Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Actes 16
Bible en Swahili de l’est


1 Basi akafika Derbe na Listra, na hapo palikuwa na mwanafunzi mmoja jina lake Timotheo, mwana wa mwanamke Myahudi aliyeamini; lakini babaye alikuwa Myunani.
Actes 14.6 1 Corinthiens 4.17 Actes 19.22 1 Timothée 1.2 Actes 17.14
2 Mtu huyo alishuhudiwa vema na ndugu waliokaa Listra na Ikonio.
1 Timothée 5.25 Actes 6.3 Actes 16.40 2 Timothée 3.15 1 Timothée 3.7
3 Paulo akamtaka huyo afuatane naye, akamtwaa akamtahiri kwa ajili ya Wayahudi waliokuwako pande zile; kwa maana wote walijua ya kuwa babaye ni Myunani.
Galates 2.3 Galates 5.6 1 Corinthiens 9.20 1 Corinthiens 7.19 Actes 15.37
4 Basi walipokuwa wakipita kati ya miji ile, wakawapa zile amri zilizoamriwa na mitume na wazee walioko Yerusalemu, ili wazishike.
Actes 15.28-15.29 Actes 15.2 Actes 11.30 Actes 15.6
5 Makanisa yakatiwa nguvu katika ile Imani, hesabu yao ikaongezeka kila siku.
Actes 9.31 Actes 2.47 Actes 6.7 Actes 15.41 1 Thessaloniciens 3.2
6 Wakapita katika nchi ya Frigia na Galatia, wakikatazwa na Roho Mtakatifu, wasilihubiri lile neno katika Asia.
Actes 18.23 1 Pierre 1.1 Galates 1.2 Galates 3.1 2 Timothée 4.10
7 Walipofika kukabili Misia wakajaribu kuenda Bithinia, lakini Roho wa Yesu hakuwapa ruhusa,
1 Pierre 1.1 Actes 8.29 Romains 8.9 Galates 4.6 Philippiens 1.19
8 wakapita Misia wakatelemkia Troa.
2 Corinthiens 2.12 2 Timothée 4.13 Actes 20.5 Actes 16.11
9 Paulo akatokewa na maono usiku; alimwona mtu wa Makedonia amesimama, akimsihi, na kumwambia, Vuka, uje Makedonia utusaidie.
Actes 19.21 Actes 18.5 Romains 15.26 Actes 27.23-27.24 Actes 10.32-10.33

