Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 18.30
Bible en Swahili de l’est


Louanges après la délivrance

1 Wewe, Bwana, nguvu zangu, nakupenda sana;
2 Samuel 22.1-22.51 Colossiens 1.11 1 Jean 4.19 Esaïe 12.1-12.6 Psaumes 34.19
2 Bwana ni jabali langu, na boma langu, na mwokozi wangu, Mungu wangu, mwamba wangu ninayemkimbilia, Ngao yangu, na pembe ya wokovu wangu, na ngome yangu.
Psaumes 144.2 Psaumes 28.1 Jérémie 16.19 Proverbes 18.10 2 Samuel 22.3
3 Nitamwita Bwana astahiliye kusifiwa, Hivyo nitaokoka na adui zangu.
2 Samuel 22.4 Romains 8.31-8.39 Psaumes 50.15 Luc 1.71 Psaumes 145.3
4 Kamba za mauti zilinizunguka, Mafuriko ya uovu yakanitia hofu.
Psaumes 116.3 Matthieu 27.24-27.25 2 Corinthiens 1.9 Marc 14.33-14.34 Jonas 2.2-2.7
5 Kamba za kuzimu zilinizunguka, Mitego ya mauti ikanikabili.
Psaumes 88.3-88.8 Psaumes 86.13 Psaumes 88.15-88.17 Ecclésiaste 9.12 Actes 2.24
6 Katika shida yangu nalimwita Bwana, Na kumlalamikia Mungu wangu. Akaisikia sauti yangu hekaluni mwake, Kilio changu kikaingia masikioni mwake.
Psaumes 50.15 Psaumes 34.15 2 Samuel 22.7 Psaumes 18.3-18.4 Psaumes 120.1
7 Ndipo nchi iliyotikisika na kutetemeka, Misingi ya milima ikasuka-suka; Ikatikisika kwa sababu alikuwa na ghadhabu.
Actes 4.31 Juges 5.4 Actes 16.25-16.26 Zacharie 14.4 Psaumes 68.7-68.8
8 Kukapanda moshi kutoka puani mwake, Moto ukatoka kinywani mwake ukala, Makaa yakawashwa nao.
Psaumes 21.9 Lévitique 10.2 Nombres 16.35 Apocalypse 11.5 Psaumes 74.1
9 Aliziinamisha mbingu akashuka, Kukawa na giza kuu chini ya miguu yake.
Deutéronome 33.26 Psaumes 144.5-144.15 2 Samuel 22.10 Jean 13.7 Apocalypse 20.11
10 Akapanda juu ya kerubi akaruka, Naam, aliruka upesi juu ya mabawa ya upepo.
Psaumes 104.3 Psaumes 99.1 2 Samuel 22.11-22.12 Ezéchiel 10.20-10.22 Psaumes 80.1
11 Alifanya giza kuwa mahali pake pa kujificha, Kuwa hema yake ya kumzunguka. Giza la maji na mawingu makuu ya mbinguni.
Psaumes 97.2 Deutéronome 4.11 Joël 2.2 Psaumes 91.1 Psaumes 81.7
12 Toka mwangaza uliokuwa mbele zake Kukapita mawingu yake makuu. Mvua ya mawe na makaa ya moto.
Josué 10.11 Matthieu 17.5 Exode 9.23-9.24 Psaumes 104.2 Habakuk 3.4-3.5
13 Bwana alipiga radi mbinguni, Yeye Aliye juu akaitoa sauti yake, Mvua ya mawe na makaa ya moto.
Psaumes 104.7 Psaumes 29.3-29.4 1 Samuel 7.10 Psaumes 78.48 Apocalypse 4.5
14 Akaipiga mishale yake akawatawanya, Naam, umeme mwingi sana, akawatapanya.
Psaumes 144.6 Habakuk 3.11 Deutéronome 32.23 Josué 10.10 Deutéronome 32.42
15 Ndipo ilipoonekana mikondo ya maji, Misingi ya ulimwengu ikafichuliwa, Ee Bwana, kwa kukemea kwako, Kwa mvumo wa pumzi ya puani mwako.
