Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Samuel 17.46
Bible en Swahili de l’est


Victoire de David contre Goliath

1 Wakati huo Wafilisti walikusanya majeshi yao kwa vita, nao wakakusanyika huko Soko, ulio mji wa Yuda, wakatua kati ya Soko na Azeka, katika Efes-damimu.
Josué 15.35 1 Samuel 13.5 2 Chroniques 28.18 1 Chroniques 11.13 Josué 10.10-10.11
2 Naye Sauli na watu wa Israeli wakakusanyika, wakatua katika bonde la Ela, nao wakapanga vita juu ya hao Wafilisti.
1 Samuel 21.9 1 Samuel 17.19
3 Wafilisti wakasimama juu ya mlima upande huu, na Waisraeli wakasimama juu ya mlima upande huu, napo palikuwa na hilo bonde katikati.
4 Ndipo akatoka shujaa katika kambi ya Wafilisti, aliyeitwa Goliathi, wa Gathi, ambaye urefu wake ulikuwa mikono sita na shibiri moja.
Josué 11.22 1 Samuel 21.9-21.10 1 Samuel 27.4 1 Chroniques 11.23 2 Samuel 21.16-21.22
5 Alikuwa na chapeo ya shaba kichwani, tena amevaa darii ya shaba; na uzani wake ile darii ya shaba ulikuwa shekeli elfu tano za shaba.
6 Tena amevaa mabamba ya shaba miguuni mwake, naye alikuwa na mkuki wa shaba kati ya mabega; yake.
1 Samuel 17.45 1 Rois 10.16 2 Chroniques 9.15
7 Na mti wa fumo lake ulikuwa kama mti wa mfumaji; na kichwa cha mkuki wake kilikuwa shekeli mia sita za chuma uzito wake; na mtu aliyemchukulia ngao yake akamtangulia.
2 Samuel 21.19 1 Chroniques 11.23 1 Samuel 17.41 1 Chroniques 20.5
8 Naye akasimama, akawapigia kelele majeshi ya Israeli akawaambia, Mbona mmetoka kupanga vita? Je! Mimi si Mfilisti, na ninyi si watumishi wa Sauli? Jichagulieni mtu, akanishukie mimi.
1 Samuel 8.17 2 Samuel 11.11 1 Chroniques 21.3 1 Samuel 17.26
9 Kama akiweza kupigana nami na kuniua, sisi tutakuwa watumwa wenu; nami nikimshinda yeye na kumwua, ninyi mtakuwa watumwa wetu, na kututumikia.
1 Samuel 11.1
10 Yule Mfilisti akasema, Nayatukana leo majeshi ya Israeli; nipeni mtu tupigane.
2 Samuel 21.21 1 Samuel 17.45 1 Samuel 17.36 1 Samuel 17.25-17.26 Néhémie 2.19
11 Basi Sauli na Israeli wote waliposikia maneno hayo ya Mfilisti, wakafadhaika na kuogopa sana.
Josué 1.9 Deutéronome 31.8 Esaïe 57.11 Proverbes 28.1 Esaïe 51.12-51.13
12 Basi Daudi alikuwa mwana wa yule Mwefrathi, wa Bethlehemu ya Yuda, aliyeitwa jina lake Yese; naye huyo alikuwa na wana wanane; na yeye mwenyewe alikuwa mzee siku za Sauli, na mkongwe miongoni mwa watu.
1 Samuel 16.10-16.11 1 Samuel 16.18 Genèse 35.19 1 Samuel 17.58 1 Chroniques 2.13-2.16
13 Nao wale wana watatu wa Yese waliokuwa wakubwa walikuwa wamefuatana na Sauli kwenda vitani, na majina ya hao wanawe watatu waliokwenda vitani ni haya, mzaliwa wa kwanza Eliabu, na wa pili wake Abinadabu, na wa tatu Shama.