L’Évangile à Philippes

10 Basi alipokwisha kuyaona yale maono, mara tukataka kutoka kwenda Makedonia, kwa kuwa tuliona hakika ya kwamba Mungu ametuita tuwahubiri Habari Njema.
Psaumes 119.60 Actes 27.1-28.16 Actes 21.1-21.18 Proverbes 3.27-3.28 2 Corinthiens 2.12-2.13
11 Basi tukang’oa nanga kutoka Troa, tukafika Samothrake kwa tanga moja, na siku ya pili tukafika Neapoli;
Actes 16.8 Actes 21.1
12 na kutoka hapo tukafika Filipi, mji wa Makedonia, mji ulio mkuu katika jimbo lile, mahali walipohamia Warumi; tukawa katika mji huu, tukikaa siku kadha wa kadha.
1 Thessaloniciens 2.2 Philippiens 1.1 Actes 20.6 Actes 16.21 Actes 16.9
13 Hata siku ya sabato tukatoka nje ya lango, tukaenda kando ya mto, ambapo tukadhani ya kuwa pana mahali pa kusali; tukaketi, tukasema na wanawake waliokutana pale.
Actes 13.14 Actes 18.4 Actes 16.6 Luc 13.10 Actes 20.7
14 Mwanamke mmoja, jina lake Lidia, mwenye kuuza rangi ya zambarau, mwenyeji wa Thiatira, mcha Mungu, akatusikiliza, ambaye moyo wake ulifunguliwa na Bwana, ayatunze maneno yaliyonenwa na Paulo.
Luc 24.45 Actes 18.7 Apocalypse 1.11 Cantique 5.4 Apocalypse 3.7
15 Hata alipokwisha kubatizwa, yeye na nyumba yake, akatusihi, akisema, Kama mmeniona kuwa mwaminifu kwa Bwana, ingieni nyumbani mwangu mkakae. Akatushurutisha.
Actes 11.14 Hébreux 13.2 Genèse 19.3 Luc 24.29 Actes 16.33
16 Ikawa tulipokuwa tukienda mahali pale pa kusali, kijakazi mmoja aliyekuwa na pepo wa uaguzi akatukuta, aliyewapatia bwana zake faida nyingi kwa kuagua.
Esaïe 8.19 1 Samuel 28.7 Galates 5.20 Exode 7.11-7.12 Lévitique 19.31
17 Akamfuata Paulo na sisi akipiga kelele, akisema, Watu hawa ni watumishi wa Mungu aliye juu, wenye kuwahubiria njia ya wokovu.
Marc 5.7 Daniel 6.20 Daniel 3.26 1 Pierre 2.16 Luc 4.34
18 Akafanya hayo siku nyingi. Lakini Paulo akasikitika, akageuka akamwambia yule pepo, Nakuamuru kwa jina la Yesu Kristo, mtoke huyu. Akamtoka saa ile ile.
Marc 16.17 Marc 1.34 Luc 10.17-10.19 Colossiens 2.15 Actes 3.6
19 Basi bwana zake walipoona ya kuwa tumaini la faida yao limewapotea, wakawakamata Paulo na Sila, wakawakokota mpaka sokoni mbele ya wakuu wa mji;
Actes 21.30 Actes 8.3 Jacques 2.6 Actes 17.6 Actes 16.16
20 wakawachukua kwa makadhi, wakasema, Watu hawa wanachafua sana mji wetu, nao ni Wayahudi;
Actes 28.22 Esdras 4.12-4.15 Actes 17.6-17.8 Actes 19.34 Esther 3.8-3.9
21 tena wanatangaza habari ya desturi zisizokuwa halali kwetu kuzipokea wala kuzifuata, kwa kuwa sisi tu Warumi.
Actes 16.12 Esther 3.8 Jérémie 10.3 Actes 26.3
22 Makutano wote wakaondoka wakawaendea, makadhi wakawavua nguo zao kwa nguvu, wakatoa amri wapigwe kwa bakora.
1 Thessaloniciens 2.2 2 Corinthiens 11.23-11.25 2 Corinthiens 6.5 Actes 22.22-22.26 Hébreux 11.36
23 Na walipokwisha kuwapiga mapigo mengi, wakawatupa gerezani, wakamwamuru mlinzi wa gereza awalinde sana.
Actes 5.23 Luc 21.12 Actes 12.18 1 Samuel 23.22-23.23 Apocalypse 1.9
24 Naye akiisha kupata amri hii akawatupa katika chumba cha ndani, akawafunga miguu kwa mkatale.
Job 33.11 Job 13.27 Jérémie 29.26 Jérémie 38.26 Psaumes 105.18
25 Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza.
Psaumes 77.6 Jacques 1.2 Job 35.10 1 Pierre 1.6-1.8 Psaumes 119.62
26 Ghafula pakawa tetemeko kuu la nchi, hata misingi ya gereza ikatikisika, na mara hiyo milango ikafunguka, vifungo vya wote vikalegezwa.
Actes 4.31 Actes 12.7 Actes 12.10 Actes 5.19 Psaumes 102.20
27 Yule mlinzi wa gereza akaamka, naye alipoona ya kuwa milango ya gereza imefunguka, alifuta upanga, akataka kujiua, akidhani ya kuwa wafungwa wamekimbia.
Actes 12.19 Actes 16.23-16.24 2 Samuel 17.23 Matthieu 27.5 1 Samuel 31.4-31.5
28 Ila Paulo akapaza sauti yake kwa nguvu, akisema, Usijidhuru, kwa maana sisi sote tupo hapa.
Exode 20.13 Luc 23.34 Ecclésiaste 7.17 Psaumes 35.14 Luc 22.51
29 Akataka taa ziletwe, akarukia ndani, akitetemeka kwa hofu, akawaangukia Paulo na Sila;
Jérémie 10.10 Psaumes 99.1 Actes 9.5-9.6 Psaumes 119.120 Jérémie 5.22
30 kisha akawaleta nje akasema, Bwana zangu, yanipasa nifanye nini nipate kuokoka?
Actes 2.37 Actes 22.10 Luc 3.10 Actes 16.17 Actes 9.6
31 Wakamwambia, Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako.
Actes 2.38-2.39 Jean 1.12 Esaïe 45.22 Jean 3.36 Marc 16.16
32 Wakamwambia neno la Bwana, yeye na watu wote waliomo nyumbani mwake.
1 Thessaloniciens 2.8 Romains 1.14 Romains 1.16 1 Timothée 1.13-1.16 Colossiens 1.27-1.28
33 Akawakaribisha saa ile ile ya usiku, akawaosha mapigo yao, kisha akabatizwa, yeye na watu wake wote wakati uo huo.
Actes 16.25 Actes 16.15 1 Corinthiens 1.16 Matthieu 25.35-25.40 Actes 16.23
34 Akawaleta juu nyumbani kwake, akawaandalia chakula, akafurahi sana, yeye na nyumba yake yote, maana amekwisha kumwamini Mungu.
Actes 2.46 Actes 8.39 Actes 11.14 Philémon 1.7 1 Jean 3.18
35 Kulipopambauka makadhi wakawatuma wakubwa wa askari wakisema, Waacheni watu wale waende zao.
Jérémie 5.22 Actes 4.21 Actes 5.40 Psaumes 76.10
36 Yule mlinzi wa gereza akamwarifu Paulo maneno haya akisema, Makadhi wametuma watu ili mfunguliwe; basi, sasa tokeni nje, enendeni zenu kwa amani.
Actes 15.33 Jean 14.27 Exode 4.18 2 Rois 5.19 1 Samuel 25.35
37 Paulo akawaambia, Wametupiga mbele ya watu wote bila kutuhukumu, na sisi tu Warumi, tena wametutupa gerezani; na sasa wanataka kututoa kwa siri? Sivyo, lakini na waje wenyewe wakatutoe.
Actes 22.25-22.29 Psaumes 82.1-82.2 Proverbes 28.1 Psaumes 94.20 Actes 16.20-16.24
38 Wakubwa wa askari wakawapasha makadhi habari za maneno haya; nao wakaogopa, waliposikia ya kwamba hao ni Warumi.
Actes 22.29 Matthieu 14.5 Matthieu 21.46
39 Wakaja wakawasihi; na walipokwisha kuwatoa nje, wakawaomba watoke katika mji ule.
Matthieu 8.34 Marc 5.17 Exode 11.8 Esaïe 60.14 Daniel 6.23
40 Nao wakatoka gerezani wakaingia nyumbani mwa Lidia; na walipokwisha kuonana na ndugu wakawafariji, wakaenda zao.
Actes 16.14 2 Corinthiens 4.8-4.12 1 Thessaloniciens 3.2-3.3 2 Corinthiens 1.3-1.7 2 Corinthiens 4.16-4.18

Cette Bible est dans le domaine public.