1 Basi ikiwako faraja yo yote katika Kristo, yakiwako matulizo yo yote ya mapenzi, ukiwako ushirika wo wote wa Roho, ikiwako huruma yo yote na rehema,
Colossiens 3.12  1 Jean 4.12  2 Corinthiens 13.14  Psaumes 133.1  1 Jean 4.7-4.8  
 2 ijalizeni furaha yangu, ili mwe na nia moja, wenye mapenzi mamoja, wenye roho moja, mkinia mamoja.
Romains 12.16  1 Corinthiens 1.10  1 Pierre 3.8-3.9  2 Corinthiens 13.11  Jean 3.29  
 3 Msitende neno lo lote kwa kushindana wala kwa majivuno; bali kwa unyenyekevu, kila mtu na amhesabu mwenziwe kuwa bora kuliko nafsi yake.
Romains 12.10  Ephésiens 4.2  Ephésiens 5.21  Galates 5.26  1 Pierre 5.5  
 4 Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.
1 Corinthiens 10.24  Romains 15.1  Jacques 2.8  Matthieu 18.6  1 Corinthiens 10.32-10.33  
 5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;
Matthieu 11.29  1 Jean 2.6  1 Pierre 2.21  1 Pierre 4.1  Matthieu 20.26-20.28  
 6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;
Jean 5.18  Hébreux 1.3  2 Corinthiens 4.4  Apocalypse 21.6  Hébreux 13.8  
 7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;
2 Corinthiens 8.9  Matthieu 20.28  Jean 1.14  Galates 4.4  Romains 8.3  
 8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.
Jean 10.18  Hébreux 12.2  Matthieu 26.39  2 Corinthiens 8.9  1 Pierre 3.18  
 9 Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;
Matthieu 28.18  Hébreux 2.9  1 Pierre 3.22  Esaïe 52.13  Psaumes 110.5  
 10 ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;Esaïe 45.23-45.25  Matthieu 28.18  Hébreux 1.6  Apocalypse 5.13-5.14  Apocalypse 20.13  
 11 na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.
Jean 13.13  1 Jean 4.15  Romains 14.9  Psaumes 110.1  1 Corinthiens 12.3  
 12 Basi, wapendwa wangu, kama vile mlivyotii sikuzote, si wakati mimi nilipokuwapo tu, bali sasa zaidi sana mimi nisipokuwapo, utimizeni wokovu wenu wenyewe kwa kuogopa na kutetemeka.
2 Pierre 1.5-1.10  1 Corinthiens 15.58  Luc 13.23-13.24  Philippiens 3.13-3.14  1 Pierre 2.11  
 13 Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.
Hébreux 13.21  2 Corinthiens 3.5  2 Timothée 1.9  Ephésiens 1.5  Ephésiens 2.8  
 14 Yatendeni mambo yote pasipo manung’uniko wala mashindano,
1 Pierre 4.9  1 Corinthiens 10.10  Proverbes 13.10  Jacques 1.20  Matthieu 20.11  
 15 mpate kuwa wana wa Mungu wasio na lawama, wala udanganyifu, wasio na ila kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka; ambao kati ya hao mnaonekana kuwa kama mianga katika ulimwengu,
Matthieu 5.14-5.16  Matthieu 5.45  1 Pierre 2.12  Tite 2.10  Deutéronome 32.5  
 16 mkishika neno la uzima; nipate sababu ya kuona fahari katika siku ya Kristo, ya kuwa sikupiga mbio bure wala sikujitaabisha bure.
Galates 2.2  2 Corinthiens 1.14  1 Thessaloniciens 2.19  1 Jean 1.1  1 Thessaloniciens 3.5  
 17 Naam, hata nikimiminwa juu ya dhabihu na ibada ya imani yenu, nafurahi; tena nafurahi pamoja nanyi nyote.
2 Timothée 4.6  2 Corinthiens 12.15  Romains 15.16  Philippiens 1.20  1 Jean 3.16  
 18 Nanyi vivyo hivyo furahini, tena furahini pamoja nami.
Jacques 1.2-1.4  Philippiens 4.4  Philippiens 3.1  Ephésiens 3.13  
 19 Walakini natumaini katika Bwana Yesu kumtuma Timotheo afike kwenu karibu, nifarijiwe na mimi, nikiijua hali yenu.
Philippiens 1.1  1 Corinthiens 4.17  1 Thessaloniciens 3.2  Philémon 1.5-1.7  1 Thessaloniciens 3.6-3.8  
 20 Maana sina mtu mwingine mwenye nia moja nami, atakayeiangalia hali yenu kweli kweli.
1 Corinthiens 16.10  Philippiens 2.2  2 Timothée 1.5  1 Timothée 1.2  Jean 12.6  
 21 Maana wote wanatafuta vyao wenyewe, sivyo vya Kristo Yesu.
1 Corinthiens 10.24  1 Corinthiens 13.5  2 Timothée 3.2  Philippiens 2.4  Esaïe 56.11  
 22 Ila mwajua sifa yake, ya kuwa ametumika pamoja nami kwa ajili ya Injili, kama mwana na baba yake.
1 Corinthiens 4.17  1 Timothée 1.2  2 Timothée 1.2  2 Corinthiens 2.9  2 Timothée 3.10  
 23 Basi, natumaini kumtuma huyo mara, hapo nitakapojua yatakayonipata.
1 Samuel 22.3  Philippiens 2.19  
 24 Nami naamini katika Bwana ya kuwa nitakuja na mimi mwenyewe hivi karibu.
Philémon 1.22  3 Jean 1.14  Philippiens 1.25-1.26  2 Jean 1.12  Romains 15.28-15.29  
 25 Lakini naliona imenilazimu kumtuma kwenu Epafrodito, ndugu yangu, mtenda kazi pamoja nami, askari pamoja nami; tena ni mtume wenu na mhudumu wa mahitaji yangu.
Philippiens 4.18  Philémon 1.1-1.2  Philippiens 4.3  Philémon 1.24  2 Timothée 2.3-2.4  
 26 Kwa kuwa alikuwa na shauku kwenu ninyi nyote, akahuzunika sana, kwa sababu mlisikia ya kwamba alikuwa hawezi.
Romains 12.15  Philippiens 1.8  Philippiens 1.3  1 Pierre 1.6  Actes 21.13  
 27 Kwa maana alikuwa hawezi kweli kweli, karibu na kufa; lakini Mungu alimhurumia; wala si yeye peke yake, ila na mimi pia; nisiwe na huzuni juu ya huzuni.
Jérémie 8.18  Actes 9.39-9.41  Esaïe 27.8  Psaumes 30.1-30.3  Jérémie 45.3  
 28 Kwa hiyo nimefanya bidii nyingi zaidi kumtuma, ili mtakapomwona tena mpate kufurahi, nami nipunguziwe huzuni yangu.
Actes 20.38  Genèse 45.27-45.28  2 Corinthiens 2.3  Philippiens 2.26-2.27  Jean 16.22  
 29 Mpokeeni, basi, katika Bwana, kwa furaha yote, mkawahesabu watu kama huyu kuwa watu wa kuheshimiwa.
1 Corinthiens 16.18  Romains 16.2  1 Timothée 5.17  1 Thessaloniciens 5.12  Luc 2.10-2.11  
 30 Maana kwa ajili ya kazi ya Kristo alikaribia kufa akaponza roho yake; ili kusudi ayatimize yaliyopungua katika huduma yenu kwangu.
1 Corinthiens 16.17  Actes 20.24  Philippiens 4.10  1 Corinthiens 16.10  Matthieu 25.36-25.40