Psaumes 106.9 Exode 15.8 Psaumes 76.6 2 Rois 19.7 Esaïe 30.33
16 Alipeleka kutoka juu akanishika, Na kunitoa katika maji mengi.
Psaumes 144.7 2 Samuel 22.17 Exode 2.10 Jonas 2.5-2.6 Apocalypse 17.15
17 Akaniokoa na adui yangu mwenye nguvu, Na wale walionichukia, Maana walikuwa na nguvu kuliko mimi.
Psaumes 35.10 Hébreux 2.14-2.15 Psaumes 142.6 Psaumes 118.7 Ephésiens 6.10-6.12
18 Walinikabili siku ya msiba wangu, Lakini Bwana alikuwa tegemeo langu.
Deutéronome 32.35 Abdias 1.10-1.14 Psaumes 59.16 2 Samuel 22.19 Psaumes 46.11
19 Akanitoa akanipeleka panapo nafasi, Aliniponya kwa kuwa alipendezwa nami.
Psaumes 118.5 Psaumes 31.8 Psaumes 37.23 Psaumes 18.36 Job 36.16
20 Bwana alinitendea sawasawa na haki yangu, Sawasawa na usafi wa mikono yangu akanilipa.
Psaumes 24.4 Proverbes 11.18 Matthieu 6.4 1 Samuel 24.19-24.20 Job 22.30
21 Maana nimezishika njia za Bwana, Wala sikumwasi Mungu wangu.
Psaumes 119.102 Psaumes 17.4 1 Jean 2.19 1 Thessaloniciens 2.10 Psaumes 119.10-119.11
22 Hukumu zake zote zilikuwa mbele yangu, Wala amri zake sikujiepusha nazo.
Psaumes 119.30 Psaumes 119.128 Psaumes 119.112 Jean 5.14 Psaumes 119.117
23 Nami nalikuwa mkamilifu mbele zake, Nikajilinda na uovu wangu.
Psaumes 17.3 1 Chroniques 29.17 Psaumes 11.7 1 Samuel 26.23 Matthieu 5.29-5.30
24 Mradi Bwana amenilipa sawasawa na haki yangu, Sawasawa na usafi wa mikono yangu mbele zake.
Matthieu 10.41-10.42 Ruth 2.12 1 Samuel 26.23 2 Thessaloniciens 1.6-1.7 Hébreux 6.16
25 Kwa mtu mwenye fadhili utakuwa mwenye fadhili; Kwa mkamilifu utajionyesha kuwa mkamilifu;
Matthieu 5.7 Matthieu 18.33-18.35 Psaumes 41.1-41.4 Psaumes 62.12 1 Rois 8.32
26 Kwake ajitakasaye utajionyesha kuwa mtakatifu; Na kwa mpotovu utajionyesha kuwa mkaidi.
Proverbes 3.34 Lévitique 26.23-26.24 Lévitique 26.27-26.28 Romains 2.9 Psaumes 109.17-109.19
27 Maana Wewe utawaokoa watu wanaoonewa, Na macho ya kiburi utayadhili.
Psaumes 101.5 Jacques 2.5 Psaumes 34.19 Psaumes 10.4 Psaumes 9.18
28 Kwa kuwa Wewe unaiwasha taa yangu; Bwana Mungu wangu aniangazia giza langu.
Job 18.6 Psaumes 132.17 Job 29.3 1 Rois 11.36 1 Pierre 2.9
29 Maana kwa msaada wako nafuatia jeshi, Kwa msaada wa Mungu wangu naruka ukuta.
Ephésiens 6.10-6.13 2 Samuel 22.30 2 Corinthiens 12.9-12.10 1 Corinthiens 15.10 Psaumes 144.1