1 Chroniques 2.13 2 Samuel 13.3 2 Samuel 21.21 2 Samuel 13.32 1 Samuel 17.28
14 Naye huyo Daudi alikuwa mdogo wa wote; na hao watatu waliokuwa wakubwa wakafuatana na Sauli.
1 Samuel 16.11 Genèse 25.23
15 Basi Daudi alikuwa akienda kwa Sauli na kurudi ili awalishe kondoo za baba yake huko Bethlehemu.
1 Samuel 16.11 1 Samuel 16.19-16.23
16 Naye yule Mfilisti hukaribia asubuhi na jioni, akajitokeza siku arobaini.
Luc 4.2 Matthieu 4.2
17 Ndipo Yese akamwambia Daudi mwanawe, Haya! Sasa uwachukulie ndugu zako efa ya bisi, na mikate hii kumi, ipeleke upesi kambini kwa ndugu zako;
1 Samuel 25.18 Matthieu 7.11 Luc 11.13 2 Samuel 17.28 Ruth 2.14
18 ukampelekee akida wa elfu yao jibini hizi kumi, ukawaangalie, wa hali gani, kisha uniletee jawabu yao.
Genèse 37.14 1 Samuel 16.20 Actes 15.36 2 Samuel 17.29 Job 10.10
19 Basi Sauli, na watu wote wa Israeli, walikuwa katika bonde la Ela, wakipigana na Wafilisti.
20 Daudi akaondoka asubuhi na mapema, akawaacha kondoo pamoja na mchungaji, akavitwaa vitu vile, akaenda, kama Yese alivyomwamuru; akafika penye magari, wakati lile jeshi walipokuwa wakitoka kwenda kupigana, wakipiga kelele za vita.
1 Samuel 26.5 Luc 19.43 1 Samuel 26.7 Ephésiens 6.1-6.2 1 Samuel 17.28
21 Nao Waisraeli na Wafilisti wakajipanga, jeshi hili likikabili jeshi hili.
22 Basi Daudi akaviacha vile vyombo vyake katika mkono wa mlinda vyombo, akalikimbilia jeshi, akafika, akawasalimu ndugu zake.
Matthieu 10.12-10.13 Luc 10.5-10.6 Esaïe 10.28 Juges 18.15 Genèse 37.14
23 Hata alipokuwa akisema nao, kumbe! Yule shujaa alitokea, yule Mfilisti wa Gathi, jina lake Goliathi, akitoka katika jeshi la Wafilisti, akasema maneno yale yale; naye Daudi akayasikia.
1 Samuel 17.8-17.10
24 Na watu wote wa Israeli walipomwona yule mtu wakakimbia, wakaogopa sana.
Lévitique 26.36 1 Samuel 17.11 Esaïe 7.2 Nombres 13.33 Deutéronome 32.30
25 Watu wa Israeli wakasema, Je! Mmemwona mtu huyu aliyepanda huko? Hakika ametokea ili awatukane Israeli; basi, itakuwa, mtu yule atakayemwua, mfalme atamtajirisha kwa utajiri mwingi, naye atamwoza binti yake, na kuifanya mbari ya baba yake kuwa huru katika Israeli.
Josué 15.16 Apocalypse 3.12 Apocalypse 3.21 Apocalypse 2.7 Matthieu 17.26
26 Daudi akaongea na watu waliosimama karibu, akisema, Je! Atafanyiwaje yeye atakayemwua Mfilisti huyo, na kuwaondolea Israeli aibu hii? Maana Mfilisti huyu asiyetahiriwa ni nani hata awatukane majeshi ya Mungu aliye hai?
Deutéronome 5.26 1 Samuel 11.2 1 Samuel 14.6 1 Samuel 17.10 1 Samuel 17.36
27 Nao watu wakamjibu vivyo hivyo, wakisema, Ndivyo atakavyofanyiwa mtu yule atakayemwua.
1 Samuel 17.25
28 Naye Eliabu, mkubwa wake, alisikia hapo alipoongea na watu; na hasira yake Eliabu ikawaka juu ya Daudi, akasema, Mbona wewe umeshuka hapa? Na kondoo wale wachache umemwachia nani kule nyikani? Mimi nakujua kiburi chako, na ubaya wa moyo wako; maana umeshuka ili upate kuvitazama vita.
Matthieu 10.36 Proverbes 18.19 Genèse 37.8 Genèse 37.4 Genèse 37.11
29 Naye Daudi akamjibu, Je! Mimi nimekosa nini sasa? Je! Si neno kubwa hilo?
Proverbes 15.1 Actes 11.2-11.4 1 Corinthiens 2.15 1 Pierre 3.9
30 Naye akamgeukia ili kumwelekea mtu mwingine, akasema naye jinsi ile ile; na watu wakamjibu tena jinsi ile ile kama ya kwanza.
