Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Corinthiens 15.16
Bible en Swahili de l’est


Rappel de l’Évangile : la résurrection

1 Basi, ndugu zangu, nawaarifu ile injili niliyowahubiri; ambayo ndiyo mliyoipokea, na katika hiyo mnasimama,
Romains 5.2 Romains 2.16 1 Pierre 5.12 Galates 1.6-1.12 2 Corinthiens 1.24
2 na kwa hiyo mnaokolewa; ikiwa mnayashika sana maneno niliyowahubiri isipokuwa mliamini bure.
Hébreux 3.6 Hébreux 3.14 Ephésiens 2.8 Romains 1.16 2 Timothée 1.9
3 Kwa maana naliwatolea ninyi hapo mwanzo yale niliyoyapokea mimi mwenyewe, ya kuwa Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama yanenavyo maandiko;
1 Pierre 2.24 1 Corinthiens 11.23 Actes 26.22-26.23 Esaïe 53.1-53.12 Galates 1.4
4 na ya kuwa alizikwa; na ya kuwa alifufuka siku ya tatu, kama yanenavyo maandiko;
Matthieu 12.40 Actes 26.22-26.23 Osée 6.2 Psaumes 16.10-16.11 Esaïe 53.9-53.12
5 na ya kuwa alimtokea Kefa; tena na wale Thenashara;
Marc 16.14 Actes 10.41 1 Corinthiens 1.12 Luc 24.34-24.49 Jean 20.19-20.26
6 baadaye aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano pamoja; katika hao wengi wanaishi hata sasa, ila baadhi yao wamelala;
Matthieu 28.16-28.17 Matthieu 28.10 1 Thessaloniciens 4.13 1 Corinthiens 15.18 1 Thessaloniciens 4.15
7 baadaye akamtokea Yakobo; tena na mitume wote;
Luc 24.50 Actes 1.2-1.12 Actes 12.17 Luc 24.33 Luc 24.36
8 na mwisho wa watu wote, alinitokea mimi, kama ni mtu aliyezaliwa si kwa wakati wake.
1 Corinthiens 9.1 Actes 9.17 Actes 26.16 Actes 18.9 Actes 9.3-9.6
9 Maana mimi ni mdogo katika mitume, nisiyestahili kuitwa mitume, kwa sababu naliliudhi Kanisa la Mungu.
Actes 8.3 2 Corinthiens 12.11 Ephésiens 3.7-3.8 1 Timothée 1.13-1.15 Actes 22.4-22.5
10 Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa hivi nilivyo; na neema yake iliyo kwangu ilikuwa si bure, bali nalizidi sana kufanya kazi kupita wao wote; wala si mimi, bali ni neema ya Mungu pamoja nami.
2 Corinthiens 3.5 Galates 2.8 Philippiens 2.13 Ephésiens 3.7-3.8 2 Corinthiens 12.11
11 Basi, kama ni mimi, kama ni wale, ndivyo tuhubirivyo, na ndivyo mlivyoamini.
1 Corinthiens 15.3-15.4 1 Corinthiens 2.2
12 Basi, ikiwa Kristo anahubiriwa ya kwamba amefufuka katika wafu, mbona baadhi yenu husema kwamba hakuna kiyama ya wafu?
Actes 23.8 2 Timothée 2.18 Actes 26.8 Actes 17.32 1 Corinthiens 15.13-15.19
13 Lakini kama hakuna kiyama ya wafu, Kristo naye hakufufuka;
1 Thessaloniciens 4.14 1 Corinthiens 15.20 Actes 23.8 Apocalypse 1.18 Romains 4.24-4.25
14 tena kama Kristo hakufufuka, basi, kuhubiri kwetu ni bure na imani yenu ni bure.
Jacques 2.20 1 Thessaloniciens 4.14 1 Corinthiens 15.17 Matthieu 15.9 Esaïe 49.4
15 Naam, na sisi tumeonekana kuwa mashahidi wa uongo wa Mungu; kwa maana tulimshuhudia Mungu ya kuwa alimfufua Kristo, ambaye hakumfufua, ikiwa wafu hawafufuliwi.
Actes 2.24 Actes 10.39-10.42 Job 13.7-13.10 Actes 20.21 Actes 4.10
16 Maana kama wafu hawafufuliwi, Kristo naye hakufufuka.
17 Na kama Kristo hakufufuka, imani yenu ni bure; mngalimo katika dhambi zenu.
Romains 4.25 1 Corinthiens 15.14 1 Pierre 1.3 Hébreux 10.4-10.12 Actes 5.31
18 Na hapo wao nao waliolala katika Kristo wamepotea.
Apocalypse 14.13 1 Corinthiens 15.6 1 Thessaloniciens 4.13-4.14 1 Thessaloniciens 4.16