30 Mungu, njia yake ni kamilifu, Ahadi ya Bwana imehakikishwa, Yeye ndiye ngao yao. Wote wanaomkimbilia.
Psaumes 12.6 Deutéronome 32.4 Apocalypse 15.3 Psaumes 17.7 Proverbes 30.5
31 Maana ni nani aliye Mungu ila Bwana? Ni nani aliye mwamba ila Mungu wetu?
Psaumes 86.8 1 Samuel 2.2 Esaïe 45.5 Deutéronome 32.31 Deutéronome 32.39
32 Mungu ndiye anifungaye mshipi wa nguvu, Naye anaifanya kamilifu njia yangu.
Esaïe 45.5 2 Corinthiens 3.5 2 Samuel 22.33 Psaumes 91.2 Psaumes 28.7
33 Miguu yangu anaifanya kuwa ya kulungu, Na kunisimamisha mahali pangu pa juu.
Habakuk 3.19 Deutéronome 32.13 2 Samuel 2.18 2 Samuel 22.14 Deutéronome 33.29
34 Ananifundisha mikono yangu vita, Mikono yangu ikaupinda upinde wa shaba.
Psaumes 144.1 Jérémie 49.35 Psaumes 46.9 Esaïe 28.6 Esaïe 45.1
35 Nawe umenipa ngao ya wokovu wako, Mkono wako wa kuume umenitegemeza, Na unyenyekevu wako umenikuza.
2 Samuel 22.36 Deutéronome 33.29 2 Corinthiens 10.1 Psaumes 5.12 Jacques 3.17-3.18
36 Umezifanyizia nafasi hatua zangu, Na miguu yangu haikuteleza.
Proverbes 4.12 2 Samuel 22.37 Job 36.16 Luc 12.50 Luc 24.46-24.48
37 Nitawafuatia adui zangu na kuwapata, Wala sitarudi nyuma hata wakomeshwe.
Psaumes 35.5 Psaumes 3.7 Nombres 24.17-24.19 Apocalypse 6.2 Psaumes 118.11-118.12
38 Nitawapiga-piga wasiweze kusimama, Wataanguka chini ya miguu yangu.
2 Samuel 8.1-8.18 2 Samuel 18.7-18.8 2 Samuel 22.39 1 Samuel 23.5 Psaumes 47.3
39 Nawe hunifunga mshipi wa nguvu kwa vita, Hunitiishia chini yangu walioniondokea.
Psaumes 18.32 Psaumes 34.21 2 Samuel 22.40-22.41 1 Corinthiens 15.25-15.28 Proverbes 8.36
40 Naam, adui zangu umewafanya wanipe visogo, Nao walionichukia nimewakatilia mbali.
Psaumes 21.12 Psaumes 94.23
41 Walipiga yowe, lakini hakuna wa kuokoa, Walimwita Bwana lakini hakuwajibu,
Proverbes 1.28 Job 27.9 Esaïe 59.1-59.2 Jérémie 14.12 Psaumes 50.22
42 Nikawaponda kama mavumbi mbele ya upepo, Nikawatupa nje kama matope ya njiani.
2 Rois 13.7 Zacharie 10.5 Esaïe 10.6 Malachie 4.3 Esaïe 41.15-41.16
43 Umeniokoa na mashindano ya watu, Umenifanya niwe kichwa cha mataifa. Watu nisiowajua walinitumikia.
2 Samuel 3.1 Esaïe 55.5 Esaïe 52.15 Apocalypse 11.15 Romains 15.18
44 Kwa kusikia tu habari zangu, Mara wakanitii. Wageni walinijia wakinyenyekea.
Psaumes 81.15 Psaumes 66.3 Deutéronome 33.29 Romains 10.16-10.17 Psaumes 68.30
45 Wageni nao walitepetea, Walitoka katika ngome zao wakitetemeka.
Michée 7.17 Jacques 1.11 Esaïe 24.4 Apocalypse 6.16
46 Bwana ndiye aliye hai; Na ahimidiwe mwamba wangu; Na atukuzwe Mungu wa wokovu wangu;
Psaumes 18.2 Apocalypse 1.18 2 Samuel 22.47 Luc 1.47 Psaumes 57.11
47 Ndiye Mungu anipatiaye kisasi; Na kuwatiisha watu chini yangu.
Psaumes 47.3 Psaumes 144.2 Deutéronome 32.35 Nahum 1.2 Romains 12.19
48 Huniponya na adui zangu; Naam, waniinua juu yao walioniinukia, Na kuniponya na mtu wa jeuri.
Psaumes 140.1 Psaumes 89.13 Philippiens 2.9 Psaumes 140.11 Psaumes 86.14
49 Basi, Bwana, nitakushukuru kati ya mataifa, Nami nitaliimbia jina lako.
Romains 15.9 2 Samuel 22.50-22.51 1 Timothée 6.13 Psaumes 108.1 Psaumes 30.12
50 Ampa mfalme wake wokovu mkuu, Amfanyia fadhili masihi wake,Daudi na mzao wake hata milele.
Psaumes 144.10 2 Samuel 7.13 Actes 2.34-2.36 Galates 3.16 Psaumes 89.20-89.38

Cette Bible est dans le domaine public.