Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Proverbes 7.2
Bible en Swahili de l’est


La femme débauchée

1 Mwanangu, yashike maneno yangu, Na kuziweka amri zangu akiba kwako.
Proverbes 1.8 Jean 14.23 Apocalypse 22.9 Apocalypse 1.3 Jean 15.20
2 Uzishike amri zangu ukaishi, Na sheria yangu kama mboni ya jicho lako.
Psaumes 17.8 Lévitique 18.5 Deutéronome 32.10 1 Jean 2.3-2.4 Proverbes 4.4
3 Zifunge katika vidole vyako; Ziandike juu ya kibao cha moyo wako.
Deutéronome 11.18-11.20 Esaïe 30.8 Proverbes 3.3 Deutéronome 6.8-6.9 Jérémie 31.33
4 Mwambie hekima, Wewe ndiwe umbu langu; Mwite ufahamu jamaa yako mwanamke.
Proverbes 4.6-4.8 Matthieu 12.49-12.50 Cantique 8.1 Proverbes 2.2-2.4 Job 17.14
5 Wapate kukulinda na malaya, Na mgeni akubembelezaye kwa maneno yake.
Proverbes 2.16 Proverbes 6.24 Proverbes 5.3
6 Maana katika dirisha la nyumba yangu Nalichungulia katika shubaka yake;
Juges 5.28 Genèse 26.8 2 Samuel 6.16
7 Nikaona katikati ya wajinga, Nikamtambua miongoni mwa vijana, Kijana mmoja asiyekuwa na akili,
Proverbes 6.32 Proverbes 1.22 Romains 16.18-16.19 Matthieu 15.16 Proverbes 9.4
8 Akipita njiani karibu na pembe yake, Akiishika njia iendayo nyumbani kwake,
Proverbes 5.8 Proverbes 7.12 2 Timothée 2.22 1 Corinthiens 6.18 Jude 1.23
9 Wakati wa magharibi, wakati wa jioni, Usiku wa manane, gizani.
Job 24.13-24.15 Romains 13.12-13.14 Exode 12.6 Genèse 39.11 Ephésiens 5.11
10 Na tazama, mwanamke akamkuta, Ana mavazi ya kikahaba, mwerevu wa moyo;
Genèse 38.14-38.15 1 Timothée 2.9 Apocalypse 17.3-17.5 Esaïe 3.16-3.24 2 Corinthiens 11.2-11.3
11 Ana kelele, na ukaidi; Miguu yake haikai nyumbani mwake.
Proverbes 9.13 Tite 2.5 1 Timothée 5.13-5.14 Proverbes 25.24 Proverbes 27.14-27.15
12 Mara yu katika njia kuu, mara viwanjani, Naye huotea kwenye pembe za kila njia.
Proverbes 23.28 Proverbes 9.14 Ezéchiel 16.31 Ezéchiel 16.24-16.25 Jérémie 2.36
13 Basi akamshika, akambusu, Akamwambia kwa uso usio na haya,
Genèse 39.12 Genèse 39.7 Apocalypse 2.20 Ezéchiel 3.7-3.9 Nombres 31.16
14 Kwangu ziko sadaka za amani; Leo hivi nimeziondoa nadhiri zangu;
Lévitique 7.11 Deutéronome 12.6-12.7 Lévitique 7.15-7.16 Proverbes 21.27 Proverbes 17.1
15 Ndiyo maana nikatoka nikulaki, Nikutafute uso wako kwa bidii, nami nimekuona.
16 Nimetandika kitanda changu, magodoro mazuri, Kwa matandiko ya Kimisri yenye mistari.
Esaïe 19.9 Ezéchiel 27.7 Cantique 1.16 Cantique 3.7-3.10 Proverbes 31.22
17 Nimetia kitanda changu manukato, Manemane na udi na mdalasini.
Psaumes 45.8 Cantique 4.13-4.14 Cantique 3.6 Exode 30.23 Esaïe 57.7-57.9
18 Haya, na tushibe upendo hata asubuhi, Tujifurahishe nafsi zetu kwa mahaba.
19 Maana mume wangu hayumo nyumbani, Amekwenda safari ya mbali;
Matthieu 20.11 Luc 12.45-12.46 Matthieu 24.43 Marc 13.34-13.36 Matthieu 24.48
20 Amechukua mfuko wa fedha mkononi; Atarudi wakati wa mwezi mpevu.
2 Chroniques 2.4
21 Kwa maneno yake mengi na ulaini akamshawishi, Kwa ubembelezi wa midomo yake akamshinda.
Proverbes 5.3 Psaumes 12.2 Proverbes 7.5 Luc 14.23 Actes 16.15
22 Huyo akafuatana naye mara hiyo, Kama vile ng’ombe aendavyo machinjoni; Au mpumbavu kuadhibiwa katika pingu;
Job 13.27 Actes 14.13 Jérémie 20.2 Actes 16.24
23 Hata mshale umchome maini; Kama ndege aendaye haraka mtegoni; Wala hajui ya kuwa ni hasara ya nafsi yake.
Ecclésiaste 9.12 Nombres 25.8-25.9 Proverbes 1.17 Proverbes 9.18
24 Basi, wanangu, nisikilizeni sasa, Mkayaangalie maneno ya kinywa changu.
Proverbes 5.7 Proverbes 4.1 Proverbes 8.32-8.33 1 Corinthiens 4.14-4.15 Galates 4.19
25 Moyo wako usizielekee njia zake, Wala usipotee katika mapito yake.
Proverbes 5.8 Matthieu 5.28 Proverbes 6.25 Proverbes 4.14-4.15 Esaïe 53.6
26 Maana amewaangusha wengi waliojeruhi, Naam, jumla ya waliouawa naye ni jeshi kubwa.
Néhémie 13.26 1 Pierre 2.11 Juges 16.21 2 Corinthiens 12.21 2 Samuel 12.9-12.11
27 Nyumba yake ni njia ya kwenda kuzimu, Hushuka mpaka vyumba vya mauti.
Proverbes 5.5 Proverbes 9.18 Proverbes 2.18-2.19 Apocalypse 22.15 Ecclésiaste 7.26

Cette Bible est dans le domaine public.