Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Philippiens 2.25
Bible en Swahili de l’est


1 Basi ikiwako faraja yo yote katika Kristo, yakiwako matulizo yo yote ya mapenzi, ukiwako ushirika wo wote wa Roho, ikiwako huruma yo yote na rehema,
Colossiens 3.12 1 Jean 4.12 2 Corinthiens 13.14 1 Jean 4.7-4.8 1 Corinthiens 12.13
2 ijalizeni furaha yangu, ili mwe na nia moja, wenye mapenzi mamoja, wenye roho moja, mkinia mamoja.
Romains 12.16 1 Corinthiens 1.10 1 Pierre 3.8-3.9 2 Corinthiens 13.11 Romains 15.5-15.6
3 Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.
Romains 12.10 Ephésiens 4.2 Ephésiens 5.21 Galates 5.26 1 Pierre 5.5
4 Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.
1 Corinthiens 10.24 Romains 15.1 Jacques 2.8 Romains 12.15 Matthieu 18.6
5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;
Matthieu 11.29 1 Jean 2.6 1 Pierre 2.21 1 Pierre 4.1 Matthieu 20.26-20.28
6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;
Hébreux 1.3 Jean 5.18 2 Corinthiens 4.4 Apocalypse 21.6 Hébreux 13.8
7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;
2 Corinthiens 8.9 Matthieu 20.28 Jean 1.14 Galates 4.4 Romains 8.3
8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.
Jean 10.18 Hébreux 12.2 Matthieu 26.39 Romains 5.19 2 Corinthiens 8.9
9 Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;
Matthieu 28.18 Hébreux 2.9 1 Pierre 3.22 Psaumes 110.5 Hébreux 1.4
10 ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;
Esaïe 45.23-45.25 Matthieu 28.18 Apocalypse 5.13-5.14 Hébreux 1.6 Jean 5.28-5.29
11 na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.
Jean 13.13 Romains 14.9 1 Jean 4.15 1 Pierre 1.21 Psaumes 110.1
12 Basi, wapendwa wangu, kama vile mlivyotii sikuzote, si wakati mimi nilipokuwapo tu, bali sasa zaidi sana mimi nisipokuwapo, utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka.
2 Pierre 1.5-1.10 1 Corinthiens 15.58 Luc 13.23-13.24 Philippiens 3.13-3.14 1 Pierre 2.11
13 Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.
Hébreux 13.21 2 Corinthiens 3.5 2 Timothée 1.9 Ephésiens 2.8 Ephésiens 1.9
14 Yatendeni mambo yote pasipo manung’uniko wala mashindano,
1 Pierre 4.9 1 Corinthiens 10.10 Jacques 1.20 Matthieu 20.11 Actes 15.2
15 mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama, wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka; ambao kati ya hao mnaonekana kuwa kama mianga katika ulimwengu,
Matthieu 5.14-5.16 Matthieu 5.45 1 Pierre 2.12 Deutéronome 32.5 1 Corinthiens 1.8
16 mkishika neno la uzima; nipate sababu ya kuona fahari katika siku ya Kristo, ya kuwa sikupiga mbio bure wala sikujitaabisha bure.
Galates 2.2 2 Corinthiens 1.14 1 Jean 1.1 1 Thessaloniciens 3.5 Psaumes 71.17
17 Naam, hata nikimiminwa juu ya dhabihu na ibada ya imani yenu, nafurahi; tena nafurahi pamoja nanyi nyote.
2 Timothée 4.6 2 Corinthiens 12.15 Romains 15.16 Colossiens 1.24 Philippiens 1.20
18 Nanyi vivyo hivyo furahini, tena furahini pamoja nami.
Jacques 1.2-1.4 Philippiens 4.4 Philippiens 3.1 Ephésiens 3.13

Missions de Timothée et d’Épaphrodite

19 Walakini natumaini katika Bwana Yesu kumtuma Timotheo afike kwenu karibu, nifarijiwe na mimi, nikiijua hali yenu.
1 Corinthiens 4.17 1 Thessaloniciens 3.2 Philippiens 1.1 2 Thessaloniciens 1.3 Jacques 4.15
20 Maana sina mtu mwingine mwenye nia moja nami, atakayeiangalia hali yenu kweli kweli.
Philippiens 2.2 1 Corinthiens 16.10 Proverbes 31.29 1 Corinthiens 1.10-1.11 Philippiens 2.22
21 Maana wote wanatafuta vyao wenyewe, sivyo vya Kristo Yesu.
1 Corinthiens 10.24 1 Corinthiens 13.5 2 Timothée 3.2 Philippiens 2.4 2 Corinthiens 5.14-5.15
22 Ila mwajua sifa yake, ya kuwa ametumika pamoja nami kwa ajili ya Injili, kama mwana na baba yake.
1 Corinthiens 4.17 1 Timothée 1.2 2 Timothée 1.2 2 Corinthiens 2.9 2 Corinthiens 8.24
23 Basi, natumaini kumtuma huyo mara, hapo nitakapojua yatakayonipata.
1 Samuel 22.3 Philippiens 2.19
24 Nami naamini katika Bwana ya kuwa nitakuja na mimi mwenyewe hivi karibu.
Philémon 1.22 2 Jean 1.12 Romains 15.28-15.29 Philippiens 2.19 3 Jean 1.14
25 Lakini naliona imenilazimu kumtuma kwenu Epafrodito, ndugu yangu, mtenda kazi pamoja nami, askari pamoja nami; tena ni mtume wenu na mhudumu wa mahitaji yangu.
Philippiens 4.18 Philémon 1.1-1.2 Philippiens 4.3 Philémon 1.24 2 Timothée 2.3-2.4
26 Kwa kuwa alikuwa na shauku kwenu ninyi nyote, akahuzunika sana, kwa sababu mlisikia ya kwamba alikuwa hawezi.
Philippiens 1.8 Romains 12.15 Romains 1.11 Ephésiens 3.13 Matthieu 11.28
27 Kwa maana alikuwa hawezi kweli kweli, karibu na kufa; lakini Mungu alimhurumia; wala si yeye peke yake, ila na mimi pia; nisiwe na huzuni juu ya huzuni.
Ecclésiaste 9.1-9.2 2 Rois 20.1 Psaumes 107.18-107.22 Esaïe 43.2 Psaumes 30.10-30.11
28 Kwa hiyo nimefanya bidii nyingi zaidi kumtuma, ili mtakapomwona tena mpate kufurahi, nami nipunguziwe huzuni yangu.
Genèse 46.29-46.30 2 Timothée 1.4 1 Jean 1.3-1.4 Actes 20.38 Genèse 45.27-45.28
29 Mpokeeni, basi, katika Bwana, kwa furaha yote, mkawahesabu watu kama huyu kuwa watu wa kuheshimiwa.
1 Corinthiens 16.18 Romains 16.2 1 Timothée 5.17 1 Thessaloniciens 5.12 Esaïe 52.7
30 Maana kwa ajili ya kazi ya Kristo alikaribia kufa akaponza roho yake; ili kusudi ayatimize yaliyopungua katika huduma yenu kwangu.
1 Corinthiens 16.17 Actes 20.24 Philippiens 4.10 Philippiens 2.17 2 Corinthiens 12.15

Cette Bible est dans le domaine public.