Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Philippiens 2.5
Bible en Swahili de l’est


1 Basi ikiwako faraja yo yote katika Kristo, yakiwako matulizo yo yote ya mapenzi, ukiwako ushirika wo wote wa Roho, ikiwako huruma yo yote na rehema,
Colossiens 3.12 2 Corinthiens 13.14 1 Jean 4.12 Psaumes 133.1 1 Jean 4.7-4.8
2 ijalizeni furaha yangu, ili mwe na nia moja, wenye mapenzi mamoja, wenye roho moja, mkinia mamoja.
Romains 12.16 1 Corinthiens 1.10 1 Pierre 3.8-3.9 2 Corinthiens 13.11 Jean 3.29
3 Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.
Romains 12.10 Ephésiens 4.2 Ephésiens 5.21 Galates 5.26 1 Pierre 5.5
4 Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.
1 Corinthiens 10.24 Romains 15.1 Jacques 2.8 1 Corinthiens 10.32-10.33 1 Corinthiens 12.22-12.26
5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;
Matthieu 11.29 1 Jean 2.6 1 Pierre 2.21 1 Pierre 4.1 Matthieu 20.26-20.28
6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;
Hébreux 1.3 Jean 5.18 2 Corinthiens 4.4 Apocalypse 21.6 Hébreux 13.8
7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;
2 Corinthiens 8.9 Matthieu 20.28 Jean 1.14 Galates 4.4 Romains 8.3
8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.
Jean 10.18 Hébreux 12.2 Matthieu 26.39 1 Pierre 3.18 Romains 5.19
9 Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;
Hébreux 2.9 Matthieu 28.18 1 Pierre 3.22 Esaïe 52.13 Psaumes 110.5
10 ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;
Esaïe 45.23-45.25 Matthieu 28.18 Apocalypse 5.13-5.14 Hébreux 1.6 Romains 14.10-14.11
11 na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.
Jean 13.13 1 Jean 4.15 Romains 14.9 1 Corinthiens 8.6 1 Jean 4.2
12 Basi, wapendwa wangu, kama vile mlivyotii sikuzote, si wakati mimi nilipokuwapo tu, bali sasa zaidi sana mimi nisipokuwapo, utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka.
2 Pierre 1.5-1.10 1 Corinthiens 15.58 Luc 13.23-13.24 Philippiens 3.13-3.14 1 Pierre 2.11
13 Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.
Hébreux 13.21 2 Corinthiens 3.5 2 Timothée 1.9 Ephésiens 2.8 Ephésiens 1.9
14 Yatendeni mambo yote pasipo manung’uniko wala mashindano,
1 Pierre 4.9 1 Corinthiens 10.10 Jacques 1.20 Matthieu 20.11 Actes 15.2
15 mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama, wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka; ambao kati ya hao mnaonekana kuwa kama mianga katika ulimwengu,
Matthieu 5.14-5.16 Matthieu 5.45 1 Pierre 2.12 Tite 2.10 Deutéronome 32.5
16 mkishika neno la uzima; nipate sababu ya kuona fahari katika siku ya Kristo, ya kuwa sikupiga mbio bure wala sikujitaabisha bure.
Galates 2.2 2 Corinthiens 1.14 1 Jean 1.1 1 Thessaloniciens 3.5 Psaumes 71.17
17 Naam, hata nikimiminwa juu ya dhabihu na ibada ya imani yenu, nafurahi; tena nafurahi pamoja nanyi nyote.
2 Timothée 4.6 2 Corinthiens 12.15 Romains 15.16 1 Jean 3.16 1 Pierre 2.5
18 Nanyi vivyo hivyo furahini, tena furahini pamoja nami.
Jacques 1.2-1.4 Philippiens 4.4 Philippiens 3.1 Ephésiens 3.13

Missions de Timothée et d’Épaphrodite

19 Walakini natumaini katika Bwana Yesu kumtuma Timotheo afike kwenu karibu, nifarijiwe na mimi, nikiijua hali yenu.
Philippiens 1.1 1 Corinthiens 4.17 1 Thessaloniciens 3.2 Philippiens 2.28 Philippiens 2.23-2.25
20 Maana sina mtu mwingine mwenye nia moja nami, atakayeiangalia hali yenu kweli kweli.
1 Corinthiens 16.10 Philippiens 2.2 1 Samuel 18.1 1 Samuel 18.3 Jean 10.13
21 Maana wote wanatafuta vyao wenyewe, sivyo vya Kristo Yesu.
1 Corinthiens 10.24 1 Corinthiens 13.5 2 Timothée 3.2 Philippiens 2.4 Esaïe 56.11
22 Ila mwajua sifa yake, ya kuwa ametumika pamoja nami kwa ajili ya Injili, kama mwana na baba yake.
1 Corinthiens 4.17 1 Timothée 1.2 2 Corinthiens 2.9 2 Timothée 1.2 1 Timothée 1.18
23 Basi, natumaini kumtuma huyo mara, hapo nitakapojua yatakayonipata.
1 Samuel 22.3 Philippiens 2.19
24 Nami naamini katika Bwana ya kuwa nitakuja na mimi mwenyewe hivi karibu.
Philémon 1.22 2 Jean 1.12 Romains 15.28-15.29 Philippiens 2.19 3 Jean 1.14
25 Lakini naliona imenilazimu kumtuma kwenu Epafrodito, ndugu yangu, mtenda kazi pamoja nami, askari pamoja nami; tena ni mtume wenu na mhudumu wa mahitaji yangu.
Philippiens 4.18 Philémon 1.1-1.2 Philémon 1.24 Philippiens 4.3 2 Timothée 2.3-2.4
26 Kwa kuwa alikuwa na shauku kwenu ninyi nyote, akahuzunika sana, kwa sababu mlisikia ya kwamba alikuwa hawezi.
Romains 12.15 Philippiens 1.8 Proverbes 12.25 2 Samuel 13.39 Jean 11.35-11.36
27 Kwa maana alikuwa hawezi kweli kweli, karibu na kufa; lakini Mungu alimhurumia; wala si yeye peke yake, ila na mimi pia; nisiwe na huzuni juu ya huzuni.
2 Corinthiens 2.7 Job 5.19 Actes 9.37 Jean 11.3-11.4 Ecclésiaste 9.1-9.2
28 Kwa hiyo nimefanya bidii nyingi zaidi kumtuma, ili mtakapomwona tena mpate kufurahi, nami nipunguziwe huzuni yangu.
Philippiens 2.26-2.27 Jean 16.22 Genèse 48.11 Genèse 46.29-46.30 2 Timothée 1.4
29 Mpokeeni, basi, katika Bwana, kwa furaha yote, mkawahesabu watu kama huyu kuwa watu wa kuheshimiwa.
1 Corinthiens 16.18 Romains 16.2 1 Timothée 5.17 1 Thessaloniciens 5.12 Ephésiens 4.9-4.12
30 Maana kwa ajili ya kazi ya Kristo alikaribia kufa akaponza roho yake; ili kusudi ayatimize yaliyopungua katika huduma yenu kwangu.
1 Corinthiens 16.17 Actes 20.24 Philippiens 4.10 Philémon 1.13 Philippiens 4.18

Cette Bible est dans le domaine public.