Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 10.26
Bible en Swahili de l’est


1 Akawaita wanafunzi wake kumi na wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu, wawatoe, na kupoza magonjwa yote na udhaifu wa kila aina.
Marc 6.7-6.13 Luc 9.1-9.6 Marc 3.13-3.15 Luc 24.49 Actes 1.8
2 Na majina ya hao mitume kumi na wawili ni haya; Wa kwanza Simoni aliyeitwa Petro, na Andrea nduguye; Yakobo wa Zebedayo, na Yohana nduguye;
Matthieu 4.18 Actes 1.13 Matthieu 4.21 Hébreux 3.1 Jean 20.2
3 Filipo, na Bartholomayo; Tomaso, na Mathayo mtoza ushuru; Yakobo wa Alfayo, na Thadayo;
Marc 3.18 Actes 1.13 Matthieu 9.9 Jean 20.24-20.29 Jean 1.43-1.46
4 Simoni Mkananayo, na Yuda Iskariote, naye ndiye mwenye kumsaliti.
Matthieu 26.14 Jean 13.2 Matthieu 26.47 Jean 6.71 Luc 22.3
5 Hao Thenashara Yesu aliwatuma, akawaagiza, akisema, Katika njia ya Mataifa msiende, wala katika mji wo wote wa Wasamaria msiingie.
Jean 4.9 Luc 9.2 2 Rois 17.24-17.41 Actes 1.8 Actes 8.1
6 Afadhali shikeni njia kuwaendea kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.
Jérémie 50.6 Esaïe 53.6 Actes 3.26 Actes 13.46 Psaumes 119.176
7 Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia.
Matthieu 3.2 Esaïe 61.1 Luc 9.60 Actes 28.31 Matthieu 4.17
8 Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure.
Actes 3.6 Actes 4.30 Actes 20.33-20.35 Actes 5.12-5.15 2 Rois 5.20-5.27
9 Msichukue dhahabu, wala fedha, wala mapesa mishipini mwenu;
Luc 22.35 Luc 9.3-9.5 1 Corinthiens 9.7-9.27 Luc 10.4-10.12 Marc 6.8-6.11
10 wala mkoba wa safari, wala kanzu mbili, wala viatu, wala fimbo; maana mtenda kazi astahili posho lake.
Luc 10.7-10.12 1 Timothée 5.17-5.18 1 Corinthiens 9.4-9.14 Luc 3.11 2 Timothée 4.13
11 Na mji wo wote au kijiji cho chote mtakachoingia, tafuteni ni nani humo aliye mtu mwaminifu; mkae kwake hata mtakapotoka.
1 Rois 17.9-17.24 Genèse 19.1-19.3 Actes 16.15 Job 31.32 3 Jean 1.7-1.8
12 Nanyi mkiingia katika nyumba isalimuni.
1 Samuel 25.6 Luc 10.5-10.6 2 Corinthiens 5.20 Actes 10.36 3 Jean 1.14
13 Na nyumba ile ikistahili, amani yenu na iifikilie; la, kwamba haistahili, amani yenu na iwarudie ninyi.
Psaumes 35.13 Luc 10.6 2 Corinthiens 2.16
14 Na mtu asipowakaribisha wala kuyasikiliza maneno yenu, mtokapo katika nyumba ile, au mji ule, kung’uteni mavumbi ya miguuni mwenu.
Actes 13.51 Actes 18.6 Néhémie 5.13 Actes 20.26-20.27 Luc 10.10-10.11
15 Amin, nawaambia, itakuwa rahisi nchi ya Sodoma na Gomora kustahimili adhabu ya siku ya hukumu, kuliko mji ule.
2 Pierre 2.9 1 Jean 4.17 Matthieu 12.36 2 Pierre 3.7 2 Pierre 2.6
16 Angalieni, mimi nawatuma kama kondoo kati ya mbwa-mwitu; basi iweni na busara kama nyoka, na kuwa watu wapole kama hua.
Luc 10.3 Actes 20.29 Philippiens 2.15 1 Corinthiens 14.20 2 Corinthiens 11.3
17 Jihadharini na wanadamu; kwa maana watawapeleka mabarazani, na katika masinagogi yao watawapiga;
Marc 13.9 Matthieu 23.34 Actes 26.11 Luc 12.11 Matthieu 5.22
18 nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa.
Matthieu 8.4 2 Timothée 4.16-4.17 Psaumes 2.1-2.6 Actes 24.1-24.26 Apocalypse 1.9
19 Lakini hapo watakapowapeleka, msifikiri-fikiri jinsi mtakavyosema; maana mtapewa saa ile mtakayosema.
Marc 13.11-13.13 Exode 4.12 Matthieu 6.25 Luc 12.11 2 Timothée 4.17
20 Kwa kuwa si ninyi msemao, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu.
Actes 4.8 Luc 21.15 Actes 6.10 2 Pierre 1.21 2 Samuel 23.2
21 Na ndugu atamsaliti nduguye ili auawe, na baba atamsaliti mwana, na wana watawainukia wazazi wao, na kuwafisha.
Michée 7.5-7.6 Zacharie 13.3 Marc 13.12-13.13 Luc 12.51-12.53 Luc 21.16-21.17
22 Nanyi mtakuwa mkichukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu; lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka.
