Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jean 12.30
Bible en Swahili de l’est


Marie verse du parfum sur les pieds de Jésus

1 Basi, siku sita kabla ya Pasaka, Yesu alifika Bethania, alipokuwapo Lazaro, yeye ambaye Yesu alimfufua katika wafu.
Matthieu 21.17 Jean 11.55 Marc 14.3-14.8 Luc 24.50 Jean 11.1
2 Basi wakamwandalia karamu huko; naye Martha akatumikia; na Lazaro alikuwa mmojawapo wa wale walioketi chakulani pamoja naye.
Luc 22.27 Luc 10.38-10.42 Matthieu 26.6 Jean 11.43-11.44 Luc 5.29
3 Basi Mariamu akatwaa ratli ya marhamu ya nardo safi yenye thamani nyingi, akampaka Yesu miguu, akamfuta miguu kwa nywele zake. Nayo nyumba pia ikajaa harufu ya marhamu.
Jean 11.2 Luc 7.37-7.38 Psaumes 132.2 Marc 14.3-14.9 Matthieu 26.6-26.13
4 Basi Yuda Iskariote, mmojawapo wa wanafunzi wake, ambaye ndiye atakaye kumsaliti, akasema,
Matthieu 10.4 Jean 13.2 Jean 13.26 Jean 6.70-6.71 Jean 18.2-18.5
5 Mbona marhamu hii haikuuzwa kwa dinari mia tatu, wakapewa maskini?
Matthieu 20.2 Amos 8.5 Jean 6.7 Malachie 1.10-1.13 Exode 5.8
6 Naye aliyasema hayo, si kwa kuwahurumia maskini; bali kwa kuwa ni mwivi, naye ndiye aliyeshika mfuko, akavichukua vilivyotiwa humo.
Jean 13.29 Jacques 2.6 Jacques 2.2 2 Rois 12.14-12.15 Psaumes 50.16-50.20
7 Basi Yesu alisema, Mwache aiweke kwa siku ya maziko yangu.
Matthieu 26.12 Psaumes 109.31 Zacharie 3.2 Matthieu 27.57-27.60 Jean 19.38-19.42
8 Kwa maana maskini mnao sikuzote pamoja nanyi; bali mimi hamnami sikuzote.
Deutéronome 15.11 Marc 14.7 Matthieu 26.11 Jean 8.21 Jean 12.35
9 Basi watu wengi katika Wayahudi walipata kujua ya kuwa yeye yuko huko, nao wakaja, si kwa ajili yake Yesu tu, ila wamwone na Lazaro, ambaye Yesu alimfufua katika wafu.
Actes 3.10-3.11 Jean 11.43-11.45 Actes 4.14
10 Nao wakuu wa makuhani wakafanya shauri la kumwua Lazaro naye;
Genèse 4.4-4.10 Matthieu 2.16 Luc 16.31 Exode 10.3 Jean 11.57
11 maana kwa ajili yake wengi katika Wayahudi walijitenga, wakamwamini Yesu.
Jean 11.45 Jean 12.18 Jacques 3.14-3.16 Jean 11.48 Actes 13.45

