Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 49.19
Bible en Swahili de l’est


Prophétie sur Ammon

1 Habari za wana wa Amoni. Bwana asema hivi, Je, Israeli hana wana? Je! Hana mrithi? Basi, mbona Malkamu anamiliki Gadi, na watu wake wanakaa katika miji yake?
2 Chroniques 20.1 Ezéchiel 25.2-25.10 Amos 1.13-1.15 Deutéronome 23.3 Jérémie 25.21
2 Basi, kwa sababu hiyo, tazama, siku zinakuja, asema Bwana, nitakaposikizisha mshindo wa vita juu ya Raba, mji wa Amoni, nao utakuwa magofu ya ukiwa, na binti zake watateketezwa kwa moto; ndipo Israeli watawamiliki wao waliokuwa wakimmiliki, asema Bwana.
Jérémie 4.19 Ezéchiel 21.20 Deutéronome 3.11 Amos 1.14 Ezéchiel 25.4-25.6
3 Piga yowe, Ee Heshboni, Kwa maana Ai umeangamizwa; Lieni, enyi binti za Raba, Mjivike nguo za magunia; Ombolezeni, mkipiga mbio Huko na huko kati ya maboma; Maana Malkamu atakwenda kuhamishwa, Makuhani wake na wakuu wake pamoja.
Jérémie 48.7 Esaïe 15.2 Jérémie 48.37 1 Rois 11.5 Jérémie 4.8
4 Mbona unajisifu kwa sababu ya mabonde, bonde lako litiririkalo, Ee binti mwenye kuasi? Utumainiaye hazina zako, ukisema, Ni nani atakayenijilia?
1 Timothée 6.17 Jérémie 21.13 Jérémie 9.23 Jérémie 48.7 Psaumes 62.10
5 Tazama, nitaleta hofu juu yako, asema Bwana, Bwana wa majeshi, itakayotoka kwa wote wakuzungukao; nanyi mtafukuzwa nje, kila mtu mbali kabisa, wala hapana mtu wa kuwakusanya wapoteao.
Jérémie 46.5 Jérémie 49.29 Jérémie 20.4 2 Rois 7.6-7.7 Job 15.21
6 Lakini baada ya hayo nitawarudisha wana wa Amoni walio utumwani, asema Bwana.
Jérémie 48.47 Jérémie 49.39 Esaïe 23.18 Jérémie 46.26 Esaïe 19.18-19.23