Matthieu 24.13 Marc 13.13 Apocalypse 2.10 Jacques 1.12 Matthieu 10.39
23 Lakini watakapowafukuza katika mji huu, kimbilieni mwingine; kwa maana ni kweli nawaambia, Hamtaimaliza miji ya Israeli, hata ajapo Mwana wa Adamu.
Actes 17.10 Matthieu 16.28 Actes 8.1 Matthieu 25.13 Actes 13.50-13.51
24 Mwanafunzi hampiti mwalimu wake, wala mtumwa hampiti bwana wake.
Jean 15.20 Jean 13.16 Luc 6.40 2 Samuel 11.11 Hébreux 12.2-12.4
25 Yamtosha mwanafunzi kuwa kama mwalimu wake, na mtumwa kuwa kama bwana wake. Ikiwa wamemwita mwenye nyumba Beelzebuli, je! Si zaidi wale walio wa nyumbani mwake?
Marc 3.22 Matthieu 12.24 Matthieu 9.34 Luc 11.15 Jean 7.20
26 Basi, msiwaogope, kwa maana hakuna neno lililositirika, ambalo halitafunuliwa; wala lililofichwa, ambalo halitajulikana.
Marc 4.22 Luc 8.17 1 Corinthiens 4.5 Esaïe 41.14 Esaïe 43.1-43.2
27 Niwaambialo ninyi katika giza, lisemeni katika nuru; na msikialo kwa siri, lihubirini juu ya nyumba.
Actes 5.20 Jean 16.13 Actes 5.28 Jean 16.29 Jean 16.1
28 Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua na roho; afadhali mwogopeni yule awezaye kuangamiza mwili na roho pia katika jehanum.
Esaïe 8.12-8.13 Luc 12.4-12.5 2 Thessaloniciens 1.8-1.10 Esaïe 51.12 Luc 16.22-16.26
29 Je! Mashomoro wawili hawauzwi kwa senti moja? Wala hata mmoja haanguki chini asipojua Baba yenu;
Luc 12.6-12.7 Psaumes 104.27-104.30
30 lakini ninyi, hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote.
1 Samuel 14.45 2 Samuel 14.11 Luc 21.18 Actes 27.34 1 Rois 1.52
31 Msiogope basi; bora ninyi kuliko mashomoro wengi.
Matthieu 6.26 Psaumes 8.5 1 Corinthiens 9.9-9.10 Matthieu 12.11-12.12 Luc 12.24
32 Basi, kila mtu atakayenikiri mbele ya watu, nami nitamkiri mbele za Baba yangu aliye mbinguni.
Apocalypse 3.5 2 Timothée 1.8 Romains 10.9-10.10 1 Jean 4.15 Jean 9.22
33 Bali mtu ye yote atakayenikana mbele ya watu, nami nitamkana mbele za Baba yangu aliye mbinguni.
2 Timothée 2.12 1 Jean 2.23 Marc 8.38 Luc 9.26 2 Pierre 2.1
34 Msidhani ya kuwa nimekuja kuleta amani duniani; la! Sikuja kuleta amani, bali upanga.
Luc 12.49-12.53 Actes 14.4 Actes 13.45-13.50 Actes 14.2 Jean 7.40-7.52
35 Kwa maana nalikuja kumfitini mtu na babaye, na binti na mamaye, na mkwe na mkwe mtu;
Matthieu 10.21 Michée 7.5-7.6 Luc 21.16 Marc 13.12 Matthieu 24.10
36 na adui za mtu ni wale wa nyumbani mwake.
Michée 7.6 Psaumes 55.13 2 Samuel 16.11 Psaumes 41.9 1 Samuel 17.28
37 Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.
Luc 14.26 Matthieu 22.37 Philippiens 3.7-3.9 2 Corinthiens 5.14-5.15 Jean 21.15-21.17
38 Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili.
Matthieu 16.24 Luc 14.27 Marc 8.34 Luc 9.23-9.24 Jean 19.17
39 Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona.
Luc 17.33 Jean 12.25 Marc 8.35-8.36 Matthieu 16.25-16.26 Apocalypse 2.10
40 Awapokeaye ninyi, anipokea mimi; naye anipokeaye mimi, ampokea yeye aliyenituma.
Galates 4.14 Luc 10.16 Matthieu 18.5 Luc 9.48 Jean 13.20
41 Ampokeaye nabii kwa kuwa ni nabii, atapata thawabu ya nabii; naye ampokeaye mwenye haki kwa kuwa ni mwenye haki, atapata thawabu ya mwenye haki.
3 Jean 1.5-1.8 2 Rois 4.8-4.10 2 Rois 4.16-4.17 2 Jean 1.8 2 Rois 4.32-4.37
42 Na mtu awaye yote atakayemnywesha mmojawapo wa wadogo hawa ngaa kikombe cha maji ya baridi, kwa kuwa ni mwanafunzi, amin, nawaambia, haitampotea kamwe thawabu yake.
Matthieu 25.40 Hébreux 6.10 Matthieu 18.10 Luc 6.35 Marc 9.41-9.42

Cette Bible est dans le domaine public.