Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Luc 21
Bible en Swahili de l’est


1 Akainua macho yake akawaona matajiri wakitia sadaka zao katika sanduku la hazina.
Marc 12.41-12.44 Jean 8.20 Matthieu 27.6 2 Chroniques 36.18 Josué 6.19
2 Akamwona mjane mmoja maskini akitia mle senti mbili.
Marc 12.42
3 Akasema, Hakika nawaambia, huyu mjane maskini ametia zaidi kuliko wote;
2 Corinthiens 8.12 Marc 14.8-14.9 2 Corinthiens 9.6-9.7 Exode 35.21-35.29 Luc 9.27
4 maana, hao wote walitia sadakani katika mali iliyowazidi, bali huyu katika umaskini wake ametia vyote alivyokuwa navyo.
Luc 8.43 Luc 15.12 Actes 4.34 Actes 2.44-2.45

Discours sur le mont des Oliviers

5 Na watu kadha wa kadha walipokuwa wakiongea habari za hekalu, jinsi lilivyopambwa kwa mawe mazuri na sadaka za watu, alisema,
Matthieu 24.1-24.51 Jean 2.20 Marc 13.1-13.37
6 Haya mnayoyatazama, siku zitakuja ambapo halitasalia jiwe juu ya jiwe ambalo halitabomoshwa.
Lamentations 4.1 Lamentations 2.6-2.8 2 Chroniques 7.20-7.22 Esaïe 64.10-64.11 Actes 6.13-6.14
7 Wakamwuliza wakisema, Mwalimu, mambo hayo yatakuwa lini? Nayo ni nini ishara ya kuwa mambo hayo ya karibu kutukia?
Actes 1.6-1.7 Matthieu 24.3 Daniel 12.6 Luc 21.27-21.28 Daniel 12.8
8 Akasema, Angalieni, msije mkadanganyika, kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, Mimi ndiye; tena, Majira yamekaribia. Basi msiwafuate hao.
2 Thessaloniciens 2.3 1 Jean 4.1 Ephésiens 5.6 Jérémie 29.8 Marc 13.5-13.6
9 Nanyi mtakaposikia habari za vita na fitina, msitishwe; maana, hayo hayana budi kutukia kwanza, lakini ule mwisho hauji upesi.
Matthieu 24.6-24.8 Marc 13.7-13.8 Luc 21.28 Esaïe 51.12-51.13 Luc 21.18-21.19
10 Kisha aliwaambia, Taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme;
Marc 13.8 Actes 2.19-2.20 2 Chroniques 15.5-15.6 Hébreux 12.27 Zacharie 14.13
11 kutakuwa na matetemeko makubwa ya nchi; na njaa na tauni mahali mahali; na mambo ya kutisha na ishara kuu kutoka mbinguni.
Matthieu 24.29-24.30 Luc 21.25-21.27
12 Lakini, kabla hayo yote hayajatokea, watawakamata na kuwaudhi; watawapeleka mbele ya masinagogi, na kuwaua magerezani, mkipelekwa mbele ya wafalme na maliwali kwa ajili ya jina langu.
Actes 8.3 Apocalypse 2.10 Matthieu 23.34-23.36 1 Pierre 4.12-4.14 Actes 16.22-16.26
13 Na hayo yatakuwa ushuhuda kwenu.
Philippiens 1.12 2 Thessaloniciens 1.5 1 Thessaloniciens 3.3-3.4 Philippiens 1.28
14 Basi, kusudieni mioyoni mwenu, kutofikiri-fikiri kwanza mtakavyojibu;
Marc 13.11 Luc 12.11-12.12 Matthieu 10.19-10.20
15 kwa sababu mimi nitawapa kinywa na hekima ambayo watesi wenu wote hawataweza kushindana nayo wala kuipinga.
Jérémie 1.9 Ephésiens 6.19 Colossiens 4.3-4.4 2 Timothée 4.16-4.17 Actes 24.25
16 Nanyi mtasalitiwa na wazazi wenu, na ndugu zenu, na jamaa zenu, na rafiki zenu, nao watawafisha baadhi yenu.
Apocalypse 6.9 Luc 12.53 Jérémie 9.4 Actes 12.2 Marc 13.12
17 Nanyi mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu.
Jean 15.21 Luc 6.22 Jean 15.19 2 Corinthiens 4.5 Jean 17.14
18 Walakini hautapotea hata unywele mmoja wa vichwa vyenu.
Matthieu 10.30 Luc 12.7 1 Samuel 14.45 1 Samuel 25.29 Actes 27.34
19 Nanyi kwa subira yenu mtaziponya nafsi zenu.
Romains 5.3 Hébreux 10.36 Matthieu 10.22 Jacques 1.3 Romains 2.7