19 Kama katika maisha haya tu tumemtumaini Kristo, sisi tu maskini kuliko watu wote.
2 Timothée 3.12 1 Pierre 1.21 Jean 16.33 1 Corinthiens 6.3-6.4 1 Thessaloniciens 1.3
20 Lakini sasa Kristo amefufuka katika wafu, limbuko lao waliolala.
1 Pierre 1.3 Actes 26.23 1 Corinthiens 15.23 Apocalypse 1.5 Colossiens 1.18
21 Maana kwa kuwa mauti ililetwa na mtu, kadhalika na kiyama ya wafu ililetwa na mtu.
Romains 6.23 Jean 11.25 Romains 5.12-5.17 1 Corinthiens 15.22
22 Kwa kuwa kama katika Adamu wote wanakufa, kadhalika na katika Kristo wote watahuishwa.
Romains 5.12-5.21 Jean 5.21-5.29 Genèse 2.17 Genèse 3.19 Genèse 3.6
23 Lakini kila mmoja mahali pake; limbuko ni Kristo; baadaye walio wake Kristo, atakapokuja.
1 Corinthiens 15.20 1 Corinthiens 15.52 2 Corinthiens 10.7 1 Thessaloniciens 2.19 1 Corinthiens 3.23
24 Hapo ndipo mwisho, atakapompa Mungu Baba ufalme wake; atakapobatilisha utawala wote, na mamlaka yote, na nguvu.
Daniel 7.14 Daniel 7.27 Matthieu 28.18 Esaïe 9.7 Daniel 2.44
25 Maana sharti amiliki yeye, hata awaweke maadui wake wote chini ya miguu yake.
Psaumes 110.1 Matthieu 22.44 Psaumes 2.6-2.10 Psaumes 45.3-45.6 Hébreux 1.13
26 Adui wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti.
2 Timothée 1.10 Apocalypse 20.14 Apocalypse 21.4 Hébreux 2.14 1 Corinthiens 15.55
27 Kwa kuwa, Alivitiisha vitu vyote chini ya miguu yake. Lakini atakaposema, Vyote vimetiishwa, ni dhahiri ya kuwa yeye aliyemtiishia vitu vyote hayumo.
Matthieu 28.18 Psaumes 8.6 Matthieu 11.27 1 Pierre 3.22 Hébreux 2.8
28 Basi, vitu vyote vikiisha kutiishwa chini yake, ndipo Mwana mwenyewe naye atatiishwa chini yake yeye aliyemtiishia vitu vyote, ili kwamba Mungu awe yote katika wote.
1 Corinthiens 3.23 Philippiens 3.21 1 Corinthiens 11.3 1 Corinthiens 12.6 Psaumes 18.39
29 Au je! Wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu watafanyaje? Kama wafu hawafufuliwi kamwe, kwa nini kubatizwa kwa ajili yao?
Romains 6.3-6.4 Matthieu 20.22 1 Corinthiens 15.16 1 Corinthiens 15.32
30 Na sisi, kwa nini tumo hatarini kila saa?
2 Corinthiens 4.7-4.12 Romains 8.36-8.39 Galates 5.11 2 Corinthiens 6.9 1 Corinthiens 15.31
31 Naam, ndugu, kwa huku kujisifu kwangu niliko nako juu yenu katika Kristo Yesu Bwana wetu, ninakufa kila siku.
Romains 8.36 2 Corinthiens 4.10-4.11 1 Thessaloniciens 2.19 1 Corinthiens 4.9-4.13 2 Corinthiens 11.23
32 Ikiwa, kwa jinsi ya kibinadamu, nalipigana na hayawani wakali kule Efeso, nina faida gani? Wasipofufuliwa wafu, na tule, na tunywe, maana kesho tutakufa.
Esaïe 22.13 Luc 12.19 Esaïe 56.12 Galates 3.15 2 Corinthiens 1.8-1.10
33 Msidanganyike; Mazungumzo mabaya huharibu tabia njema.
Proverbes 13.20 Matthieu 24.4 1 Corinthiens 5.6 Ephésiens 5.6 1 Corinthiens 6.9
34 Tumieni akili kama ipasavyo, wala msitende dhambi; kwa maana wengine hawamjui Mungu. Ninanena hayo niwafedheheshe.
Romains 13.11 1 Corinthiens 6.5 1 Thessaloniciens 4.5 Jean 5.14 Hébreux 5.11-5.12
35 Lakini labda mtu atasema, Wafufuliwaje wafu? Nao huja kwa mwili gani?
Ezéchiel 37.3 Jean 3.9 Jean 9.10 Ecclésiaste 11.5 Job 11.12
36 Ewe mpumbavu! Uipandayo haihuiki, isipokufa;
Jean 12.24 Luc 12.20 Ephésiens 5.15 Romains 1.22 Luc 11.40
37 nayo uipandayo, huupandi mwili ule utakaokuwa, ila chembe tupu, ikiwa ni ya ngano au nyingineyo;
38 lakini Mungu huipa mwili kama apendavyo, na kila mbegu mwili wake.