1 Samuel 17.26-17.27
31 Na maneno hayo aliyosema Daudi yaliposikiwa, watu wakamweleza Sauli; naye akatuma mtu kwenda kumwita.
Proverbes 22.29
32 Daudi akamwambia Sauli, Asizimie moyo mtu ye yote kwa ajili ya huyu; mimi mtumishi wako nitakwenda kupigana na Mfilisti huyu.
1 Samuel 16.18 Deutéronome 20.1-20.3 Psaumes 3.6 Nombres 14.9 Psaumes 27.1-27.3
33 Sauli akamwambia Daudi, Huwezi wewe kumwendea Mfilisti huyu upigane naye; maana wewe u kijana tu; na huyu ni mtu wa vita tangu ujana wake.
Nombres 13.31 1 Samuel 17.42 Deutéronome 9.2 Apocalypse 13.4 1 Samuel 17.56
34 Daudi akamwambia Sauli, Mtumishi wako alikuwa akichunga kondoo za baba yake, na alipokuwa akija simba, au dubu, akamkamata mwana-kondoo wa lile kundi,
35 mimi hutoka nikamfuata, nikampiga, nikampokonya kinywani mwake; na akinirukia, humshika ndevu zake, nikampiga, nikamwua.
Amos 3.12 Daniel 6.22 Juges 14.5-14.6 2 Timothée 4.17-4.18 2 Samuel 23.20
36 Mtumishi wako alimwua simba na dubu pia; na huyu Mfilisti asiyetahiriwa atakuwa kama mmoja wao, kwa sababu amewatukana majeshi ya Mungu aliye hai.
1 Samuel 17.26 1 Samuel 17.10 Actes 5.38-5.39 Ezéchiel 32.27-32.32 Esaïe 36.18
37 Daudi akasema, Bwana aliyeniokoa na makucha ya simba, na makucha ya dubu, ataniokoa na mkono wa Mfilisti huyu. Sauli akamwambia Daudi, Enenda, na Bwana atakuwa pamoja nawe.
1 Chroniques 22.11 1 Chroniques 22.16 1 Samuel 20.13 2 Timothée 4.17-4.18 Psaumes 138.7-138.8
38 Ndipo Sauli akamvika Daudi mavazi yake ya vita, akamtia chapeo cha shaba kichwani, akamvika dirii.
39 Naye Daudi akajifunga upanga juu ya mavazi yake, akajaribu kwenda; maana alikuwa hajavijaribu. Daudi akamwambia Sauli, Siwezi kwenda na vitu hivi, maana sikuvijaribu. Basi Daudi akavivua.
Zacharie 4.6 2 Corinthiens 10.4-10.5 Osée 1.7
40 Akaichukua fimbo yake mkononi, akajichagulia mawe laini matano katika kijito cha maji, akayatia katika mfuko wa kichungaji aliokuwa nao, maana ni mkoba wake, na kombeo lake alikuwa nalo mkononi mwake, akamkaribia yule Mfilisti.
Juges 20.16 Matthieu 10.10 Juges 7.16-7.20 1 Corinthiens 1.27-1.29 Juges 15.15-15.16
41 Huyo Mfilisti naye akamsogelea Daudi na kumkaribia; na mtu yule aliyemchukulia ngao yake akamtangulia.
42 Hata Mfilisti alipotazama huku na huku, akamwona Daudi akamdharau; kwa kuwa ni kijana tu mwekundu, tena ana sura nzuri.
1 Samuel 16.12 1 Samuel 17.33 Psaumes 123.3-123.4 1 Rois 20.18 Proverbes 16.18
43 Mfilisti akamwambia Daudi, Je! Mimi ni mbwa hata umenijia kwa fimbo? Mfilisti akamlaani Daudi kwa miungu yake.
1 Samuel 24.14 2 Samuel 3.8 2 Rois 8.13 2 Samuel 9.8 2 Samuel 16.9
44 Mfilisti akamwambia Daudi, Njoo huku kwangu; nyama yako nitawapa ndege wa angani na wanyama wa mwituni.
Ezéchiel 28.9-28.10 1 Rois 20.10-20.11 Ecclésiaste 9.11-9.12 Ezéchiel 28.2 Proverbes 18.12
45 Ndipo Daudi akamwambia yule Mfilisti, Wewe unanijia mimi na upanga, na fumo, na mkuki, bali mimi ninakujia wewe kwa jina la Bwana wa majeshi, Mungu wa majeshi ya Israeli uliowatukana.
