 Jean 6.12 Psaumes 145.15-145.16 2 Rois 4.42-4.44 Matthieu 14.20-14.21
43 Wakaokota vipande vilivyomegwa vya kuweza kujaza vikapu kumi na viwili; na vipande vya samaki pia.
Marc 8.19-8.20
44 Na walioila ile mikate wapata elfu tano wanaume.
45 Mara akawalazimisha wanafunzi wake wapande mashuani, watangulie kwenda ng’ambo hata Bethsaida, wakati yeye alipokuwa akiwaaga mkutano.
Jean 6.15-6.21 Marc 8.22 Matthieu 14.22-14.33 Marc 6.32 Matthieu 11.21
46 Hata alipokwisha kuagana nao akaenda zake mlimani kuomba.
Matthieu 6.6 Marc 1.35 Luc 6.12 Matthieu 14.23 1 Pierre 2.21
47 Na kulipokuwa jioni mashua ilikuwa katikati ya bahari, na yeye yu peke yake katika nchi kavu.
Jean 6.16-6.17 Matthieu 14.23
48 Akawaona wakitaabika kwa kuvuta makasia, kwa maana upepo ulikuwa wa mbisho; hata ilipopata kama zamu ya nne ya usiku akawaendea, akitembea juu ya bahari; akataka kuwapita.
Luc 12.38 Luc 24.28 Esaïe 54.11 Genèse 32.26 Jean 1.13
49 Nao walipomwona anatembea juu ya bahari, walidhani ya kuwa ni kivuli, wakapiga yowe,
Luc 24.37 Matthieu 14.25-14.26 Job 9.8 Job 4.14-4.16
50 kwa kuwa wote walimwona, wakafadhaika. Mara akasema nao, akawaambia, Changamkeni; ni mimi, msiogope.
Matthieu 14.27 Esaïe 43.2 Jean 6.19-6.20 Luc 24.38-24.41 Jean 20.19-20.20
51 Akapanda mle chomboni walimo; upepo ukakoma; wakashangaa sana mioyoni mwao;
Marc 4.39 Marc 4.41 Marc 5.42 Psaumes 107.28-107.30 Marc 2.12
52 kwa maana hawakufahamu habari za ile mikate, lakini mioyo yao ilikuwa mizito.
Marc 8.17-8.21 Marc 3.5 Matthieu 16.9-16.11 Romains 11.7 Marc 16.14
53 Hata walipokwisha kuvuka, walifika nchi ya Genesareti, wakatia nanga.
Jean 6.24-6.25 Matthieu 14.34-14.36 Luc 5.1
54 Nao wakiisha kutoka mashuani, mara watu walimtambua,
Philippiens 3.10 Psaumes 9.10
55 wakaenda mbio, wakizunguka nchi ile yote, wakaanza kuwachukua vitandani walio hawawezi, kwenda kila mahali waliposikia kwamba yupo.
Matthieu 4.24 Marc 2.1-2.3 Marc 3.7-3.11
56 Na kila alikokwenda, akiingia vijijini, au mijini, au mashambani, wakawaweka wagonjwa sokoni, wakamsihi waguse ngaa pindo la vazi lake; nao wote waliomgusa wakapona.
Matthieu 9.20 Nombres 15.38-15.39 Marc 3.10 Luc 6.19 Actes 5.15

Cette Bible est dans le domaine public.