20 Lakini, hapo mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, ndipo jueni ya kwamba uharibifu wake umekaribia.
Luc 19.43 Daniel 9.27 Luc 21.7 Marc 13.14 Matthieu 24.15
21 Ndipo walio katika Uyahudi na wakimbilie milimani, na walio katikati yake wakimbilie nje, na walio katika mashamba wasiuingie.
Apocalypse 18.4 Jérémie 35.11 Genèse 19.17 Proverbes 22.3 Jérémie 37.12
22 Kwa kuwa siku hizo ndizo za mapatilizo, ili yatimizwe yote yaliyoandikwa.
Osée 9.7 Esaïe 63.4 Esaïe 34.8 Matthieu 1.22 Jérémie 51.6
23 Ole wao wenye mimba na wanaonyonyesha katika siku hizo! Kwa kuwa kutakuwa na shida nyingi katika nchi, na hasira juu ya taifa hili.
Luc 23.29 1 Thessaloniciens 2.16 Matthieu 21.44 Matthieu 21.41 Marc 13.17
24 Wataanguka kwa ukali wa upanga, nao watatekwa nyara na kuchukuliwa katika mataifa yote; na Yerusalemu utakanyagwa na Mataifa, hata majira ya Mataifa yatakapotimia.
Romains 11.25 Apocalypse 11.2 Esaïe 63.18 Daniel 12.7 Daniel 9.27
25 Tena, kutakuwa na ishara katika jua, na mwezi, na nyota; na katika nchi dhiki ya mataifa wakishangaa kwa uvumi wa bahari na msukosuko wake;
Esaïe 13.10 Daniel 12.1 Esaïe 13.13-13.14 Esaïe 51.15 Joël 2.30-2.31
26 watu wakivunjika mioyo kwa hofu, na kwa kutazamia mambo yatakayoupata ulimwengu. Kwa kuwa nguvu za mbinguni zitatikisika.
Matthieu 24.29 Deutéronome 28.65-28.67 Hébreux 10.26-10.27 Lévitique 26.36 Deutéronome 28.32-28.34
27 Hapo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika wingu pamoja na nguvu na utukufu mwingi.
Matthieu 26.64 Apocalypse 1.7 Daniel 7.13 Marc 13.26 Matthieu 24.30
28 Basi mambo hayo yaanzapo kutokea, changamkeni, mkaviinue vichwa vyenu, kwa kuwa ukombozi wenu umekaribia.
Romains 8.23 Ephésiens 4.30 Esaïe 25.8-25.9 Luc 18.7 Romains 8.19
29 Akawaambia mfano; Utazameni mtini na miti mingine yote.
Marc 13.28-13.30 Matthieu 24.32-24.35
30 Wakati iishapo kuchipuka, mwaona na kutambua wenyewe ya kwamba majira ya mavuno yamekwisha kuwa karibu.
Luc 12.57
31 Nanyi kadhalika, mwonapo mambo hayo yanaanza kutokea, tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu u karibu.
1 Pierre 4.7 Matthieu 16.1-16.4 Jacques 5.9 Luc 12.51-12.57 Hébreux 10.37
32 Amin, nawaambieni, Kizazi hiki hakitapita hata hayo yote yatimie.
Matthieu 24.34 Marc 13.30 Luc 11.50-11.51 Matthieu 23.36 Matthieu 16.28
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
Matthieu 5.18 Esaïe 40.8 1 Pierre 1.25 Marc 13.31 Matthieu 24.35
34 Basi, jiangalieni, mioyo yenu isije ikalemewa na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha haya; siku ile ikawajia ghafula, kama mtego unasavyo;
Marc 4.19 1 Pierre 4.3-4.7 Matthieu 13.22 Luc 12.45-12.46 Osée 4.11
35 kwa kuwa ndivyo itakavyowajilia watu wote wakaao juu ya uso wa dunia nzima.
Apocalypse 16.15 Psaumes 11.6 Ecclésiaste 9.12 Luc 17.37 Esaïe 24.17-24.18
36 Basi, kesheni ninyi kila wakati, mkiomba, ili mpate kuokoka katika haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.
1 Pierre 5.8 Luc 18.1 1 Corinthiens 16.13 1 Jean 2.28 Matthieu 25.13
37 Basi, kila mchana alikuwa akifundisha hekaluni, na usiku huenda kulala katika mlima uitwao wa Mizeituni.
Matthieu 21.17 Matthieu 21.1 Marc 11.19 Luc 22.39 Matthieu 26.55
38 Na watu wote walikuwa wakiamka mapema waende hekaluni ili kumsikiliza.
Jean 8.1-8.2

Cette Bible est dans le domaine public.