Prophétie sur Édom

7 Habari za Edomu. Bwana wa majeshi asema hivi, Je! Hapana tena hekima katika Temani? Mashauri yamewapotea wenye busara? Je! Imetoweka hekima yao?
Genèse 25.30 Genèse 36.11 Jérémie 49.20 Genèse 36.15 Jérémie 25.21
8 Kimbieni, rudini nyuma, kaeni chini sana, enyi mnaokaa Dedani; maana nitaleta msiba wa Esau juu yake, wakati nitakapomwangalia.
Jérémie 25.23 Jérémie 46.21 Esaïe 21.13 Jérémie 49.30 Jérémie 49.32
9 Je! Kama wachuma zabibu wangekujia, wasingeacha zabibu ziokotwe? Kama wangekujia wevi usiku, wasingeharibu hata watakapopata vya kutosha?
Abdias 1.5-1.6 Esaïe 17.6
10 Lakini nimemwacha Esau hana kitu, nimepafunua mahali pake pa siri, wala hataweza kujificha; kizazi chake kimeangamizwa, na ndugu zake, na jirani zake, naye mwenyewe hayuko.
Esaïe 17.14 Malachie 1.3-1.4 Esaïe 45.3 Abdias 1.9 Jérémie 23.24
11 Waache watoto wako wasio na baba, mimi nitawahifadhi hai, na wajane wako na wanitumaini mimi.
Psaumes 68.5 Osée 14.3 Proverbes 23.10-23.11 Deutéronome 10.18 Malachie 3.5
12 Maana Bwana asema hivi, Tazama, wale wasioandikiwa kunywea kikombe, watakinywea, ni hakika; na wewe je! U mtu ambaye hataadhibiwa kabisa? Hukosi utaadhibiwa, naam, kunywa utakunywa.
Jérémie 25.28-25.29 Abdias 1.16 Jérémie 46.27 Jérémie 30.11 Jérémie 25.15
13 Kwa maana nimeapa kwa nafsi yangu, asema Bwana, kwamba Bozra utakuwa ajabu, na aibu, na ukiwa, na laana; na miji yake yote itakuwa ukiwa wa daima.
Genèse 22.16 Genèse 36.33 Esaïe 34.6 Jérémie 44.26 Esaïe 63.1
14 Nimepata habari kwa Bwana, Na mjumbe ametumwa kati ya mataifa, Akisema, Jikusanyeni, mkaujie, Mkainuke kwenda vitani.
Esaïe 30.4 Esaïe 37.7 Matthieu 24.6 Abdias 1.1-1.4 Ezéchiel 7.25-7.26
15 Maana nimekufanya mdogo kati ya mataifa, Na kudharauliwa katika watu.
Luc 1.51 1 Samuel 2.30 Psaumes 53.5 1 Samuel 2.7-2.8 Michée 7.10
16 Katika habari za kuogofya kwako, Kiburi cha moyo wako kimekudanganya, Wewe ukaaye katika pango za majabali, Ushikaye kilele cha milima; Ujapofanya kioto chako juu sana kama tai, Nitakushusha kutoka huko; asema Bwana.
Job 39.27 Amos 9.2 Esaïe 14.13-14.15 Proverbes 29.23 Jérémie 48.28-48.29
17 Na Edomu atakuwa ajabu; kila mtu apitaye atashangaa, na kuzomea, kwa sababu ya mapigo yake yote.
Jérémie 50.13 Ezéchiel 35.7 Jérémie 49.13 Jérémie 51.37 1 Rois 9.8
18 Kama vile vilivyotokea wakati wa kuangushwa Sodoma na Gomora, na miji iliyokuwa karibu nayo, asema Bwana; hapana mtu atakayekaa huko, wala hapana mwanadamu atakayekaa huko kama mgeni akaavyo.
Jérémie 49.33 Deutéronome 29.23 Amos 4.11 Job 18.15-18.18 Sophonie 2.9
19 Angalia, atapanda kama simba toka kiburi cha Yordani juu ya malisho yasiyonyauka; lakini nitamkimbiza ghafula ayaache; na yeye aliye mteule nitamweka juu yake; maana ni nani aliye kama mimi? Tena ni nani atakayeniandikia muda? Tena ni mchungaji yupi atakayesimama mbele zangu?
Jérémie 12.5 Exode 15.11 Job 9.19 Job 41.10 Jérémie 50.44-50.46
20 Basi, lisikieni shauri la Bwana; Alilolifanya juu ya Edomu; Na makusudi yake aliyoyakusudia Juu yao wakaao Temani; Hakika watawaburura, naam, wadogo wa kundi; Hakika malisho yao yatafadhaika kwa ajili yao.
Jérémie 50.45 Malachie 1.3-1.4 Jérémie 49.7 Actes 4.28 Job 6.19-6.20
21 Nchi yatetemeka kwa sauti ya kuanguka kwao; Kuna kilio, sauti yake yasikiwa katika Bahari ya Shamu.
Jérémie 50.46 Ezéchiel 32.10 Esaïe 14.4-14.15 Apocalypse 18.10 Ezéchiel 26.15-26.18
22 Tazama, atapanda na kuruka kama tai, na kutandaza mabawa yake juu ya Bozra; na mioyo ya mashujaa wa Edomu siku hiyo itakuwa kama moyo wa mwanamke katika utungu wake.
Jérémie 48.40-48.41 Esaïe 13.8 Osée 8.1 Deutéronome 28.49 Jérémie 49.24

Prophétie sur Damas

23 Habari za Dameski. Hamathi umetahayarika, na Arpadi pia; Maana wamesikia habari mbaya; Wameyeyuka kabisa; Huzuni iko baharini, haiwezi kutulia.
2 Rois 18.34 Esaïe 10.9 Genèse 14.15 Esaïe 57.20 Genèse 15.2
24 Dameski umedhoofika; Umejigeuza kukimbia; tetemko limeushika; Dhiki na huzuni zimeupata, Kama za mwanamke katika utungu wake.
25 Imekuwaje mji wa sifa haukuachwa, mji wa furaha yangu?
Jérémie 51.41 Jérémie 33.9 Daniel 4.30 Apocalypse 18.16-18.19 Apocalypse 18.10
26 Kwa hiyo vijana wake wataanguka katika njia kuu zake, na watu wote wa vita watanyamazishwa katika siku hiyo, asema Bwana wa majeshi.
Jérémie 50.30 Jérémie 11.22 Amos 4.10 Lamentations 2.21 Ezéchiel 27.27
27 Nami nitawasha moto katika ukuta wa Dameski, nao utayateketeza majumba ya Ben-hadadi.
1 Rois 15.18-15.20 Amos 1.3-1.5 2 Rois 13.3 2 Rois 13.5 1 Rois 20.1-20.22

