Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Actes 22.21
Bible en Swahili de l’est


1 Enyi wanaume, ndugu zangu na baba zangu, nisikilizeni, nikijitetea mbele yenu sasa.
Actes 7.2 Actes 25.16 Actes 26.1-26.2 Actes 25.8 Actes 23.1
2 Waliposikia kwamba anasema nao kwa lugha ya Kiebrania wakazidi kunyamaza; akasema,
Actes 21.40
3 Mimi ni mtu wa Kiyahudi, nalizaliwa Tarso, mji wa Kilikia, ila nililelewa katika mji huu, miguuni pa Gamalieli, nikafundishwa sheria ya baba zetu kwa usahihi, nikawa mtu wa jitihadi kwa Mungu kama ninyi nyote mlivyo leo hivi;
Actes 9.11 Actes 5.34 Actes 26.5 Philippiens 3.5-3.6 Actes 21.20
4 nikawaudhi watu wa Njia hii hata kuwaua, nikawafunga, nikiwatia gerezani, wanaume na wanawake.
Actes 22.19-22.20 Actes 8.1-8.4 Actes 26.9-26.11 Actes 19.9 Actes 19.23
5 Kama Kuhani Mkuu naye anishuhudiavyo, na wazee wa baraza wote pia, ambao nalipokea barua kwao kuwapelekea ndugu wale, nikaenda Dameski, ili niwalete wale waliokuwa huko hata Yerusalemu, hali wamefungwa, ili waadhibiwe.
Luc 22.66 Actes 9.1-9.2 Actes 5.21 Actes 26.10 Actes 22.1
6 Ikawa nilipokuwa nikisafiri, nikikaribia Dameski, wakati wa adhuhuri, ghafula nuru kuu ilitoka mbinguni, ikanimulikia pande zote.
Actes 9.3-9.8 Apocalypse 1.16 Genèse 15.2 Matthieu 17.2 2 Samuel 8.6
7 Nikaanguka nchi, nikasikia sauti ikiniambia, Sauli, Sauli, mbona unaniudhi?
Jérémie 2.9 Genèse 3.9 Exode 3.4 Esaïe 43.22-43.26 Matthieu 25.45
8 Nikajibu, Wewe u nani, Bwana? Akaniambia, Mimi ni Yesu Mnazareti, ambaye wewe unaniudhi.
Actes 26.9 Matthieu 10.40-10.42 Matthieu 2.23 Actes 6.14 1 Corinthiens 12.26-12.27
9 Na wale waliokuwa pamoja nami waliiona ile nuru, lakini hawakuisikia ile sauti ya yule aliyesema nami.
Actes 9.7 Daniel 10.7 Actes 26.13 Jean 12.29-12.30
10 Nikasema, Nifanye nini, Bwana? Bwana akaniambia, Simama, uingie Dameski, na huko utaambiwa habari za mambo yote yaliyoamriwa uyafanye.
Actes 16.30 Actes 26.16-26.18 Psaumes 25.8-25.9 Psaumes 143.8-143.10 Actes 2.37
11 Na nilipokuwa sioni kwa sababu ya fahari ya nuru ile, nikaongozwa na mikono yao waliokuwa pamoja nami, nikaingia Dameski.
Actes 9.8-9.9 Esaïe 42.16 Actes 13.11
12 Basi mtu mmoja, Anania, mtauwa kwa kuifuata sheria, aliyeshuhudiwa wema na Wayahudi wote waliokaa huko,
Actes 10.22 Actes 6.3 Actes 9.10-9.18 1 Timothée 3.7 Luc 2.25
13 Akanijia, akasimama karibu nami, akaniambia, Ndugu yangu Sauli, uone. Nikamwinulia macho yangu saa ile ile.
Philémon 1.16 Actes 9.17-9.18
14 Akasema, Mungu wa baba zetu amekuchagua wewe upate kujua mapenzi yake, na kumwona yule Mwenye haki, na kuisikia sauti itokayo katika kinywa chake.