Entrée triomphale de Jésus à Jérusalem

12 Nayo siku ya pili yake watu wengi walioijia sikukuu walisikia ya kwamba Yesu anakuja Yerusalemu;
Marc 11.7-11.10 Luc 19.35-19.38 Matthieu 21.4-21.9 Jean 11.55-11.56
13 wakatwaa matawi ya mitende, wakatoka nje kwenda kumlaki, wakapiga makelele, Hosana! Ndiye mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana, Mfalme wa Israeli!
Psaumes 118.25-118.26 Jean 1.49 Marc 11.8-11.10 Matthieu 21.9-21.11 Luc 19.35-19.38
14 Naye Yesu alikuwa amepata mwana-punda, akampanda, kama vile iliyoandikwa,
Zacharie 9.9 Matthieu 21.1-21.7 Marc 11.1-11.7 Luc 19.29-19.35
15 Usiogope, binti Sayuni; tazama, Mfalme wako anakuja, amepanda mwana-punda.
Zacharie 9.9 Esaïe 41.14 Esaïe 62.11 Juges 5.10 2 Samuel 16.2
16 Mambo hayo wanafunzi wake hawakuyafahamu hapo kwanza; lakini Yesu alipotukuzwa, ndipo walipokumbuka ya kwamba ameandikiwa hayo, na ya kwamba walimtendea hayo.
Jean 7.39 Jean 2.22 Jean 12.23 Jean 14.26 Marc 9.32
17 Basi wakamshuhudia wale mkutano waliokuwapo pamoja naye alipomwita Lazaro kutoka kaburini, akamfufua.
Jean 11.45-11.46 Jean 5.35-5.39 Jean 12.9 1 Jean 5.9-5.12 Jean 11.42
18 Na kwa sababu hiyo mkutano walikwenda kumlaki, kwa kuwa wamesikia ya kwamba ameifanya ishara hiyo.
Jean 12.11
19 Basi Mafarisayo wakasemezana wao kwa wao, Mwaona kwamba hamfai neno lo lote; tazameni, ulimwengu umekwenda nyuma yake.
Psaumes 22.27 Jean 3.26 Jean 17.21 1 Jean 2.2 Actes 5.27-5.28
20 Palikuwa na Wayunani kadha wa kadha miongoni mwa watu waliokwea kwenda kuabudu kwenye sikukuu.
Jean 7.35 Actes 17.4 Marc 7.26 1 Rois 8.41-8.43 Actes 8.27
21 Basi hao walimwendea Filipo, mtu wa Bethsaida ya Galilaya, wakamwomba, wakisema, Bwana, sisi tunataka kumwona Yesu.
Matthieu 15.22-15.28 Jean 6.5-6.7 Romains 15.8-15.12 Matthieu 8.9-8.12 Jean 1.43-1.47
22 Filipo akaenda, akamwambia Andrea; kisha Andrea na Filipo wakamwambia Yesu.
Matthieu 10.5 Luc 9.49-9.50 Marc 10.13-10.14 Jean 1.40-1.41 Jean 6.8
23 Naye Yesu akawajibu, akasema, Saa imefika atukuzwe Mwana wa Adamu.
Jean 13.31-13.32 Marc 14.41 Matthieu 25.31 Esaïe 55.5 Esaïe 53.10-53.12
24 Amin, amin, nawaambia, Chembe ya ngano isipoanguka katika nchi, ikafa, hukaa hali iyo hiyo peke yake; bali ikifa, hutoa mazao mengi.
1 Corinthiens 15.36-15.38 Hébreux 2.9-2.10 Esaïe 53.10-53.12 Psaumes 72.16 Psaumes 22.22-22.31
25 Yeye aipendaye nafsi yake ataiangamiza; naye aichukiaye nafsi yake katika ulimwengu huu ataisalimisha hata uzima wa milele.
Matthieu 10.39 Matthieu 16.25 Luc 17.33 Marc 8.35 Luc 14.26
26 Mtu akinitumikia, na anifuate; nami nilipo, ndipo na mtumishi wangu atakapokuwapo. Tena mtu akinitumikia, Baba atamheshimu.
1 Samuel 2.30 2 Corinthiens 5.8 Jean 17.24 Jean 14.3 Jean 10.27
27 Sasa roho yangu imefadhaika; nami nisemeje? Baba, uniokoe katika saa hii? Lakini ni kwa ajili ya hayo nilivyoifikia saa hii.
Jean 13.21 Luc 22.53 Jean 18.37 Hébreux 5.7 Luc 22.44
28 Baba, ulitukuze jina lako. Basi ikaja sauti kutoka mbinguni, Nimelitukuza, nami nitalitukuza tena.
Matthieu 3.17 2 Pierre 1.17 Matthieu 17.5 Marc 1.11 Jean 11.4
29 Basi mkutano uliosimama karibu wakasikia, walisema ya kwamba kumekuwa ngurumo; wengine walisema, Malaika amesema naye.
Actes 23.8-23.9 Apocalypse 14.2 Job 37.2-37.5 Apocalypse 6.1 Exode 20.18
30 Yesu akajibu, akasema, Sauti hiyo haikuwako kwa ajili yangu, bali kwa ajili yenu.
Jean 11.42 2 Corinthiens 8.9 Jean 11.15 Jean 5.34