2 Chroniques 32.8 1 Samuel 17.36 1 Samuel 17.10 2 Samuel 22.33-22.35 Philippiens 4.13
46 Siku hii ya leo Bwana atakuua mkononi mwangu, nami nitakupiga, na kukuondolea kichwa chako, nami leo nitawapa ndege wa angani na wanyama wa nchi mizoga ya majeshi ya Wafilisti, ili kwamba dunia nzima wajue ya kuwa yuko Mungu katika Israeli.
1 Rois 8.43 Esaïe 52.10 Josué 4.24 2 Rois 19.19 Deutéronome 28.26
47 Nao jamii ya watu wote pia wajue ya kwamba Bwana haokoi kwa upanga wala kwa mkuki; maana vita ni vya Bwana, naye atawatia ninyi mikononi mwetu.
Zacharie 4.6 Osée 1.7 1 Samuel 14.6 Psaumes 44.6-44.7 2 Chroniques 20.15-20.17
48 Ikawa, hapo Mfilisti alipojiinua, akaenda akamkaribia Daudi, ndipo Daudi naye akapiga mbio, akalikimbilia jeshi ili akutane na yule Mfilisti.
Proverbes 28.1 Psaumes 27.1
49 Daudi akatia mkono wake mfukoni, akatwaa humo jiwe moja, akalitupa kwa kombeo lake, akampiga Mfilisti katika kipaji cha uso; jiwe hilo likamwingilia kipajini, akaanguka chini kifudifudi.
1 Corinthiens 1.27-1.28 2 Rois 9.24 1 Rois 22.34
50 Hivyo Daudi akamshinda yule Mfilisti kwa kombeo na jiwe, akampiga Mfilisti, akamwua; walakini Daudi hakuwa na upanga mkononi mwake.
Juges 3.31 1 Samuel 23.21 Juges 15.15 1 Samuel 21.9 1 Samuel 13.22
51 Ndipo Daudi akapiga mbio, akasimama juu ya Mfilisti, akautwaa upanga wake, akaufuta alani mwake, akamwua, akamkata kichwa kwa upanga huo. Nao Wafilisti walipoona ya kuwa shujaa wao amekufa, wakakimbia.
1 Samuel 21.9 Hébreux 11.34 2 Samuel 23.21 Esther 7.10 Hébreux 2.14
52 Nao watu wa Israeli na wa Yuda wakainuka, na kupiga kelele, nao wakawafuata Wafilisti mpaka ufikapo Gathi, na mpaka malango ya Ekroni. Nao majeruhi wa Wafilisti wakaanguka kando ya njia iendayo Shaarimu, mpaka Gathi, na mpaka Ekroni.
Josué 15.11 Josué 15.45-15.46 2 Samuel 23.10 1 Samuel 14.21-14.22 Juges 7.23
53 Kisha wana wa Israeli wakarudi kutoka katika kuwafukuza Wafilisti, wakateka nyara marago yao.
Jérémie 4.20 Jérémie 30.16 2 Rois 7.7-7.16
54 Naye Daudi akakitwaa kichwa chake yule Mfilisti na kukileta Yerusalemu; lakini silaha zake akaziweka hemani mwake.
Exode 16.33 Josué 4.7-4.8 1 Samuel 21.9
55 Basi Sauli, hapo alipomwona Daudi akitoka ili kumwendea yule Mfilisti, alimwambia Abneri, jemadari wa jeshi, Je! Abneri, kijana huyu ni mwana wa nani? Abneri akamjibu, Ee mfalme, kama iishivyo roho yako, mimi siwezi kusema.
1 Samuel 16.21-16.22 1 Samuel 17.58
56 Basi mfalme akasema, Uliza wewe, kijana huyu ni mwana wa nani.
57 Hata na Daudi alipokuwa yuarudi kutoka katika kumwua yule Mfilisti, Abneri alimtwaa, akamleta mbele ya Sauli, naye anacho kichwa chake yule Mfilisti mkononi mwake.
1 Samuel 17.54
58 Basi Sauli akamwuliza, Wewe, kijana, u mwana wa nani? Naye Daudi akamjibu, Mimi ni mwana wa mtumishi wako, Yese, mtu wa Bethlehemu.
1 Samuel 17.12 1 Samuel 16.18-16.19

Cette Bible est dans le domaine public.