Actes 26.16 1 Corinthiens 9.1 1 Corinthiens 15.8 Actes 9.17 Galates 1.12
15 Kwa maana utakuwa shahidi wake kwa watu wote, wa mambo hayo uliyoyaona na kuyasikia.
Actes 23.11 Actes 4.20 Actes 1.22 Actes 26.20 Actes 26.16-26.18
16 Basi sasa, unakawilia nini? Simama, ubatizwe, ukaoshe dhambi zako, ukiliitia jina lake.
Actes 2.38 1 Corinthiens 6.11 Hébreux 10.22 1 Corinthiens 12.13 1 Pierre 3.21
17 Ikawa nilipokwisha kurudi Yerusalemu, nilipokuwa nikisali ndani ya hekalu, nikawa hali ya kuzimia roho,
2 Corinthiens 12.1-12.4 Actes 9.26-9.28 Galates 1.18 Apocalypse 1.10 Actes 26.20
18 nikamwona, naye akiniambia, Hima, utoke Yerusalemu upesi, kwa sababu hawatakubali ushuhuda wako katika habari zangu.
Matthieu 10.14 Actes 3.19 Actes 9.29 Ezéchiel 3.6-3.7 Luc 21.21
19 Nami nikasema, Bwana, wanajua hao ya kuwa mimi nalikuwa nikiwafunga gerezani wale wanaokuamini na kuwapiga katika kila sinagogi.
Matthieu 10.17 Actes 22.4 Actes 8.3 Actes 9.1 Actes 26.9-26.12
20 Na damu ya Stefano shahidi wako ilipomwagwa, mimi nami nilikuwa nikisimama karibu, nikikubali, na kuzitunza nguo zao waliomwua.
Actes 8.1 Actes 7.58 Apocalypse 2.13 Romains 1.32 Apocalypse 17.6
21 Naye akaniambia, Enenda zako; kwa kuwa mimi nitakutuma uende mbali kwa watu wa Mataifa.
Actes 9.15 Romains 15.16 Romains 11.13 1 Timothée 2.7 Galates 1.15-1.16
22 Wakamsikiliza mpaka neno lile, wakapaza sauti zao, wakisema, Mwondoe huyu katika nchi, kwa maana haifai aishi.
Actes 25.24 Actes 21.36 Jean 19.15 Actes 7.54-7.57 Luc 23.18
23 Walipokuwa wakipiga kelele na kutupa mavazi yao na kurusha-rusha mavumbi juu,
Ecclésiaste 10.3 Actes 7.58 Actes 26.11 Actes 7.53 2 Samuel 16.13
24 yule jemadari akaamuru aletwe ndani ya ngome, akisema aulizwe habari zake kwa kupigwa mijeledi, ili ajue sababu hata wakampigia kelele namna hii.
Actes 23.10 Actes 21.34 Actes 22.25-22.29 Actes 16.22-16.23 Hébreux 11.35
25 Hata walipokwisha kumfunga kwa kamba, Paulo akamwambia yule akida aliyesimama karibu, Je! Ni halali ninyi kumpiga mtu aliye Mrumi naye hajakuhumiwa bado?
Actes 16.37 Actes 27.1 Actes 27.3 Matthieu 27.54 Actes 25.16
26 Yule akida aliposikia, akaenda akamwarifu yule jemadari, akisema, Unataka kufanya nini? Kwa maana mtu huyu ni Mrumi.
Actes 23.27 Actes 22.29
27 Jemadari akaja, akamwuliza, Niambie, u Mrumi? Akasema, Ndiyo.
28 Jemadari akajibu, Mimi nalipata wenyeji huu kwa mali nyingi. Paulo akasema, Na mimi ni Mrumi wa kuzaliwa.
29 Basi wale waliokuwa tayari kumwuliza wakaondoka wakamwacha. Na yule jemadari naye akaogopa, alipojua ya kuwa ni Mrumi, na kwa sababu amemfunga.
Hébreux 11.35 Actes 22.24-22.26 Actes 21.33 Actes 16.38-16.39
30 Siku ya pili yake akitaka kujua hakika, ni kwa sababu gani ameshitakiwa na Wayahudi, akamfungua, akawaamuru wakuu wa makuhani na baraza yote wakutane. Akamleta Paulo chini, akamweka mbele yao.
Actes 23.28 Actes 21.33 Actes 26.29 Actes 21.11 Actes 5.21

Cette Bible est dans le domaine public.