Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Marc 11.23
Bible en Swahili de l’est


Entrée triomphale de Jésus à Jérusalem

1 Hata walipokaribia Yerusalemu karibu na Bethfage na Bethania, kukabili mlima wa Mizeituni, aliwatuma wawili katika wanafunzi wake,
Jean 12.14-12.19 Zacharie 14.4 Luc 19.29-19.40 Jean 8.1 Actes 1.12
2 akawaambia, Nendeni mpaka kile kijiji kinachowakabili; na katika kuingia ndani yake, mara mtaona mwana-punda amefungwa, asiyepandwa na mtu bado; mfungueni, kamleteni.
Matthieu 21.2-21.3 Luc 19.30-19.31
3 Na mtu akiwaambia, Mbona mnafanya hivi? Semeni, Bwana anamhitaji na mara atamrudisha tena hapa.
2 Corinthiens 8.9 Actes 10.36 Psaumes 24.1 Actes 1.24 Hébreux 2.7-2.9
4 Wakaenda zao, wakamwona mwana-punda amefungwa penye mlango, nje katika njia kuu, wakamfungua.
Luc 19.32-19.34 Matthieu 21.6-21.7 Matthieu 26.19 Hébreux 11.8 Jean 2.5
5 Baadhi ya watu waliosimama huko wakawaambia, Mnafanya nini kumfungua mwana-punda?
6 Wakawaambia kama Yesu alivyowaagiza, nao wakawaruhusu.
7 Wakamletea Yesu yule mwana-punda, wakatandika mavazi yao juu yake; akaketi juu yake.
Luc 19.35-19.36 Zacharie 9.9 Matthieu 21.7-21.8 Matthieu 21.4-21.5 2 Rois 9.13
8 Watu wengi wakatandaza mavazi yao njiani, na wengine matawi waliyoyakata mashambani.
Lévitique 23.40
9 Nao watu waliotangulia na wale waliofuata wakapaza sauti, Hosana; ndiye mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana;
Psaumes 118.25-118.26 Matthieu 23.39 Matthieu 21.9 Jean 19.15 Jean 12.13
10 umebarikiwa na ufalme ujao, wa baba yetu Daudi. Hosana juu mbinguni.
Luc 2.14 Psaumes 148.1 Ezéchiel 37.24-37.25 Osée 3.5 Luc 1.31-1.33
11 Naye akaingia Yerusalemu hata ndani ya hekalu; na alipokwisha kutazama yote pande zote, kwa kuwa ni wakati wa jioni, akatoka, akaenda Bethania pamoja na wale Thenashara.
Malachie 3.1 Luc 21.37-21.38 Jean 8.1-8.2 Matthieu 21.10-21.17 Luc 19.41-19.45