31 Sasa hukumu ya ulimwengu huu ipo; sasa mkuu wa ulimwengu huu atatupwa nje.
2 Corinthiens 4.4 Jean 14.30 Ephésiens 6.12 Jean 16.8-16.11 1 Jean 3.8
32 Nami nikiinuliwa juu ya nchi, nitawavuta wote kwangu.
Jean 6.44 Jean 8.28 Jean 3.14 Hébreux 2.9 1 Timothée 2.6
33 Aliyanena hayo akionyesha ni mauti gani atakayokufa.
Jean 18.32 Jean 21.19
34 Basi mkutano wakamjibu, Sisi tumesikia katika torati ya kwamba Kristo adumu hata milele; nawe wasemaje ya kwamba imempasa Mwana wa Adamu kuinuliwa? Huyu Mwana wa Adamu ni nani?
Esaïe 9.7 Psaumes 110.4 Daniel 7.14 Psaumes 72.17-72.19 Matthieu 8.20
35 Basi Yesu akawaambia, Nuru ingaliko pamoja nanyi muda kidogo. Enendeni maadamu mnayo nuru hiyo, giza lisije likawaweza; maana aendaye gizani hajui aendako.
Jean 16.16 Jean 12.46 Jean 7.33 Jean 8.12 Ephésiens 5.8
36 Maadamu mnayo nuru, iaminini nuru hiyo, ili mpate kuwa wana wa nuru. Hayo aliyasema Yesu, akaenda zake, akajificha wasimwone.
Jean 8.59 Luc 16.8 1 Thessaloniciens 5.5 Ephésiens 5.8 Actes 13.47-13.48
37 Walakini ajapokuwa amefanya ishara nyingi namna hiyo mbele yao, hawakumwamini;
Jean 11.42 Matthieu 11.20 Jean 1.11 Jean 15.24 Luc 16.31
38 ili litimie lile neno la nabii Isaya alilolisema, Bwana, ni nani aliyezisadiki habari zetu; Na mkono wa Bwana amefunuliwa nani?
Esaïe 53.1 Romains 10.16 Galates 1.16 Esaïe 51.5 2 Corinthiens 3.14-3.18
39 Ndiyo sababu wao hawakuweza kusadiki; kwa maana Isaya alisema tena,
Jean 5.44 Esaïe 44.18-44.20 Jean 10.38 Jean 6.44 2 Pierre 2.14
40 Amewapofusha macho, Ameifanya mizito mioyo yao; Wasije wakaona kwa macho yao, Wakafahamu kwa mioyo yao, Wakaongoka, nikawaponya.
Esaïe 6.10 Matthieu 13.13-13.15 Marc 4.12 Luc 8.10 Psaumes 147.3
41 Maneno hayo aliyasema Isaya, kwa kuwa aliuona utukufu wake, akataja habari zake.
Esaïe 6.9-6.10 Esaïe 6.1-6.5 Hébreux 1.3 Jean 1.14 Jean 1.18
42 Walakini hata katika wakuu walikuwamo wengi waliomwamini; lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakumkiri, wasije wakatengwa na sinagogi.
Jean 7.13 Jean 9.22 Esaïe 51.7 Esaïe 57.11 Matthieu 10.32
43 Kwa maana walipenda utukufu wa wanadamu kuliko utukufu wa Mungu.
Jean 5.44 Luc 16.15 Matthieu 23.5-23.7 Jean 5.41 1 Pierre 1.7-1.8
44 Naye Yesu akapaza sauti, akasema, Yeye aniaminiye mimi, haniamini mimi bali yeye aliyenipeleka.
Matthieu 10.40 Jean 5.24 Jean 13.20 1 Pierre 1.21 Jean 11.43
45 Naye anitazamaye mimi amtazama yeye aliyenipeleka.
2 Corinthiens 4.6 Hébreux 1.3 Jean 15.24 Colossiens 1.15 1 Jean 5.20
46 Mimi nimekuja ili niwe nuru ya ulimwengu, ili kila mtu aniaminiye mimi asikae gizani.
Jean 8.12 Esaïe 42.7 Jean 9.5 Jean 3.19 Jean 12.35-12.36
47 Na mtu akiyasikia maneno yangu, asiyashike, mimi simhukumu; maana sikuja ili niuhukumu ulimwengu, ila niuokoe ulimwengu.
Jean 3.17 Jean 12.48 Matthieu 18.10 1 Jean 4.14 Jean 8.15-8.16
48 Yeye anikataaye mimi, asiyeyakubali maneno yangu, anaye amhukumuye; neno hilo nililolinena ndilo litakalomhukumu siku ya mwisho.
Romains 2.16 Luc 10.16 2 Thessaloniciens 1.8 Hébreux 9.27-9.28 Hébreux 10.29-10.31
49 Kwa sababu mimi sikunena kwa nafsi yangu tu; bali Baba aliyenipeleka, yeye mwenyewe ameniagiza nitakayonena na nitakayosema.
Jean 17.8 Jean 14.10 Jean 8.26 Jean 5.30 Jean 3.11
50 Nami najua ya kuwa agizo lake ni uzima wa milele; basi hayo ninenayo mimi, kama Baba alivyoniambia, ndivyo ninenavyo.
Jean 6.68 Jean 17.3 Jean 20.31 Jean 6.63 1 Timothée 1.16

Cette Bible est dans le domaine public.