Marc 4.26-4.29 1 Corinthiens 3.7 Esaïe 61.11 Genèse 1.11-1.12 Psaumes 104.14
39 Nyama yote si nyama moja; ila nyingine ni ya wanadamu, nyingine ya hayawani, nyingine ya ndege, nyingine ya samaki.
Genèse 1.20-1.26
40 Tena kuna miili ya mbinguni, na miili ya duniani; lakini fahari yake ile ya mbinguni ni mbali, na fahari yake ile ya duniani ni mbali.
41 Kuna fahari moja ya jua, na fahari nyingine ya mwezi, na fahari nyingine ya nyota; maana iko tofauti ya fahari hata kati ya nyota na nyota.
Esaïe 24.23 Psaumes 8.3 Job 31.26 Psaumes 19.4-19.6 Genèse 1.14
42 Kadhalika na kiyama ya watu. Hupandwa katika uharibifu; hufufuliwa katika kutokuharibika;
Daniel 12.3 Matthieu 13.43 Romains 8.21 Psaumes 16.10 Actes 13.34-13.37
43 hupandwa katika aibu; hufufuliwa katika fahari; hupandwa katika udhaifu; hufufuliwa katika nguvu;
Colossiens 3.4 Marc 12.24-12.25 Matthieu 22.29-22.30 Philippiens 3.10 1 Corinthiens 6.14
44 hupandwa mwili wa asili; hufufuliwa mwili wa roho. Ikiwa uko mwili wa asili, na wa roho pia uko.
1 Corinthiens 15.50 Jean 20.26 Luc 24.31 Jean 20.19
45 Ndivyo ilivyoandikwa, Mtu wa kwanza, Adamu, akawa nafsi iliyo hai; Adamu wa mwisho ni roho yenye kuhuisha.
Romains 8.2 Jean 5.21 Jean 6.57 Jean 6.33 Genèse 2.7
46 Lakini hautangulii ule wa roho, bali ule wa asili; baadaye huja ule wa roho.
Ephésiens 4.22-4.24 Colossiens 3.9-3.10 Romains 6.6
47 Mtu wa kwanza atoka katika nchi, ni wa udongo. Mtu wa pili atoka mbinguni.
Jean 3.31 Genèse 2.7 Genèse 3.19 Jean 6.33 Actes 10.36
48 Kama alivyo yeye wa udongo, ndivyo walivyo walio wa udongo; na kama alivyo yeye wa mbinguni, ndivyo walivyo walio wa mbinguni.
Philippiens 3.20-3.21 Jean 3.6 Genèse 5.3 Job 14.4 1 Corinthiens 15.21-15.22
49 Na kama tulivyoichukua sura yake yule wa udongo, kadhalika tutaichukua sura yake yeye aliye wa mbinguni.
Romains 8.29 Genèse 5.3 2 Corinthiens 3.18 1 Jean 3.2 Matthieu 13.43
50 Ndugu zangu, nisemayo ni haya, ya kuwa nyama na damu haziwezi kuurithi ufalme wa Mungu; wala uharibifu kurithi kutokuharibika.
Matthieu 16.17 Ephésiens 4.17 Galates 5.16 1 Corinthiens 7.29 Colossiens 2.4
51 Angalieni, nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika,
Philippiens 3.21 1 Thessaloniciens 4.14-4.17 1 Corinthiens 15.20 1 Corinthiens 2.7 1 Corinthiens 13.2
52 kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika.
Matthieu 24.31 Jean 5.25 Esaïe 27.13 Zacharie 9.14 Jean 5.28
53 Maana sharti huu uharibikao uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa uvae kutokufa.
2 Corinthiens 5.2-5.4 1 Jean 3.2 Romains 13.12-13.14 Ephésiens 4.24 Romains 2.7
54 Basi huu uharibikao utakapovaa kutokuharibika, na huu wa kufa utakapovaa kutokufa, hapo ndipo litakapokuwa lile neno lililoandikwa, Mauti imemezwa kwa kushinda.
Esaïe 25.8 Apocalypse 20.14 Apocalypse 21.4 Hébreux 2.14-2.15 Luc 20.36
55 Ku wapi, Ewe mauti, kushinda kwako? U wapi, Ewe mauti, uchungu wako?
Osée 13.14 Psaumes 49.8-49.15 Psaumes 89.48 Actes 9.5 Ecclésiaste 2.15-2.16
56 Uchungu wa mauti ni dhambi, na nguvu za dhambi ni torati.
Romains 4.15 Galates 3.10-3.13 Romains 7.5-7.13 Romains 6.23 Romains 5.15
57 Lakini Mungu na ashukuriwe atupaye kushinda kwa Bwana wetu Yesu Kristo.
2 Corinthiens 2.14 Romains 8.37 1 Jean 5.4-5.5 Jean 16.33 Proverbes 21.31
58 Basi, ndugu zangu wapendwa, mwimarike, msitikisike, mkazidi sana kutenda kazi ya Bwana sikuzote, kwa kuwa mwajua ya kwamba taabu yenu siyo bure katika Bwana.
Galates 6.9 2 Chroniques 15.7 Hébreux 6.10 2 Pierre 3.17-3.18 Colossiens 1.23

Cette Bible est dans le domaine public.