Jésus dans le temple

12 Hata asubuhi yake walipotoka Bethania aliona njaa.
Matthieu 21.18-21.22 Matthieu 4.2 Jean 4.31-4.33 Luc 4.2 Jean 19.28
13 Akaona kwa mbali mtini wenye majani, akaenda ili labda aone kitu juu yake; na alipoufikilia hakuona kitu ila majani; maana si wakati wa tini.
Luc 13.6-13.9 Matthieu 21.19 Luc 12.6-12.7 Luc 10.31 Esaïe 5.7
14 Akajibu, akauambia, Tangu leo hata milele mtu asile matunda kwako. Wanafunzi wake wakasikia.
Matthieu 21.19 Matthieu 21.33 Matthieu 12.33-12.35 Matthieu 7.19 Matthieu 3.10
15 Wakafika Yerusalemu, naye akaingia ndani ya hekalu, akaanza kuwafukuza wale waliokuwa wakiuza na kununua ndani ya hekalu, akazipindua meza za wabadili fedha, na viti vyao wauzao njiwa;
Matthieu 21.12-21.16 Jean 2.13-2.17 Luc 19.45-19.47 Deutéronome 14.25-14.26
16 wala hakuacha mtu achukue chombo kati ya hekalu.
17 Akafundisha, akasema, Je! Haikuandikwa, Nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala kwa mataifa yote? Bali ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang’anyi.
Esaïe 56.7 Jérémie 7.11 Luc 19.46 Jean 2.16 Osée 12.7
18 Wakuu wa makuhani na waandishi wakapata habari wakatafuta jinsi ya kumwangamiza; maana walimwogopa, kwa sababu mkutano wote walishangaa kwa mafundisho yake.
Matthieu 7.28 Marc 12.12 1 Rois 22.18 Matthieu 21.15 Matthieu 21.45-21.46
19 Na kulipokuwa jioni alitoka mjini.
Luc 21.37 Marc 11.11 Jean 12.36
20 Na asubuhi walipokuwa wakipita, waliuona ule mtini umenyauka toka shinani.
Hébreux 6.8 Marc 11.14 Job 20.5-20.7 Matthieu 13.6 Job 18.16-18.17
21 Petro akakumbuka habari yake, akamwambia, Rabi, tazama, mtini ulioulaani umenyauka.
Proverbes 3.33 Matthieu 23.7 1 Corinthiens 16.22 Matthieu 25.41 Zacharie 5.3-5.4
22 Yesu akajibu, akamwambia, Mwaminini Mungu.
Marc 9.23 Psaumes 62.8 Jean 14.1 2 Chroniques 20.20 Colossiens 2.12
23 Amin, nawaambia, Ye yote atakayeuambia mlima huu, Ng’oka ukatupwe baharini, wala asione shaka moyoni mwake, ila aamini kwamba hayo asemayo yametukia, yatakuwa yake.
Matthieu 17.20 Jean 15.7 Jean 14.13 Psaumes 37.4 1 Corinthiens 13.2
24 Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu.
Matthieu 21.22 1 Jean 5.14-5.15 1 Jean 3.22 Jacques 1.5-1.6 Matthieu 18.19
25 Nanyi, kila msimamapo na kusali, sameheni, mkiwa na neno juu ya mtu; ili na Baba yenu aliye mbinguni awasamehe na ninyi makosa yenu.
Colossiens 3.13 Matthieu 6.14-6.15 Luc 6.37 Ephésiens 4.32 Jacques 2.13
26 Lakini kama ninyi hamsamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu.]
27 Wakafika Yerusalemu tena; hata alipokuwa akitembea hekaluni, walimwendea wakuu wa makuhani, na waandishi, na wazee,
Matthieu 21.23-21.27 Luc 20.1-20.8 Actes 4.5-4.8 Psaumes 2.1-2.5 Actes 4.27-4.28
28 wakamwambia, Ni kwa mamlaka gani unatenda mambo haya? Naye ni nani aliyekupa mamlaka hii uyatende haya?
Exode 2.14 Nombres 16.13 Nombres 16.3 Actes 7.27-7.28 Actes 7.51
29 Yesu akawaambia, Nitawauliza neno moja, nanyi mnijibu, kisha nitawaambia ni kwa mamlaka gani nayatenda haya.
Esaïe 52.13 Matthieu 21.24 Luc 20.3-20.8
30 Ubatizo wa Yohana ulitoka mbinguni, au kwa wanadamu? Nijibuni.
Luc 3.1-3.20 Matthieu 3.1-3.17 Marc 1.1-1.11 Marc 9.13 Jean 1.15-1.36
31 Wakasemezana wao kwa wao, wakisema, Kama tukisema, Ulitoka mbinguni, atasema, Mbona, basi, hamkumwamini?
Jean 1.15 Jean 3.29-3.36 Matthieu 21.25-21.27 Matthieu 11.7-11.14 Matthieu 21.31-21.32
32 Ila tukisema, Ulitoka kwa wanadamu, -- waliogopa watu; maana watu wote walimwona Yohana kuwa nabii halisi.
Matthieu 21.46 Matthieu 14.5 Actes 5.26 Marc 6.20 Luc 20.19
33 Wakamjibu Yesu, wakasema, Hatujui. Yesu akawaambia, Wala mimi siwaambii ninyi ni kwa mamlaka gani nayatenda haya.
Matthieu 21.27 Esaïe 29.9-29.14 Job 5.13 Luc 22.66-22.69 2 Thessaloniciens 2.10-2.12

Cette Bible est dans le domaine public.