Prophétie sur Kédar et Hatsor

28 Habari za Kedari, na za falme za Hazori, ambazo Nebukadreza, mfalme wa Babeli, alizipiga. Bwana asema hivi, Ondokeni, pandeni hata Kedari, mkawateke nyara wana wa mashariki.
Genèse 25.13 Esaïe 11.14 Juges 6.3 Ezéchiel 27.21 Esaïe 21.16-21.17
29 Hema zao na makundi yao watayatwaa; watachukulia mbali mapazia yao kwa faida yao wenyewe, na vyombo vyao vyote, na ngamia zao; nao watawapigia kelele wakisema, Hofu ziko pande zote.
Jérémie 46.5 Jérémie 6.25 Habakuk 3.7 Psaumes 120.5 Psaumes 31.13
30 Kimbieni ninyi, enendeni mbali mkitanga-tanga, kaeni chini sana, enyi mkaao Hazori, asema Bwana; maana Nebukadreza, mfalme wa Babeli, amefanya shauri juu yenu, naye amekusudia neno juu yenu.
Jérémie 25.9 Esaïe 10.7 Jérémie 27.6 Jérémie 25.24-25.25
31 Ondokeni, pandeni hata taifa lililo katika hali ya raha, likaalo bila kuhangaika, asema Bwana; wasio na malango wala makomeo, wakaao peke yao.
Ezéchiel 38.11 Nombres 23.9 Michée 7.14 Deutéronome 33.28 Esaïe 47.8
32 Na ngamia zao watakuwa mateka, na wingi wa makundi yao utakuwa nyara; nami nitawatawanya hata pepo zote watu wale wanyoao denge; nami nitaleta msiba wao toka pande zao zote, asema Bwana.
Jérémie 9.26 Jérémie 49.36 Ezéchiel 5.10 Ezéchiel 12.14-12.15 Jérémie 25.23
33 Na Hazori utakuwa kao la mbwa-mwitu; ukiwa milele; hapana mtu atakayekaa huko, wala hapana mwanadamu atakayekaa huko kama mgeni akaavyo.
Jérémie 51.37 Jérémie 9.11 Jérémie 10.22 Esaïe 13.20-13.22 Sophonie 2.9

Prophétie sur Élam

34 Neno la Bwana lililomjia Yeremia, nabii, juu ya Elamu, mwanzo wa kumiliki kwake Sedekia, mfalme wa Yuda, kusema,
Genèse 14.1 Genèse 10.22 Daniel 8.2 Jérémie 25.25 Esaïe 21.2
35 Bwana wa majeshi asema hivi, Tazama nitauvunja upinde wa Elamu, ulio mkuu katika nguvu zao.
Esaïe 22.6 Psaumes 46.9 Jérémie 51.56 Jérémie 50.29 Jérémie 50.14
36 Na juu ya Elamu nitazileta pepo nne, toka pembe nne za mbinguni, nami nitawatawanya hata pepo nne zote, wala hapana taifa ambalo hawatalifikilia watu wa Elamu waliofukuzwa.
Jérémie 49.32 Ezéchiel 5.10 Apocalypse 7.1 Amos 9.9 Daniel 8.8
37 Nami nitawafadhaisha watu wa Elamu mbele ya adui zao, na mbele ya hao wanaowatafuta roho zao; nami nitawaletea mabaya, naam, hasira yangu kali, asema Bwana; nami nitautuma upanga uwafuatie, hata nitakapowaangamiza;
Jérémie 9.16 Jérémie 48.2 Ezéchiel 12.14 Jérémie 49.22 Jérémie 49.29
38 nami nitaweka kiti changu cha enzi huko Elamu, nami nitawaharibu, mfalme na wakuu, watoke huko, asema Bwana.
Daniel 7.9-7.14 Jérémie 43.10
39 Lakini itakuwa, katika siku za mwisho, nitawarudisha wafungwa wa Elamu, asema Bwana.
Jérémie 48.47 Ezéchiel 16.53-16.55 Jérémie 49.6 Michée 4.1 Amos 9.14

Cette Bible est dans le domaine public.